Tuko
JF-Expert Member
- Jul 29, 2010
- 11,178
- 7,319
Ni miaka miaka miwili na nusu tu, lakini baadhi ya watu wanaanza kusahau. Sasa imekuwa kawaida kusikia baadhi ya watu wakisema kuwa CHADEMA iligoma kuishirikisha CUF kwenye kambi rasmi ya upinzani bungeni. Hii sio sawa na ni lazima tukumbushane au tuwaonyeshe kuwa hatujasahau...
Wakati bunge linaanza mwaka 2010, uongozi wa CHADEMA ukiongozwa na Mbowe walifanya juhudi kubwa sana za kuvitaka vyama vyote vya upinzani waungane ili waunde kambi rasmi ya upinzani bungeni. NCCR waligoma kutokana na mgogoro wa kisiasa ulioibuka kati ya mwenyekiti wao Mbatia na Mdee katika kampeni za ubunge Kawe, na Mbatia alikataa suluhu na kulipeleka suala lile mahakamani. TLP na UDP nao waliungana na NCCR.
CHADEMA haikuwa na jinsi zaidi ya kuiapproach CUF wakiamini kwamba kama chama cha tatu kwa ukubwa bungeni, wangekubali kishiriki katika kambi ile. CHADEMA wakiongozwa na Mbowe na CUF wakiongozwa na Hamad Rashid, walifanya majadiliano marefu lakini kwa masikitiko ya wengi CUF walikataa, wakishikilia msimamo kuwa CDM watafute suluhu kwanza na NCCR kama walitaka kushirikiana na CUF katika upinzani.
Huku NCCR waking'ang'ania mahakamani, na CUF wakilazimisha suluhu kwanza kati ya CHADEMA na NCCR, CHADEMA hawakuwa na jinsi zaidi ya kuunda kambi rasmi ya upinzani bungeni, huku Mbowe akiahidi kuwa pale wenzao watakapokuwa tayari basi watashiriki katika kambi rasmi ya upinzani bungeni.
CUF wakati huo wakiwa wametoka katika mashamsham ya mahusiano yao mapya na CCM huko Zanzibar, waliwaongoza NCCR, TLP na UDP kuungana na CCM na kubadilisha vifungu vya kanuni za bunge ili kuinyima CHADEMA mandate ya kuongoza zile kamati tatu za bunge.
Leo hii baada ya kugundua kuwa mshirika wao CCM hana nia njema nao, CUF wanatembea barabarani wakiilaumu CHADEMA kwa kukataa kuishirikisha kwenye kambi rasmi ya upinzani!!!
Mi nawashauiri warudi hukohuko kwa mshirika mwenzao, wakae wayamalize mambo yao ya ndani hayo. CHADEMA ilishasonga mbele na haihitaji tena msaada wenu, kwani kwa miaka miwili na nusu hii sapoti iliyopata kutoka kwa nguvu ya umma inatosha kuwawezesha kutetea rasilimali za nchi hii kwa nafasi yao...
Wakati bunge linaanza mwaka 2010, uongozi wa CHADEMA ukiongozwa na Mbowe walifanya juhudi kubwa sana za kuvitaka vyama vyote vya upinzani waungane ili waunde kambi rasmi ya upinzani bungeni. NCCR waligoma kutokana na mgogoro wa kisiasa ulioibuka kati ya mwenyekiti wao Mbatia na Mdee katika kampeni za ubunge Kawe, na Mbatia alikataa suluhu na kulipeleka suala lile mahakamani. TLP na UDP nao waliungana na NCCR.
CHADEMA haikuwa na jinsi zaidi ya kuiapproach CUF wakiamini kwamba kama chama cha tatu kwa ukubwa bungeni, wangekubali kishiriki katika kambi ile. CHADEMA wakiongozwa na Mbowe na CUF wakiongozwa na Hamad Rashid, walifanya majadiliano marefu lakini kwa masikitiko ya wengi CUF walikataa, wakishikilia msimamo kuwa CDM watafute suluhu kwanza na NCCR kama walitaka kushirikiana na CUF katika upinzani.
Huku NCCR waking'ang'ania mahakamani, na CUF wakilazimisha suluhu kwanza kati ya CHADEMA na NCCR, CHADEMA hawakuwa na jinsi zaidi ya kuunda kambi rasmi ya upinzani bungeni, huku Mbowe akiahidi kuwa pale wenzao watakapokuwa tayari basi watashiriki katika kambi rasmi ya upinzani bungeni.
CUF wakati huo wakiwa wametoka katika mashamsham ya mahusiano yao mapya na CCM huko Zanzibar, waliwaongoza NCCR, TLP na UDP kuungana na CCM na kubadilisha vifungu vya kanuni za bunge ili kuinyima CHADEMA mandate ya kuongoza zile kamati tatu za bunge.
Leo hii baada ya kugundua kuwa mshirika wao CCM hana nia njema nao, CUF wanatembea barabarani wakiilaumu CHADEMA kwa kukataa kuishirikisha kwenye kambi rasmi ya upinzani!!!
Mi nawashauiri warudi hukohuko kwa mshirika mwenzao, wakae wayamalize mambo yao ya ndani hayo. CHADEMA ilishasonga mbele na haihitaji tena msaada wenu, kwani kwa miaka miwili na nusu hii sapoti iliyopata kutoka kwa nguvu ya umma inatosha kuwawezesha kutetea rasilimali za nchi hii kwa nafasi yao...