Tuwe wawazi; hivi kimuziki tunaweza kuwafikia watu wa Afrika Magharibi kweli?

Kwenye suala la lugha umezungumza jambo lenye ukweli sana, nchi nyingi za West Africa huwa wanaimba kiingereza na kifaransa, lugha ambazo zinazungumzwa sana duniani. Kiufupi wasaniii wote wakubwa barani Afrika ambao wamewahi kushinda tuzo kubwa kama Grammy, aidha wanaimba kiingereza, kifaransa au wanafanya folk-music kama Lady Smith Black Mambazo.
lugha haina mahusiano ya moja kwa moja na mafanikio ya kimuziki maana muziki wenyewe ni lugha ambayo mtu yoyote anaweza kuoilewa tatizo liko kwenye uwekezaji ie vipaji vipya, tekinologia,ubunifu n.k
 
lugha haina mahusiano ya moja kwa moja na mafanikio ya kimuziki maana muziki wenyewe ni lugha ambayo mtu yoyote anaweza kuoilewa tatizo liko kwenye uwekezaji ie vipaji vipya, tekinologia,ubunifu n.k
Fanani hawezi kuifikia hadhira bila matumizi ya lugha, hivyo binafsi naamini lugha ina mchango mkubwa tu. Japo nakubaliana pia na ulichokisema kwamba umahiri, ubunifu na matumizi ya teknolojia yana mchango mkubwa sana. Kuna watengenezaji muziki (Classical Composers) kama Mozart, Bach, Prokofiev, Enio Morricone na John Coltraine wao wanapiga vyombo tu na muziki wao bado unasikilizwa mpaka leo.

Kama unaimba kwa kutumia lugha yako ukitaka kutoka basi lazima utengenezaji wako wa muziki uwe umejaa ubunifu wa hali ya juu sana. Mfano Black Mambazo Lady Smith wana Grammy Awards kibao na wanaimba kwa lugha asilia, lakini aina ya uimbaji wao iko kitaalamu sana (Too Sophisticated), hata kama huelewi maneno lakini kama unafahamu muziki lazima utajua hawa jamaa ni wataalamu.

Watanzania utaalamu wa muziki hatuna, watengenezaji muziki asilia (Traditional Composers) hatuna. Sisi tumezoea muziki wa studio (FL) tu. Kiasi kwamba hata ukisikiliza hupati kitu cha ziada kabisa, hili limetugharimu sana hata kwenye kufanya Live Perfomance....
 
Fanani hawezi kuifikia hadhira bila matumizi ya lugha, hivyo binafsi naamini lugha ina mchango mkubwa tu. Japo nakubaliana pia na ulichokisema kwamba umahiri, ubunifu na matumizi ya teknolojia yana mchango mkubwa sana. Kuna watengenezaji muziki (Classical Composers) kama Mozart, Bach, Prokofiev, Enio Morricone na John Coltraine wao wanapiga vyombo tu na muziki wao bado unasikilizwa mpaka leo.

Kama unaimba kwa kutumia lugha yako ukitaka kutoka basi lazima utengenezaji wako wa muziki uwe umejaa ubunifu wa hali ya juu sana. Mfano Black Mambazo Lady Smith wana Grammy Awards kibao na wanaimba kwa lugha asilia, lakini aina ya uimbaji wao iko kitaalamu sana (Too Sophisticated), hata kama huelewi maneno lakini kama unafahamu muziki lazima utajua hawa jamaa ni wataalamu.

Watanzania utaalamu wa muziki hatuna, watengenezaji muziki asilia (Traditional Composers) hatuna. Sisi tumezoea muziki wa studio (FL) tu. Kiasi kwamba hata ukisikiliza hupati kitu cha ziada kabisa, hili limetugharimu sana hata kwenye kufanya Live Perfomance....
tujiulize Kwanza
ilikuweje wakina Biti Siti muziki wao ulikubalika huko bara Hindi wakitumia kiswahili
ilikuweje wakina Bibi kidude waliweza kufanya matamasha hata huko ujerumani kwa kiswahili
vipi Jaguar waliwezaje kwenda mpaka huko japani kutumbuiza muziki wao kwa kiswahili
:N.B. hao waliwezaje kupeleka muziki wao duniani kwa kutumia lugha mama kwa teknologia ya zamani hawa wa leo wanakwama wapi na wana kila kitu teknologia(social media),pesa n.k
 
tujiulize Kwanza
ilikuweje wakina Biti Siti muziki wao ulikubalika huko bara Hindi wakitumia kiswahili
ilikuweje wakina Bibi kidude waliweza kufanya matamasha hata huko ujerumani kwa kiswahili
vipi Jaguar waliwezaje kwenda mpaka huko japani kutumbuiza muziki wao kwa kiswahili
:N.B. hao waliwezaje kupeleka muziki wao duniani kwa kutumia lugha mama kwa teknologia ya zamani hawa wa leo wanakwama wapi na wana kila kitu teknologia(social media),pesa n.k
Muziki wa Bibi Kidude unaangukia kwenye genre ya Folk-Music, ukiusikiliza sana ulikuwa na utaalamu (Sophisticated) ambao hata leo hii wasanii wetu wengi hawana. Kuanzia kwenye sauti (vocals), upigaji wa vyombo ambapo alichanganya muziki wa mwambao na Afro-Jazz huku akifanya uimbaji wa papo kwa papo (Live Perfomance). Hiki cha kuchanganya muziki wa kiafrika na Jazz ndicho kiliwafanya watu kama Remmy Ongala kufika mbali kwasababu walifanya muziki kitaalamu.
 
Hili nalo lina ukweli mkubwa tu, wasomi wanaongozwa kwa kufanyiwa rejea hapa Afrika ni Wanaijeria, Wakenya na Waafrika Kusini. Kama umesoma fasihi (Literature) utakumbuka vitabu vingi tulivyovitumia vilikuwa vimetoka ule ukanda. Wole Soyinka, Chinua Achebe, Ayi Kwei Armah, Danny B. Safo hawa walikuwa ni kizazi hicho, leo hii kuna wakina Chimamanda, yaani kila kizazi lazima watoe mtu wa maana ambaye anazungumzia masuala muhimu ya Afrika.
Nafikiri sababu kuu ni wao kuandika kwa kiingereza. Lakini katika uandishi wote hao wako level moja au chini ya Kezilahabi na Shaaban Robert. Na kuna waandishi wengine bora sana wa kiswahili, lakini kwasababu ya lugha ndiyo maana tunawasikia sana hao wa nchi hizo.
 
Nimekua nikiangalia mashabiki wa mziki wa kwetu kwa muda mrefu, kuna wanaosema nchi yetu ina mwanamziki bora Afrika nzima!
Nasikitika lakini sina namna nabaki kushangaa tu.

Afrika Magharibi wanatuzidi ktk sehemu zote iwe ni burudani, elimu,Biashara, utamaduni,uigizaji,michezo,comedy nk!

Youssor N'Dor, salif Keita,Sekouba Bambino,Toumane Diabate, Amadou Balake,Coumba Gawlo,Habib Faye,Jimi Mbaye, Gnonas Pedro,Oumoh Sangare,Thione Sekh,Bonkana Maiga,Mbalou Kante na wengine wengi tu ukiwasikiliza unajua wanajua barabara zao, mziki wao unazungumza sehemu ipi barani Afrika wanatokea.

Mziki umechanganywa na Siasa,tamaduni zao,imani zao,asili zao,uelewa wao,ukomavu wao na uzoefu wao!

West Africa wanafahamika sehemu nyingi zaidi ya dunia, wana tuzo zisizo na idadi, wana vipato vikubwa sana kulinganisha na wa kwetu.

Tanzania tumebarikiwa ujuaji mwingi,kujikweza kwingi,kujiona tunastahili kuheshimiwa kuliko wengine,tunahitaji tuonekane tuna pesa nyingi kuliko tulivyo!

Mfano rahisi ni Youssor N'Dor ana utajiri wa usd 145 milioni, lakini sisi hatuelewi hayo tunataka tutambulike tuko juu ya wote.
Screenshot_20211126-093418_Google.jpg
 
Nafikiri sababu kuu ni wao kuandika kwa kiingereza. Lakini katika uandishi wote hao wako level moja au chini ya Kezilahabi na Shaaban Robert. Na kuna waandishi wengine bora sana wa kiswahili, lakini kwasababu ya lugha ndiyo maana tunawasikia sana hao wa nchi hizo.
Kwenye uandishi tatizo siyo lugha peke yake, tatizo ni kwamba watanzania hawana utamaduni wa kupenda kujisomea.
Hivyo kama waandishi wetu hawatasomwa na kuanza kutambulika na sisi, unategemea nani atawatambua huko nje ??
 
Wazungu husema hivi "Once is an accident, twice is a coincidence and thrice is a pattern

Ule ukanda wa Afrika Magharibi wana kitu cha ziada ambacho nadhani hakionekani lakini kipo tu. Ukifuatilia historia utatambua kwamba watu wenye asili ya ukanda ule ndiyo wanaotawala sehemu kubwa ya tasnia ya burudani hapa duniani, hasahasa muziki. Historia inatuambia wao ndiyo hupeperusha bendera ya muziki wa Afrika tokea vizazi.

Wasanii wakubwa duniani kama Fela Kuti, Youssou N'Dour, Mory Kante, Angelique Kidjo, Salif Keita, Baaba Maal ambao wana mchango mkubwa kwenye muziki Afrika na duniani kote wametokea ule ukanda. Lakini zaidi ya haya, yapo ambayo yananishangaza zaidi. Mosi, baada ya kizazi cha wakina Fela Kuti kuondoka kimezaliwa kizazi kingine kipya ambacho kinaendelea kupeperusha bendera kwa nguvu sana kuliko kile cha kwanza.

Pili, wamegundua vifaa vingi vya muziki ambavyo vinatumiwa sana duniani mfano Akoting limegunduliwa Senegal, Balafon inatumika sana Ghana, Udu limegunduliwa Nigeria, Alagaita imegunduliwa Nigeria, Ngoma ya Djembe imegunduliwa kule Burkina Faso, hata Shekere nazo zimegunduliwa ule ukanda. Kiufupi ukifuatilia sana dhana nyingi za muziki za wabantu zimeanzia kule Afrika Magharibi.

Tatu, hata wale ndugu zao wa karibu ambao waliuzwa utumwani barani Marekani wamekuwa ni ndiyo vinara wakubwa kwenye tasnia nzima ya burudani na michezo. Kama unafuatilia muziki vizuri utatambua kwamba wamarekani weusi wamegundua na kuchangia vipengele (Genres) nyingi za muziki ambazo tunazikiliza leo hii. Muziki wa Jazz (Jazz Music) ndiyo ulizaa Blues, Soul, Rock and Roll, pamoja na Pop ambazo tunazipenda leo. Utafiti wa kisayansi (DNA/ Ancestry Tracing) unasema kwamba wale wasanii wametokea ule ukanda.

Nawapenda sana wasanii wetu kutoka huu ukanda, lakini kila nikifuatilia muziki wao kwa ukaribu halafu nikalinganisha na kile wenzetu wanatengeneza huwa nabaki nawaza sana. Ushawishi wa ukanda wa Magharibi umekuwa mkubwa sana kwenye muziki wa Afrika Mashariki hadi kupelekea sisi kuwaiga wao bila hata kufahamu kwamba tunawaiga, Kuanzia kwenye midundo hadi aina ya uimbaji.

Jambo kubwa ambalo mimi nimefanikiwa kulitambua kidogo ni kwamba sanaa hasa muziki na burudani nyingine ni sehemu za utamaduni wa kila jamii. Hivyo jamii yoyote ambayo hupenda sana utamaduni wake huweza kuwa na muziki wake na hata hufanikiwa sana kuusambaza. Kabla ya mkoloni muziki ulitumika kama sehemu ya ibada, sehemu ya masimulizi na sehemu ya burudani: Hata sasa iko hivi japo muziki ambao huwa tunatumia ni ule wa Magharibi na Mashariki ya Kati.

Baada ya mkoloni kuondoka ni jamii chache za kiafrika zilifanikiwa kutunza yale ya kale na zimekuwa na kitu cha kuionesha dunia ambacho dunia haina. Hivyo dunia ya leo imekuwa tayari kusikiliza na kujifunza kwasababu ni kitu kipya ambacho kimebeba taswira yote ya jamii fulani ambayo ilitengwa hapo mwanzo wakati dunia inaendeshwa na mtu mweupe. Leo hata umsikilize mtu kama Burna Boy au Sarkodie ambao mmoja huimba Afro-Pop na mwingine huimba Hip-Hop lazima utayasikia mahadhi ya muziki wa Afrika Magharibi.

Sisi tulikuwa ni Bakurutu na Taarab ambayo binafsi naamini ilibebe taswira nzima ya utamaduni wetu na ingeendelea kubeba mpaka leo hii kwasababu muziki hukua (Evolves), lakini sijui nini kilitokea hapa katikati muziki ule ukafa. Ukifuatilia wasanii wengi wa Tanzania waliofahamika huko duniani hata kabla ya Diamond Platnumz walikuwa ni wazee wetu wa Bakurutu. Taarab nayo japo wengi tuliikebhei ilikuwa na aina ya uimbaji ambao ulikuwa unaendana na Soprano (Msanii wetu Zuchu ana aina hii ya uimbaji na kama angepata waalimu wazuri angefanya makubwa sana sanaaa)

Leo hii tuko Amapiano, tuko Sebene, tuko Nigeria na hatuna muziki wetu kabisa ambao unatutambulisha. Mimi binafsi napenda kila aina muziki mradi tu uone aina ya utaalamu (Sophistication) na ubunifu (creativity) hivyo sipingi uimbaji wa Amapiano, Sebene au Western AfricaAfro-Pop. Lakini ukweli ni kwamba Tanzania ina wasanii wachache sana ambao wanaweza kutoa nyimbo leo ambayo itakuwa kusikilizwa na vizazi vijavyo na kuwafundisha kitu, au hata kutengeneza muziki ambao unaweza kusikilizwa na jamii nyingine duniani na kujifunza kitu.

Leo hii nikiwasikiliza wakina Asa, Burna Boy, Cobhams Asuquo, Omah Lay, Timi Dakollo, Becca Africa, Sarkodie, nabaki nasema Hiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii Baghosha. Inabidi tukaze buti na kufanya jitihada za ziada kukuza muziki wetu, tusiishie kulalamika kwamba ni lini wasanii wetu watatambulika vizuri dunia na kuchukua tuzo kubwa na za heshima kama Grammy.

Ki ukweli wanamuziki wetu wengi kama sio wote ni kama wamebahatisha tu kwa ajili ya maisha magumu kuwa wanamuziki, kwa maana hiyo muziki hawaujui zaidi ya kuganga njaa tu.
 
Nimekua nikiangalia mashabiki wa mziki wa kwetu kwa muda mrefu, kuna wanaosema nchi yetu ina mwanamziki bora Afrika nzima!
Nasikitika lakini sina namna nabaki kushangaa tu.

Afrika Magharibi wanatuzidi ktk sehemu zote iwe ni burudani, elimu,Biashara, utamaduni,uigizaji,michezo,comedy nk!

Youssor N'Dor, salif Keita,Sekouba Bambino,Toumane Diabate, Amadou Balake,Coumba Gawlo,Habib Faye,Jimi Mbaye, Gnonas Pedro,Oumoh Sangare,Thione Sekh,Bonkana Maiga,Mbalou Kante na wengine wengi tu ukiwasikiliza unajua wanajua barabara zao, mziki wao unazungumza sehemu ipi barani Afrika wanatokea.

Mziki umechanganywa na Siasa,tamaduni zao,imani zao,asili zao,uelewa wao,ukomavu wao na uzoefu wao!

West Africa wanafahamika sehemu nyingi zaidi ya dunia, wana tuzo zisizo na idadi, wana vipato vikubwa sana kulinganisha na wa kwetu.

Tanzania tumebarikiwa ujuaji mwingi,kujikweza kwingi,kujiona tunastahili kuheshimiwa kuliko wengine,tunahitaji tuonekane tuna pesa nyingi kuliko tulivyo!

Mfano rahisi ni Youssor N'Dor ana utajiri wa usd 145 milioni, lakini sisi hatuelewi hayo tunataka tutambulike tuko juu ya wote.View attachment 2027940
Hatari sana,baada ya kuona alichokifanya WizKid kule London juzi nikasema sasa basi tenaa...
 
Kuhusu lugha nakataa, miziki ya Congo Zaire iliimbwa Kwa lingala Kwa kiasi kikubwa na ikatamba sana. Nyimbo za kihindi watu wanaziimba na kuzipenda mfano Kuch Kuch hotae bila kuilewa lugha.

Kuna bendi ya mchiriku inaitwa jagwa , jamaa wanagonga shoo tena Kwa Kiswahili mpaka wazungu wanapagawa.
 
Kuhusu lugha nakataa, miziki ya Congo Zaire iliimbwa Kwa lingala Kwa kiasi kikubwa na ikatamba sana. Nyimbo za kihindi watu wanaziimba na kuzipenda mfano Kuch Kuch hotae bila kuilewa lugha.

Kuna bendi ya mchiriku inaitwa jagwa , jamaa wanagonga shoo tena Kwa Kiswahili mpaka wazungu wanapagawa.

Lugha ina sehemu yake ambayo ni kubwa, japo kiukweli muziki wenyewe jinsi ulivyo ni lugha tosha ambayo inajitosheleza. Ndiyo maana nikasema kwamba wale waliosomea pindi wanaposikia muziki hufahamu tu kama huyu msanii ni mtaalamu au mbabaishaji.
 
Kuna hizi band zingefika mbali na kuutangaza mziki wa Tanzani lakini mpaka leo sijui nini sababu ya kupotea,

Kuna The Kilimanjaro band, Tatu nane, Chuchu Sound na nyimbo za Taarabu za mwambao hasa zenye mahadhi ya taratibu zingeendelezwa tungefika mbali na mziki wa asili ya Tanzania.

Nchi zilizofika mbali ki mziki zaidi waliegemea kwenye mziki asili na kuchanganya vionjo vipya!

Ukiangalia km walivyofanya Hugh Masekele na Simon Paul, Mahlathini & Mahotela queens, Soul Brothers,Chicco Twala,Pat Shange,Yvonne Chakachaka,Brenda Fassie, Black Mambazo nk mziki wao ulitembea nchi mbalimbali.

Tanzania hatutaki kujifunza bali tunachukua mziki wowote tuna copy na kuingiza sokoni basi.
 
Nimekua nikiangalia mashabiki wa mziki wa kwetu kwa muda mrefu, kuna wanaosema nchi yetu ina mwanamziki bora Afrika nzima!
Nasikitika lakini sina namna nabaki kushangaa tu.

Afrika Magharibi wanatuzidi ktk sehemu zote iwe ni burudani, elimu,Biashara, utamaduni,uigizaji,michezo,comedy nk!

Youssor N'Dor, salif Keita,Sekouba Bambino,Toumane Diabate, Amadou Balake,Coumba Gawlo,Habib Faye,Jimi Mbaye, Gnonas Pedro,Oumoh Sangare,Thione Sekh,Bonkana Maiga,Mbalou Kante na wengine wengi tu ukiwasikiliza unajua wanajua barabara zao, mziki wao unazungumza sehemu ipi barani Afrika wanatokea.

Mziki umechanganywa na Siasa,tamaduni zao,imani zao,asili zao,uelewa wao,ukomavu wao na uzoefu wao!

West Africa wanafahamika sehemu nyingi zaidi ya dunia, wana tuzo zisizo na idadi, wana vipato vikubwa sana kulinganisha na wa kwetu.

Tanzania tumebarikiwa ujuaji mwingi,kujikweza kwingi,kujiona tunastahili kuheshimiwa kuliko wengine,tunahitaji tuonekane tuna pesa nyingi kuliko tulivyo!

Mfano rahisi ni Youssor N'Dor ana utajiri wa usd 145 milioni, lakini sisi hatuelewi hayo tunataka tutambulike tuko juu ya wote.View attachment 2027940
Lakini pia kumbuka kuwa West Africans waliwahi kupata contact na Europeans. Shule kwao ziliwahi sana, walianza biashara na wazungu kabla yetu, miaka mingi kabla yetu.

Ni kama hapa kwetu, makabila ambayo yaliwahi kupata contact na wazungu yako mbele kielimu na kiuchumi.
 
Kuna hizi band zingefika mbali na kuutangaza mziki wa Tanzani lakini mpaka leo sijui nini sababu ya kupotea,

Kuna The Kilimanjaro band, Tatu nane, Chuchu Sound na nyimbo za Taarabu za mwambao hasa zenye mahadhi ya taratibu zingeendelezwa tungefika mbali na mziki wa asili ya Tanzania.

Nchi zilizofika mbali ki mziki zaidi waliegemea kwenye mziki asili na kuchanganya vionjo vipya!

Ukiangalia km walivyofanya Hugh Masekele na Simon Paul, Mahlathini & Mahotela queens, Soul Brothers,Chicco Twala,Pat Shange,Yvonne Chakachaka,Brenda Fassie, Black Mambazo nk mziki wao ulitembea nchi mbalimbali.

Tanzania hatutaki kujifunza bali tunachukua mziki wowote tuna copy na kuingiza sokoni basi.
Muziki wa Tanzania ulianza kuanguka pale ambapo tulianza kufanya biashara na kujikuta kwamba wanaoendesha muziki ni Media-Kubwa, Promoters, Labels na Managers na siyo msanii na kipaji chake. Hivyo hawa watu wasipoupenda muziki wako au kama wewe hutakubali kuwapa pesa wakunyonye basi huwezi kutoka.

Ndiyo hapa sasa unakutana na watu wakubwa wenye ushawishi kama Ruge Mutahaba, Saidi Fela, Clouds Media, Kiss-Fm ambao kiuhalisia wao hawana vipaji vyovyote vya muziki lakini wanakula, wanalala, wanavaa na kuendesha magari ya gharama kwa kunyonya vipaji vya wenzao. Wao ukiwauliza wanasema ni biashara na wasanii na watanzania bila hata kustuka tunakubali kabisa ni biashara.

Clouds Fm na Ruge Mutahaba wamechangia sana kudorora kwa muziki wa Tanzania, yaani wana sehemu kubwa sana. Kuna wasanii wengi sana, na miziki ya aina nyingi (traditional genres) imepotezwa kwenye ramani. Iko kama Marekani na Uingereza, ambako miaka ya zamani kama 50's, 60's na 70's ilikuwa rahisi sana kwa wasanii kutoka kimuziki.

Ilikuwa ni suala la uhusiano baina ya msanii na kipaji chake pamoja na mtengeneza muziki (Producer), media zilikuwa haziingilii sana. Record Labels kama Motown chini Berry Goldy ndiyo ilisaidia sana muziki wa watu weusi kama Jazz, Soul and Blues kupata mafanikio makubwa sana nchini marekani. Berry Goldy alipigia sana muziki huu debe na kuhakikisha unasikiwa Marekani yote. Motown ndiyo iliwatoa wakina Marvin Gaye, Smokie Robinson, The Jackson 5, Diana Rose na wengine.

Lakini sasa watu walivyoona kwamba muziki unatengeneza pesa ndefu ndiyo mambo yakageuka juu chini, media zikaingilia, siaza za kibaguzi zikaingilia, promoters wakaingialia, lebels zikabadilika na managers wakawa na nguvu kuliko msanii. Hivyo msanii akawa anafanya kama wao wanavyotaka, na vipaji vingi vikaanza kuzimwa.

Ndiyo maana leo hii unabaki unashangaa inakuwaje msanii mkali wa Jazz, Soul na Blues kama Jeniffer Hudson anafunikwa na watu Adele ambao kimsingi ni wazungu. Au msanii mwenye uwezo mkubwa kama Keri Hilson anapotezwa kabisa kwenye ramani kwasababu tu ameshindana na Beyonce, ilhali Keri Hilson ana kipaji sana kuliko Beyonce. Jibu ni rahisi Media zina nguvu kuliko msanii na ndizo zinaongoza mwelekeo mzima wa muziki.

Tanzania nasisi tulikutwa na kitu cha namna hiyo kwamba media zimekuwa na nguvu kuliko msanii. Ukaanza udalali kwamba muziki wa aina fulani fulani ndiyo upigwe, na ili wasanii wapigwe ni lazima kuwe na mkataba wa kulipana baina ya msanii na media. Sasa ukiangalia Tanzania tulikuwa na media kubwa ngapi kipindi hicho, utafahamu jinsi gani muziki wetu uliangushwa.

SOCIAL MEDIA is the best thing to ever happen in Africa, naamini bila mtandao sidhani kama wasanii kama Diamond Platnumz angeweza hata kushinda vita yake dhidi ya Ruge Mutahaba na Clouds Media. Binafsi kuna wasanii wengi ambao niliwafahamu kupitia Kiss-Fm African Beats, lakini kwenye Clouds walikuwa hawapigwi kabisa.

Hili inabidi tulitazame kwa undani, na tulifanyie utafiti mkubwa,.........
 
Kaka asante kwa andiko lako hili zuri sana. Mimi napenda sana muziki, lakini pia napenda kuchimbua muziki. Hoja zako zote nakubaliana nazo humo.

Kwanini sisi tumepigwa gap?

—Kuna sababu za Kihistoria ulizozieleza hapo [utumwa, na uwekezaji wa wazungu maeneo hayo] yalichangia mambo mawili, moja ni ubepari, hii ilichangia Hakimiliki kushamiri mapema sana maeneo hayo [kinyume kabisa na hapa kwetu], pili uwekezaji na biashara kati ya west afrika na ulaya imechangia jambo kubwa sana—WEST AFRICANS DIASPORA. Hili ni gap kubwa sana walilotupiga hawa jamaa. Diaspora ndio inatoa connections ya wanaijeria kuingia huko Ulaya, kupata deals na hatimaye muziki wao kuzidi kupenya mainstream and international.

—Pili, sisi Tanzania hapa hatuna muziki wetu. Hatuna muziki wetu kwa sababu za kijiografia na kihistoria. Muziki wote barani afrika, umetokana na traditional music na kupelekwa mainstream. Ukitazama nchi kama Congo au Nigeria utagundua Aina zao za muziki zimetokana na kabila fulani kuwa kubwa and dominant, kitu ambacho kwetu vilizimwa enzi za Nyerere, mbaya zaidi sera za ujamaa, ziliathiri sana muziki, zilizuia ubunifu, zilididimiza mahusiano ya kimuziki ya Tanzania na Dunia na kubwa zaidi sera za ujamaa zilidumaza sana Diaspora yetu. Hivyo hatua na mazingira ya asili ya kupeleka muziki wetu duniani na mbaya zaidi hakuna juhudi za makusudi zilizofanywa za kupeleka muziki huu duniani kama alivyofanya Mobutu kwa muziki wa Rumba, kiasi cha kufanya matamasha maalumu kwenye Rumble of the jungle fight, kwa kuwaleta hadi kina James brown, ili tu kuutangaza muziki wa Kongo.

Kwa sasa ndio tunaamka, lakini ukitazama, hakuna juhudi zenye mkakati wenye maono ya kuipeleka sanaa yetu katika level hizo. Kila msanii unaona anapambana anavyoweza. Hivyo, sidhani kama kuna siku muziki wetu utakuwa na hadhi yoyote duniani.
 
Kaka asante kwa andiko lako hili zuri sana. Mimi napenda sana muziki, lakini pia napenda kuchimbua muziki. Hoja zako zote nakubaliana nazo humo.

Kwanini sisi tumepigwa gap?

—Kuna sababu za Kihistoria ulizozieleza hapo [utumwa, na uwekezaji wa wazungu maeneo hayo] yalichangia mambo mawili, moja ni ubepari, hii ilichangia Hakimiliki kushamiri mapema sana maeneo hayo [kinyume kabisa na hapa kwetu], pili uwekezaji na biashara kati ya west afrika na ulaya imechangia jambo kubwa sana—WEST AFRICANS DIASPORA. Hili ni gap kubwa sana walilotupiga hawa jamaa. Diaspora ndio inatoa connections ya wanaijeria kuingia huko Ulaya, kupata deals na hatimaye muziki wao kuzidi kupenya mainstream and international.

—Pili, sisi Tanzania hapa hatuna muziki wetu. Hatuna muziki wetu kwa sababu za kijiografia na kihistoria. Muziki wote barani afrika, umetokana na traditional music na kupelekwa mainstream. Ukitazama nchi kama Congo au Nigeria utagundua Aina zao za muziki zimetokana na kabila fulani kuwa kubwa and dominant, kitu ambacho kwetu vilizimwa enzi za Nyerere, mbaya zaidi sera za ujamaa, ziliathiri sana muziki, zilizuia ubunifu, zilididimiza mahusiano ya kimuziki ya Tanzania na Dunia na kubwa zaidi sera za ujamaa zilidumaza sana Diaspora yetu. Hivyo hatua na mazingira ya asili ya kupeleka muziki wetu duniani na mbaya zaidi hakuna juhudi za makusudi zilizofanywa za kupeleka muziki huu duniani kama alivyofanya Mobutu kwa muziki wa Rumba, kiasi cha kufanya matamasha maalumu kwenye Rumble of the jungle fight, kwa kuwaleta hadi kina James brown, ili tu kuutangaza muziki wa Kongo.

Kwa sasa ndio tunaamka, lakini ukitazama, hakuna juhudi zenye mkakati wenye maono ya kuipeleka sanaa yetu katika level hizo. Kila msanii unaona anapambana anavyoweza. Hivyo, sidhani kama kuna siku muziki wetu utakuwa na hadhi yoyote duniani.
Wewe jamaa una akili nyingi sana na zile za ziada, kuanzia leo ntaanza kukufuatilia kwa ukaribu. Hoja zako zote mbili zimebeba hoja zote ambazo tumezichangia kwenye mjadala huu na kuongezea mambo muhimu kama siasa za kijamaa. Kiufupi Mzee Nyerere alileta The Cultural Revolution hapa nchini Tanzania ambapo tamaduni zilionekana kitu kiovu kabisa na mbaya zaidi ujamaa ulikataza kabisa muziki wa nje ya Afrika kupigwa Tanzania, hivyo tasnia iliganda kabisa.

Lakini umeongelea kitu kikubwa sana cha hakimiliki (Intellectual Property Rights), ambapo nchi za wenzetu kimekuwa na nguvu sana huku serikali zikifanya jitihada za ziada kabisa. Tanzania umiliki binafsi wa mali lilikuwa ni jambo haramu na tumetunga The Copyright and Neighbouring Act mwaka 1999, sheria ambayo inasimamia hakimiliki. Hii sheria nayo ina walakini na mpaka sasa hatuna wataalamu wengi wa sheria za hakimiliki nchini Tanzania.

Wasanii wanakwama sana, wananyonywa na kuibiwa bila kupewa stahiki zao (Proper Incentives) ambazo zitatoa motisha kwa sanaa yetu kukua. Hili halipo tu kwenye muziki, hata kwenye mpira lipo, angalia jinsi timu zinavyojiendesha zikijiita za wananchi. Hivi kweli bado watu wanaamini kabisa mpira unaweza kukua kwa namna ambavyo Simba SC na Yanga zimekuwa zikiendeshwa kwa miaka mingi ???

Yaani SIASA ZA UJAMAA zimeleta laana kubwa sana nchini, huwa nashangaa sana kuona watu bado wanakuwa wanazikumbuka na kuzitamani.....
 
Tazama video hii ya Ferre Gola.

Modernization of traditional music. Na hii ndio inafanya muziki wa Kongo, au Afrika Magharibi, uzidi kuwa bidhaa pendwa duniani.
 
Nazidi kupata vitu vipya vya kwa nini tuko nyuma sana?
Ktk thread no 38,39 mmeandika vitu mhimu mno.

Siasa za awamu ya kwanza zimeturudisha nyuma mno ktk mambo mengi.

Sijajua Mw Nyerere aliona utamaduni utamkwamisha vipi ktk kutawala nchi.

Sijui pia mawasiliano na Watanzania waliokua nje ya nchi aliyahofia sababu kwa nia ipi.

Nchi ilifungwa kwenye kila kitu.
Wafanyabiashara walifirisiwa kwa maagizo tu. Na ndio maana makampuni makubwa mengi pia ya kurekodi yalihamishia shughuri zao nchini jirani.ì

Wengi wanamsoma Mwl kwenye maandishi lakini tulioyaishi maisha ya kipindi chake tunajua ni siasa zilizompamba kuliko uhalisia!

Kakwamisha mno Watanzania kujua habari zozote za nje ya nchi kasoro Habari za Uchina zinazohusu ujamaa basi.

Hii ndio imeathiri kila kitu, Watanzania walio wengi ni miaka 20 tu iliyopita ndio wameanza kupata habari na kusafiri nje ya nchi.

Mziki wowote bila utamaduni hauwezi kueleweka umetoka wapi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom