Tuwe wawazi; hivi kimuziki tunaweza kuwafikia watu wa Afrika Magharibi kweli?

MALCOM LUMUMBA

JF-Expert Member
Jul 26, 2012
20,897
63,783
Wazungu husema hivi "Once is an accident, twice is a coincidence and thrice is a pattern

Ule ukanda wa Afrika Magharibi wana kitu cha ziada ambacho nadhani hakionekani lakini kipo tu. Ukifuatilia historia utatambua kwamba watu wenye asili ya ukanda ule ndiyo wanaotawala sehemu kubwa ya tasnia ya burudani hapa duniani, hasahasa muziki. Historia inatuambia wao ndiyo hupeperusha bendera ya muziki wa Afrika tokea vizazi.

Wasanii wakubwa duniani kama Fela Kuti, Youssou N'Dour, Mory Kante, Angelique Kidjo, Salif Keita, Baaba Maal ambao wana mchango mkubwa kwenye muziki Afrika na duniani kote wametokea ule ukanda. Lakini zaidi ya haya, yapo ambayo yananishangaza zaidi. Mosi, baada ya kizazi cha wakina Fela Kuti kuondoka kimezaliwa kizazi kingine kipya ambacho kinaendelea kupeperusha bendera kwa nguvu sana kuliko kile cha kwanza.

Pili, wamegundua vifaa vingi vya muziki ambavyo vinatumiwa sana duniani mfano Akoting limegunduliwa Senegal, Balafon inatumika sana Ghana, Udu limegunduliwa Nigeria, Alagaita imegunduliwa Nigeria, Ngoma ya Djembe imegunduliwa kule Burkina Faso, hata Shekere nazo zimegunduliwa ule ukanda. Kiufupi ukifuatilia sana dhana nyingi za muziki za wabantu zimeanzia kule Afrika Magharibi.

Tatu, hata wale ndugu zao wa karibu ambao waliuzwa utumwani barani Marekani wamekuwa ni ndiyo vinara wakubwa kwenye tasnia nzima ya burudani na michezo. Kama unafuatilia muziki vizuri utatambua kwamba wamarekani weusi wamegundua na kuchangia vipengele (Genres) nyingi za muziki ambazo tunazikiliza leo hii. Muziki wa Jazz (Jazz Music) ndiyo ulizaa Blues, Soul, Rock and Roll, pamoja na Pop ambazo tunazipenda leo. Utafiti wa kisayansi (DNA/ Ancestry Tracing) unasema kwamba wale wasanii wametokea ule ukanda.

Nawapenda sana wasanii wetu kutoka huu ukanda, lakini kila nikifuatilia muziki wao kwa ukaribu halafu nikalinganisha na kile wenzetu wanatengeneza huwa nabaki nawaza sana. Ushawishi wa ukanda wa Magharibi umekuwa mkubwa sana kwenye muziki wa Afrika Mashariki hadi kupelekea sisi kuwaiga wao bila hata kufahamu kwamba tunawaiga, Kuanzia kwenye midundo hadi aina ya uimbaji.

Jambo kubwa ambalo mimi nimefanikiwa kulitambua kidogo ni kwamba sanaa hasa muziki na burudani nyingine ni sehemu za utamaduni wa kila jamii. Hivyo jamii yoyote ambayo hupenda sana utamaduni wake huweza kuwa na muziki wake na hata hufanikiwa sana kuusambaza. Kabla ya mkoloni muziki ulitumika kama sehemu ya ibada, sehemu ya masimulizi na sehemu ya burudani: Hata sasa iko hivi japo muziki ambao huwa tunatumia ni ule wa Magharibi na Mashariki ya Kati.

Baada ya mkoloni kuondoka ni jamii chache za kiafrika zilifanikiwa kutunza yale ya kale na zimekuwa na kitu cha kuionesha dunia ambacho dunia haina. Hivyo dunia ya leo imekuwa tayari kusikiliza na kujifunza kwasababu ni kitu kipya ambacho kimebeba taswira yote ya jamii fulani ambayo ilitengwa hapo mwanzo wakati dunia inaendeshwa na mtu mweupe. Leo hata umsikilize mtu kama Burna Boy au Sarkodie ambao mmoja huimba Afro-Pop na mwingine huimba Hip-Hop lazima utayasikia mahadhi ya muziki wa Afrika Magharibi.

Sisi tulikuwa ni Bakurutu na Taarab ambayo binafsi naamini ilibebe taswira nzima ya utamaduni wetu na ingeendelea kubeba mpaka leo hii kwasababu muziki hukua (Evolves), lakini sijui nini kilitokea hapa katikati muziki ule ukafa. Ukifuatilia wasanii wengi wa Tanzania waliofahamika huko duniani hata kabla ya Diamond Platnumz walikuwa ni wazee wetu wa Bakurutu. Taarab nayo japo wengi tuliikebhei ilikuwa na aina ya uimbaji ambao ulikuwa unaendana na Soprano (Msanii wetu Zuchu ana aina hii ya uimbaji na kama angepata waalimu wazuri angefanya makubwa sana sanaaa)

Leo hii tuko Amapiano, tuko Sebene, tuko Nigeria na hatuna muziki wetu kabisa ambao unatutambulisha. Mimi binafsi napenda kila aina muziki mradi tu uone aina ya utaalamu (Sophistication) na ubunifu (creativity) hivyo sipingi uimbaji wa Amapiano, Sebene au Western AfricaAfro-Pop. Lakini ukweli ni kwamba Tanzania ina wasanii wachache sana ambao wanaweza kutoa nyimbo leo ambayo itakuwa kusikilizwa na vizazi vijavyo na kuwafundisha kitu, au hata kutengeneza muziki ambao unaweza kusikilizwa na jamii nyingine duniani na kujifunza kitu.

Leo hii nikiwasikiliza wakina Asa, Burna Boy, Cobhams Asuquo, Omah Lay, Timi Dakollo, Becca Africa, Sarkodie, nabaki nasema Hiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii Baghosha. Inabidi tukaze buti na kufanya jitihada za ziada kukuza muziki wetu, tusiishie kulalamika kwamba ni lini wasanii wetu watatambulika vizuri dunia na kuchukua tuzo kubwa na za heshima kama Grammy.
 
Ninapenda kusikiliza Jazz na huwa ninasikiliza ya Latin America na Congo. Ukiacha West Africa hata Congo ni wazuri sana kwa muziki.
Latin America na Congo wana aina zao za muziki na zinatambulika kwamba ni sehemu ya tamaduni zao. Kikubwa zaidi ni kwamba muziki wa Afrika husikilizwa sana Marekani lakini hawa wenzetu wanasikilizwa sana hadi barani Ulaya sehemu ambayo ni Culturally Conservative. Mtu kama Papa Wemba na Lokua Kanza ni maarafu sana kule Ubelgiji na Ufaransa na ukisikiliza kazi zao ni lazima ukubali kwamba hawa jamaa hawana mchezo.
 
Sio kimuziki tu hata KIAKILI tumeachwa mbali.

Sisi wazee wa connection; fikiria yule dogo anatoa ndogo Kwa kufurahia kabisa, daah
 
Kumaliza ubishi kuwe na mashindano ya muziki kitaifa na kimataifa kama ilivyo kwa soka, unachaguliwa muziki mmoja kama ule wa msela wa Kinondoni aliyeimbwa na Lady JD simkumbuki jina, kama siyo Halfani basi ayub. Not sure anyway au Malaika nakupenda malaika, halafu bendi zishindane kuuimba kwa vionjo mbalimbali mpaka kugombania ngao au kombe la dunia🦮🐕‍🦺halafu kwa ngazi ya taifa refa awe Kingwangala
 
Sio kimuziki tu hata KIAKILI tumeachwa mbali.
**Sisi wazee wa connection
Hili nalo lina ukweli mkubwa tu, wasomi wanaongozwa kwa kufanyiwa rejea hapa Afrika ni Wanaijeria, Wakenya na Waafrika Kusini. Kama umesoma fasihi (Literature) utakumbuka vitabu vingi tulivyovitumia vilikuwa vimetoka ule ukanda. Wole Soyinka, Chinua Achebe, Ayi Kwei Armah, Danny B. Safo hawa walikuwa ni kizazi hicho, leo hii kuna wakina Chimamanda, yaani kila kizazi lazima watoe mtu wa maana ambaye anazungumzia masuala muhimu ya Afrika.
 
Hili nalo lina ukweli mkubwa tu, wasomi wanaongozwa kwa kufanyiwa rejea hapa Afrika ni Wanaijeria, Wakenya na Waafrika Kusini. Kama umesoma fasihi (Literature) utakumbuka vitabu vingi tulivyovitumia vilikuwa vimetoka ule ukanda.
Sisi tuna wasomi njaa. Yaan mtu ana PhD anakubali post ya U-DC huko Chaka sijui Kaliua, Kakonko hukoo miaka 10 , sawa na darasa la 4 anayejua kusoma na kuandika tu.
 
TANZANIA HAKUNA MZIKI KUNA MAJUNGU
Majigambo ni sehemu ya sehemu muhimu ndani ya tamaduni, utayakuta ndani ya kila jamii. Utofauti unakuja pale katika matumizi ya fasihi na sanaa ya muziki ili kuweza kuyafikisha kwa hadhira. Nadhani hapa ndipo tatizo linapoanza sasa, yaani leo ukisikiliza mziki wa Tanzania unahisi roho kuchafukwa, uchafu ni mwingi sanaa.
 
West Africa wanaibeba Africa kwa mengi ikiwemo hata mpira, walianza kucheza nje kitambo leo sisi ndio kwanza tuna samatta, wachezaji wao huvuna mamilioni kila leo na kurudi kuwekeza kwao, hata kiutajiri wasanii wa west wana mafanikio makubwa ya pesa kuliko wasanii wetu huku east, angalia kwa mfano legendary wetu akina nature, inspector, Dudu baya, Banana, 20 per cent, afande sele hao wote na wengine wengi wako hoi kiuchumi lakini chek legendary wao psuare, 2 face, Dbanj, jmartins, hawa hutowaona wako hoi kiuchumi kamwe.
 
West Africa wanaibeba Africa kwa mengi ikiwemo hata mpira, walianza kucheza nje kitambo leo sisi ndio kwanza tuna samatta, wachezaji wao huvuna mamilioni kila leo na kurudi kuwekeza kwao, hata kiutajiri wasanii wa west wana mafanikio makubwa ya pesa kuliko wasanii wetu huku east, angalia kwa mfano legendary wetu akina nature, inspector, Dudu baya, Banana, 20 per cent, afande sele hao wote na wengine wengi wako hoi kiuchumi lakini chek legendary wao psuare, 2 face, Dbanj, jmartins, hawa hutowaona wako hoi kiuchumi kamwe.
Wanatumia mbinu gani hadi kufika kule atii, maana siku ile nimeona Diamond Platnumz kawekwa kundi moja na Burna Boy na Wiz-Kid ili wagombee tuzo nikasema hiiiiiiiii, hata kama nampenda kijana wetu lakini pale ilikuwa ni ngumu sana kwake. Hata wale wanaharakati wa Twitter niliowana ni wapumbavu tu wasiokuwa na ufahamu na mambo, kiukweli bila hata kampeni Diamond Platnumz alikuwa hatoboi.

Like seriously, unashindanishwa na msanii mwenzako ambaye ameshinda tuzo ya Grammy na walimu wake wakubwa wa muziki ni wakina Femi Kuti na Angelique Kidjo. Aina ya muziki anaofanya yule jamaa mbali na kuburudisha pamoja na utaalamu, unakufanya uyaangalie matatizo ya yanayoikumba jamii ya kinaijeria na Afrika katika mtazamo mwingine.

Wale jamaa sijui wana kitu gani asiee.......
 
Wanatumia mbinu gani hadi kufika kule atii, maana siku ile nimeona Diamond Platnumz kawekwa kundi moja na Burna Boy na Wiz-Kid ili wagombee tuzo nikasema hiiiiiiiii, hata kama nampenda kijana wetu lakini pale ilikuwa ni ngumu sana kwake. Hata wale wanaharakati wa Twitter niliowana ni wapumbavu tu wasiokuwa na ufahamu na mambo, kiukweli bila hata kampeni Diamond Platnumz alikuwa hatoboi.

Like seriously, unashindanishwa na msanii mwenzako ambaye ameshinda tuzo ya Grammy na walimu wake wakubwa wa muziki ni wakina Femi Kuti na Angelique Kidjo. Aina ya muziki anaofanya yule jamaa mbali na kuburudisha pamoja na utaalamu, unakufanya uyaangalie matatizo ya yanayoikumba jamii ya kinaijeria na Afrika katika mtazamo mwingine.

Wale jamaa sijui wana kitu gani asiee.......

Ushaelezea mwanzo kabisa njia ya kimuziki iliyoandaliwa mapema na akina fella kuti na wenzie lakini, wale wa west ni rahisi kufika europe na amerika na walifika kule muda mrefu kuliko sisi, wao kwenda kule utakuta ana ndugu yake Raia wa kule, utakuta baadhi au clubs nyingi wanamiliki watu wenye asili ya west africa sasa kwa namna hii unadhani watakosa kutoboa, hata fursa za kusoma toka zamani wanachangamkia sana na ndio maana utakuta wana hadi wanasheria huko, madaktari, wakufunzi, marubani wengi, na hood ya west wanabebana sana yaani msanii kutoka ghana akiwa US basi watajaa wote anzia cameroon, burkina, guinea, togo, Nigeria na nchi nyingine yaani wana ile kitu inaitwa west support popote walipo
 
Na nchi yoyote duniani unayoijua huwezi kukosa watu wa west africa ni mara chache tena kwa mfano watoto wa kino au magomeni wanaoenda labda hapo south kuuza madawa au matunda matajiri wao ni wa nigeria yaani jamaa ukiacha hustle lakini wana vision sana
 
Siyo kwamba mziki wetu ni mbaya Ila tulikosa ubunifu na kama miaka minne nyuma tulikosa ule muendelezo WA kupiga hatua na yote ni sababu tulikosa watu wengi wanaotambulika kimataifa Nigeria kinachowapa backup ni kuwa na watu wengi wanaotambulika kimataifa na kingine mziki wao unalipa kwaiyo kulipia collabo au kuomba collabo na kuilipia inakuwa raisi kidogo kama unakumbuka kipindi p square wako Moto walikuja apa wengi wakaomba Collab Ila aliyefanikisha ni mmoja AY naye hakuwa na muendelezo WA kutafuta nyingi zaidi na zaidi mziki wetu hauna pesa nyingi na kibaya ata kimataifa wengi hawana uwezo WA kulipia collabo na wasanii wa nje na kingine lugha yetu haina wazungumzaji wengi duniani tukubali tukatae lugha ni platform kubwa sana ya mziki wenu kufika mbali Congo Wana backup ya France na Belgium Africa magharibi kuna backup ya France na uingereza na nchi nyingi zinazozungumza kingereza Latin kuna kihispaniola Kwa madiba kuna kingereza na lugha zao za asili kwaiyo lugha ni platform kubwa snaa ya kutufikisha mbali na si mbaya tulichanganya kiswangish ili kuteka solo la nje diamond alifanya ivyo kwenye Ngoma Ile alifanya na Neyo ilimrusha sana mbali naye akatela kajikuta ata kujaza ukumbi WA watu 400 ni kazi akiwa nchi zaa wenzutu
 
Wazungu husema hivi "Once is an accident, twice is a coincidence and thrice is a pattern

Ule ukanda wa Afrika Magharibi wana kitu cha ziada ambacho nadhani hakionekani lakini kipo tu. Ukifuatilia historia utatambua kwamba watu wenye asili ya ukanda ule ndiyo wanaotawala sehemu kubwa ya tasnia ya burudani hapa duniani, hasahasa muziki. Historia inatuambia wao ndiyo hupeperusha bendera ya muziki wa Afrika tokea vizazi.

Wasanii wakubwa duniani kama Fela Kuti, Youssou N'Dour, Mory Kante, Angelique Kidjo, Salif Keita, Baaba Maal ambao wana mchango mkubwa kwenye muziki Afrika na duniani kote wametokea ule ukanda. Lakini zaidi ya haya, yapo ambayo yananishangaza zaidi. Mosi, baada ya kizazi cha wakina Fela Kuti kuondoka kimezaliwa kizazi kingine kipya ambacho kinaendelea kupeperusha bendera kwa nguvu sana kuliko kile cha kwanza.

Pili, wamegundua vifaa vingi vya muziki ambavyo vinatumiwa sana duniani mfano Akoting limegunduliwa Senegal, Balafon inatumika sana Ghana, Udu limegunduliwa Nigeria, Alagaita imegunduliwa Nigeria, Ngoma ya Djembe imegunduliwa kule Burkina Faso, hata Shekere nazo zimegunduliwa ule ukanda. Kiufupi ukifuatilia sana dhana nyingi za muziki za wabantu zimeanzia kule Afrika Magharibi.

Tatu, hata wale ndugu zao wa karibu ambao waliuzwa utumwani barani Marekani wamekuwa ni ndiyo vinara wakubwa kwenye tasnia nzima ya burudani na michezo. Kama unafuatilia muziki vizuri utatambua kwamba wamarekani weusi wamegundua na kuchangia vipengele (Genres) nyingi za muziki ambazo tunazikiliza leo hii. Muziki wa Jazz (Jazz Music) ndiyo ulizaa Blues, Soul, Rock and Roll, pamoja na Pop ambazo tunazipenda leo. Utafiti wa kisayansi (DNA/ Ancestry Tracing) unasema kwamba wale wasanii wametokea ule ukanda.

Nawapenda sana wasanii wetu kutoka huu ukanda, lakini kila nikifuatilia muziki wao kwa ukaribu halafu nikalinganisha na kile wenzetu wanatengeneza huwa nabaki nawaza sana. Ushawishi wa ukanda wa Magharibi umekuwa mkubwa sana kwenye muziki wa Afrika Mashariki hadi kupelekea sisi kuwaiga wao bila hata kufahamu kwamba tunawaiga, Kuanzia kwenye midundo hadi aina ya uimbaji.

Jambo kubwa ambalo mimi nimefanikiwa kulitambua kidogo ni kwamba sanaa hasa muziki na burudani nyingine ni sehemu za utamaduni wa kila jamii. Hivyo jamii yoyote ambayo hupenda sana utamaduni wake huweza kuwa na muziki wake na hata hufanikiwa sana kuusambaza. Kabla ya mkoloni muziki ulitumika kama sehemu ya ibada, sehemu ya masimulizi na sehemu ya burudani: Hata sasa iko hivi japo muziki ambao huwa tunatumia ni ule wa Magharibi na Mashariki ya Kati.

Baada ya mkoloni kuondoka ni jamii chache za kiafrika zilifanikiwa kutunza yale ya kale na zimekuwa na kitu cha kuionesha dunia ambacho dunia haina. Hivyo dunia ya leo imekuwa tayari kusikiliza na kujifunza kwasababu ni kitu kipya ambacho kimebeba taswira yote ya jamii fulani ambayo ilitengwa hapo mwanzo wakati dunia inaendeshwa na mtu mweupe. Leo hata umsikilize mtu kama Burna Boy au Sarkodie ambao mmoja huimba Afro-Pop na mwingine huimba Hip-Hop lazima utayasikia mahadhi ya muziki wa Afrika Magharibi.

Sisi tulikuwa ni Bakurutu na Taarab ambayo binafsi naamini ilibebe taswira nzima ya utamaduni wetu na ingeendelea kubeba mpaka leo hii kwasababu muziki hukua (Evolves), lakini sijui nini kilitokea hapa katikati muziki ule ukafa. Ukifuatilia wasanii wengi wa Tanzania waliofahamika huko duniani hata kabla ya Diamond Platnumz walikuwa ni wazee wetu wa Bakurutu. Taarab nayo japo wengi tuliikebhei ilikuwa na aina ya uimbaji ambao ulikuwa unaendana na Soprano (Msanii wetu Zuchu ana aina hii ya uimbaji na kama angepata waalimu wazuri angefanya makubwa sana sanaaa)

Leo hii tuko Amapiano, tuko Sebene, tuko Nigeria na hatuna muziki wetu kabisa ambao unatutambulisha. Mimi binafsi napenda kila aina muziki mradi tu uone aina ya utaalamu (Sophistication) na ubunifu (creativity) hivyo sipingi uimbaji wa Amapiano, Sebene au Western AfricaAfro-Pop. Lakini ukweli ni kwamba Tanzania ina wasanii wachache sana ambao wanaweza kutoa nyimbo leo ambayo itakuwa kusikilizwa na vizazi vijavyo na kuwafundisha kitu, au hata kutengeneza muziki ambao unaweza kusikilizwa na jamii nyingine duniani na kujifunza kitu.

Leo hii nikiwasikiliza wakina Asa, Burna Boy, Cobhams Asuquo, Omah Lay, Timi Dakollo, Becca Africa, Sarkodie, nabaki nasema Hiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii Baghosha. Inabidi tukaze buti na kufanya jitihada za ziada kukuza muziki wetu, tusiishie kulalamika kwamba ni lini wasanii wetu watatambulika vizuri dunia na kuchukua tuzo kubwa na za heshima kama Grammy.
Muziki wa Tanzania upo lakini unakosa nguvu kwasababu kadhaa.

Kwanza wasanii wengi ( au niseme wanaofanya Muziki ) wanatokea familia zenye njaa na hivyo watu hawafanyi just muziki, watu wanapambana kivyovyote ilimradi wapate hela.

Kwa maana nyingine sasa hivi watu wanapambana kuingiza chochote mfukoni na siyo kufanya muziki.

Hali hii imechagizwa sana na kukosekana kwa nguvu sawia kwenye muziki pamoja na aina ya tabia ya waswahili kuwa mabingwa wa mihemko na ushabiki.

Mihemko na ushabiki mbaya sana.

Sasa hivi mtu kupanda jukwaani kufanya tamasha siyo lazima awe anajua sana muziki. Inategemea zaidi promotion aliyopewa na wadau husika.

Na hili ni tatizo dunia nzima, ila Tanzania tumrathirika zaidi.
 
Muziki wa Tanzania upo lakini unakosa nguvu kwasababu kadhaa.

Kwanza wasanii wengi ( au niseme wanaofanya Muziki ) wanatokea familia zenye njaa na hivyo watu hawafanyi just muziki, watu wanapambana kivyovyote ilimradi wapate hela.

Kwa maana nyingine sasa hivi watu wanapambana kuingiza chochote mfukoni na siyo kufanya muziki.

Hali hii imechagizwa sana na kukosekana kwa nguvu sawia kwenye muziki pamoja na aina ya tabia ya waswahili kuwa mabingwa wa mihemko na ushabiki.

Mihemko na ushabiki mbaya sana.

Sasa hivi mtu kupanda jukwaani kufanya tamasha siyo lazima awe anajua sana muziki. Inategemea zaidi promotion aliyopewa na wadau husika.

Na hili ni tatizo dunia nzima, ila Tanzania tumrathirika zaidi.
Siyo vizuri kumsema vibaya marehemu, lakini unapozungumzia anguko la muziki nchini Tanzania huwezi kuacha vyombo kama Clouds FM pamoja na ndugu Ruge Mutahaba. Pia siasa imechangia kwa kiwango kikubwa sana kuanguka kwa tasnia ya burudani nchini Tanzania: Nadhani siku inabidi tufanye mjadala mpana kuhusu haya.
 
Siyo kwamba mziki wetu ni mbaya Ila tulikosa ubunifu na kama miaka minne nyuma tulikosa ule muendelezo WA kupiga hatua na yote ni sababu tulikosa watu wengi wanaotambulika kimataifa Nigeria kinachowapa backup ni kuwa na watu wengi wanaotambulika kimataifa na kingine mziki wao unalipa kwaiyo kulipia collabo au kuomba collabo na kuilipia inakuwa raisi kidogo kama unakumbuka kipindi p square wako Moto walikuja apa wengi wakaomba Collab Ila aliyefanikisha ni mmoja AY naye hakuwa na muendelezo WA kutafuta nyingi zaidi na zaidi mziki wetu hauna pesa nyingi na kibaya ata kimataifa wengi hawana uwezo WA kulipia collabo na wasanii wa nje na kingine lugha yetu haina wazungumzaji wengi duniani tukubali tukatae lugha ni platform kubwa sana ya mziki wenu kufika mbali Congo Wana backup ya France na Belgium Africa magharibi kuna backup ya France na uingereza na nchi nyingi zinazozungumza kingereza Latin kuna kihispaniola Kwa madiba kuna kingereza na lugha zao za asili kwaiyo lugha ni platform kubwa snaa ya kutufikisha mbali na si mbaya tulichanganya kiswangish ili kuteka solo la nje diamond alifanya ivyo kwenye Ngoma Ile alifanya na Neyo ilimrusha sana mbali naye akatela kajikuta ata kujaza ukumbi WA watu 400 ni kazi akiwa nchi zaa wenzutu
Kwenye suala la lugha umezungumza jambo lenye ukweli sana, nchi nyingi za West Africa huwa wanaimba kiingereza na kifaransa, lugha ambazo zinazungumzwa sana duniani. Kiufupi wasaniii wote wakubwa barani Afrika ambao wamewahi kushinda tuzo kubwa kama Grammy, aidha wanaimba kiingereza, kifaransa au wanafanya folk-music kama Lady Smith Black Mambazo.
 
AY naye hakuwa na muendelezo WA kutafuta nyingi zaidi na zaidi mziki wetu
kwa upande namsifu Ambwene hakuna mbinafsi kama walivyo hawa wa sasa ukiangalia kollabo nyingine walizopiga hawa wa sasa ni kutokana na connection kutoka kwake na ndio ali-pioneer hizo kolabo kutoka hapo hawa wanaokuja ni wabinafsi, wafitini, wanajikweza halafu hawajui na hawajafika popote zaidi ya kelele za hapa nyumbani
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom