Tuwe wakweli, teuzi hizi za Rais zina walakini

Vyamavingi

JF-Expert Member
Oct 3, 2014
5,745
5,446
Wadau, salaam! Kwa kawaida mimi hutafakari kila jambo linalotokea nchini mwetu.

Wiki iliyopita rais wetu mpendwa JPM alifanya teuzi kwa nafasi za makatibu wakuu, wakuu wa mikoa na wilaya ili kuboresha utendaji wa serikali. Hata hivyo miongoni mwa wateule ni Adam Malima aliyeteuliwa kuwa mkuu wa mkoa wa Mara, na Alexander Mnyeti kuwa mkuu wa mkoa ambao siukumbuki.

Nimewataja hao wawili kwa kuwa Adam Malima alikuwa na kesi ya jina mahakamani kwa tuhuma za kumzuia askari wa jeshi la polisi kutimiza wajibu wake na baada ya uteuzi wake DPP amefuta kesi dhidi yake. Alexander Mnyeti yeye anachunguzwa na PCCB kwa tuhuma za rushwa na kwa kitendo cha DPP kumfutia kesi Malima sidhani kama PCCB wataendelea na uchunguzi dhidi ya Mnyeti.

Mwalimu Nyerere aliwahi kutoa mfano wa mke wa Kaisari kutuhumiwa kusaliti ndoa yake na Kaisari akamwacha. Alipoulizwa sababu za kumwacha mkewe ilihali ilithibitika kuwa tuhuma dhidi yake hazikuthibitishwa; Kaisari alijibu kuwa mke wa Kaisari hapaswi kutuhumiwa.

Hata kama wateule hao wa rais wanatuhumiwa tu, kimaadili na kwa kanuni za utawala bora uteuzi wao haukupaswa kufanyika hadi baada ya vyombo vinavyohusika -PCCB na Mahakama kuwasafisha dhidi ya tuhuma zao.

Ili kujenga utawala wa sheria kama ambavyo serikali ya JPM imekuwa ikisisitiza, ni vema Rais ajiepushe na teuzi za namna hiyo ili kujenga heshima yake binafsi, heshima ya taasisi yake,na heshima ya serikali na vyombo vyake vya dola kwa ujumla.

Vv
 
Pole sana kwa kutojua Mnyeti kawa mkuu wa mkoa gani. Pia kumbuka Nyerere sio msahafu.
Teuzi anazofanya Raisi anafanya kwa mujibu wa sheria. ukisema wateule wa raisi wana tuhuma basi jaribu kufahamu japo kidogo kuwa tuhuma zinazotambulika ni zile zinazotolewa na vyombo husika, vinavyotambulika.

Kama tuhuma zenu mnazifanya kisiasa haziwezi kumzuia raisi kufanya uteuzi. Pia kuwepo kwa kesi mahakamani hakumzui Raisi kifanya uteuzi. Raisi hatakiwi kufanya uteuzi kama anayetaka kumteua katiwa hatiani kwa kosa la jinai, au kuna mashataka yanayomkabili katika tume ya maadili ya viongozi.

Kupeleka taarifa TAKUKURU hakumfanyi mtu kuwa na hatia au kuingia kwenye "tuhuma" itakayokwamisha uteuzi au promotion kwa mujibu wa sheria.
 
Pole sana kwa kutojua Mnyeti kawa mkuu wa mkoa gani. Pia kumbuka Nyerere sio msahafu.
Teuzi anazofanya Raisi anafanya kwa mujibu wa sheria. ukisema wateule wa raisi wana tuhuma basi jaribu kufahamu japo kidogo kuwa tuhuma zinazotambulika ni zile zinazotolewa na vyombo husika, vinavyotambulika.

Kama tuhuma zenu mnazifanya kisiasa haziwezi kumzuia raisi kufanya uteuzi. Pia kuwepo kwa kesi mahakamani hakumzui Raisi kifanya uteuzi. Raisi hatakiwi kufanya uteuzi kama anayetaka kumteua katiwa hatiani kwa kosa la jinai, au kuna mashataka yanayomkabili katika tume ya maadili ya viongozi.

Kupeleka taarifa TAKUKURU hakumfanyi mtu kuwa na hatia au kuingia kwenye "tuhuma" itakayokwamisha uteuzi au promotion kwa mujibu wa sheria.
Your Lordship, sitaki kukujibu maana wewe ni mtaalamu wetu wa sheria. Lakini kidogo tu, your Lordship, Kitwanga alikuwa na kosa gani?
 
Wadau, salaam! Kwa kawaida mimi hutafakari kila jambo linalotokea nchini mwetu.

Wiki iliyopita rais wetu mpendwa JPM alifanya teuzi kwa nafasi za makatibu wakuu, wakuu wa mikoa na wilaya ili kuboresha utendaji wa serikali. Hata hivyo miongoni mwa wateule ni Adam Malima aliyeteuliwa kuwa mkuu wa mkoa wa Mara, na Alexander Mnyeti kuwa mkuu wa mkoa ambao siukumbuki.

Nimewataja hao wawili kwa kuwa Adam Malima alikuwa na kesi ya jina mahakamani kwa tuhuma za kumzuia askari wa jeshi la polisi kutimiza wajibu wake na baada ya uteuzi wake DPP amefuta kesi dhidi yake. Alexander Mnyeti yeye anachunguzwa na PCCB kwa tuhuma za rushwa na kwa kitendo cha DPP kumfutia kesi Malima sidhani kama PCCB wataendelea na uchunguzi dhidi ya Mnyeti.

Mwalimu Nyerere aliwahi kutoa mfano wa mke wa Kaisari kutuhumiwa kusaliti ndoa yake na Kaisari akamwacha. Alipoulizwa sababu za kumwacha mkewe ilihali ilithibitika kuwa tuhuma dhidi yake hazikuthibitishwa; Kaisari alijibu kuwa mke wa Kaisari hapaswi kutuhumiwa.

Hata kama wateule hao wa rais wanatuhumiwa tu, kimaadili na kwa kanuni za utawala bora uteuzi wao haukupaswa kufanyika hadi baada ya vyombo vinavyohusika -PCCB na Mahakama kuwasafisha dhidi ya tuhuma zao.

Ili kujenga utawala wa sheria kama ambavyo serikali ya JPM imekuwa ikisisitiza, ni vema Rais ajiepushe na teuzi za namna hiyo ili kujenga heshima yake binafsi, heshima ya taasisi yake,na heshima ya serikali na vyombo vyake vya dola kwa ujumla.

Vv
Mkubwa anajiona yupo juu ya sheria hata hivyo msameheni kwani gari lishamshinda tunangojea ajali tu.au atajikuta kabaki peke yake
 
Your Lordship, sitaki kukujibu maana wewe ni mtaalamu wetu wa sheria. Lakini kidogo tu, your Lordship, Kitwanga alikuwa na kosa gani?
Kiongozi, Kitwanga alifanya kosa la dhahiri. Alishindwa kuwakilisha hoja ya serikali (kupitia wizara yake) sababu ikiwa ni ulevi wa pombe. Hili ni kosa la kinidhamu mkuu, liko wazi.
 
Kiongozi, Kitwanga alifanya kosa la dhahiri. Alishindwa kuwakilisha hoja ya serikali (kupitia wizara yake) sababu ikiwa ni ulevi wa pombe. Hili ni kosa la kinidhamu mkuu, liko wazi.
Mh, Rafiki yangu mwema, alipimwa? Hapakuwa na ushahidi kama wa Mnyeti kama ulivyosema. Zilikuwa tuhuma tu! Anyway tuyaache.
Your Lordship, naomba uangalie kwenye uzi wa legal doc nina kashida kidgo. Tafadhali.
 
Pole sana kwa kutojua Mnyeti kawa mkuu wa mkoa gani. Pia kumbuka Nyerere sio msahafu.
Teuzi anazofanya Raisi anafanya kwa mujibu wa sheria. ukisema wateule wa raisi wana tuhuma basi jaribu kufahamu japo kidogo kuwa tuhuma zinazotambulika ni zile zinazotolewa na vyombo husika, vinavyotambulika.

Kama tuhuma zenu mnazifanya kisiasa haziwezi kumzuia raisi kufanya uteuzi. Pia kuwepo kwa kesi mahakamani hakumzui Raisi kifanya uteuzi. Raisi hatakiwi kufanya uteuzi kama anayetaka kumteua katiwa hatiani kwa kosa la jinai, au kuna mashataka yanayomkabili katika tume ya maadili ya viongozi.

Kupeleka taarifa TAKUKURU hakumfanyi mtu kuwa na hatia au kuingia kwenye "tuhuma" itakayokwamisha uteuzi au promotion kwa mujibu wa sheria.
Nadhani mahaba uliyonayo yamekufanya hata usielewe content ya mtoa mada, pole sana.
 
Wadau, salaam! Kwa kawaida mimi hutafakari kila jambo linalotokea nchini mwetu.

Wiki iliyopita rais wetu mpendwa JPM alifanya teuzi kwa nafasi za makatibu wakuu, wakuu wa mikoa na wilaya ili kuboresha utendaji wa serikali. Hata hivyo miongoni mwa wateule ni Adam Malima aliyeteuliwa kuwa mkuu wa mkoa wa Mara, na Alexander Mnyeti kuwa mkuu wa mkoa ambao siukumbuki.

Nimewataja hao wawili kwa kuwa Adam Malima alikuwa na kesi ya jina mahakamani kwa tuhuma za kumzuia askari wa jeshi la polisi kutimiza wajibu wake na baada ya uteuzi wake DPP amefuta kesi dhidi yake. Alexander Mnyeti yeye anachunguzwa na PCCB kwa tuhuma za rushwa na kwa kitendo cha DPP kumfutia kesi Malima sidhani kama PCCB wataendelea na uchunguzi dhidi ya Mnyeti.

Mwalimu Nyerere aliwahi kutoa mfano wa mke wa Kaisari kutuhumiwa kusaliti ndoa yake na Kaisari akamwacha. Alipoulizwa sababu za kumwacha mkewe ilihali ilithibitika kuwa tuhuma dhidi yake hazikuthibitishwa; Kaisari alijibu kuwa mke wa Kaisari hapaswi kutuhumiwa.

Hata kama wateule hao wa rais wanatuhumiwa tu, kimaadili na kwa kanuni za utawala bora uteuzi wao haukupaswa kufanyika hadi baada ya vyombo vinavyohusika -PCCB na Mahakama kuwasafisha dhidi ya tuhuma zao.

Ili kujenga utawala wa sheria kama ambavyo serikali ya JPM imekuwa ikisisitiza, ni vema Rais ajiepushe na teuzi za namna hiyo ili kujenga heshima yake binafsi, heshima ya taasisi yake,na heshima ya serikali na vyombo vyake vya dola kwa ujumla.

Vv
Vyamavingi, mengine uwe mpole, Urais ni Taasisi, si Magufuli peke yake anaeamua, japo wengi mtandaoni mnaamini hivyo.
 
Mh, Rafiki yangu mwema, alipimwa? Hapakuwa na ushahidi kama wa Mnyeti kama ulivyosema. Zilikuwa tuhuma tu! Anyway tuyaache.
Your Lordship, naomba uangalie kwenye uzi wa legal doc nina kashida kidgo. Tafadhali.
Hahahaaaa. hakupimwa. Waliomuona ndio walitoa uamuzi.
Ok mkuu, ngoja niingie huko.
 
Pole sana kwa kutojua Mnyeti kawa mkuu wa mkoa gani. Pia kumbuka Nyerere sio msahafu.
Teuzi anazofanya Raisi anafanya kwa mujibu wa sheria. ukisema wateule wa raisi wana tuhuma basi jaribu kufahamu japo kidogo kuwa tuhuma zinazotambulika ni zile zinazotolewa na vyombo husika, vinavyotambulika.

Kama tuhuma zenu mnazifanya kisiasa haziwezi kumzuia raisi kufanya uteuzi. Pia kuwepo kwa kesi mahakamani hakumzui Raisi kifanya uteuzi. Raisi hatakiwi kufanya uteuzi kama anayetaka kumteua katiwa hatiani kwa kosa la jinai, au kuna mashataka yanayomkabili katika tume ya maadili ya viongozi.

Kupeleka taarifa TAKUKURU hakumfanyi mtu kuwa na hatia au kuingia kwenye "tuhuma" itakayokwamisha uteuzi au promotion kwa mujibu wa sheria.
Endelea kuwapa darasa bavicha, wamezidi viherehere na threads kuhusu Magufuli daily.
 
Wapo wanaCCM wengi wasiopendezwa na mwenendo wa uongozi wa Magufuli, tena waliompigia kura kabisa. Kwa hiyo si kila anatekosoa ni wa upinzani.

No one is guilt till proven by the Court!

Nchi haiendeshwi kwa hotuba za Nyerere, hata Yeye alikuwa anatuhumiwa kwa udini Mbona hakukaa pembeni kupisha uchunguzi!
Nyerere alikuwa ni Mwanasiasa na alikuwa na Blaanblaa za Kisiasa sio kila alichokuwa anasema Basi ndio mfanye Sheria au kanuni
 
No one is guilt till proven by the Court!

Nchi haiendeshwi kwa hotuba za Nyerere, hata Yeye alikuwa anatuhumiwa kwa udini Mbona hakukaa pembeni kupisha uchunguzi!
Nyerere alikuwa ni Mwanasiasa na alikuwa na Blaanblaa za Kisiasa sio kila alichokuwa anasema Basi ndio mfanye Sheria au kanuni
Nyerere ni mwanafalsafa, na hiyo ndio nguvu yake kuu. Zaidi ya yote, Nyerere alimtolea mfano Kaisari na kuoanisha sifa za uongozi na jinsi inavyompasa kiongozi kuwa. Kwa taarifa yako tu Warumi ndio walioweka misingi ya elimu ya uongozi, ndio maana leo bado unamsoma Machiavelli aliyeishi karne nyingi zilizopita. Tena ndio maana hata Kanisa Katoliki linafuata utitiri wa hatua za kufuata na kum-study mwanafunzi anayeandaliwa kuwa padri tangu akiwa Seminari ya awali.

BTW nashangazwa sana, I na utetezi kwa hoja dhaifu kama hizo. Nimekuwa very precise kwa uteuzi wa Malima na Mnyeti na sijawagusa wateule wengine kwa sababu hawana tuhuma zozote. Uteuzi uko pale, nguvu na haki za rais kikatiba ziko palepale, rais wetu angeweza kukwepa mtazamo huo kwa kuwateua Malima na Mnyeti baada ya kusafishwa na vyombo husika.

Vv
 
Back
Top Bottom