Tuwe wakweli, tatizo la nchi hii ni Mawaziri au Rais wa nchi?

Tatizo mawaziri wote wanalinda naslai ya chama,bora wafisadi serikalini kuilinda ccm,ndiyo maana fedha zinaliwa wa kuwapigia kelele hayupo zaidi ya kufanya usanii.
 
Tatizo si Rais wala Mawaziri wake isipokuwa ni wananchi wenyewe kuhongwa kipindi cha uchaguzi na kukubali kuchagua viongozi wabovu kwa hiyo sisi ndo wabovu,hatutaki kukataa rushwa
 
Tatizo si Rais wala Mawaziri wake isipokuwa ni wananchi wenyewe kuhongwa kipindi cha uchaguzi na kukubali kuchagua viongozi wabovu kwa hiyo sisi ndo wabovu,hatutaki kukataa rushwa

Inachotakiwa ni kupokea hela yao alafu kwenye kura unawatosa!

Ugumu uko wapi wakati kura ni siri yako??!!

Hata hizo rushwa wanazotoa hawa mafisadi bado ni kodi zetu kwahiyo bora kuipokea na kisha kuwatosa.
 
Tatzo ni udhaifu wa Rais wenu huyu kwa kushndwa kuwawajibisha walioko chini kwa kutotekeleza wajibu wao. Yaani iko hivi,rais achukue rushwa huko juu kwa juu,unadhani huku chini policcm,maafisa wa kutoka halmashauri,tanesco na maafisa wote wa serikali kiujumla unadhani wataogopa kuchukua rushwa? Hapana,kikubwa kinachotakiwa mkuu wa kaya atangulie kuwa msafi ili awe na nguvu ya kuwawajibisha wa chini yake watakao leta upumbu.vu juu yao.
 
Mzigo wote wa matatizo ya kiutawala ya nchi hii anaubeba rais mwenyewe hata makamu rais hahusiki licha ya mawaziri na waziri mkuu. Mfano kama mtu mfano wa Dr Harrison Mwakyembe angekuwa ndiye rais hali ingekuwa tofauti kabisa na ilivyo sasa hivi hata kama baraza la mawaziri ndio hili hili. Let us call a spade a spade.
 
Tatizo la nchi hii ni UDHAIFU wa BUNGE LA JAMUHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA, kama kweli wabunge wangekuwa makini hasa wabunge waliowengi(CCM) nchi hii ingekuwa mbali sana, hebu fikilia ni mra ngapi mawazi(SERIKALI) imetoa taarifa za uongo na bado wabunge wameshindwa kuwawajibisha mawaziri na serikali kwa ujumla, nimalizie kwa mfano wabunge wamwwahi kuomba wapewe majina ya makampuni yaliyopata ruzuku wakati wa msukosuko wa kiuchuma mpaka sasa kwa nninavyofahamu serikali haijatoa majina na BUNGE LIMESHINDWA KUIWAJIBISHA SERIKALI,mpo hapo
 
Kila taarifa ya CAG na ile ya kamati za bunge kuhusu mahesabu ya serikali zinapowasilishwa bungeni ndio mwanzo wa kusema nchii mawaziri akiwemo waziri mkuu ni mizigo na wanapaswa kufukuzwa.

Hata hivyo,mabadiliko yoyote ya serikali hii ya awamu ya nne ni mpaka bunge lishinikize licha ya uozo na uzembe wa watendaji hawa ukiwa ni jambo la wazi kabisa.

Sasa watanzania wenzangu,tukiwa wakweli na tusiwe na hata chembe ya unafiki,hapa tatizo ni mawaziri au Raisi anaewateua?

Labda swalil la msingi ni kuwa ikiwa anaewateua atakuwa muwajibikaji itawezekana mawaziri wawe wazembe?

Naomba maoni yako.

Mi nadhani ni mfumo uliotengenezwa hapo awali wa kuogopana kwa viongozi ndiyo unasababisha watoe maamuzi yasiyo sahihi, ya kuoneana aibu. Ingekuwa kila kiongozi akikosea wote wanakuwa na uwezo wa kumnyooshea kidole ili aachie ngazi, wangekuwa wanafanya kazi kufuata kanuni zinavyosema. Badala yake kila mmoja anaficha ukweli kumlinda mwenzake muovu.
 
Tatizo tunalo sisi kwa kukubali kuhongwa kofia,kanga,10000 na kukubali kuwaweka watu wasiyo na sifa ya uongozi sasa tunalalamika nini tutulie ili tujifunze,kipindi kingine haihitaji kampeni kufunguliwa macho ,tumesha jifunza na tumeelewa,sasa maamuzi kwetu
 
Nadhani si Rais wala Mawaziri wenye matatizo, nadhani system nzima ndiyo yenye matatizo, yaani system yenyewe ndiyo ipo hivyo. Tunachohitaji ni vyama 2 au 3 tu vya siasa.

Ok, kwa hiyo tukiwa na vyama vitatu kama CCM, TLP na UDP Basi matatizo ndio yataisha?
 
Wewe
kama Rais unavyovunja Baraza la Mawaziri mara tatu ndani ya vipindi
viwili unadhihirisha ulivyo dhaifu wewe na serikali yako.
 
Tatizo ni sisi wananchi tumesahau kama tunao uwezo wa kuwajibisha wanasiasa dhaifu kwenye sanduku la kura!

Hao mawaziri wasiotimiza majukumu yao walichaguliwa na wananchi tena kwa kura nyingi. Lakini, uchaguzi ukifika watapita tena licha ya kuwa na rekodi mbaya za uongozi.

Hizi shida tumejitakia wenyewe!
 
Mimi George wa Joseph, nikiwa na akili timamu, naapa ya kwamba yote nitakayoyachangia hapa ni ukweli mtupu: TATIZO LA NCHI YETU LINATOKANA NA SISI WANANCHI NA KATIBA TULIYO NAYO
 
"Mtoto umleavyo ndivyo akuwavyo"(alivyo tulea na kutukuza kwa miaka8,leo tuko kama alivyotaka tuwe yeye)


"Asiye funzwa na babaye,hufunzwa na walimwengu"(baba katususa na sasa tunafunzwa na ulimwengu)

Misemo haidanganyi aise duu
 
Tatizo ni hiki chama chakavu chenye viongozi na wanachama waliochakaa kifikira
 
Kila taarifa ya CAG na ile ya kamati za bunge kuhusu mahesabu ya serikali zinapowasilishwa bungeni ndio mwanzo wa kusema nchii mawaziri akiwemo waziri mkuu ni mizigo na wanapaswa kufukuzwa.

Hata hivyo,mabadiliko yoyote ya serikali hii ya awamu ya nne ni mpaka bunge lishinikize licha ya uozo na uzembe wa watendaji hawa ukiwa ni jambo la wazi kabisa.

Sasa watanzania wenzangu,tukiwa wakweli na tusiwe na hata chembe ya unafiki,hapa tatizo ni mawaziri au Raisi anaewateua?

Labda swalil la msingi ni kuwa ikiwa anaewateua atakuwa muwajibikaji itawezekana mawaziri wawe wazembe?

Naomba maoni yako.


Tatizo si mawaziri au raisi tatizo ni sisi wenyewe wa Afrika. Waa Afrika wote akili zetu zimeinamia upande mmoja. Leo hii hata kama ni wewe ukipata nafasi kama hiyo ya uwaziri hutakua tofauti na hao mawaziri wengine.
Kama walivyo sema wengine hapa Mh Rais kabadilisha mara kadha baraza la mawaziri lakini bado hakuna mabadiliko sasa mnafikiri Mh. Rais atakua na kazi ya kubadilisha baraza kila mwezi??
Ili tuwe na maendeleo inabidi wa TZ wote wabadilike na tuanze kufikiria na kujadili juu ya maendeleo. Na msingi wa maendeleo ya nchi ni wana nchi kuipenda na kuitunza nchi Yao. Sasa leo hii kama rushwa na ufisadi haitaisha basi tutaendelea kuwa maskini milele.
Mna fikiri maendeleo ya ulaya au western countries yamekujaje???
Mawaziri wa TZ utaona ni matajiri kuliko wa ulaya, kila mtu akipata post nzuri lazima ajifikirie mwenyewe kwanza kabla ya nchi yake
 
Ok, kwa hiyo tukiwa na vyama vitatu kama CCM, TLP na UDP Basi matatizo ndio yataisha?

Ndiyo mkuu, mimi naamini vyama vingi vilivyopo sasa kama vitaungana tukapata chama kimoja basi upinzani utakuwa na nguvu zaidi kulinganisha na ilivyo sasa fujo tupu hadi wapo wanaodai hakuna vyama vya siasa isipokuwa wanaharakati tu!
 
Back
Top Bottom