Tuwe wakweli na kuacha upotoshaji: hivi tangu lini watoto wa shule wa kike wakapewa maternity leave?

Dr Akili

JF-Expert Member
Aug 21, 2011
4,953
4,326
1. Tangia tupate uhuru (na hata kabla yake) haijawahi kutokea mtoto wa shule (mwanafunzi) wa kike akipata mimba alipatiwa likizo ya uzazi na kurejea shuleni baada ya likizo hiyo.

2. Ni wanafunzi wa kike wa vyuo vikuu tu pekee ndiyo waliostahili na wanaendelea kustahili likizo hiyo ya uzazi. Hata wanafunzi wa vyuo vingine visivyokuwa vyuo vikuu hawastahili likizo hiyo.

3. Kama ndivyo hivyo, ni upotoshaji mkubwa kwamba ni katika awamu hii tu ya tano chini ya raisi Magufuli ndipo likizo hii ya uzazi ndipo imefutwa. Si kweli hata kidogo kwamba kabla ya awamu hii ya tano wanafunzi hawa walikuwa wanaruhusiwa kurudi shuleni baada ya kujifungua. Kama wapo waliorudi shuleni walifanya hivyo kwa wazazi wao ku forge uhamisho kwenye shule zingine ki ujanja ujanja au kwa njia za rushwa au kuwapeleka shule za binafsi (private schools). Nothing has changed. Sana sana kwa sasa mifumo mibadala ya elimu kwa watu wazima au mtu ye yeyote aliyeikoasa elimu hii ilianzishwa long time ago ambao hata hawa drop outs wanaruhusiwa kujiunga.

4. Katika awamu ya nne chini ya raisi Kikwete ili kudhibiti mimba hizi za utotoni na ongezeko la watoto wa mitaani bunge la JMT lilitunga sheria kali kwa wanaume (ikiwemo wanafunzi wa kiume) wanaowabebesha mimba watoto hawa wa kike wanafunzi na wasio wanafunzi ili mradi tu umri wao uko chini ya miaka 18. Wanaume hawa hufungwa jela kwa miaka 30 chini ya sheria hii. Hivyo adhabu kwa mwanafunzi wa kiume anayembebesha mimba mwanafunzi mwenzake wa kike ni kubwa sana inayoangamiza kabisa ndoto za mtoto huyu wa kiume ukilinganisha na ile ya mtoto wa kike. Tulitegemea hawa wanaharakati pamoja na Zitto wangalipigia kelele mtoto wa kiume (30 yrs jail) badala ya huyu wa kike ambaye aliachwa status quo na sheria hiyo.

5. Mila, maadili, desturi, tamaduni na dini zetu haziwezi hata siku moja kumfurahia mtoto wa kike mwenye umri wa miaka 10 hadi 16 (wa darasa la 4 hadi kidato cha 6) kuruhusu kufanya tendo hilo la ndoa (tena bila kinga) hadi kubeba ujauzito. Hata kutoa mimba hatuwezi kuruhusu. Hata kumiliki simu haturuhusu. Kuwapata maternity leave ndiyo sahau kabisa, haturuhusu. Hata kuwapa dawa za majira (contraceptives) na kugawa condomns kwenye shule zetu haturuhusu.

6. Ni upotoshaji mkubwa Zitto anaposema kwamba ndani hakuna uhuru wa kuzungumza haya. Kila siku yuko twiter, instragram na mitandao ya jamii. Nani kamzuia kuyazungumuza hayo kwenye forum zake hizo pendwa? Zitto kila kukicha anaitisha press conferences. Nani kamzuia kuzungumza hayo kwenye hizo press conferences. Zitto ni mbunge na ni hodari sana kuongea akiwa bungeni. Na bunge ndilo lenye mamlaka ya kutunga sheria pamoja na hiyo sheria anayoitaka yeye ya maternity leave kwa watoto wa shule wa kike! Nani kamzuia kuzungumuza hoja yake hiyo bungeni au kupeleka mswaada binafsi? Anajuwa hoja yake hiyo haitaungwa mkono na walio wengi ambacho ndicho principle ya democrasy - rule of the majority, yeye anataka kulazimisha rule of the minority?

Eti anasema mkopo utabagua watoto wengi sana wa kike! Yaani anathubutu kusema uwongo kwamba watoto wengi sana wa kike walioko mashuleni wanadungwa mimba? Pathetic. Ukweli ni kuwa ni asilimia ndogo sana (less than 1%) na jitihada zinaendelea kuchukuliwa kupunguza idadi hiyo. Hata hizo pesa za WB zingesaidia pia kupunguza idadi hii ya mimba na maambukizi ya UKIMWI kwa watoto wetu hawa wa kike kwa kuwajengea mabweni and so on.
 
Kama haijawahi kutokea haina maana kua ndio sheria kua haitatokea tena.
Kwa kua jambo halijawahi kufanyika haina maana kua ndio halitafanyika tena.

Elimu ni haki ya msingi ya binadamu(basic human right) kama vile maisha, lengo la elimu ni kumuwezesha mtu maarifa ili akabiliane na mazingira yanayomzunguka.

Hakuna sababu yoyote inaweza kumnyima mtu haki yake ya kupata elimu labda tu awe amekataa mwenyewe(kama vile mtu anaweza kukataa haki ya kuishi mwenyewe, akajinyonga ama akajiua), vinginevyo hakuna sababu yoyote inapaswa kumnyima haki yake au kumnyang'anya haki yake ya elimu.

Yaani mtoto kapata mimba badala ya kumsaidia tunamuadhibu kwa kumnyang'anya haki yake ya kupata elimu, yeye atakua mjinga, mwanane pia atakua mjinga, tunaambukiza mtoto na mwanae ujinga. Hili halikubaliki.

Watoto wa miaka 12, 13, 14 kupata mimba sababu tunazijua, wanarubuniwa na kwa kua hawajui mabadiliko ya miili yao wanajikuta wamepata mimba, na wala hawajielewi, tunapaswa kuwasaidia sio kuwakomoa.

Hakuna hoja ya kumnyima mtu elimu kisa kapata mimba, huo ni uhayawani.
 
Tafadhali acha kututanya siye ni wajinga kama wewe!
Haki ya kuishi... Haki ya elimu... Haki ya maisha Bora ni kwa kila mtu... Awe wa kike au wa kiume!!
Hoja ya mtoa mada Iko wazi kwamba suala la maternity leave kwa wanafunzi halijawahi kuwepo na Sheria zilizotungwa na bunge haziruhusu hillo.
Haki inaambatana na wajibu siku zote kama kuna haki haimbatani na wajibu nitashangaa.
Mfano: Huwezi kwenda kusoma chuoni bila ada ukijibasibu Kwamba unahaki Yakupata elimu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama haijawahi kutokea haina maana kua ndio sheria kua haitatokea tena.
Kwa kua jambo halijawahi kufanyika haina maana kua ndio halitafanyika tena.

Elimu ni haki ya msingi ya binadamu(basic human right) kama vile maisha, lengo la elimu ni kumuwezesha mtu maarifa ili akabiliane na mazingira yanayomzunguka.

Hakuna sababu yoyote inaweza kumnyima mtu haki yake ya kupata elimu labda tu awe amekataa mwenyewe(kama vile mtu anaweza kukataa haki ya kuishi mwenyewe, akajinyonga ama akajiua), vinginevyo hakuna sababu yoyote inapaswa kumnyima haki yake au kumnyang'anya haki yake ya elimu.

Yaani mtoto kapata mimba badala ya kumsaidia tunamuadhibu kwa kumnyang'anya haki yake ya kupata elimu, yeye atakua mjinga, mwanane pia atakua mjinga, tunaambukiza mtoto na mwanae ujinga. Hili halikubaliki.

Watoto wa miaka 12, 13, 14 kupata mimba sababu tunazijua, wanarubuniwa na kwa kua hawajui mabadiliko ya miili yao wanajikuta wamepata mimba, na wala hawajielewi, tunapaswa kuwasaidia sio kuwakomoa.

Hakuna hoja ya kumnyima mtu elimu kisa kapata mimba, huo ni uhayawani.
Kwangu mimi naona kuna madhara kuwaacha watoto wajawazito nawanaonyonyesha mashuleni italeta shida kubwa zaidi.
Lakini hawazuiliwi kuendelea na masomo kwenye smile za private baada ya kujifungua

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yaani mtoto kapata mimba badala ya kumsaidia tunamuadhibu kwa kumnyang'anya haki yake ya kupata elimu, yeye atakua mjinga, mwanane pia atakua mjinga, tunaambukiza mtoto na mwanae ujinga. Hili halikubaliki.
Sasa na hako katoto kenzake kakiume kalikompachika mimba (kwa kuigiza mchezo wa baba na mama) mbona tunakafunga jela miaka 30, kanakosa haki yake ya kupata elimu na katatoka kakiwa kazee kasikokuwa na elimu na hata huyo mtoto wa kenyewe hakajui na kenyewe hakamjui!. Nani kati ya hao watoto wa shule waliofanya hilo tendo la kikubwa (kujamiana bila kinga) anastahili kuhurumiwa, wa kike au wa kiume? Mimi niko upande wa hako katoto kakiume. Kama ni sheria tupige kelele kwenye hii ya kuwafunga jela miaka 30 hawa watoto wa kiume. Na ni mara nyingi hivi vitoto vya kike vilivyolelewa visivyo ndivyo huvishawishi hivi vitoto vya kidume.
 
mkuu wapi wanaruhusu mtoto alojifungua akaendelee na shule private? mbna hawatoi uhamisho?
Huko private ni hela yako tu. Hata kama una umri wa miaka 60 watakuchukua tu. Mitihani utaifanya kama private candidate ikibidi othetwise kama school candidate wao.
 
Hoja ya mtoa mada Iko wazi kwamba suala la maternity leave kwa wanafunzi halijawahi kuwepo na Sheria zilizotungwa na bunge haziruhusu hillo.
Haki inaambatana na wajibu siku zote kama kuna haki haimbatani na wajibu nitashangaa.
Mfano: Huwezi kwenda kusoma chuoni bila ada ukijibasibu Kwamba unahaki Yakupata elimu

Sent using Jamii Forums mobile app
Sasa sheria si zinabadilishwa kila kukicha kuendana na matakwa ya wakati huu.

Wekeni fine kubwa au adhabu ila sio kumzuia kuendelea na masomo imagine watoto elfu 5000 wanaacha shule kila mwaka kisa ujauzito!!

Elimu ni basic bora anyimwe ajira ila sio elimu hakuna faida yeyote ya adhabu hii. Kama issue ni maadili kuporomoka lina namna ya kusolve sio kuzuia elimu!!
 
Daaah,ukistaajabu ya "k****a,utayaona ya Dr A***i.
Two wrongs dont make it right.
Tafuta mtu hapo ulipo,akutafsirie maana ya huo msemo.
Sasa na hako katoto kenzake kakiume kalikompachika mimba (kwa kuigiza mchezo wa baba na mama) mbona tunakafunga jela miaka 30, kanakosa haki yake ya kupata elimu na katatoka kakiwa kazee kasikokuwa na elimu na hata huyo mtoto wa kenyewe hakajui na kenyewe hakamjui!. Nani kati ya hao watoto wa shule waliofanya hilo tendo la kikubwa (kujamiana bila kinga) anastahili kuhurumiwa, wa kike au wa kiume? Mimi niko upande wa hako katoto kakiume. Kama ni sheria tupige kelele kwenye hii ya kuwafunga jela miaka 30 hawa watoto wa kiume. Na ni mara nyingi hivi vitoto vya kike vilivyolelewa visivyo ndivyo huvishawishi hivi vitoto vya kidume.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwangu mimi naona kuna madhara kuwaacha watoto wajawazito nawanaonyonyesha mashuleni italeta shida kubwa zaidi.
Lakini hawazuiliwi kuendelea na masomo kwenye smile za private baada ya kujifungua

Sent using Jamii Forums mobile app
Madhara gani?? Mbona huko mitaani watoto ndio wanaona machafu zaidi.... Wanahudhuria vigodoro, wanaskiliza video chafu za bongo fleva, movie za ajabu wanaangalia majumbani then ndio aje kuharibika kisa kaona mwenzie ana mimba??
Tusigeuze shule kama kisiwa, maadili yameharibika kuanzia majumbani unakuta tokea dada kazalia home kabla ya ndoa cjui mama mdogo kazalia nyumbani ssa huyu denti trend gani atafuata??

Matatizo ya mimba hayawi solved kwa kuongeza wasiojua kusoma na kuandika mtaani!!!
 
Namba 6 yako jibu lake lipo hapa
 

Attachments

  • 2274816_1579240845745.png
    2274816_1579240845745.png
    86.7 KB · Views: 1
Daaah,ukistaajabu ya "k****a,utayaona ya Dr A***i.
Two wrongs dont make it right.
Tafuta mtu hapo ulipo,akutafsirie maana ya huo msemo.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mwanangu kua uyaone! Huu msemo unakufaa sana. Subiri katoto kako ka kike utakakozaa katakapobebeshwa mimba kwa ridhaa ya kenyewe na kupachikwa virusi vya hiv, yote haya yakitokana na wewe kukadekeza kwenye kutokalea kwenye maadili yetu ya kitanzania. Hatuwezi kukarudisha kwenye shule kalikopachikiwa mimba kakaeneze virusi hivyo vya hiv na kuwafundisha wenzake tabia hiyo mbaya ya knyewe. Never.
 
Kama haijawahi kutokea haina maana kua ndio sheria kua haitatokea tena.
Kwa kua jambo halijawahi kufanyika haina maana kua ndio halitafanyika tena.

Elimu ni haki ya msingi ya binadamu(basic human right) kama vile maisha, lengo la elimu ni kumuwezesha mtu maarifa ili akabiliane na mazingira yanayomzunguka.

Hakuna sababu yoyote inaweza kumnyima mtu haki yake ya kupata elimu labda tu awe amekataa mwenyewe(kama vile mtu anaweza kukataa haki ya kuishi mwenyewe, akajinyonga ama akajiua), vinginevyo hakuna sababu yoyote inapaswa kumnyima haki yake au kumnyang'anya haki yake ya elimu.

Yaani mtoto kapata mimba badala ya kumsaidia tunamuadhibu kwa kumnyang'anya haki yake ya kupata elimu, yeye atakua mjinga, mwanane pia atakua mjinga, tunaambukiza mtoto na mwanae ujinga. Hili halikubaliki.

Watoto wa miaka 12, 13, 14 kupata mimba sababu tunazijua, wanarubuniwa na kwa kua hawajui mabadiliko ya miili yao wanajikuta wamepata mimba, na wala hawajielewi, tunapaswa kuwasaidia sio kuwakomoa.

Hakuna hoja ya kumnyima mtu elimu kisa kapata mimba, huo ni uhayawani.
Mtoto wa kiume mkampa mimba mwanafunzi wenzake adhabu yake ni kufungwa jela miaka 30 kwa mujibu wa sheria.
Huyu wa kike tusipo mrudisha shule unasema ni haki yake inabidi arudi ili asiharibikiwe maisha yake, je na huyu wa kiume tulie muweka jela miaka 30 wewe mpigania haki unamzungumziaje huyu???
Mana hawa wote wawili ni watoto kwanini haki hii isipiganiwe kwa wote??

Huoni hii sheria inampora mtoto wa kiume hiyo haki ya Elimu unayo isema??
 
Kua uyaone! Subiri katoto kako ka kike utakakozaa katakapobebeshwa mimba kwa ridhaa ya kwake na kupachikwa virusi vya hiv kwa wewe kukadekeza kwenye maadili ya kitanzania. Hatuwezi kukarudisha kwenye shule kalikopachikiwa mimba kakaeneze virusi hivyo vya hiv na kuwafundisha wenzake tabia hiyo mabaya ya kwake. Never.
Kuna watoto wengine wanapewa mimba kwa kubakwa wala sio hiari Yao.
Embu kuwa muelewa ndugu. Halafu fikiria binti yako ndio kafanyiwa hivyo. Acha kuwa myopia
 
Namba 6 yako jibu lake lipo hapa
Hii issue ni ya tangia mwaka 2018. Tangia hapo Zitto Kabwe kafanya mikutano mingi tu ya hadharani katika jimbo lake la Kigoma mjini. Hakuwahi kuthubutu kuliongelea suala hilo kwa wananchi wa jimbo lake maana anajua angekipata cha mtema kuni. Ameenda kuliongea kwa LGBT wenzake.
 
Kuna watoto wengine wanapewa mimba kwa kubakwa wala sio hiari Yao.
Embu kuwa muelewa ndugu. Halafu fikiria binti yako ndio kafanyiwa hivyo. Acha kuwa myopia
Usivutie upande mmoja mkuu hili jambo ni pana mno.
Hivi siku mwanao wa kiume akimpa mimba mwezake je utaunga mkono aende jela miaka 30??
Na kumbuka sheria zote hizi zimekuja kwa lengo la kumlinda mtoto wa kike.

Na ukiiondoa sheria hii ujue kabisa unawaweka hatarini zaidi hawa watoto wa kike Mana hapatakuwa na woga tena, Kama watu wanaenda jela na bado wanafanya je isipo kuwepo hali itakuwaje?? Au je tuendelee kuwapora watoto wa kiume haki yao ya Elimu kwa makosa yao ya kitoto?? mana nao ni watoto ni mihemko tu ya mabadiliko ya mwili Kama ilivyo kwa huyu mtoto wa kike.
Ukiruhusu wenye mimba kurudi shuleni ndio linakuwa jambo la hatari zaidi mana sasa watu wataona kawaida tu, unadhani tunalipeleka wapi hili taifa, siku ukikuta nusu ya wanafunzi wa O level wana mimba, je utashangilia kwamba ulikuwa mwanaharakati ulipigania haki ya watoto wa kike kweli?
 
Back
Top Bottom