Tuwe Wakweli: Kama Wabunge wa CHADEMA wa Viti Maalumu wasingeenda Bungeni ruzuku ingepungua sana chama kingeendeshwaje?

Utaratibu wa viti maalum unapaswa kuwa hivi.

1. Uchaguzi mkuu ukishafanyika, tume ya uchaguzi inatangaza nafasi za viti maalum kulingana na kila chama kilivyopata kura.

2. Chama husika kinafanya mchakato wake wa ndani kupendekeza majina ya wanawake kutoka chama chao. (Kila chama kina utaratibu wake wa ndani kulingana na katiba ya chama husika, na mchakato huo unaweza kuanza hata kabla ya uchaguzi, lakini hauwezi kukamilika mpaka uchaguzi uishe. Kwanini? Huwezi kujua chama kitapata nafasi ngapi kabla ya uchaguzi)

3. Chama husika kinaweka orodha ya majina iliyoyapendekeza kwa umma.

4. Katibu mkuu wa chama husika anawasilisha orodha ya majina yaliyopendekezwa na chama chake kwenda NEC.

5. NEC inaweka wazi kwa umma orodha ya majina ya wanawake waliopendekezwa kupewa hivyo viti maalum.

6. NEC inawasilisha rasmi hiyo orodha kwa spika wa bunge.

7. Spika wa bunge anaweka wazi kwa umma orodha ya majina ya wanawake wa chama husika walioteuliwa kuwa wabunge wa viti maalum.

8. Wabunge walioteuliwa wanaampa ndani ya bunge mbele ya spika siku ya kikao cha bunge.
Chadema walifanya mchakato wa ndani wa kuwapata wagombea wa viti maalumu?

Kwa kawaida huwa wanatumia utaratibu gani?
 
Kwa nini haijalishi wamepatikanaje?Kwani hawawezi kupatikana kwa njia haramu na ambazo ziko nje ya kanuni pamoja na sheria kitu ambacho ni cha kujali?
Kama ni njia haramu zitafanyika ndani ya chama ikiwemo kupeleka mahawara na madada lakini hiyo NEC haiwahusu!
 
Kama ni njia haramu zitafanyika ndani ya chama ikiwemo kupeleka mahawara na madada lakini hiyo NEC haiwahusu!
Unaelewa kuwa sheria inamnyima haki mwenyekiti wa NEC kupokea jina la viti maalum la mtu ambae yupo jela?ilikuwaje NEC wakapokea jina na Nusrat ambae alikuwa jela?
 
Kuna tofauti kati ya kuwa Jela na kuwa mahabusu ( rumande)!
Vyote sheria inakataza.Huwezi kupeleka NEC jina la mtu ambae yupo mahabusu tena mtu huyo ana kesi ambayo haina dhamana.Utakuwa una akili timamu kupeleka jina NEC la mtu ambae yupo mahabusu na ambae kesi yake haina dhamana?
 
Vyote sheria inakataza.Huwezi kupeleka NEC jina la mtu ambae yupo mahabusu tena mtu huyo ana kesi ambayo haina dhamana.Utakuwa una akili timamu kupeleka jina NEC la mtu ambae yupo mahabusu ambae kesi yake haina dhamana?
Katiba ya nchi inasema mtu yoyote atahesabiwa kuwa hana hatia hadi pale mahakama itakapomuhukumu.

Henje alihukumiwa lini?
 
Katiba ya nchi inasema mtu yoyote atahesabiwa kuwa hana hatia hadi pale mahakama itakapomuhukumu.

Henje alihukumiwa lini?
Unachoongea ni sahihi kabisa lakini sheria inakataza kupeleka NEC jina la mtu ambae yupo mahabusu kwa kesi ambayo haina dhamana kwa sababu kwa namna yoyote ile hakuna jinsi mtu huyo anaweza kutoka mahabusu na kwenda kutumikia wananchi bungeni kwa sababu kesi yake haina dhamana.Hiyo ndiyo logic nyuma ya hiyo sheria.
 
Kwanza nawapongeza CHADEMA kwa kuwatendea haki Wanawake wa Tanzania kwa sababu viti vile ni mali yao siyo ya chama.

Pili shughuli za uendeshaji wa chama zinahitaji fedha na wabunge 19 ni mtaji mzuri wa kutunisha mfuko wa ruzuku.

Tatu na mwisho CHADEMA HQ msiwasikilixe hawa makamanda wanaopiga kelele mitandaoni ilhali hawakichangii chama kwa namna yoyote ile na hata mkiitisha maandamano wanajificha nyuma ya kompyuta.

Hongereni chama kikuu cha upinzani.

Maendeleo hayana vyama!
Navyofahamu ruzuku inatolewa kwa idadi ya wabunge wa majimbo. Labda kama kila mbunge viti maalum wakubaliane kutoa mchango kusaidia chama. Ukweli chadema huenda wakawa malofa wa kipato.😂😂
 
Kwanza nawapongeza CHADEMA kwa kuwatendea haki Wanawake wa Tanzania kwa sababu viti vile ni mali yao siyo ya chama.

Pili shughuli za uendeshaji wa chama zinahitaji fedha na wabunge 19 ni mtaji mzuri wa kutunisha mfuko wa ruzuku.

Tatu na mwisho CHADEMA HQ msiwasikilixe hawa makamanda wanaopiga kelele mitandaoni ilhali hawakichangii chama kwa namna yoyote ile na hata mkiitisha maandamano wanajificha nyuma ya kompyuta.

Hongereni chama kikuu cha upinzani.

Maendeleo hayana vyama!
Nawe ukikosa kazi utahamia mitaa ya Kinondoni au Ohio?
 
Kwanza nawapongeza CHADEMA kwa kuwatendea haki Wanawake wa Tanzania kwa sababu viti vile ni mali yao siyo ya chama.

Pili shughuli za uendeshaji wa chama zinahitaji fedha na wabunge 19 ni mtaji mzuri wa kutunisha mfuko wa ruzuku.

Tatu na mwisho CHADEMA HQ msiwasikilixe hawa makamanda wanaopiga kelele mitandaoni ilhali hawakichangii chama kwa namna yoyote ile na hata mkiitisha maandamano wanajificha nyuma ya kompyuta.

Hongereni chama kikuu cha upinzani.

Maendeleo hayana vyama!
Hahaha..yawezekana, Hahahaha ila ukweli wauma sana..
 
Back
Top Bottom