Tuwe makini tunaposafiri na mabasi

kanyela mumo

JF-Expert Member
Jun 16, 2016
2,034
2,106
Eti dereva katoka Dar vizuri kwenda Tanga, kafika Korogwe kwenye chakula, kawapa muda wa kula abiria dakika kumi.

Abiria wote wameenda na muda, kasoro Dereva. Mara katokea na chupa kubwa ya maji ya kilimanjaro.. Jasho jepesi usoni.. Halafu unakuta mtu unamuona na bado unakuwa na amani, kweli kabisa mtu na akili zako unatulia kabisa..

Matokeo yake kaua mwendesha baiskeli na basi kupinduka. Watu watatu hapo hapo.. Wawili hospitalini.. Jumla watano. Majeruhi ndio usiseme.. Duuh!! Kama kweli ni dereva, angemgonga mmoja akaokoa basi, ila bwana Dereva kaangusha basi na mwendesha baiskeli kamgonga.. Duuh Dereva..

N:B Tuwe makini tunapo safiri na mabasi, kuwa huru kwasababu umetoa pesa.. Pesa yako inaisha pindi ukifa tu.
 
Eti dereva katoka Dar vizuri kwenda Tanga, kafika korogwe kwenye chakula, kawapa muda wa kura abiria dakika kumi. Abiria wote wameenda na muda, kasoro Dereva. Mara katokea na chupa kubwa ya maji ya kilimanjaro.. Jasho jepesi usoni.. Harafu unakuta mtu unamuona na bado unakuwa na amani, kweli kabisa mtu na akili zako unatulia kabisa.. Matokeo yake kaua mwendesha baiskeli na basi kupinduka. Watu watatu hapo hapo.. Wawili hospitalini.. Jumla watano. Majerui ndio usiseme.. Duuh!! Kama kweli ni dereva, angemgonga mmoja akaokoa basi, ila bwana Dereva kaangusha basi na mwendesha baiskeli kamgonga.. Duuh Dereva..

N:B Tuwe makini tunapo safiri na mabasi, kuwa huru kwasababu umetoa pesa.. Pesa yako inaisha pindi ukifa tu.

Jamaa anapoint, ila mpangilio na Mtiririko wa Maelezo yake ni ZERO.
 
Hueleweki mkuu, fafanua zaidi kama una GPA ya 3.5 na kuendelea.

kijana hatushiriki kichwa kimoja na wewe hivyo jieleze vizuri!

Jamaa anapoint, ila mpangilio na Mtiririko wa Maelezo yake ni ZERO. Kama Mmoja wao walio fukuzwa UDOM hii Majuzi.

Umeandika kitu gani hii mbona hueleweki
No kuhusiana na hii ajali iliyotokea leo asubuhi mkoani Tanga wilaya ya korogwe
 
kijana hatushiriki kichwa kimoja na wewe hivyo jieleze vizuri!

Ni kweli unachosema kwa sababu always huwa sieleweki hata kwenye life style mkuu.. Soon nategemea kuwa kioo cha jamii hivyo ipo siku tutashare kichwa na wewe kufikia lengo, japo kwa sasa uwezo unao, ila hujaamua kwa sababu hujajua umuhimu wake.. Ntakuwa njia ya Watanzani.. Binafsi ni Nabii wa kwanza Mwaafrika.
 
Naona jamaa kaandika Insha anayoijua mwenyewe badala ya kutoa taarifa ya tukio husika kwa usahihi wake.
 
Naona jamaa kaandika Insha anayoijua mwenyewe badala ya kutoa taarifa ya tukio husika kwa usahihi wake.

Ni kweli ila kuna muda ukifikia levo ya kuelewa sana hasa kwa kuchunguza chochote na kufikia kwa kina lazima usieleweke au uwe mjinga..
 
Back
Top Bottom