IslamTZ
JF-Expert Member
- Nov 22, 2010
- 309
- 182
Mimi ni katika watu waliosikitishwa sana na kesi ya ugadi aliyobambikiwa Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe. Hii inaonesha suala la haki za raia lina mushkili sana. Fikiria kama inaweza kufanyika hivi kwa mtu mkubwa kama Mbowe, vipi hali zetu sisi wa kawaida?
Hata hivyo, wakati tukishinikiza Mbowe aachiwe, nawaomba ndugu zangu tuwakumbuke na wale wengine ambao wapo mahabusu kwa kesi ya ugaidi kwa hadi miaka hadi 10 sasa bila hata kesi kusikilizwa!
Yaani ni kama washahukumiwa kabisa. Afadhali ingeandikwa tu kwenye sheria ya ugaidi kuwa ukikamatwa na tuhuma hizo ndio tayari ushakutwa na makosa, tujue moja.
Hata hivyo, wakati tukishinikiza Mbowe aachiwe, nawaomba ndugu zangu tuwakumbuke na wale wengine ambao wapo mahabusu kwa kesi ya ugaidi kwa hadi miaka hadi 10 sasa bila hata kesi kusikilizwa!
Yaani ni kama washahukumiwa kabisa. Afadhali ingeandikwa tu kwenye sheria ya ugaidi kuwa ukikamatwa na tuhuma hizo ndio tayari ushakutwa na makosa, tujue moja.