Tuwasaidie ushauri wale wenye vipato vya chini, wanaoolewa au kuoa kwa matajiri.

chief swetu

JF-Expert Member
Aug 13, 2015
210
228
Jamani wana-Jf kuna wahanga wakubwa sana wa- kisaikolojia, ambao ni baadhi ya watu wa kipato cha chini sana(mafukara) lakini wamepata bahati ya kupendwa na watoto wa kike/kiume wa matajiri, waliokataa kuingia kwenye mahusiano na watoto wa matajiri kwa kuhofia uwezo wao kiuchumi baadhi yao habari za vitisho wanazo kutoka kwa wazazi wa matajiri.

Lakin pia waliokubali kuingia kwenye mahusiano na hata ndoa baadhi yao familia zmewapokea vyema, lakin wale wenzangu na mm imekua ni mateso, kilio na kusaga meno. Kila unalofanya hata kama jema aisee ni dharau na kebehi mpk unataman kuvunja ndoa.

Hata la kufanya hatulioni. Kwa Wale wahanga wenzangu tupeane maarifa jinsi ya kuishi na hawa watu, kibaya zaidi wale tulioingia nao kwenye mahusiano ndo hawataki kabisa kusikia habari inayoitwa kuachana.
 
Ningekuwa mdada ningeolewa na mtu mwenye hela maana kuna siku walikuja watoto kazini kwangu i.e mke na mume na mtoto wote wana lia, baba analia, mama analia, mtoto analia nikashindwa nimbembeleze nani

BORA AISEHH WADADA MUOLEWE NA WENYE HELA TU
 
Ushauri ni kwamba:

Waoane watu waliopendana na kuridhiana bila kujali hali yao ya kiuchumi.

ILA, mwanamke akimpata mwanaume mwenye pesa na mali halafu ana HEKIMA katika mali zake, huyo mwanamke ana bahati sana na atulie na kumshukuru Mungu siku zote.

Mwanaume kumpata mke mwenye pesa na mali, hata akikupenda vipi bado hutokaa ujiamini completely katika jamii hasa kwa ndugu zake, Pia ipo siku mkeo atadevelop dharau kwako.
 
Mwanaume akiwa mambo safi mke maskini si shida saaan,mana kijamii mwanaume ndo anahudumia mke
Ila the other way round yataka hekima ya juu sana..
Kama mwanamke couple type 2 ukiweza kuikwepa js do so,sio kwa nia mbaya ila inapunguza unnecessary complications hasa kama vipato vimepishana saaaana
 
Back
Top Bottom