Tuwapeni pole CUF kwa msiba

Mtu wa Pwani

JF-Expert Member
Dec 26, 2006
4,184
671
inna lillahi wa inna ilayhi rajiiun, mola ampuzishe kwa amani


Kada muhimu wa CUF Mara afariki

Na Mashaka Baltazar, Musoma

MWANASIASA machachari ambaye pia alikuwa Kamishna wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa tiketi ya CUF, Bw. Julius Masaka (49), amefariki dunia katika hospitali ya mkoa wa Mara, mjini hapa.

Taarifa iliyotolewa jana na mtoto wa marehemu, Bw. Frank Masaka, zilisema Bw. Masaka alifariki dunia juzi muda mfupi baada ya kufanyiwa upasuaji katika chumba cha upasuaji cha hospitali hiyo.

"Baba alipelekwa katika chumba cha upasuaji akiwa anazungumza vizuri na hata jana (juzi) usiku tulizungumza vizuri na hatukuwa na matarajio kuwa angefariki dunia, baada ya kutoka huko alirudi akiwa amenyamaza na ndipo tukashituka kuona hazungumzi," alisema Frank huku akitokwa machozi.

Alisema kabla ya kupelekwa hospitalini Bw. Masaka alitoa maelezo, kwamba alikunywa bia ambayo ilimpa utata katika baa moja mashuhuri ya mjini hapa (jina linahifadhiwa) na kabla ya hapo, alipigiwa simu aliyodai kuwa mpigaji alikuwa akimhitaji hapo, ili wapate kinywaji na kudai huenda iliwekwa sumu.

Ilidaiwa na Frank, kwamba mara baada ya baba yake kuinywa bia hiyo, alianza kusikia tumbo likimuuma na kuomba msaada wa kupelekwa kujisaidia.

Baada ya kutoka kujisaidia, alilala katika baa hiyo kabla ya mkewe kuitwa na kumpeleka hospitalini Oktoba 12 mwaka huu.

Aidha, habari kutoka familia ya marehemu Masaka, zilisema kabla ya mazishi mwili wa marehemu utafanyiwa uchunguzi wa kina, ili kubaini chanzo cha kifo chake. Mganga Mkuu wa Hospitali ya Musoma, Bw. Valentino Bhangi, hakupatikana kuzungumzia kifo hicho.

Marehemu Masaka alizaliwa katika kata ya Bweri mjini hapa na kuhitimu elimu ya msingi shule ya msingi Azimio mwaka 1972, na kuanza siasa na kuwa Katibu wa CCM tawi la Nyasho, ambalo lilikuwa limeunganisha kata tatu za Bweri, Nyakato na Nyasho na baada ya hapo, alikwenda kusoma katika Chuo cha Siasa cha Murutunguru, Ukerewe, Mwanza.

Mwaka 1992 alijiunga na NCCR-Mageuzi, akiwa na wadhifa wa Katibu Kata wa kata ya Nyakato na mwaka 1993 alipandishwa cheo na kuwa Katibu wa NCCR-Mageuzi wa Wilaya ya Musoma Mjini wadhifa alioendelea nao hadi mwaka 1999 alipohamia TLP.

Aliteuliwa kuwa Katibu wa TLP wa Mkoa wa Mara tangu wakati huo hadi mwaka 2003 alipojiengua TLP na kujiunga na CUF na kuteuliwa kuwa mjumbe wa Kamati Tendaji ya Wilaya ya Musoma Mjini.

Marehemu Masaka aliteuliwa kuwa Kamishna wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi mwaka 2004 akiwa Msimamizi Mkuu katika kikao cha CUF kilichofanyika Julai 2004.

source majira
 
Poleni wana cuf na wapigania haki na usawa na kwa watanzania wote kwa ujumla. Mungu ailaze roho ya marehemu pema peponi Ameni
 
napenda kutoa pole kwa familia ya marehemu, viongozi wa cuf, na raia wote wa hiyo sehemu !

Mungu amlaze mahali pema peponi, amina !
 
kulikoni? hivi yawezekana marehemu ameuliwa kwa sumu?


Mwili wa kada wa CUF kuchunguzwa



*Wafuasi waandamana kutaka watakaobainika kumuua wabanwe

Na Mashaka Baltazar, Musoma

MGANGA Mkuu wa Hospitali ya Mkoa wa Mara, Bw. Valentino Bangi, amesema mwili wa marehemu Julius Masaka (49), aliyefariki dunia Jumatatu iliyopita hospitalini hapo utafanyiwa uchunguzi.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, alisema kwa mujibu wa sheria, endapo kuna utata juu ya kifo cha mtu yeyote, utaratibu utafanyika ili kuchunguza.

Bw. Bhangi alisema Jeshi la Polisi mkoani hapa ndilo lenye dhamana hiyo kulingana na malalamiko yanayowafikia kuhusu kifo cha mtu mwenye utata.

"Kwa mujibu wa taratibu zetu za kazi, mwili wa marehemu utafanyiwa uchunguzi wa kina, ili kubaini tatizo na chanzo cha kifo chake, lakini jukumu hilo ni la Polisi, kwani ndio wenye dhamana ya kufanya hivyo baada ya kupata malalamiko kutokana na kifo chenye utata kwa mtu yeyote," alisema Bw. Bhangi

Mwandishi wa habari hii alishuhudia baadhi ya sampuli kutoka mwili wa marehemu vikiwa vimechukuliwa na askari wa upelelezi kwa ajili ya kwenda kufanyia uchunguzi zaidi, walidai kuwa viungo hivyo vya ndani vitapelekwa kwa Mkemia Mkuu.

Awali akizungumzia hali halisi ya kifo cha baba yake, mtoto wa marehemu, Frank, alidai kuwa baba yake alifariki dunia baada ya kufanyiwa upasuaji katika chumba cha upasuaji hospitalini hapo.

Kabla ya kukimbizwa hospitalini, Bw. Masaka alikaririwa akidai alipigiwa simu akiitwa kwenye baa (jina linahifadhiwa) akapate kinywaji aina ya bia na huenda bia hiyo ilikuwa imewekwa sumu na baada ya kuinywa alianza kulalamika maumivu ya tumbo na kuomba msaada wa kupelekwa kujisaidia.

Katika hatua nyingine wanachama wa CUF, jana alasiri waliandamana wakidai kuwa kifo cha kada wao kilipangwa wakidai uchunguzi wa kina ufanywe na kuwatia mbaroni wahusika. Maandamano hayo yalianzia nyumbani kwa marehemu katika kitongoji cha Nyakato.

Waandamanaji hao walipitia katika barabara za Mukendo, Shaaban, Kennedy, Nyerere hadi Iringo ziliko ofisi za chama hicho, kabla ya kurejea nyumbani kwa marehemu, ambapo mazishi yanatarajiwa kufanyika leo saa tano asubuhi.

Marehemu ameacha mjane na watoto wanne na atazikwa katika makaburi ya Wakristo, Nyakato.

source majira
 
Napenda kuungana na waombolezaji wengine wa Msiba huu kuwapa pole Familia ya Marehemu na Chama cha CUF,

Bwana alitoa na Bwana Ametwaa jina la Bwana libarikiwe
 
mungu awape subra wana familia kwenye msiba huu mzito unaotaka kujazwa fikira za utata
 
Ndo njia tutakayopita wote, Bwana ametoa bwana ametwaa jina la bwana libarikiwe!
 
Poleni wana-CUF na watanzania kwa ujumla.Naamini mtayaendeleza mazuri aliyoyaacha marehemu.
Wembe.
 
Hata Baba Yangu Walimuweke Sumu kwenye Pombe Hapo Musoma Wakaamua Mbwaa hao,. Ila aliyeshiriki huo Mpango hakumaliza Mwaka nae Akafariki dunia.. MUSOMA
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom