Tuwaokoe Watanzania China tusisubiri matanga

Suphian Juma

Senior Member
Apr 2, 2019
133
546
NIMEPOKEA UJUMBE WA WANAFUNZI WATANZANIA CHINA, SERIKALI IWATAFAKARI UPYA KABLA HATUJAWAPOTEZA WOTE 400!

Na: Suphian Juma

Pamoja na kwamba Serikali ya Tanzania, kupitia Waziri Mkuu, Majaliwa leo Januari 30, 2020 Bungeni kutoa wito kwamba wanafunzi wanaosoma China walio likizoni kutorudi China kutokana na tafrani ya virusi vya Corona, mimi Suphian Juma nimetaarifiwa na Wanafunzi Watanzania kadhaa kuhusu hali tete wanaoyopitia huko mjini Wuhan.

Kwa kauli ya Waziri Mkuu, Majaliwa nadhani Serikali ya Magufuli imejikita zaidi kuwaokoa wanafunzi walio likizo na imeweka umakini kiasi kwa wanafunzi na Watanzania waishio China hususan katika mji wa Wuhan, na kutoweka umakini wa kutosha kwa Watanzania kiasi cha wao kuhisi kutengwa, na kuona uhai wao kuwa hatarini zaidi ukizingatia huduma za muhimu nako hawazipati ipasavyo kwa mujibu wa ujumbe walionitumia.

Aidha wanasema si kweli China haiwapi ruhusa ya kutoka mjini Wuhan kurudi Tanzania, China wameukubalia Ubalozi wa Tanzania China na Balozi za nchi zingine, kufanya mpango waondoke ila ubalozi wetu umekuwa mzito kuwaruhusu licha ya wao kuwa tayari kujigharamia nauli ya kurudi nyumbani ilmradi waokoe maisha yao.

Kiufupi wanasema wamebaki wanaishi ndani mithili ya wafungwa, wakisongwa na mawazo, wakikosa uhuru wa kutoka nje ya vyuo na makazi yao kwa hofu ya kushambuliwa na virusi hivo hatari vinavyouua kwa muda mchache tu wakikushambulia.

Ufuatao ni ujumbe wa moja ya wanafunzi walionitumia.

Hello kaka Suphian hope mko poa, katika kuwapigania Watanzania.

Nakutaarifu juu ya hali ya Watanzania zaidi ya 400 waishio ndani ya mji wa Wuhan, mji ambao virus vya korona vilianzia.

Hali inatisha na huduma za msingi zinazidi kuzolota, nchi zinazojitambua zinazidi kuwaondoa raia wake huku serikali yetu ikiendelea kuleta siasa tu bila kuchukua hatua.

Siku mbili zilizopita Serikali yetu ilitoa press release kupitia ubalozi wake hapa China kuwa serikali ya China imegoma kutoa ruhusa kwa watu wa Wuhan kuondoka na kama wakitaka kutoka watawekwa kwenye quarantine kwa siku 14 ndo waruhusiwe kuondoka.

Jambo hilo ni uongo kama uongo mwingine wautoao, nchi zingine wakisha-organize usafiri wanatoa taarifa Serikalini ndege yao inaruhusiwa kutua Wuhan watu wanapanda nchi ndo inajua pa kwenda kuwachunguzia, I mean nchi yaweza kututoa huku ikatuweka hata pori la Burigi kwa siku 14 then tukaruhusiwa kwenda makwetu.

Huku vyuoni wanaendelea ku pressurize wanafunzi waombe Balozi zao ziwaondoe eneo la hatari wao wanaendelea kusisitiza Serikali ya China ndo kikwazo.

Huku vyuoni wanaendelea ku pressurize wanafunzi waombe Balozi zao ziwaondoe eneo la hatari wao wanaendelea kusisitiza Serikali ya China ndo kikwazo.

Mwisho wa nukuu.

Binafsi kama Mtanzania ninayejua thamani ya uhai wa kila Mtanzania, na wajibu wangu na haki yangu ya Kikatiba ya kuwasemea na kulinda uhai na UTU wa Watanzania wenzetu popote waliopo, NAITAKA Serikali ya Tanzania chini ya Rais Magufuli IWATAFAKARI UPYA Watanzania wenzetu hawa, ichukue hatua za dharura ikiwemo kuwahamisha Watanzania hawa kutoka kutoka mji athirika na Corona na kuwapeleka pahali salama.

Tiba ni bora zaidi ya Kinga, tusisubiri wafe, tuanze kusema ni mipango ya Mungu wakati ni uzembe wetu.

NB: Nimeambatanisha na email na nakala za barua walizonitumia wanafunzi walizotumiwa kutoka moja ya Chuo wanachosoma China na pia barua kutoka Ubalozi wa Tanzania nchini China.

Suphian Juma,
Afisa Habari, ACT Wazalendo, Tanzania.
Januari 30, 2020.

20200130_190833.jpeg
20200130_190909.jpeg
20200130_191014.jpeg
20200130_191158.jpeg
20200130_191235.jpeg
20200130_191303.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sielewi ni kwa nini baadhi ya taarifa za serikali wakati fulani huwa haziko sahihi. Siasa za kijinga ndiyo mzigo walioubeba waafrika!
 
I doubt kama hilo litashugulikiwa kwa uzito na udharura wake..
Kwa sasa serikali ipo busy inatafakari namna ya kupambana na zzk na wanaharakati waliosababisha WB isitoe mkopo.
 
Ni jambo lililojema kuwarudisha nyumban lakin side effect zake ni zipi? Je wizara inautayari wa kupambana na effects hizo?

Ilitabiriwa kua ugonjwa huu utauwa watu zaid ya milion 33

Sent using Jamii Forums mobile app
 
NIMEPOKEA UJUMBE WA WANAFUNZI WATANZANIA CHINA, SERIKALI IWATAFAKARI UPYA KABLA HATUJAWAPOTEZA WOTE 400!

Na: Suphian Juma

Pamoja na kwamba Serikali ya Tanzania, kupitia Waziri Mkuu, Majaliwa leo Januari 30, 2020 Bungeni kutoa wito kwamba wanafunzi wanaosoma China walio likizoni kutorudi China kutokana na tafrani ya virusi vya Corona, mimi Suphian Juma nimetaarifiwa na Wanafunzi Watanzania kadhaa kuhusu hali tete wanaoyopitia huko mjini Wuhan.

Kwa kauli ya Waziri Mkuu, Majaliwa nadhani Serikali ya Magufuli imejikita zaidi kuwaokoa wanafunzi walio likizo na imeweka umakini kiasi kwa wanafunzi na Watanzania waishio China hususan katika mji wa Wuhan, na kutoweka umakini wa kutosha kwa Watanzania kiasi cha wao kuhisi kutengwa, na kuona uhai wao kuwa hatarini zaidi ukizingatia huduma za muhimu nako hawazipati ipasavyo kwa mujibu wa ujumbe walionitumia.

Aidha wanasema si kweli China haiwapi ruhusa ya kutoka mjini Wuhan kurudi Tanzania, China wameukubalia Ubalozi wa Tanzania China na Balozi za nchi zingine, kufanya mpango waondoke ila ubalozi wetu umekuwa mzito kuwaruhusu licha ya wao kuwa tayari kujigharamia nauli ya kurudi nyumbani ilmradi waokoe maisha yao.

Kiufupi wanasema wamebaki wanaishi ndani mithili ya wafungwa, wakisongwa na mawazo, wakikosa uhuru wa kutoka nje ya vyuo na makazi yao kwa hofu ya kushambuliwa na virusi hivo hatari vinavyouua kwa muda mchache tu wakikushambulia.

Ufuatao ni ujumbe wa moja ya wanafunzi walionitumia.

Hello kaka Suphian hope mko poa, katika kuwapigania Watanzania.

Nakutaarifu juu ya hali ya Watanzania zaidi ya 400 waishio ndani ya mji wa Wuhan, mji ambao virus vya korona vilianzia.

Hali inatisha na huduma za msingi zinazidi kuzolota, nchi zinazojitambua zinazidi kuwaondoa raia wake huku serikali yetu ikiendelea kuleta siasa tu bila kuchukua hatua.

Siku mbili zilizopita Serikali yetu ilitoa press release kupitia ubalozi wake hapa China kuwa serikali ya China imegoma kutoa ruhusa kwa watu wa Wuhan kuondoka na kama wakitaka kutoka watawekwa kwenye quarantine kwa siku 14 ndo waruhusiwe kuondoka.

Jambo hilo ni uongo kama uongo mwingine wautoao, nchi zingine wakisha-organize usafiri wanatoa taarifa Serikalini ndege yao inaruhusiwa kutua Wuhan watu wanapanda nchi ndo inajua pa kwenda kuwachunguzia, I mean nchi yaweza kututoa huku ikatuweka hata pori la Burigi kwa siku 14 then tukaruhusiwa kwenda makwetu.

Huku vyuoni wanaendelea ku pressurize wanafunzi waombe Balozi zao ziwaondoe eneo la hatari wao wanaendelea kusisitiza Serikali ya China ndo kikwazo.

Huku vyuoni wanaendelea ku pressurize wanafunzi waombe Balozi zao ziwaondoe eneo la hatari wao wanaendelea kusisitiza Serikali ya China ndo kikwazo.

Mwisho wa nukuu.

Binafsi kama Mtanzania ninayejua thamani ya uhai wa kila Mtanzania, na wajibu wangu na haki yangu ya Kikatiba ya kuwasemea na kulinda uhai na UTU wa Watanzania wenzetu popote waliopo, NAITAKA Serikali ya Tanzania chini ya Rais Magufuli IWATAFAKARI UPYA Watanzania wenzetu hawa, ichukue hatua za dharura ikiwemo kuwahamisha Watanzania hawa kutoka kutoka mji athirika na Corona na kuwapeleka pahali salama.

Tiba ni bora zaidi ya Kinga, tusisubiri wafe, tuanze kusema ni mipango ya Mungu wakati ni uzembe wetu.

NB: Nimeambatanisha na email na nakala za barua walizonitumia wanafunzi walizotumiwa kutoka moja ya Chuo wanachosoma China na pia barua kutoka Ubalozi wa Tanzania nchini China.

Suphian Juma,
Afisa Habari, ACT Wazalendo, Tanzania.
Januari 30, 2020.

View attachment 1341489View attachment 1341490View attachment 1341493View attachment 1341495View attachment 1341496View attachment 1341497

Sent using Jamii Forums mobile app
Si vema kutafuta umaarufu wa kisiasa katika masuala ya msingi yanayohusu afya za binadamu. Msingi wa Bwana Suphian Juma ni mawasiliano aliyodai ameyapata kutoka kwa mwanafunzi mmoja.

Asichojua ni kwamba Serikali nayo inapokea hourly reports kuhusu hali ya ugonjwa huo kutoka Ubalozi wa Tanzania Nchini China ambao unapata taarifa za mara kwa mara kutoka kwa Mamlaka za Serikali ya China pamoja na kutoka kwa Watanzani waishio Nchini China kupitia Jumuiya ya Wanafunzi watanzania waliopo Wuhan na Timu ya Madaktari watanzania waliopo masomoni Wuhan.

Ukipitia ukurasa wa Twitter @wutasa2018 na Instagram wa Jumuiya ya Wanafunzi ambayo inawakilisha wanafunzi 420 walipo China utapata picha halisi.....wanafunzi wote wapo salama; wanaendelea kufuata masharti yaliyotangazwa na Mamlaka za China ili kujiepusha na ugonjwa huo na wanasubiria kumalizika kwa siku 14 za Quarantine ili waweze kuchukua hatua zitakazofuata ikiwa ni pamoja na kuondoka Wuhan baada ya kuthibitika ni salama kufanya hivyo.

Serikali ya China kupitia Wizara yake ya Mambo ya Nje imeomba nchi zote kutoa ushirikiano kukabiliana na ugonjwa huo na imeeleza wazi hatu ya kwanza na muhimu kabisa ya kukabiliana na ugonjwa huo ni Early Detection & Isolation. Hayo ndiyo yanayofanyika sasa. Ndio msingi wa "lockdown" ya mji wa Wuhan- hakuna ndege; treni wala gari linaloruhusiwa kuingia wala kutoka. Kwa ujumla China imeomba mataifa yote yakubaliane na mpango wao wa kukabiliana na ugonjwa huo - unaojumuisha katika siku 14 watu kuwa isolated. Mataifa machache tu kama Marekani na Japan ndio yamesisitiza lazima yaondoe raia wake na wamekubali masharti ya China. Mataifa mengine kama Ujerumani; Uingereza; Thailand yanafanya tathmini kama yafuate njia ya Marekani. Mataifa mengine yote yaliyobaki ikiwemo Canada; mataifa ya Afrika; Mataifa ya Mashariki ya Kati; Mataifa ya Latin America yamekubaliana na mpango wa China wa kuachana na mawazo ya Evacuation hadi hapo siku 14 zitakapotimia.

Balozi za Mataifa mbalimbali Ya Afrika; Ulaya; Asia yaliyopo nchini China zimetoa press statement kwa wananchi wao zikibeba ujumbe uliotolewa Rasmi na Serikali ya China kwa jumuiya ya kimataifa iliyopo Beijing. Ujumbe huo ndio umetolewa Pia na Ubalozi wa Tanzania Nchini China.

Katika kipindi hiki, sio vema kutafuta political millage bali unahitajika utulivu na kuviacha vyombo vinavyohusika viendelee kufanya kazi zake bila kuwakatisha tamaa.

kwa urahisi wa rejea soma maandiko mbalimbali ya taarifa kwa umma yaliyotolewa na Jumuiya ya Wanafunzi Watanzania waliopo China
 

Attachments

  • EDC7FBA7-663E-4F60-929B-7402D001F42F.jpeg
    EDC7FBA7-663E-4F60-929B-7402D001F42F.jpeg
    80 KB · Views: 1
  • 00FD1A1D-C35F-4338-9C58-E66DB3736D3D.jpeg
    00FD1A1D-C35F-4338-9C58-E66DB3736D3D.jpeg
    28.4 KB · Views: 1
  • AAF0EB86-D812-4B48-8F59-F3E6437ABB32.jpeg
    AAF0EB86-D812-4B48-8F59-F3E6437ABB32.jpeg
    223.6 KB · Views: 1
  • D36A4245-8C87-4783-90D8-FD5971D284F1.jpeg
    D36A4245-8C87-4783-90D8-FD5971D284F1.jpeg
    194.4 KB · Views: 1
Inawezekana mzee baba amesha amua afazali hao watu 400 wafie tuu huko huko kuliko kuhangaika nao kuwaokoa. Hatuna pesa za kuchezea sie bajet yetu ni kununua Ndege tuu.
Maendeleo haya vyama.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni jambo lililojema kuwarudisha nyumban lakin side effect zake ni zipi? Je wizara inautayari wa kupambana na effects hizo?

Ilitabiriwa kua ugonjwa huu utauwa watu zaid ya milion 33

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni muhimu kusoma kwa umakini tamko la WHO lililotolewa leo juu ya hatua za kufanya

 
Back
Top Bottom