Tuwalipishe gharama mafisadi

John Mnyika

JF-Expert Member
Jun 16, 2006
712
1,240
"Lakini tusiishie kuwazomea tu. Hawa ni wahalifu, watu wanaofanya matendo ambayo tayari yanatambulika kama rushwa na ambayo hayakubaliki kisheria kwa sababu ni makosa ya jinai. Pamoja na maelezo yangu kuhusu dhana ya munkari (ukiweza ondoa kwa mkono wako; huwezi kemea usikike; huwezi hata hilo, nuna uonekana umechukia), bado kuwazomea watu wanaotenda makosa ya jinai hakutoshi.

Iko sugu iliyojengeka hivi leo, na sugu hiyo wamejivisha mafisadi wa kila aina nchini kama kinga dhidi ya mashambulizi yote yanayoelekezwa kwao alimradi tu mashambulizi hayo ni ya maneno matupu na wala hayawasababishii maumivu ya kimwili wala hasara ya kifedha.

Wanazisikia shutuma dhidi yao; wanasoma magazeti, au hata kama wameacha kusoma kwa kutotaka kujiona wanavyodhalilishwa, bado wanaambiwa na ndugu zao na maswahiba zao jinsi wanavyoandikwa na kusemwa na kulaaniwa, lakini wao wamekuwa wasadiki wakubwa wa falsafa ya ‘maneno matupu hayavunji mfupa’ au ‘watasema mchana, usiku watalala”. Alimradi hakuna hatua madhubuti za kuwafanya walipe na waumie kutokana na matendo yao hawatakuwa na motisha wa kuyaacha, hasa kama yanawaletea manufaa fulani fulani, na manufaa haya tunayajua.

Dawa mujarrab ya kuwafanya wakome kufanya upuuzi wao ni wa kuwafanya walipe gharama kubwa ili upuuzi wao uwe ghali. Hii ndiyo njia pekee ya kutokomeza utamaduni wa kutoadhibika (impunity) ambao umetawala mwenendo wa siasa katika Tanzania."

Chanzo: http://www.raiamwema.co.tz/07/12/5/4.php
 
John,

Idea nzuri, lakini vitu viwili.

1.Mwanzo naona kama umeanza ghafla, kulikuwa na kitu kabla ya hapo na huu ni muendelezo au ndiyo "fiery oratory" on paper?

2.The strategy is short on specifics, just exactly how will we make them pay?
 
John,

Idea nzuri, lakini vitu viwili.

1.Mwanzo naona kama umeanza ghafla, kulikuwa na kitu kabla ya hapo na huu ni muendelezo au ndiyo "fiery oratory" on paper?

2.The strategy is short on specifics, just exactly how will we make them pay?


Pundit

1. Tazama chanzo, ni makala ya Jenerali Ulimwengu- nimeanzia hapo kwa kuwa ndio kuna kipeo cha makala yenyewe na kitovu cha hoja yake.

2. Ndio maana nimeweka hapa tuijadili- ameibua hoja ya kuwalipisha. Sasa maswali ya kujiuliza na masuala ya kujadili- Je, ni sawa tuwalipishe gharama? Kwa nini? Kama ni sawa; Je, tuwalipishe kwa namna gani? Gharama kiasi gani?

Ujumbe wa Jenerali Ulimwengu ni kwamba tusiishie katika maneno tu, tusiishie tu kutaja mafisadi, tusiishie tu kukwerwa na ufisadi. Tufanye vitendo na moja ya kitendo muhimu ni kuwalipisha gharama mafisadi!

JJ
 
Mnhyika acha kuwa kama ndugu yako wa baba tofauti Mtikila,Just hit the point,Chadema Mnataka nini??tupo tayari kufuata mkakati wenu@ any cost.
 
Of course kama wrongdoing inathibitishwa kuwalipisha ni wajibu. Vitu vifuatavyo vinaweza kuwa points za kuanzia.

1.Wapelekwe katika vyombo vya sheria vilivyo competent na impoartial ili kuondoa uwezekano wa majungu na witchunting.Only once wakikutwa na hatia katika vyombo hivi ndiyo hatua zinazofuatia hapa chini zichukuliwe.Najua tatizo linakuwa ni jinsi gani tunapata an impartial justice system.

2. If guilty at 1 above,of course waachishwe utumishi, kama ni wa umma wapigwe marufuku kushiriki katika uongozi wa vyombo vya umma. Wafungwe accordingly.



3. Wlipishwe gharama walizolitia taifa au fedha walizokwiba. Kama Waziri katoa msamaha wa kodi ya shillingi bilioni 4 ukapitishwa na cabinet, cabinet ichukue collective responsibility na kulipa, ama sivyo mali zao zitaifishwe kufidia.This way watakuwa makini zaidi katika kufanya maamuzi.Kuna mzee mmoja ana busara sana alikuwa anafanya kazi ya mamlaka, watu wa chini yake wakawa wanaomba mihela mingi kifujaji thinking kwamba mzee atatoa kwa sababu si mali ya umma, mzee akawauliza "Hivi kweli hii ingekuwa kampuni ya baba yako ungetumia fedha hizi jinsi hii" ilibidi mafisadi wakae kimya.People must take ownership of their decisions.

4.Kama mapato yanayolipwa pamoja na ya kutaifisha mali hayatafikia kiwango cha hujuma, mtoa rushwa naye alipishwe kilichobaki.

Tunahitaji kuondoa mianya ya ufisadi.Kwa mujibu wa sheria za kiungumtu za miosamaha ya kodi kwa mfano, inakuwa vigumu kumshitaki waziri kwa kusamehe kodi kwa sababu hakuna a clearly defined criteria ya wapi msamaha utolewe.
 
Mafisadi, Guilty? Undoubtedly!

How do you then proceed??? That's where the real challenge is. Kulipishwa gharama, fidia, hasara, riba and what not, ni matokeo, na everyone knows this. How do we make the judicial system work with full authority (without the influence of the fisadi's)? How do we do this? Mpaka sasa tunaonekana kushindwa.

I wonder, What does it take for a country kwenda Mahakama kuu ya Dunia? Kwanini tusiende Mahakama kuu ya Dunia? Tutakuwa tuna-execrise our right being a member state, maybe tukiomba advisory opinions, serikali yetu itaona tuko serious!
 
Tuchukua stance ya china, baada ya kulipa/kufilisiwa, mafisadi kupigwa risasi au kunyongwa hadi kufa, ili wafutike kabisa,maana hao wamelaaniwa.
 
I believe at this moment we can not afford to make them pay anything, what we learned is to pressurize central government to conduct judiciary review.

We need new laws and regulations, we need to educate our citizen concern effects of corruptions. We need to work hard to build our national with solidarity and strength to every aspects.

You politician need to change the whole Tanzania political spectrum by quit pointing finger and start take actions. It is time to focus more in our community, and stop wining. CHADEMA and many other political parties needs to start working with our village communities and build more schools, educate our children's about HIV/Health-care, we need to bring hopes to our children's and not hatred.

To help cleaning environments does not need good or bad government, it surely needs people. You as politician you need to be a model figure. Together we can change our country. God Bless Tanzania
 
Mijadala ya enzi hizi ilikuwa mifupi ...kufikisha replies 100 ni shughuli.lakini comments zilikuwa zina thamani sana.
 
Tulipendekeza (JJ) tuwalipishe enzi hizo.
Yupo jamaa ameanza kudeal nao ili walau sheria ichukue mkondo wake pasipo uonevu.
Wale waliotupendekezea adhabu kwa mafisadi ninawashangaa wanawatetea as if hawakutuibia.
JJ na timu yako hebu sasa semeni mnataka nini?
 
Tulipendekeza (JJ) tuwalipishe enzi hizo.
Yupo jamaa ameanza kudeal nao ili walau sheria ichukue mkondo wake pasipo uonevu.
Wale waliotupendekezea adhabu kwa mafisadi ninawashangaa wanawatetea as if hawakutuibia.
JJ na timu yako hebu sasa semeni mnataka nini?
Yaani haileweki wanachokihitaji hawa jamaa.
Kilichobaki CCM iwaletee maendeleo wananchi na kuwaacha hawa jamaa wakiwa wanaharakati.
 

Similar Discussions

2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom