Tuwakatae wanasiasa watawala wanaochochea udini - JF shujaa

Hawa viongozi waliopo CCM ndio waliokuwa na chama tangu enzi za TANU na kuundwa kwa CCM 1977 na wametawala taifa mpaka leo hii. Inamaana CCM wanajua kama kuna watu waliodhulumi au kunyanyaswa na wanawajibu wa kujibu hilo kwani hakuna watu wengine waliowahi kutawala TZ zaidi yao. Huwezi kutoa malalamiko ambayo hujui unayemlalamikia ni nani, kama ni serikali basi waliotawala miaka ya nyuma na wanaotawala sasa wapo waulizwe wajibu hoja na siyo watu wanalalamikia rai wenzao huko wakiogopa kuigusa serikali ambayo ndio mhusika mkuu. Bahati nzuri raisi anayetawala alikuwa kiongozi ndani ya CCM tangu miaka ya sabini hivyo kama kunadhuluma anazijua then aziweke wazi kwa mamlaka aliyonayo ili kila raia ajue na aliye dhulumiwa apewe haki yake. Sioni sababu ya kulalamika huku unaogopa kupambana na aliyekudhulumu kama serikali ipo , CCM ipo na sehemu ya waliotawala tangu uhuru wapo waulizeni hao na siyo kuwasumbua raia wasiojua hata mnacholalamikia ni nini. Kulalamikia raia wa kawaida kuhusu dhuluma ya watawala haiwezi kusaidi chochote wewe pambana na watawala waliokudhulumu kama unogopa kupambana nao kwa sababu ni wenzako basi ni bora ukae kimya.

Vumbi,

Naomba nikuulize mwaka 1995 kwenda chini ni nani aliyekuwa madarakani? CCM ilikuwa inatambulika kama Chama gani? Chama kama chama hakiwezi kuwa na tatizo kwasababu ndani ya chama wapo watu wabovu na wazuri. Hivyo kulaumu chama ukaacha washirika wakuu ni kama vile unalaumu nyumba wakati mjenzi ndie anayekaa humo ndani. CCM walikuwapo wazuri na watu wabaya hivyo basi wa kulaumiwa ni wahusika wakianza na baba yetu wa Taifa.
 
mkuu..hilo ulilodokeza kwenye red halina tatizo kwangu...tena ni jema ili kuwe na balance of nature...tuendelee kuishi kwa upendo...lakini hawa hawa watawala ambao wanitumia dini kama advantage ya wao kukaa madarakani na ku avoid opposition kwenye manifest na policies za chama chao hakuna hili... je wanaotumika kama shield wananufaika na nini.. sisiem ituonyeshe ilipanga kuwanufaisha vipi waislam kama under privillaged...kuwapa special boost katika education na ku reform education system zao.... hizi ni very cheap programs and awareness campaigns ....haihitaji nguvu ya serikali...lakini inahitaji sera husika. ambalo ndio ukweli wenyewe

Nkuunga mkono reform in education, welfare, jobs ni amongst the measures zinaweza kuchukuliwa kulifukia hilo tatizo. Nimetoa mfano South Africa watu weusi walikuwa wakilalama we kukawa na program inaitwa Black empowerment imefanya kazi vizuri sasa watu weusi wamekaa kimya maana sasa wamegundua tatizo sio wazungu bali wao wenyewe. Sasa ni vema kukawa na program kama hiyo Tanzania kutoa nafasi kwa waislamu wakiboronga tena hapo watakaa kimya wenyewe na mambo yataendelea mazuri.
 
Ukristo na uislamu kama nilivyowahi kusema huko nyuma hauna tatizo kabisa kwani dini zote zimeleta habari njema.

Tatizo liko kwenye uisraeli au uyahudi na uarabu.
Mataifa haya hajawahi kupatana hata kabla ya ukristo na uislamu.

Ambao wana elimu duni wamerithi dini na utaifa.
 
Nkuunga mkono reform in education, welfare, jobs ni amongst the measures zinaweza kuchukuliwa kulifukia hilo tatizo. Nimetoa mfano South Africa watu weusi walikuwa wakilalama we kukawa na program inaitwa Black empowerment imefanya kazi vizuri sasa watu weusi wamekaa kimya maana sasa wamegundua tatizo sio wazungu bali wao wenyewe. Sasa ni vema kukawa na program kama hiyo Tanzania kutoa nafasi kwa waislamu wakiboronga tena hapo watakaa kimya wenyewe na mambo yataendelea mazuri.

great.... black empowerment was a great balancing tool applied by ANC manifest...but it was then otherwise directed to ANC bigshots like Tokyo Sexkwale and forgot the majority poor south africans... that's why there were a growing incidents of Xenophobia

back to TZ unayozungunza yanawezekana asilimia 100% lakini viongozi wetu watawala hawataki kuzumzia hizli wala kutekeleza kwani hawana nia dhabiti ya kuwasaidia under privileged including muslims
 
Ndugu topical angalia wakristo wanavyojenga makanisa kwa kasi na kuyatumia. Ofisini kwangu kuna waislamu zaidi ya 80 lakini nimechunguza na kugundua kuwa wanaoenda kusali ijumaa hawazidi watano.
Kabla hujaanza kushabikia udini kwanza hamasisha waislamu kusali. Dini ni uhusiano wa mtu na mungu wake.
Huwezi kumwajiri mkristo kwa ukristo wake mbali vigezo. Angalia ufaulu wa mitihani ya kidato cha nne uone katika kumi bora waislamu wangapi na wakristo wangapi. Pia ajira inatolewa kwa vigezo vya kufaulu interview siyo udini.
 
Back
Top Bottom