Tuwahurumie Graduates, Hakuna Mwanasiasa wa kuwatetea Vijana waliomaliza Chuo

Endelea kumezeshwa ujinga kwenye vikao vya uvccm
Hivi unakubali serikali yetu iendelee kuukwepa wajibu wake kwa kutokutoa ajira au kutengeneza ajira?
Waache kuwasomesha ili waanze kujiajiri mapema.
Wapi duniani wasomi wote wameajiriwa fikiri nje
 
That is real situation

Hili ni tatizo kubwa sana kwa vijana wa sasa, Vijana ukiwapa kazi hata ndani ya Chama hawataki neno kutembelea vijijini ila ukisema kuna Safari ya China kila wakati utasikia Boss Pole na kazi

Sio Self Praise huu ndio uhalisia

Kama una vijana wamemaliza chuo au ndugu zako nita ku PM uniletee waje wajitolee kwa miezi mitatu tu, Wengi tumewajaribu lakini wavivu sana sana, Pesa wanataka kujifunza hawataki
Mkuu naomba nafasi y kujitolea
 
Utamwoneaje huruma kijana asiyejitambua?.
Vijana wengi ni mandezi waache waumie.
Hata kuandika barua ya maombi ya kazi hawajui, CV wanaandikiwa stationary, na yule wa stationary anazijaza tu walizoweka watu.
Aibu sana
Dunia ya sasa haina huruma ni lazima mtu aumize kichwa ili mkono uende kinywani. Vijana huku Arusha wanatengeneza pesa nyingi kwa masuala ya utalii. Unakuta mtu anaanza kama guide anayewapeleka wazungu mbungani na taratibu anaanzisha kampuni yake ya utalii na anatoka mazima.

Uvumilivu, kujitambua, kuwa na mtazamo chanya wenye kukaribisha watu, ni baadhi tu ya vitu ambavyo vijana wanatakiwa wawe navyo siku zote.
 
Back
Top Bottom