Tuwafahamu Watu Maarufu waliokuwa wanatajwa sana na Wanamuziki wa Band nchini Tanzania

pedeshee kifaranga toto ya kuku, pedeshee diamond totoo ya bisandra pedeshee konde baby ya kajala, haya ongezeeni....
Hahah hakuna petdeshee za hivyo mkuu kipindi hiko wenye petdeshee yao mkiwa live band akitajwa jina kule mbele toka anatoka alikokaa mpaka anafika stejin katikati hapo anaowajua wote washalamba ten ten wewe kazi yako mtaje jina tu anajua huyu mwana unakoga hela.

Jamaa walikuwa na maisha flani classic sana amtake demu wako amkatae?umempa nini wewe huyo mwanamke?
 
Kuna pedeshee mmoja alimtwanga mtu risasi mitaa ya Magomeni usalama kwa anaekumbuka alikua ni pedeshee yupi?
Ni Papaa Msofe na marehemu alikuwa muuza madini!

Ila Msofe yeye alikuwa hana mambo ya bunduki alijichanganya kwa Mchagha Masawe Alex akanunua nyumba iliyokuwa dhamana ya mkopo kati ya marehemu na Masawe so Mchagha alivyopokea hela akavunja uwa akaenda South huku nyuma Msofe akamtaka mmiliki wa awali ahame achukue nyumba yake jamaa akagoma akataka kupeleka kesi mahakamani Masawe kusikia hivyo na kuogopa kuambiwa arudishe hela akarudi akatuma kikosi kazi kikammaliza jamaa ilikuwa mapema tu saa 19:50 usiku.

Msofe aliunganishwa kwenye kesi kutokana na simu ya marehemu kukutwa na chatting kutoka # yake zilizoonyesha kutofautiana na jamaa muda mfupi kabla ya kifo chake.
 
Hawa walianza ujanja tu toka zamani
Alipotoka bukoba alipokelewa na ndg
Yake,akamuwekaga kwenye duka la dawa kino studio
Alijua mambo ya mjinimjini
Msofe naye wote walianzia salamander mjini...mambo ya mihuri,pport etc
Huko ndiko walijua michongo mingine
Kwa mtoto wa mjini zamani lazima uende salamander,azam kutega ujue na kupata a,b,c,d
Nashanga sahv mtoto wa mjini anaonekana na kutambulika
Kisa anaenda kidimbwi
Mtoto wa mjini maana yake huko mjini
Unakutana na watu,viongozi wanakupata connection au wanakupa mchongo kwa kukutumia wewwe nk
Siku mtu kwenda Juliana kidimbwi
Anaonekana umjini

Ova
Aisee..
Umenikumbusha zamani sana, ilikuwa wazee wote wa mishen town wako Salamander na Empress cinema....mara Mzee Michuzi anapita na kamera yake
 
Umenikumbusha late 90s nimemaliza O-Level, nipo home idol nasubiri majibu yatoke. mshua akanitafutia temporary job mitaa ya mjini posta kwenye ofisi ya rafiki yake.

Ofisi ilikuwa mtaa wa jamhuri jirani na ile round about ambayo inakutanisha india street na mkwepu street, almaarufu mitaa ya azam take away.

Ilikuwa kila ikifika mida ya saa tatu mpaka saa nne asubuhi, lile eneo walikuwa wanatokea mabroo smart kwelikweli kimuonekano. mkononi wamebeba vi-diary.

Walikuwa wanavaa mashati nadhifu, surauli za kadeti na viatu safi vya ngozi. kwa ujumla walikuwa wanapendeza sana, mimi mwenyewe nilikuwa nawa admire.

Siku moja nikamuuliza broo mmoja ambaye tulikuwa tunafanya kazi pale, kwamba hawa jamaa ni akina nani,mbona mda mwingi wanautumia kakaa kwenye vijiwe vya shoe shiners, hawana kazi ya kufanya?.

Akanijibu ukisikia mission town ndio hao, na hapo kwenye vijiwe vya shoeshiners ndio sehemu zao za kupanga mipango na kupeana deals mbalimbali.

Akaniambia kile kipande chote cha mtaa wa mkwepu kinachokatiza club ya billicanas mpaka kule kwenye maungio ya samora avenue, ni territory ya ma-mission town.

Hata papaa msofe alianza kujifunzia upigaji mitaa hiyo.
Duuh..
Yaani kama najikumbuka nimemaliza O level miaka ile, naeda kuegesha kwa mshikaji mitaa ya Samora, karibu na R.I.P Mzee wa Pazi basketball alikuwa na Clearing/Forward kawapa wachezaji wote dili za mishemishe za bandarini , nilikuwa nikipita sana mitaa ya Salamander.
 
Papa msofe alikuwa sana salamander samora,alianzaga enzi zile za bandika
Bandua port
Hi michezo vijana wengi enzi zile walifanya na connection zote zilikuwa zinatoka kwa wafanyakazi wa hizo taasisi..kama tra,uhamiaji,ttcl nk
Wao ndy walikuwa wanawaletea watoto wa mjini wafanye alafu wao wanakula mgao....wao

Ova
Sio Mchezo..
Halafu miaka hiyo, sio muda mrefu kurudi nyuma ilikuwa kwenda UK na nchi kadhaa ni "viza free"
Nimewapeleka sana wasomali kwa wazeewa bandika bandua na vifo na vizazi halafu hao wanakwea pipa na dili linasawazishwa mpaka airport wanakuwa wameshatonywa wanapitishwa hapo ni mpaka UK.
 
Sio Mchezo..
Halafu miaka hiyo, sio muda mrefu kurudi nyuma ilikuwa kwenda UK na nchi kadhaa ni "viza free"
Nimewapeleka sana wasomali kwa wazeewa bandika bandua na vifo na vizazi halafu hao wanakwea pipa na dili linasawazishwa mpaka airport wanakuwa wameshatonywa wanapitishwa hapo ni mpaka UK.
 
Michongo yote ilikuwa inaletwa na wahusika wenyewe kama ni bandari,tra,ttcl nk
Sasa watoto wa mjini kazi kwao
Ni kama wanatumika tu

Mjini kuna mambo mengi
Unaweza ukawa sehem au ukapatwa
Na shida fulani hujuwi wapi uanzie

Nakumbuka kulikuwa na watu wao kazi yao ni mambo ya dhamana ya kesi yyt ila syo ya kuua au bunduki
Mjini mipango

Ova
Hawa ndio wamesababisha bond mahakamani wanataka mtumishi wa serikali.
 
Ndama mtoto ya ng'ombe maisha haya yana leo na kesho
Huyu Ndama mtoto wa ng'ombe nae kaanzia hapo hapo kwenye kijiwe cha Azam kwa shoe shiner, alikua mshamba tu tunamtia makwenzi enzi zetu. kakulia kule magomeni mapipa ukitoka mjini kushotojuu kule kama unaenda kigogo. Alitoka huko kwao kigoma mdogo kaja sijui kwa ankali wake basi tukicheza mpira tunamtia mikwenzi tu. Na mtu aliemleta mjini kwenye kile kijiwe ni jamaa mmoja nimemsahau jina lake(alikua na anaweka Culkit) yeye kijiwe chake Empress pale na kina Masudi-marehemu. eti Ndama baadae akawa pedeshee daah maisha haya acha tu. Ila deals iliomuinua nasikia walimzika myahudi kumuuzia dhahabu fake. Pedeshee ndama!!!😂😂 Ila nasikia ndama baadae alivopata pesa akamuoa mnenguaji wa kikongo wa FM academia akiitwa Mirayesa na ndio wako nae mpaka sasa.
 
Ha hah ila Wakongo na njaa zao wakiamua kukupamba utapewa kila aina ya cheo,wewe warushie buku 10 tu na usikose kwenye dansi lao.ila shida wakikuzoiea wanahamishia shida zao kwako.
Siku moja nilikwenda Ngwasuma Heineken house, nilikuwa na katibu wa Wacongoman Tanzania, basi tulikula senene wa kutosha na mimi siku hiyo nilikuwa PDG, yule jamaa akawapa jina langu, basi nilivyokwenda kuwatunza nikashangaa wanalitaja jina langu halafu Nyoshi anasema baada ya Mungu ni wewe, kwakweli nilichoka aisee, hawa jamaa funga kazi.
 
Back
Top Bottom