Tuwaepuke wanasiasa wanataka kutuletea ukabila kupitia uChifu

Na hio ni sababu nyingine kuwa Samia haifai Tanganyika....yupo pale kuvuruga tu

Tanganyika (Tanzania bara) imetekwa, inaongozwa na raia wa kigeni (raia kutoka Zanzibar)
Kama ni ugenini basi ondoeni majeshi yenu ya vamizi. Mnasubiri nini?
 
Afrika imekuwa na utaratibu huu wa utawala tangu enzi na enzi. Hizi tawala zilizoletwa na wakoloni hapa Afrika zina miongo michache tu iliyopita. Tusizidharau hizi taratibu zetu za jadi, kwa sababu ya taratibu za kigeni.
Asante sana...
 
Ukiongelea uchifu unaongelea asili yetu..tamadunj..mila na miiko bila kusahau imani..wewe mlokole na mfia dini ambaye uliondolewa akili na utu wako kisa dini za wazungu na waarabu..ili wakutawale kuanzia akili na mali..unaona upuuzi kuenzi mila zako.

Bure kabisa..wewe.

#MaendeleoHayanaChama
 
Nawasalimu kwa jina la Jamuhuri ya muungano wa Tanzania.

Hizi siasa za Uchifu sio siasa salama kwa mustakabali wa nchi.

Kwanza yale maguo yenye ngozi za chui sijui wameyatoa wapi!

Niseme tu kwamba, Tanzania hakujawahi kuwa na machifu kwa muktadha wa uongozi wa kitaifa.

Machifu wa Tanzania walikuwa ni tawala chache tu ambazo zilikuwa huko kwa watu wa iringa zamani hizo.

Baadae wakoloni walipokuja, wakaunda vikundi vya wahuni wachache miongoni mwa watanzania kisha wakawavika uchifu for the benefit of white man. Hawa ndio waliohusika kuwauza wenzao utumwani.

Huu uchifu wa sasa wa Samia, sio uchifu haswa. Ni vikundi vya wachawi wanaomsimika Hangaya kwa kumpa mamlaka na utii. Ni power transfer ama alama ya utii katika mamlaka za wachawi.

Wachawi hawa wako nchi nzima. Wamejivika uchifu bandia ili kuficha sura zao halisi.

Kila mahali Rais anapopita wanamvika maguo ya kichawi.

Jamani, nchi hii inamuhitaji Mungu. Tuache kutegemea viumbe dhaifu kama mizimu.

Mungu wetu ni Mungu mwenye nguvu sana, lakini anahitaji watu wanyoofu.

Shida yenu nyinyi ni majizi na watu wa konakona, ndio maana mmemkimbia Mungu mkajikabidhi kwa viumbe wachafu na dhaifu kama majini na mizimu.

Mrudieni Mungu mwenye nguvu na mamlaka, mzitii amri zake na yeye awafanye kuwa wake.

Hayo maguo ya mizimu hayawezi kuwasaidia lolote. Mnajidaganya.
Taifa lisilo na utamaduni wake halisi ni taifa mfu!
 
Mama yenu content hana sasa atafanya nini kupata attention?

Preparation is everything, she wasn't well prepared.
 
CCM ni wakala wa shetani.
Hilo anayepinga na apinge,lakini ukweli unajulikana.
We watu wanazungusha kibatari nchi nzima kwa magharama kibao wakimini eti kibatari hicho kinamulika mpaka nje ya mipaka ya nchi kilete tumaini pale ambako hakuna tumaini, upendo pale penye chuki.....


Kwanini wasiwe wachawi?
 
Kwani kwasbb ni utaratibu wa tangu enzi km unavyosema ndo unaondoa ukweli kuwa ni ,uchawi,ushirikina,mizimu?
Hii haiondoi ukweli huu,haijalishi uliwekwa na kufuatwa na nani!
Haufai kenye nchi,tunamhitaji Mungu muumba wa mbingu na nchi sio machifu
Mkumbushe na kale kamshumaa wanakokazungusha nchi nzima wakikaabudu...
 
Hawa wameibuka kutoka wapi?
Na je wana impact gani katika maisha yetu kwa ujumla?
Sijawahi kusikia Chifu anatoa neno lolote kwenye jumuiya yetu
Hata kusifu au kukemea kitu ila ghafla tunasikia chifu wa huku na kupewa uchifu sijui nini
Kwenye uongozi wa nchi Kuna mengi Sana, tusije tukajiona tunajua sana. Mpaka rais kuamua kufanya alichofanya basi ujue kuna kitu kinawekwa sawa.
Uongozi sio rahisi tumtie Moyo mama atufikishe kwenye maendeleo
 
Kikubwa wakubwa wasijewaza kuwapa mavieite na watumishi kadhaaa, tutapigwa kama nchi. Wawakoge tu hivyooo maisha yaendeleee. Ila kwetu hatuna chief. Labda tuanzishe, na mwenye fursa ni mimi walau.
 
Kwanza uelewe kwamba CHEIF ni neno la kizungu.

Pili MACHIFU ni viongozi wa kiafrika waliowekwa na wazungu kwa ajili ya kazi za kikoloni.

Afrika haijawahi kuwa na CHEIF. Hii CHIEF ni invention ya mkoloni.

Hawa wa sasa hivi wanaoitwa MACHIFU ni wachawi wa samia.

Hakuna kitu kama CHEIF. Haya ni machawi tu yaliyotafuta chaka zuri la kujifichia.

Afrika ilikuwa na viongozi wake wa kimila, waite jina unalopenda machifu, watwala, warola, musimba, ghokoi, thyaaa, thunaaa lolote upendalo ila viongozi walikuwepo.

Tz ya leo Katika vijiji vyote nje ya mfumo rasmi kuna wazee wa kijiji wanaoheshimika ambao hata serikali haiwatambui lakini jamii husika inawatambua na kuwaheshimu, nenda katika mabaraza ya vijiji utakutana nao, na hata madiwani sijui makatibu kata mpaka mabalozi sijui wenyeviti huwa wanawaona hawa wazee kwa ajili ya baraka zao ndipo wapiganie kuiwakilisha serikali humo kijijini.

Serikali imeona kuendelea kujifanya kuwa hawa wazee hawapo wakati jamii inawatambua na kuwaheshimu si busara ikaamua iwatambue. Hakuna tatizo katika hilo labda kama upo hapa TZ kwa ajili ya kupinga, na kama ni hivyo hata ungekuwa ni mkutano wa wachungaji na mashekhe ungepinga.
 
Zamani kwetu vijijini tukisikia anakuja waziri, achilia mbali rais, siku hiyo hakuna kusoma. Barabara zinafagiliwa na wanafunzi tunapangwa barabarani kumsubiri kuanzia asubuhi hadi atakapopita. Baadae tabia hii ilipigwa marufuku.
Nimeona sasa hivi kama vile inajirudia! Kukiwa na ndege inaleta watalii, wanakusanywa wamasai kiwanja ndege wawaimbie, tazama Tz Safari Channel kama huamini. Kwa makabila yenye tamaduni fulani nayo yanarundikana mahali kwa madhumuni ya kumvisha kiongozi vipande fulani vya ngozi, kumkabidhi rungu au mkuki...nk na kumzawadia jina na cheo cha uchifu. Sasa hivi imefikia mahali inachekesha, rais SSH, pamoja kuwa ni mwanamke kapewa uchifu na jina ambalo wala halitumii!! Kama sio kujipendekeza, Afrika mwanamke kufanywa Chifu wapi na wapi!
Ukifuatilia kwa undani inaweza gundua ni suala zima la kujipendekeza viongozi mbalimbali. Wanamuona rais kama mpenda sifa fulani nao wanajua ndo pakupitia kwa maslahi binafsi. Lakini pia, Inaelekea kwa sasa, tamaduni za kale zinafufuliwa ili zisaidie kuuwa vyama pinzani - atakapotembelea eneo hilo, kabila au jamii husika inahusishwa kumpamba mkuu huyo kwa mapambio ya kisiasa na inaelekea wanafanikiwa! - hatua 1 mbele, 1 nyuma, hatusongi mbele
 
Ukiongelea uchifu unaongelea asili yetu..tamadunj..mila na miiko bila kusahau imani..wewe mlokole na mfia dini ambaye uliondolewa akili na utu wako kisa dini za wazungu na waarabu..ili wakutawale kuanzia akili na mali..unaona upuuzi kuenzi mila zako.

Bure kabisa..wewe.

#MaendeleoHayanaChama
Chifu ni neno lenye asili ya kiswahili???
 
Kikubwa wakubwa wasijewaza kuwapa mavieite na watumishi kadhaaa, tutapigwa kama nchi. Wawakoge tu hivyooo maisha yaendeleee. Ila kwetu hatuna chief. Labda tuanzishe, na mwenye fursa ni mimi walau.
Uchief unajua ni jina tu. Kwenu lazima kuna wale wazee wanaoaminika na kuheshimika ambao wanapelekewa suala lolote la kijamii kabla ya kufikishwa serikalini.
 
Back
Top Bottom