Tuungane kwa pamoja kupinga ukatili wa kimtandao dhidi ya wanawake

Idd Ninga

JF-Expert Member
Nov 18, 2012
5,136
4,297
Udalilishaji na ukatili wa kijinsia dhidi ya mwanamke umekua ukichukua nafasi katika jamii ya watumiaji wengi wa mtandao nchini Tanzania huku idadi ya wanawake na mabinti wakizidi kunyanyaswa kupitia mitandao ya kijamii.

Picha na video za udhalilishaji wa mwanamke zimekua zikisambazwa na baadhi ya watu bila ya kuona aibu.

Picha hizo na video zimekua zikisababisha maumivu na ha wakati mwingine kupeleka kifo pamoja na kumdhalilisha mwanamke huku wanajamii wakiwa ni watu wa kwanza kuliachia jambo hilo bila ya kulikemea.

Mimi kama Idd Ninga,nimeamua kusimama katika kupinga unyanyasaji wa kimtandao wanaofanyiwa wanawake kila siku,ni wajibu wetu kuwafanya wanawake na mabinti wasijutie kutumia mitandao ya kijamii.

Tuzuie kila aina ya ukatili huo.

Tutume salam kwa serikali, mashirika yasiyo yakiserikali, viongozi wa dini, vyama vya kisiasa, makundi ya kijamii na watu wote kupinga ukatili huu dhidi ya wanawake na mabinti.

#StopWomenCyberbullying
#MlindeMwanamke
#MpendeMwanamke

Tuweke Sahihi hapa

 
FB_IMG_1603396526264.jpg
 
Nakuunga mkono aslimia Mia MOJA mkuu Idd Ninga. Wanawake wameonewa Sana na sio tu kwenye mitandao, hata kwenye maisha ya kawaida. Nasimama na wewe. Napinga unyanyasaji wa mwanamke wa aina yoyote ile
 
Udalilishaji na ukatili wa kijinsia dhidi ya mwanamke umekua ukichukua nafasi katika jamii ya watumiaji wengi wa mtandao nchini Tanzania huku idadi ya wanawake na mabinti wakizidi kunyanyaswa kupitia mitandao ya kijamii.

Picha na video za udhalilishaji wa mwanamke zimekua zikisambazwa na baadhi ya watu bila ya kuona aibu.

Picha hizo na video zimekua zikisababisha maumivu na ha wakati mwingine kupeleka kifo pamoja na kumdhalilisha mwanamke huku wanajamii wakiwa ni watu wa kwanza kuliachia jambo hilo bila ya kulikemea.

Mimi kama Idd Ninga,nimeamua kusimama katika kupinga unyanyasaji wa kimtandao wanaofanyiwa wanawake kila siku,ni wajibu wetu kuwafanya wanawake na mabinti wasijutie kutumia mitandao ya kijamii.

Tuzuie kila aina ya ukatili huo.

Tutume salam kwa serikali, mashirika yasiyo yakiserikali, viongozi wa dini, vyama vya kisiasa, makundi ya kijamii na watu wote kupinga ukatili huu dhidi ya wanawake na mabinti.

#StopWomenCyberbullying
#MlindeMwanamke
#MpendeMwanamke

Tuweke Sahihi hapa

Wa kuanza nao ni wanawake wenyewe, wasijirahisi kihivyo.
 
  • Thanks
Reactions: Auz
Nakuunga mkono aslimia Mia MOJA mkuu Idd Ninga. Wanawake wameonewa Sana na sio tu kwenye mitandao, hata kwenye maisha ya kawaida. Nasimama na wewe. Napinga unyanyasaji wa mwanamke wa aina yoyote ile
Ni wakati wa kutetea.
Asante sana.
 
Wateteeni hivo hivo iko siku mtalia! unawatetea wao hawana midomo? unawasemea?? Mungu alisema tuishi nao kwa akili. wewe unaleta za kizungu hapa umetumwa?? nenda kaishi uzunguni kam hujakuja unalia humu. wanakugeuza nyeti wanakwambia ni haki yako!

Kma wewe unawatesa wape haki, kuwasemea km wao ni vilema wa midomo, wanyonge,,,, ndiyo kuwadhalilisha zaidi, ivo wewe ni mdhalilishaji mara dufu ya wale unaodhani wanawadhalilisha, kwani wana fwanyaje? ni wazi wewe unajua unavyo wafanya unadhani na sisi tunawafanya hivohivo!!! usitulishe mawazo yako, navoishi na mke wangu kwako wewe unaona namtesa? wa kwetu ndo stahili yao!

Wazungu, Waarabu wanajua walivowanyanyasa kingono watumwa wanawake vigori, mpaka leo wanafanya ivo kupitia vita, ndiyo leo hii unaona umati wa wapemba, Mulattoes, Latino America, waarabu nk! ile dhambi sasa imewatafuna weee hawana pa kupumulia, wanaisukumia kwa wanaume waafrica ! bila kujiju. wakemee wazungu wawalipe na kuomba msamaha kwa wanawake wote!!!

Wewe unarukia tu hujui , nikikuuliza mateso ya mwanamke ni yapi hujui hata moja!! waambie hao wazungu wako waache kudhamini vita BOKO haram, alshaabab, Msumbiji, Sudani, Somalia Angola wawalipe wanawake vilema, waweke soft ware ya kuminya maku ya mwanamke automatically zisionekane FB. hata kwa simu tu si vipo? uone km watakubali.

Mke kujianika utupu ndivo walivo, kuwakataza ni ukatili mbaya sana pia, wa kutaka kuwazimisha wasionekane kwenye majukwaa yao pendwa, ila wewe uonekane!! ebu nambie wewe kuona tako, ziwa, papuchi ya ke'' amedhalilika niini? kwani kuna zingine zimepinda? si sawa tu na ya mkeo? wazungu waliiga kwetu, Masai, barbaig, khoisan, wanadhalilika? wakatupa nguo! sasa mnafanya vice versa,
 
Back
Top Bottom