JamiiTalks Tutumie taarifa za Rushwa ya Ngono na Unyanyasaji sehemu ulipo, ili Mamlaka za Serikali zizifanyie kazi

Ni mwaka wa kumi nafanya kazi za utawala katika elimu ya juu. Shida kubwa hizi kesi zinapotaka kushughulikiwa, wanafunzi huwa hawatoi ushirikiano wa kutosha kwa hofu ya kwamba huko mbeleni atakwamishwa. Lakini in reality hakuna mtu anaweza kukukwamisha kwasababu tu ulimreport. Kuna haja kubwa kwa wanafunzi na jamii kujengewa uwezo na kujiamini ili kutoa taarifa za matukio kama haya.
Ahsante kwa kujioambanuwa mkuu.
Ebu naomba utuweke wazi kwa muda wa miaka kumi ukiwa kwenye kitengo cha utawala, Je hizi tuhuma ni kweli zipo?
Na kama zipo, ninyi kama utawala mmefanya juhudi zipi ili kuhakikisha mnakomesha ama kutokomeza rushwa ya ngono?
Na Je, ninyi kama wazazi mlifanya bidii zipi pamoja na kukusanya ushahidi wa kimazingira, pamoja na kulinda usiri wa shahidi/mkosewaji?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Naomba tusaidiane kutofautisha baina ya rushwa ya ngono na mapenzi binafsi?? Je mkufunzi wa chuo haruhusiwi kuwa mahusiano au hata ndoa na mwanafunzi ??mapenzi binafsi huanzia kwnye kutongozana,sasa tunatofautishaje baina ya mapenzi na rushwa??na je nikimpenda binti Nika mtongoza akanikatalia lakini by then mtihani ukaja akakamatwa kweli akinienezea nimemkamata sababu ya kuninyima atakuwa amekosea??

Sent using Jamii Forums mobile app
Pia wasituchanganye sisi tunaokula "matunda" kimasihara

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Aisee..... kama ndio hivi basi hao waomba,rushwa watakoma...Maana kwa kasi hii ya mabadiliko ya technology..hakiyanani tena Jela watakwenda wengi....Wakati una muomba mtu rushwa kumbe mwenzio ana record maongezi yenu iwe kwa,njia ya sauti.video.au text......

Aisee yajayo yana furahisha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Aisee.... hao police wahesabu kwamba kazi hawana tena... hii taarifa ikimfikia kangi kugola wameisha
Mimi nina kesi Geita mtoto wa mdogo wangu alibakwa usiku kucha na mshtakiwa akakubali lakini polisi waligeuza kibao.

Mtoto mpaka sasa anaumwa ana matatizo ya kisikolojia na hataki tena kusikia jina mwanamme. Alikuwa anamfanyia kibarua kama mjenzi yeye ni kibarua wake. Alipoenda kumsaidia kupeleka maji nyumbani akambaka. Tulienda bali lakini wakasema alishafikisha miaka 18 kesi haina maana.

Mtoto ameathirika kisaikolojia na hataki kitu chochote kuhusu mapenzi. Aliachiwa gono akatibu angalau siyo UKIMWI. Mimi mwenyewe nilihusisha mahakimu, askari na kila mtu lakini kesi ikabuma tangu 2014. Geita Geita Geita.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Katika kijiji cha Tella Mande kilichopo wilaya moshi vijijini kata ya old moshi, kaskazini mwa mji mdogo wa Kiboriloni upo mradi wa maji wa 900m ambao umesimama kwa hujuma ya mkandarasi na wahandisi wa maji. Walitandika mabomba undersize na wananchi walipopiga kelele wakayatoa na hawajaleta mengine na site hawaonekani.
Ofisi ya mradi iliyotarajiwa kugharimu 50m kama ilivyo kwenye andiko ndio kichekesho kama inavyoonekana hapa.
Wahusika wooote. Kimyaaaa.View attachment 1291311

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu,

Salaam. Watu kama nyie ni muhimu sana katika nchi hii.

Tunaomba haya maelezo uyapost kwenye hii thread hapa chini ili yaweze fanyiwa kazi na Serikali kuu. Umefanya vizuri sana kuongelea hili swala.

Hapa tunaomba taarifa za Rushwa ya Ngono na unyanyasaji kijinsia.

Karibu karibu sana.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
tatizo sio kuripoti,tatzo ni usalama wa aliyetoa ripoti au fununu

nijuavyo afrika hakunaga siri ,utawala wa sheria haufuatwi na wenye mamlaka, sasa kama hili halipo usalama wa mtu pia upo hatarini...
 
Hivi kweli kuna rushwa za maana za ngono, au ni kwaajli ya kukomoana tu?

Tuchukulie juzi yule mzee alikuwa rector wa cho gani sijui!

Kategeshewa kasichana kanafunzi kake, kisha kuishia kuaibishwa na mauzee yote hayo.

Hizi rushwa za ngono za kulengeshewa sheria ziangaliwe upya, mtatumaliza wanaume.

Maana mtu hauna hili wala lile, unakuta mwanamke anajilengesha kumbe katumwa ili akunase uingie kwenye mtego wa simba!

Na kukiwa na kuogopana kati ya mwanamke na mwanaume, dunia hii itakuwa ni tambara bovu ambalo halifai hata kwa kupigia deki siwafichi.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tahadhari ichukuliwe katika kufanyia kazi hizi cases ili tuseje tukasababisha madaktari wakawa frustrated kisa watoto wenyewe ambao wanatumia papuchi kama kinga yao ya kupata upendeleo katika kila kitu na kila huduma. Wahadhiri na madaktari ni watu muhimu sana. Siyo vizuri kukurupuka katika kuyashughikia cases na tuhuma Kama hizi. Umakini unahitajika ili kuepuka kubomoa badala ya kujenga. Mimi naona wizara ya afya iendelee kusisitiza matumizi ya kinga.
Mwanamke aruhisiwe kufungua kumshitaki mwanaume atakayekataa kutumia kinga.
BTW penzi la kulazimisha halinogi. Inawezekana hao wadada wanakubali mambo, then wasipotimiziwa ahadi zao wanaamua kuwaumbua wadeni wao.
Wanawake ni wengi jamani huku Mbeya. Sio vizuri kumlazimisha mmoja asiyekutaka au kuomba Rushwa ya ngono. Halafu wanawake wa Mbeya sio wagumu kiasi ya madaktari kuwa na ukame wa papuchi kiasi hicho.

Haya mambo huwa yananichanganya.
 
tatizo sio kuripoti,tatzo ni usalama wa aliyetoa ripoti au fununu

nijuavyo afrika hakunaga siri ,utawala wa sheria haufuatwi na wenye mamlaka, sasa kama hili halipo usalama wa mtu pia upo hatarini...
Hapana mkuu, ndo maana tukaomba tutumiwe sisi JamiiForums. Ni rahisi kifuatilia na kumpa mrejesho mhusika. Mambo yamebadilika. Usiwe na hofu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi kweli kuna rushwa za maana za ngono, au ni kwaajli ya kukomoana tu?

Tuchukulie juzi yule mzee alikuwa rector wa cho gani sijui!

Kategeshewa kasichana kanafunzi kake, kisha kuishia kuaibishwa na mauzee yote hayo.

Hizi rushwa za ngono za kulengeshewa sheria ziangaliwe upya, mtatumaliza wanaume.

Maana mtu hauna hili wala lile, unakuta mwanamke anajilengesha kumbe katumwa ili akunase uingie kwenye mtego wa simba!

Na kukiwa na kuogopana kati ya mwanamke na mwanaume, dunia hii itakuwa ni tambara bovu ambalo halifai hata kwa kupigia deki siwafichi.


Sent using Jamii Forums mobile app
Tatizo ni mwanaume kuendelea kuwa king'ang'anizi, mwanamke akikukataa mwache na sio kumtishia kuharibu maisha yake.
 
Mkuu uwezo mdogo wa binti isiwe sababu ya kumnyanyasa kingono ama kijinsia.Kuna watu mmezoea sana kutumia fursa kama hizi kunyanyasa mabinti mnaodhani hawana uwezo.

Utakuta unamdhalilisha hadharani,kwa matusi na dhihaka ili ajisalimishe kwako.Badala ya kumtia moyo afanye vizuri ,kitendo cha kumshusha na kumfanyia psychological torture,humfanya azidi kukata tamaa.

Ndio maana naamini wakufunzi wanaofanya hivi hawastahili kabisa kuwepo sio tu chuoni,hata duniani.Wakati mwingine mtu anaweza kuwa na uwezo mdogo darasani kutokana na mambo mengi ya kijamii yanayomkabili.Utakuta nyumbani anaishi na mama na wadogo zake tu na wakati yeye yuko Chuo huenda nyumbani ni wagonjwa na hawana pesa ya kujitibu.

Wewe kama mwalimu unamuhukumu kwa kumdhalilisha.Hii tabia haivumiliki
mkuu uchunguzi Tanzania, hapo watafanyia kazi majungu tu. wafanye kuangalia mwenendo wa ufaulu wa walalamikaji weng wao utakuta hawana uwezo kivile.

mkuu kuna kesi nimewahi ikuta polisi binti akidai kubakwa,mtuhumiwa akajieleza kwa kuonesha mawasiliano yao kisa ni jamaa kumpa elfu 20 badala ya 30 ya makubaliano yao

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom