Cha asubuhi
JF-Expert Member
- Jun 21, 2017
- 1,496
- 2,137
Jana wakati niko kwenye basi natoka mkoa kuanzia Mitaa ya Mbezi mpaka Kimara kuna aina flani ya bajaji nimeziona za njano hivi... sijui niziite bajaji za kichina au piki piki ila zinabeba abiria kwa mtindo wa chai maharage. Yani watu wa 4 ila wanakaa kwa kutazamana wawili kila upande!
Mwenye ufahamu anijuze kuhusu hivyo vibajaji/ pikipiki binafsi nimeona kama naweza kuvigeuza fursa ikiwa viko affordable!
dahhh eti "MTINDO WA CHAI MAHARAGE" umewaza nini kiongozi?