Tutete kidogo: Mamlaka ya CAG

GINHU

Member
Feb 7, 2011
68
14
Ndugu wa JF salamu
Hoja yangu kwa leo ni kuteta kuhusu mamlaka aliyopewa CAG.

Akihutubia kilele cha cha maadhimisho ya sikukuu ya Wafanyakazi duniani MEI MOSI, katika uwanja wa Mkwakwani, Tanga, Raisi Kikwete alielezea kwa kirefu majukumu na mamlaka ya CAG currently Bw. Uttoh (a.k.a OTTU). kwa upande wa Mamlaka, Raisi alisema, ili CAG awe na uhuru kamili, ilitungwa sheria ya kutoingiliwa ktk utendaji wake, si Raisi ama chombo kingine chochote hakiwezi kuingilia mamlaka yake. Raisi akishamteua CAG hana mamlaka ya kumwondoa na km kuna dosari yoyote katika ripoti zake, halimashauri/idara husika wanatakiwa wapeleke malalamiko yao katika mahakama ya Rufaa na si vinginevyo.

Hoja yangu hapa ndugu wanaJF ni:
1. kama huyu mteule wa Raisi hawezi kuhojiwa na mamlaka yoyote, sasa anawajibika kwa nani? na ni nani wa kumwajibisha? nauliza hivyo maana isije ikatokea mkubwa huyu akawa na bifu na ofisi fulani akaamua kutoa ripoti mbaya ili amkomoe mbaya wake.
2. Je ripoti za huyu bw mkubwa zinakaguliwa na nani?

Ndugu wanaJF naomba kutoa hoja
 
Ndugu wa JF salamu
Hoja yangu kwa leo ni kuteta kuhusu mamlaka aliyopewa CAG.

Akihutubia kilele cha cha maadhimisho ya sikukuu ya Wafanyakazi duniani MEI MOSI, katika uwanja wa Mkwakwani, Tanga, Raisi Kikwete alielezea kwa kirefu majukumu na mamlaka ya CAG currently Bw. Uttoh (a.k.a OTTU). kwa upande wa Mamlaka, Raisi alisema, ili CAG awe na uhuru kamili, ilitungwa sheria ya kutoingiliwa ktk utendaji wake, si Raisi ama chombo kingine chochote hakiwezi kuingilia mamlaka yake. Raisi akishamteua CAG hana mamlaka ya kumwondoa na km kuna dosari yoyote katika ripoti zake, halimashauri/idara husika wanatakiwa wapeleke malalamiko yao katika mahakama ya Rufaa na si vinginevyo.

Hoja yangu hapa ndugu wanaJF ni:
1. kama huyu mteule wa Raisi hawezi kuhojiwa na mamlaka yoyote, sasa anawajibika kwa nani? na ni nani wa kumwajibisha? nauliza hivyo maana isije ikatokea mkubwa huyu akawa na bifu na ofisi fulani akaamua kutoa ripoti mbaya ili amkomoe mbaya wake.
2. Je ripoti za huyu bw mkubwa zinakaguliwa na nani?

Ndugu wanaJF naomba kutoa hoja

Mkuu soma Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ibara ya 143 na 144.

Mahakama ina nguvu kikatiba kuchunguza kama CAG anatekeleza madaraka yake kwa mujibu wa katiba (ibara ya 143 (6)).

Kuhusu kumuondoa kazini pia kuna mchakato wa kikatiba ambapo kama Rais anataka kumfuta kazi itabidi ateue tume ya kumchunguza CAG.
 
Na katika nchi yetu siyo CAG peke yake bali pia majaji wa mahakama kuu na rufaa na gavana wa benki kuu.

Hizi ni nafasi nyeti sana ambazo mtu akiwa katika nafasi hizo hatakiwi kuzifanya huku akiwa na wasiwasi wa kuondolewa!
 
Mkuu soma Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ibara ya 143 na 144.

Mahakama ina nguvu kikatiba kuchunguza kama CAG anatekeleza madaraka yake kwa mujibu wa katiba (ibara ya 143 (6)).

Kuhusu kumuondoa kazini pia kuna mchakato wa kikatiba ambapo kama Rais anataka kumfuta kazi itabidi ateue tume ya kumchunguza CAG.

mkuu nashukuru sana for your directives; Nimesoma hizo ibara lakini kuna mapungufu makubwa ya kikatiba kuhusu kinga hizo alizopewa. mf kibara 144 km kuondolewa kwa CAG itabidi raisi aunde tume ya watu wasiopungua 2, ambapo mwenyekiti na nusu ya wajumbe sharti wawe ni majaji tena wa mahakama kuu ama za rufaa ktk nchi za jumuiya ya madola. Hapa ndo penye utata ktk kuwajibishwa kwa bw. mkubwa huyu. pengine kuna haja ya kulijadili upya jambo hili ktk katiba ijayo.


Naomba tuendelee kuteta ktk hili.

Asanteni
 
Back
Top Bottom