Elections 2010 Tutegemee nini katika awamu ya pili ya Kikwete?

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,789
288,011
Mkapa aliita awamu yake ya uwazi na ukweli lakini wote tunajua hakuwa muwazi wala mkweli. Pia alijiita Mr Clean lakini ukweli hakuwa na usafi wowote kwa kuhusika kwa karibu na kashfa nyingi ambazo nyingi zilitokea katika awamu yake ya pili zikiwemo ununuzi wa RADA, Ukwapuaji wa Kiwira katika mazingira ya kutatanisha, ununuzi wa ndege ya Rais, kusaini mikataba ya uchimbaji madini yetu ambayo haina maslahi, uuzwaji wa nyumba za Serikali, EPA, kusaini mkataba na wale makaburu ili kuiendesha TANESCO, kufanya biashara akiwa Ikulu n.k.

Je, awamu ya pili ya Kikwete itakua na ahueni ukilinganisha na ya kwanza katika utendaji au ndiyo hali itadidimia zaidi na kuwepo kwa kashfa nyingi kama katika awamu ya pili ya Mkapa?
 
Mkapa aliita awamu yake ya uwazi na ukweli lakini wote tunajua hakuwa muwazi wala mkweli. Pia alijiita Mr Clean lakini ukweli hakuwa na usafi wowote kwa kuhusika kwa karibu na kashfa nyingi ambazo nyingi zilitokea katika awamu yake ya pili zikiwemo ununuzi wa RADA, Ukwapuaji wa Kiwira katika mazingira ya kutatanisha, ununuzi wa ndege ya Rais, kusaini mikataba ya uchimbaji madini yetu ambayo haina maslahi, uuzwaji wa nyumba za Serikali, EPA, kusaini mkataba na wale makaburu ili kuiendesha TANESCO, kufanya biashara akiwa Ikulu n.k.

Je, awamu ya pili ya Kikwete itakua na ahueni ukilinganisha na ya kwanza katika utendaji au ndiyo hali itadidimia zaidi na kuwepo kwa kashfa nyingi kama katika awamu ya pili ya Mkapa?

Katika ile slogan ya ARI MPYA, NGUVU MPYA NA KASI MPYA ame-replace neno MPYA na kuweka ZAIDI......kwa hivyo inasomeka ARI ZAIDI, NGUVU ZAIDI na KASI ZAIDI. Sasa ukitaka kujua ZAIDI maana yake nini then ni kutafakari MAPYA tuliyoshuhudia kipindi hiki cha miaka yake mitano kinachokwisha........! Na kubwa ZAIDI ni pale 'ZUMA' atakaporudi 2015
 
tutegemee
WIZI ZAIDI
UZEMBE ZAIDI
UFISADI ZAIDI na
MATUMIZI YALIYOPITILIZA ZAIDI
 
Tutegemee kulala usingizi wa pono maana tulikuwa tumelazwa usingizi wa mang'amumang'amu
 
awamu ya pili cku zote ni lala salama na chukua chako mapema, biashara asbui ili tuagane vizuri, mkapa kwenye awamu ya pili ilikua ndio ufisadi ili kujiwekea akiba ya uzeeni kwani anajua hata watu wakipiga kelele vp anajua hatarudi!
 

Muda huu ataoshea sana ili akitoka madarakani ajulikane kuwa nae alijenga nchi si unawajua.

Siku zote muhula wa kwanza ni kufanya mambo yao na muhula wa pili kurudisha uchumi alipo ukuta na kuongeza ki % Moja ili aonekane aliutoa uchumi ulipo poromoka wakati yeye huyo huyo ndie aliye uangusha
 
Kwa kikwete tutegemee kuwabana mafisadi zaidi kwani anatazama kwa udi na uvumba donge nono lisilo na kelele kutoka Mo-ibrahim foundation baada ya kustaafu na pia hataki kuacha madoa ya first 5yrs (This are my thoughts)
 
wala sijui cha kutegemea, my expectations alipokua anaingia zilikua tofauti na alichokifanya, probably worse or better.
 
Katika ile slogan ya ARI MPYA, NGUVU MPYA NA KASI MPYA ame-replace neno MPYA na kuweka ZAIDI......kwa hivyo inasomeka ARI ZAIDI, NGUVU ZAIDI na KASI ZAIDI. Sasa ukitaka kujua ZAIDI maana yake nini then ni kutafakari MAPYA tuliyoshuhudia kipindi hiki cha miaka yake mitano kinachokwisha........! Na kubwa ZAIDI ni pale 'ZUMA' atakaporudi 2015

Tusubiri kujifia mwaya, maisha yatakuwa magumu zaidi kani kwa sasa atakuwa anajitahidi kumalizia kile kijiji chake pale Chalinze kwa mbele
 
tutegemee
WIZI ZAIDI
UZEMBE ZAIDI
UFISADI ZAIDI na
MATUMIZI YALIYOPITILIZA ZAIDI


nA safari zisizo-za lazima zaidi hata kama ni kwenye birthday as far as ni ulaya tutaenda tu..
Na excessive allowances kwa ajili ya kuwapongeza wale wote watakaomchagua tena....

Hapo vipi mpwa
 
Kwa kikwete tutegemee kuwabana mafisadi zaidi kwani anatazama kwa udi na uvumba donge nono lisilo na kelele kutoka Mo-ibrahim foundation baada ya kustaafu na pia hataki kuacha madoa ya first 5yrs (This are my thoughts)
Kwanini ategemee zawadi ya Mo-Ibrahim wakati anaweza kujitafutia mwenyewe tena zaidi ya hiyo zawadi
 
we should expect nothing............

hakuna jipya atakalolifanya .................hata aina ya ufisadi mpya hataweza kutoa kwa kuwa uwezo wa kuanzisha hana.

tutegemee ufisadi wa aina ile ile, uzembe wa aina ile ile, na kufa kwa uchumi kwa aina ile ile
 
Nilipokuwa najifunza haka kalugha kawenzetu, nilisoma kijitabu cha hadithi kilichokuwa na hadithi mojawapo iliyoitwa Snake Girls, kwakifupi, huyu mzazi alihangaika sana kupata watoto hata akenda kwa mganaga aliempatia watoto ambao asili yao ni Nyoka na msharti kwamba asije akawakosea hata siku moja na asitaje mbele yao kuwa ni product ya nyoka na sio binadamu, siku moja yule mzazi baada ya kuudhiwa sana na wale watoto, akajikuta akisema hivi "What can I expect from the head of the Snake? Mara watoto wote wakayeyuka na kuujiunga na kuwa nyoka tena na kukimbia porini, mwenye akili ameelewa.

Wikiendi njema
 
Tutegemee uteuzi wa nafasi za kamisheni na kujuana zaidi. Msione vijana wanajitolea kutembeza form za kumdhamini mikoani. Wana lao jambo.
 
Back
Top Bottom