Tutegemee kikosi kikubwa kuhamia CHADEMA

daza steven

JF-Expert Member
Aug 30, 2016
359
357
Hakuna mtu atakaye kataa kuwa mafisadi yalijaa CCM. Ndiyo maana tuliambiwa na CDM kuwa CCM imeoza na serikali yake. Je yalitoka wapi haya mafisadi?
Mwishoni mwa miaka ya 1990 Baada ya marehemu baba wa taifa Mwl Julius Kambarage Nyerere kututoka ndiyo haya majamaa yalianza kujitokeza kwa siri au chini chini na kujipenyeza katika awamu ya pili, awamu ya tatu yakajiimarisha zaidi na awamu ya nne yalikomaa na yakataka na kuchukuwa nchi kabisa.

Kwa busara kubwa ya wazee wa CCM alikubali kukaa chini na kukubali kuwa walikosea sana kuruhusu kuwepo kwa mafisadi ndani ya chama na wakatoka na azimio mmoja kuwa fisadi atambi tena ndani ya CCM na ndipo siasa za Tanzania zilibadilika siku hiyo hiyo na vita ilianza pale pale kwa kumuandaa Ndugu yetu Joni Pombe Magufuli.

Hivyo kikosi cha kwanza cha mafisadi kilitimkia CHADEMA kusaka urais, ambapo kikosi hiki kiliongwazwa na Lowasa na wenzake ambao tageti ilikuwa kupata uraisi au madaraka kamili ili kufafanya ufisadi.
Na kwabahati mbaya kikosi hiki kilifeli 2015 kupata uraisi lakini kipo.

Kikosi kingine ni kikosi cha akina Nyalandu hiki ni kikosi ambacho kinashindwa kuishi ndani ya CCM kutokana na hali ya hewa kuwa mbaya kwao kwa sasa. Kikosi kazi hiki hakikuzoea maupepo makali tena ya joto kali, hiki ni kikosi ambacho kilizoea kipupwe na viyoyozi sasa hakuna na kibaya zaidi kimeachwa nje kabisa ya nyumba na kina pigwa na upepo wamoto ambao hawajauzoea.
Hii ina kuwa ni ngumu kwao kusavaivu na lazima kikosi hiki kitimke.

Kikosi kingine hiki ni kama cha mwanzo ila tofauti chenyewe hakisaki urais ila kuendelea na kuwa wabunge.
Kikosi hiki cha mafisadi kimepata kadhia kubwa ya tishio la kutokurudi bungeni tena kupitia CCM, kwani Mh. Rais (jembe) alisha tangaza tayari kwa kumuomba Mh. Ndugai kuwa ampe majina ya wabunge wote ambao wanatokea katika kila kashfa ya ufisadi ili wakatwe majina yao katika uchaguzi ujao.

Kikosi hiki kina watu kama Vijisenti na wenzake wengi sana hivyo CDM itakuwa na mtaji mkubwa kutokana na mafisadi hawa yote kuamia kwao kwa sababu mazingira ndani ya CCM hayaruhusu fisadi kutamba ila ndani ya CDM hari ni nzuri kufanaya siasa za mafisadi.

Kuna msemo unaosema kuwa ndege wanaofanana wanaruka tundu moja hili limedhihilika tayari kwani kwani Freeman anabarikiwa na wenzake hawa na kufanya kikosi kikubwa.

Ikumbukwe kuwa mwizi ni mwizi tu si kweli kuwa mwizi akiama kutoka Morogoro na kuamia Tabora ataacha wizi tukiaminishwa hivi tutakuwa wajinga. Mwizi anabadilika kutokana na utu wake wandani.

Jambo lingine baya ndani ya CCM kwa mafisadi ni kuwa CCM kilikuwa chama cha mafisadi kama nilivyo sema mwazo na kiliakikisha kinawalinda mafisadi wake kwa nguvu zote wakati ule na ndiyo maana CHADEMA walitusaidia sana kututajia mafisadi tena kwa majina na kutoa ushaidi kama kwa Lowasa na wengine wengi.

Tofauti na sasa CCM yenyewe inasema jamani huyu ni fisadi na kumwekea mbinu za kumwondoa kama Nyalandu Chenge na wengine. Mfano Mh. Nyalandu amekuwa kilasiku ya mungu kuitwa na kuojiwa kuhusu Tembo, Twiga na vitalu alivyo gawa kwa wawekezaji ambavyo havina faida kwa taifa, Mh. hakuzoea kabisa kusumbuliwa, ndiyo maana akaterezee CHADEMA ambapo kuna nafuu na mazigira ya kumlinda na kutetewa ni makubwa.

Namaliza kwa kusema Mh. Dr Magua fuli a.k.a JEMBE kama ulikuwa uko gia namba 3 sasa maliza zote sita chimba kwani CCM hakikuwa chama cha mafisadi hata kidogo huko nyuma unachokifanya ni sahihi ongeza joto hadi hata nyuzi 600 digree sentigredi. Hata Yesu yule Mnazareti akuyauwa mapepo wachafu aliyaruhusu yawaingie nguruwe na yalienda. Hivyo hivyo mafisadi ni kama mapepo yaache yaingie kwa nguruwe huku tumechoka.

Nawasilisha kizalendo zaidi.
 
Mwaka 1995 ndiyo upinzani uliwahi kufanya vema wasomi wazuri na wataalamu wenye brain walijiunga na upinzani. Leo hii upinzani ni janga kwa taifa. Kwa sasa ccm ni makini zaidi. Sitegemee
 
Eti ndege wanaofanana waruka tundu moja??? Jamani mimi nasema kupona kwa ssm watuachie siye wanassm asilia, mazao ya akina JK wa kwanza tujenge chama lasivyo..! Watu kama nyie mtatiponza ssm wenzenu..!
 
Kumbe Nyalandu amekuwa akihojiwa mara kwa mara kuhusu uuzaji wake wa vitalu vya uwindaji.?

Sasa mbona wakati anahamia ccm hakusema kuwa hiyo ni moja ya sababu.

Wanasiasa watu wa ajabu sana.
 
NiMABADILIKO YA KWELI NA YA DHATI.

Na mimi kama IF member anasema waende Chadema wooote waliotuingiza Kwenye umaskini mkubwa nchi hii tajiri. Hawa wanastahili hata kunyongwa kwa ufisadi.

Namsihi raisi wetu ataifishe mali zao haraka sana. Hata kwaliobaki ndani ya ccm ambao wanajukikana kupata utajiri wa kibilionea wa kupindukia baada ya kuwa mawaziri/ wakuu wa taasisi ili hali ni maskini ndani ya familia zao.

Tuwashugulikie iwe fundisho kwa watu wanye tamaa ndani ya taifa hili. Wapo wabunge, madiwani na Mawazir na wastaafu Kwenye ngazi hiyo.

Magufuli Oyeeee Oyeee Oyeee
 
Yawezekana umejitahidi sana kuandika na hongera kwa kutoa yako ya moyoni mkuu.

Lakini pia siku zote shillingi huwa ina pande mbili (a coin always has two sides). Ya Nyalandu na twiga tukubali ni kweli na kama ni kweli awajibishwe kwa hilo.

Lakini je mzalendo wetu namba moja, jembe la ukweli mwenye P.h.D yake baba Jesca, mheshimiwa sana Magufuli si ni yeye aliyeuza nyumba za serikali (National Housing) kwa bei ya kutupwa tena akaenda mbali zaidi kwa kuwauzia hawara zake na wadogo zake Au huo ndio uzalendo jamani?

Ni Magufuli huyu huyu alituletea kivuko kibovu chenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 6 pesa za madafu, kivuko kikabuma hata kabla hakijarudisha pesa wakaenda kukitupa jeshini huo ndio uzalendo au sio?

Mkumbuke pia ule msala wa samaki za wachina tunalipa sasa hivi kisa tu baba Jesca na maamuzi yake ambayo mtasema ni uzalendo uliotukuka na uchungu wa maendeleo.

Lakini kama mafisadi wapi na kweli wapo hatukatai wengine ndio hao akina Nyalandu ambao tena ni majizi kwa nini ile mahaka ya mafisadi inakosa kesi? Kwa nini kesi hazingurumi mahakamani na rais alisema mahakama ya mafisadi iko tayari?

Watu mtasema wakati magufuli anauza nyumba za serikali alikuwa waziri tu na maamuzi yalikuwa chini ya waziri mkuu kipindi hicho je kwani wakati twiga wanasafirishwa hata Nyalandu si alikuwa waziri tu na maamuzi yalifikiwa na kupata baraka za baraza la mawaziri chini ya mwenyekiti na Magufuli mwenyewe akiwepo kama mmoja wa mawaziri.
 
Yawezekana umejitahidi sana kuandika na hongera kwa kutoa yako ya moyoni mkuu.

Lakini pia siku zote shillingi huwa ina pande mbili (a coin always has two sides). Ya Nyalandu na twiga tukubali ni kweli na kama ni kweli awajibishwe kwa hilo.

Lakini je mzalendo wetu namba moja, jembe la ukweli mwenye P.h.D yake baba Jesca, mheshimiwa sana Magufuli si ni yeye aliyeuza nyumba za serikali (National Housing) kwa bei ya kutupwa tena akaenda mbali zaidi kwa kuwauzia hawara zake na wadogo zake Au huo ndio uzalendo jamani?

Ni Magufuli huyu huyu alituletea kivuko kibovu chenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 6 pesa za madafu, kivuko kikabuma hata kabla hakijarudisha pesa wakaenda kukitupa jeshini huo ndio uzalendo au sio?

Mkumbuke pia ule msala wa samaki za wachina tunalipa sasa hivi kisa tu baba Jesca na maamuzi yake ambayo mtasema ni uzalendo uliotukuka na uchungu wa maendeleo.

Lakini kama mafisadi wapi na kweli wapo hatukatai wengine ndio hao akina Nyalandu ambao tena ni majizi kwa nini ile mahaka ya mafisadi inakosa kesi? Kwa nini kesi hazingurumi mahakamani na rais alisema mahakama ya mafisadi iko tayari?

Watu mtasema wakati magufuli anauza nyumba za serikali alikuwa waziri tu na maamuzi yalikuwa chini ya waziri mkuu kipindi hicho je kwani wakati twiga wanasafirishwa hata Nyalandu si alikuwa waziri tu na maamuzi yalifikiwa na kupata baraka za baraza la mawaziri chini ya mwenyekiti na Magufuli mwenyewe akiwepo kama mmoja wa mawaziri.
Wakumbuke kuwa katiba inampa kinga ya kushtakiwa MTU ambaye alitenda makosa akiwa katika majukumu ya urais tuu na sii kabla ya hapo.
Hivyo kama MTU alikula rushwa kwenye ununuzi wa vivuko, kuuza Nyumba au matengenezo ya barabara mpya anaweza shtakiwa tuu.
Tusubiri wakati muafaka yote yatakumbukwa kama wanavyo kumbukwa wale wa NAZI ya Ujerumani
 
CCM inauwezo wa kuzalisha zaidi ya vyama 20 vya siasa bila kutetereka.
 
Back
Top Bottom