Tutegemee CHADEMA kuanza kutetea wamachinga?

Etwege

JF-Expert Member
Jul 4, 2018
5,370
14,647
Baada ya jiji kuajiri wanamgambo wa kupiga wamachinga na Mama Ntilie ifikapo tarehe 18/5, angalau jiji la Dar litaanza kuonekana sasa maana moshi wa mamantilie wanaopikia kuni pembeni ya barabara ndo ulikua unaonekana.

Yaani hata Nairobi au Kigali tu walikua wanaonekana wametuacha mbali kisa haya mabanda maana kila mtu kajenga anavyojua na kuezeka anavyojua.

Kumbuka bodaboda, Mama Ntilie, machinga walikataa kushiriki maandamano ya Chadema kwa miaka 5 kwa sababu walikuwa na kazi za kufanya na walilipa kodi kupitia kitambulisho maalum.

Hao wamachinga watakaokuwa wanapigwa barabarani si watakimbilia Chadema? Watapokewa?

Bila shaka sasa baada ya kuanza kuwapiga CCM na maisha bora kwa kila mtanzania vitaimarika sana na huenda uchaguzi mkuu 2025 CCM wakazoa kura 99%
 
Yaani nyie ni vichaa sijapata kuona, yaani mnajua tulivyopinga upuuzi wenu wa kuruhusu huu ujinga wa biashara holela mkamsikiliza yule mwendazake.

Leo mnaanza kutusumbua hapa, mnatengeneza tatizo, mnakuja na suluhisho fake then mnashangilia. Mna akili kweli nyie? Naona kama vile mnastahili kwenda mirembe.
 
Bavicha mna roho mbaya sana. Hata wanyonge mnawaonea wivu! Kisa hawakushiriki maandamano yenu na hawakuwapa kura basi wamekua maadui zenu. Mnatete shamba la Mbowe huku mnashabikiwa masikini waharibiwe hata wanachokitegemea pekee.
 
Yaani nyie ni vichaa sijapata kuona, yaani mnajua tulivyopinga upuuzi wenu wa kuruhusu huu ujinga wa biashara holela mkamsikiliza yule mwendazake.

Leo mnaanza kutusumbua hapa, mnatengeneza tatizo, mnakuja na suluhisho fake then mnashangilia. Mna akili kweli nyie? Naona kama vile mnastahili kwenda mirembe
Chadema vichaa tu kama walivyo vichaa wa Milembe
 
Yaani nyie ni vichaa sijapata kuona, yaani mnajua tulivyopinga upuuzi wenu wa kuruhusu huu ujinga wa biashara holela mkamsikiliza yule mwendazake.

Leo mnaanza kutusumbua hapa, mnatengeneza tatizo, mnakuja na suluhisho fake then mnashangilia. Mna akili kweli nyie? Naona kama vile mnastahili kwenda mirembe
Je utawatetea mama ntilie watakavyoanza kupigwa?
 
Wengi wamekaa kimya sio kwamba hizi taarifa hawana lahasha. Ila wanachosubiri ni kusikia Robart Amsterdam na M'beleji (Lisu) wanasema nini kuhusu hii ishu, afu na wao ndo waanze kufuata upepo utaotokea Ulaya.
 
  • Thanks
Reactions: mmh
Magufuli ndo aliyewaruhusu kufanya kazi..pro-magu kazi kwenu.

Miji na majiji wamegeuka vituko..maturubai kila sehemu.
 
Je utawatetea mama ntilie watakavyoanza kupigwa?
Kwahio mmetengeneza Tatizo, na sasa mnataka muwapige, sio? Wakupigwa na kulaaniwa ni Nyie mliowaruhusu wafanye biashara holela eti Rais wa Wanyonge
 
WABUNGE WA CCM WANAKIAIBISHA CHAMA.

Na Thadei Ole Mushi.

Jana Waziri mkuu kakosa maswali ya kuulizwa kwenye session yake ya nusu saa alhamisi.

Huu ni umbumbumbu mkubwa kwa wabunge wetu wa CCM. Yaani Waziri mkuu anakosa maswali Bungeni wakati:-

Bei ya Sukari ipo juu.

Bei ya mafuta haishikiki.

Baadhi ya Mitandao haijashusha Bei ya Vifurushi.

Vijana wanapambana kutafuta ajira na hazipo.

Yapo mengi Sana ya kuuliza.

Mtu wa kuyatolea ufafanuzi na mwenye mamlaka yupo lakini hakuna wa kumuuliza.

Bunge la Chama kimoja na Akili za wabunge Nazo zimeungana na kuwa Moja.

Tuna Kazi kubwa Sana 2025 ya ku screen vijana wenye maarifa na weledi wagombee Ubunge. Hawa walio screeniwa na Bashiru na Polepole wanatia aibu.

Shame!!!

Ole Mushi
0712702602
 
CDM wanachosema ni kwamba " Weka misingi mizuri ya mambo haya" - miaka nenda rudi tatizo la wamachinga dar es salaam halijawahi kutatuliwa na kuisha kwa nini? CCM mmeshindwa kutatua tatizo hili badala yake huwa mnaliahirisha then mnaibuka tena kulitatua wakati limeshakuwa si tatizo tena bali ni zigo.

Hawa sasa hao wamachinga waliojazana hapo mitaa ya posta na mwingineko kote kwa maelfu unawapekeka wapi, kwa utaratibu upi?
 
CDM wanachosema ni kwamba " Weka misingi mizuri ya mambo haya" - miaka nenda rudi tatizo la wamachinga dar es salaam halijawahi kutatuliwa na kuisha kwa nini? CCM mmeshindwa kutatua tatizo hili badala yake huwa mnaliahirisha then mnaibuka tena kulitatua wakati limeshakuwa si tatizo tena bali ni zigo.

Hawa sasa hao wamachinga waliojazana hapo mitaa ya posta na mwingineko kote kwa maelfu unawapekeka wapi, kwa utaratibu upi?
Hao wamachinga aatakuwa wanapigwa barabarani si watakimbilia chadema?
Mtawapokea?
 

Similar Discussions

1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom