Etwege
JF-Expert Member
- Jul 4, 2018
- 5,370
- 14,647
Baada ya jiji kuajiri wanamgambo wa kupiga wamachinga na Mama Ntilie ifikapo tarehe 18/5, angalau jiji la Dar litaanza kuonekana sasa maana moshi wa mamantilie wanaopikia kuni pembeni ya barabara ndo ulikua unaonekana.
Yaani hata Nairobi au Kigali tu walikua wanaonekana wametuacha mbali kisa haya mabanda maana kila mtu kajenga anavyojua na kuezeka anavyojua.
Kumbuka bodaboda, Mama Ntilie, machinga walikataa kushiriki maandamano ya Chadema kwa miaka 5 kwa sababu walikuwa na kazi za kufanya na walilipa kodi kupitia kitambulisho maalum.
Hao wamachinga watakaokuwa wanapigwa barabarani si watakimbilia Chadema? Watapokewa?
Bila shaka sasa baada ya kuanza kuwapiga CCM na maisha bora kwa kila mtanzania vitaimarika sana na huenda uchaguzi mkuu 2025 CCM wakazoa kura 99%
Yaani hata Nairobi au Kigali tu walikua wanaonekana wametuacha mbali kisa haya mabanda maana kila mtu kajenga anavyojua na kuezeka anavyojua.
Kumbuka bodaboda, Mama Ntilie, machinga walikataa kushiriki maandamano ya Chadema kwa miaka 5 kwa sababu walikuwa na kazi za kufanya na walilipa kodi kupitia kitambulisho maalum.
Hao wamachinga watakaokuwa wanapigwa barabarani si watakimbilia Chadema? Watapokewa?
Bila shaka sasa baada ya kuanza kuwapiga CCM na maisha bora kwa kila mtanzania vitaimarika sana na huenda uchaguzi mkuu 2025 CCM wakazoa kura 99%