Chizi Maarifa
JF-Expert Member
- Jul 29, 2013
- 10,272
- 23,046
Watanzania kama ilivyo ada tumekuwa wanyonge mpaka basi. Tumekubali kukamuliwa kila sehemu na Serikali imeamua kuendelea kutunyonya mpaka damu.
Kifurushi cha Airtel cha Tsh 1,000 kwa GB 1 nacho kimepunguzwa. Sasa ni MB 500 kwa tsh 1000 ndani ya siku 3.
Tunajua Serikali nayo inafaidika na mnyonyo huu,mkamuo huu. Wametukamua maziwa bila kutulisha. Sasa maziwa yamekauka. Wanaanza kutukamua Damu.
Watanzania, ilipanda sukari tukanyamaza, ikapanda bei ya mafuta tukanyamaza, inapanda bei ya vifurushi tumenyamaza. Tunataka ipande nini tuamke?
Mpaka sasa natafuta Mtandao Rafiki ambao utanisaidia upande wa Data niachane na Airtel. Please tushirikishane kama Halotel, Zantel au TTCL wana offer za kufaa za Internet Bundles.
Kifurushi cha Airtel cha Tsh 1,000 kwa GB 1 nacho kimepunguzwa. Sasa ni MB 500 kwa tsh 1000 ndani ya siku 3.
Tunajua Serikali nayo inafaidika na mnyonyo huu,mkamuo huu. Wametukamua maziwa bila kutulisha. Sasa maziwa yamekauka. Wanaanza kutukamua Damu.
Watanzania, ilipanda sukari tukanyamaza, ikapanda bei ya mafuta tukanyamaza, inapanda bei ya vifurushi tumenyamaza. Tunataka ipande nini tuamke?
Mpaka sasa natafuta Mtandao Rafiki ambao utanisaidia upande wa Data niachane na Airtel. Please tushirikishane kama Halotel, Zantel au TTCL wana offer za kufaa za Internet Bundles.