Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,744
Watanzania walio wengi wameapa kuwa ikiwa patatokea kundi linalojidai kutumia nguvu za umma kumuondosha Raisi Kikwete nao pia watatumia nguvu za Umma kuhakikisha kuwa anabaki madarakani hadi mwisho wa awamu yake.
Baadhi ya waTanzania hao walidai madai yanayotolewa na vyama vichache kuwa itumike nguvu ya umma kumuondoa Mheshimiwa Raisi Kikwete madarakani ni ya makundi ambayo yamepoteza muelekeo na sasa wanataka kulisambaratisha Taifa hili lenye utulivu na amani na kuliingiza kwenye vurumai lisilojulikana mwisho wake.
WaTanzania hao ambao wengi wao wanasema sisi ni wengi kuliko walioko kwenye hayo makundi wataonyesha ni namna gani nguvu za umma zinatumika kuhakikisha Raisi waliemchagua anaendelea kubaki kwenye madaraka kwani uhakika kuwa wingi wao ndio uliomueka madarakani upo palepale na ushindi uliopatikana sio wa kubabaisha au kupapasa ni ushindi uliotangazwa na tume na ambao ndio unaotakiwa uheshimiwe.
Sasa kutokea kwa vishambenga ambavyo vinajitutumua kwenye majukwaa kuwa peoples power itafanya kazi kumuondoa Kikwete madarakani ,wananchi hao walisisitiza madai yao kuwa wanawasuburi hao ambao watakuwa mstari wa mbele kuongoza nguvu za umma na wajiandae kukutana vilevile na nguvu za Umma upande wa Uraisi ,na wamesema watajuta kuzaliwa maana wao ni wengi sana na watakuwa hawana mswalie mtume ni kumlinda Kikwete tu mpaka kieleweke ,lakini hawatamuacha Raisi waliemchagua kuchezewa na watu wachache.
Baadhi ya waTanzania hao walidai madai yanayotolewa na vyama vichache kuwa itumike nguvu ya umma kumuondoa Mheshimiwa Raisi Kikwete madarakani ni ya makundi ambayo yamepoteza muelekeo na sasa wanataka kulisambaratisha Taifa hili lenye utulivu na amani na kuliingiza kwenye vurumai lisilojulikana mwisho wake.
WaTanzania hao ambao wengi wao wanasema sisi ni wengi kuliko walioko kwenye hayo makundi wataonyesha ni namna gani nguvu za umma zinatumika kuhakikisha Raisi waliemchagua anaendelea kubaki kwenye madaraka kwani uhakika kuwa wingi wao ndio uliomueka madarakani upo palepale na ushindi uliopatikana sio wa kubabaisha au kupapasa ni ushindi uliotangazwa na tume na ambao ndio unaotakiwa uheshimiwe.
Sasa kutokea kwa vishambenga ambavyo vinajitutumua kwenye majukwaa kuwa peoples power itafanya kazi kumuondoa Kikwete madarakani ,wananchi hao walisisitiza madai yao kuwa wanawasuburi hao ambao watakuwa mstari wa mbele kuongoza nguvu za umma na wajiandae kukutana vilevile na nguvu za Umma upande wa Uraisi ,na wamesema watajuta kuzaliwa maana wao ni wengi sana na watakuwa hawana mswalie mtume ni kumlinda Kikwete tu mpaka kieleweke ,lakini hawatamuacha Raisi waliemchagua kuchezewa na watu wachache.