kmbwembwe
JF-Expert Member
- Aug 16, 2012
- 10,408
- 7,190
Yuda alisikitika yesu alipomwambia atamsaliti mara tatu kabla hapajakucha usiku ule alipotiwa mkononi mwa watesi wake.
Kwa imani ya kikristo Yesu ana umungu ndani yake kwa hiyo angeweza kumjua msaliti mapema. Kwa bahati mbaya viongozi wengi wema walisalitiwa na watu waliyowaamini kabisa na kuwafanya wasaidizi wao.
Lumumba aliyekua na msimamo madhubuti kwa faida ya watu wake alisalitiwa na joseph desire mobutu. Mtu huyo lumumba alipewa kiujasusi na wabeljiji awe karani na msaidizi wake wakati wa mazungumzo ya uhuru wa congo.
Thomas sankara alipinduliwa na kuuliwa na mtu wa karibu aliyeamini ni ndugu yake. Mtu huyo walilelewa pamoja kwenye familia moja baba yake thomas sankara akawaingiza jeshi pamoja.
Wafaransa walimtumia mtu huyo blaise compaoure kumtoa mwanamapinduzi sankara na kumuua. Kuna mifano mingi ya usaliti kusalitiwa wanamapinduzi afrika na watu wa karibu nao kwa tamaa binafsi au kutumiwa na adui wa maendeleo ya afrika.
Wanamapinduzi kote Afrika watashituka wakiona safu ya viongozi aliyoiacha Magufuli ikitimuliwa huku rushwa magendona dhuluma kwa wanyonge vikirejea.
Lazima mama atambue si kila biashara au wafanyabiashara wana faida kwa maendeleo ya nchi. Pia asisahau sisi tunajenga nchi ya ujamaa ndio maana amani imetamalaki.
Kwa imani ya kikristo Yesu ana umungu ndani yake kwa hiyo angeweza kumjua msaliti mapema. Kwa bahati mbaya viongozi wengi wema walisalitiwa na watu waliyowaamini kabisa na kuwafanya wasaidizi wao.
Lumumba aliyekua na msimamo madhubuti kwa faida ya watu wake alisalitiwa na joseph desire mobutu. Mtu huyo lumumba alipewa kiujasusi na wabeljiji awe karani na msaidizi wake wakati wa mazungumzo ya uhuru wa congo.
Thomas sankara alipinduliwa na kuuliwa na mtu wa karibu aliyeamini ni ndugu yake. Mtu huyo walilelewa pamoja kwenye familia moja baba yake thomas sankara akawaingiza jeshi pamoja.
Wafaransa walimtumia mtu huyo blaise compaoure kumtoa mwanamapinduzi sankara na kumuua. Kuna mifano mingi ya usaliti kusalitiwa wanamapinduzi afrika na watu wa karibu nao kwa tamaa binafsi au kutumiwa na adui wa maendeleo ya afrika.
Wanamapinduzi kote Afrika watashituka wakiona safu ya viongozi aliyoiacha Magufuli ikitimuliwa huku rushwa magendona dhuluma kwa wanyonge vikirejea.
Lazima mama atambue si kila biashara au wafanyabiashara wana faida kwa maendeleo ya nchi. Pia asisahau sisi tunajenga nchi ya ujamaa ndio maana amani imetamalaki.