Tutakuwa tunakosea kama tutampeleka mtu Ikulu kisa ni mwanamke au mwanaume

Shayu

Platinum Member
May 24, 2011
608
1,653
Kwa akili zetu tunatengeneza baadae ya taifa hili, ili ndio jambo la msingi tunalopaswa kulitambua, Baadae ya taifa hili itategemea mwelekeo wa fikra zetu. kila wakati lazima tutambue tutavuna tunachopanda. Mawazo yetu na fikra zetu ni mbegu. Na mwelekeo wa fikra zetu ndio utakaoamua destiny yetu. Haya mataifa ya ulaya hayakukua kwa bahati mbaya ni mipango na fikra zenye maono yaliyoongozwa vyema. Hakuna kitu kinachokuja kwa bahati mbaya vitu vyote tunavyoviona ni zao la fikra na maono ya watu.

Kwahiyo ili taifa liendelee inategemea ubora wa fikra za viongozi wake, hekima na busara zao. Kama tuna viongozi vipofu hawawezi kupeleka wananchi popote pale. Quality ya mawazo ya viongozi wetu ndio majaliwa yetu kama taifa. Nimekuwa nikiamini kila wakati hili taifa linauwezo wa kuwa taifa kubwa kama mataifa mengine lakini kama tukibadilisha fikra zetu. Na kikwazo kikubwa sana ni nature za viongozi wetu. Tuna tatizo tunapaswa kulitambua na wala sio kukataa kwamba halipo na msingi wake ni character za viongozi wanaotuongoza.

Mwalimu Nyerere alisema ili tuendelee tunahitaji watu, siasa safi, ardhi na uongozi bora. Na uongozi bora ni uongozi wenye maono. Kwahiyo tunakosa viongozi wenye maono na kwakuwa tunakosa viongozi wenye maono hatuwezi kupata siasa safi wala dira kwa taifa letu. Kwasababu tumekosa viongozi wenye maono wananchi na wenyewe wanakosa dira. Tuna viongozi wanaofikiri kuhusu leo na kushibisha matumbo yao hawafikirii zaidi ya leo. Hili ni tatizo kubwa. Tuna viongozi ambao wanaaminisha umma wachaguliwae kwasababu ni wanawake eti kwasababu pia hajawahi kuchaguliwa raisi mwanamke.

Kama ni hoja za namna hii viongozi wetu wanatoa tunajenga akili za wananchi wetu kuwa za namna gani? Kiongozi mzuri anajen ga wananchi wake kuwa wenye kufikiri. Kama taifa hatuwezi kuendelea kama tutakuwa na wananchi wasiofikiri sawa sawa. Tutakuwa tunakosea kama tutampeleka mtu ikulu sababu ni mwanamke au mwanamme. Tutakuwa sio watu wenye kufikiri. Taifa hili linahitaji binadamu mwenye maono, hekima na busara za kutuongoza, Mwenye falsafa nzuri.
 
Tutakuwa tunakosea kama tutampeleka mtu ikulu sababu ni mwanamke au mwanamme. Tutakuwa sio watu wenye kufikiri. Taifa hili linahitaji binadamu mwenye maono, hekima na busara za kutuongoza, Mwenye falsafa nzuri.
  1. Mkuu Shayu, kwanza naunga mkono hoja, ni kosa kumpeleka yoyote Ikulu yetu kwasababu ya jinsia yake, kwasababu kinachohitajika pale ikulu sio jinsia yake bali ni uwezo wake.
  2. Ni ukweli usiopingika, Tanzania na bara zima la Africa, tumeathiriwa na mfumo dume, "male chauvinism" ambao unawabagua wanawake wenye uwezo wa uongozi, kwasababu tuu ya jinsia yao ya kike.
  3. Hivyo pia ni kosa kutompeleka Ikulu rais mwanamke mwenye sifa na vigezo vyote, kisa ni mwanamke.
  4. Tanzania tuna Wanawake wengi tuu wenye uwezo wa urais yaani presidential materials lakini hawapewi nafasi kutokana na mfumo dume na hapa niliwataja baadhi Siku ya Wanawake Duniani: Je, tuna Wanawake wenye sifa za Presidential Material?
  5. Samia Suluhu Hassan ni mmoja wa wanawake hawa, pamoja na kuwa na sifa zote za urais, lakini kufuatia mfumo dume, hakuwahi kufikiriwa kusimamishwa kugombea urais kwasababu tuu ni mwanamke.
  6. Na hata baada ya kuwa Makamo wa Rais, kama JPM, asingeitwa na YEYE Mwenyewe, ile 2025, CCM isingemsimamisha Samia.
  7. Hivyo kwa sasa rais Samia ni rais wetu by default tuu kwa kudra za Mwenyeenzi Mungu, sasa 2025, tusisubirie kudra ndio zituamulie bali sasa 2025 tudhamirie kuachana na mfumo dume, tusimamushe mgombea mwanamke kwenye urais Watanzania, tuunge mkono 2025 ni zamu ya Mwanamke, ila sio lazima awe yeye bali yule aliyepangiwa na 'YEYE', kama ni yeye aliyepangiwa, then ni yeye!
  8. Mgombea mwanamke huyu, sio tumsimamishe kwasababu ya jinsia yake ya kike, no!, tumsimamishe kwasababu ya uwezo wake.
  9. Kwasababu sasa tayari tunaye rais mwanamke mwenye sifa na vigezo vyote na ameisha onyesha uwezo, then 2025, twende na Samia provided
  10. Kwasababu anayepanga nani awe rais wetu wa 2025 sio sisi bali ni YEYE Mpangaji, kama aliyempangia Samia ni YEYE, then 2025 ni Samia japo kuna akina sisi tulisikia sauti Voices From Within: Japo 2025 Tumepanga Twende na Mwanamke, Sauti Imeshauri Mama Amkabidhi Kwanza Dr. Mwinyi, Urais wa JMT, Ndipo Aje Mwanamke!
Paskali
 
Back
Top Bottom