Tutajifunza nini uchaguzi wa Afrika ya Kusini?

Mhache

JF-Expert Member
Jun 20, 2008
345
24
Dear all.

Ninaomba uppdates kwa yeyote mwenye data kuhusu uchaguzi wa Africa ya kusini. Je mnatarajia tutajifunza nini kutoka uchaguzi wa Afrika ya Kusini?
 
Kwamba Africa populism ni muhimu kuliko merit, track record na competence.

Kuona Mzee kama Mandela anaenda kumu endorse huyu fisadi Zuma ni hatari indeed.

Kudos Askofu Desmond Tutu kwa kubaki na principles regardless of the temptation.

South Africa wamepata Kikwete wao.
 
Kila niki-kopi na ku-paste updates JF inagoma...

Updates za uchaguzi zinapatikana kwenye tovuti hizi:

http://www.mg.co.za/

http://www.iol.co.za/

http://www.news24.com

Du hapa na kwa watani wetu vyama vya upinzani ndio vinalalamikia vote rigging ila naona huko Sauzi chama tawala ndio kinalalamika, kweli Zunami (Zuma Tsunami) inatisha mpaka wanataka kumwibia Msholozi kura - cheki http://www.mg.co.za/article/2009-04-22-anc-says-marked-ballot-papers-found-in-ulundi !

Wapinzani wa ANC hawatamsamehe Mbeki kwa kushindwa kumdhibiti Zuma hasa kwa kumpa JZ fursa ya kuwa karibu na watu wa chini na kujenga upopulisti wakati yeye Mbeki akiji-alienate na wananchi maskini na kukumbatia BEEs na wawekezaji - cheki http://www.mg.co.za/article/2009-04-09-how-zuma-became-mbeki !

Naona hata ANC nayo haitaki kumsamehe Mbeki kwa kuwavuruga - hebu cheki uchambuzi huu wa barua ya wazi ya Fikile Mbalula kwa Thabo Mbeki: http://pitsotsibs.blogspot.com/2009/04/fikile-mbalulas-letter-confirms-very.html
 
Last edited:
Nadhani tunachojifunza ni kuwa Waafrika bado tuna mawazo duni, ukabila udini na wakati mweingine ujinga ujinga tu!
Mzee Madiba kumpa tafu JZuma ni katika kupunguza speed ya kuvunjika kwa ANC, basically alishaona kuwa aking'ang'ania principle zake ANC itamegeka megeka, ingawa binafsi haafiki ya JZ, bado aliona ni lazima kumuunga mkono ili chama kiendelee kutawala na pia Sauzi kusijekuwa na machafuko ya aina yeyote.
Si mnakumbuka mzee JKambarage alivyompiga madongo ya nguvu Mzee Malecela baada ya kufahamu ni tishio wa changuzi lake?- Hizo ndo siasa za kiafrika! Na milele tutaendelea kuwa ombaomba na vidampa wa wazungu na wengineo, hadi hapo akili zetu zitakapo kaa sawa.
 
Back
Top Bottom