Mtalingolo
JF-Expert Member
- Aug 4, 2011
- 2,181
- 409
Upo na mkeo kwenye eneo la matanuzi, hapo mmeagizia pombe na mnasubiri msosi wanguvu mle muondoke nyumbani
Mazungumzo yenu hapo ni ya amani na vicheko kwa sana. Mara mgongeshane mikono, mara mpigane mabusu ya uhakika.
Wateja wengine wanawaangalia huku wakisema"Wale lazima watakuwa mahawara tu, mke na mume huwa hawana kawaida yakucheka na kupigana mabusu mbele ya watu"
Wewe unawasikia na unamwambia mkeo awasikilize kisha mnacheka sana maana kwenu kuoneshana upendo hadharani ni jambo la kawaida.
Mara inaingia meseji kwenye simu ya mkeo, lakini yeye badala ya kuisoma anaendelea kupiga domo na wewe, mwisho unamwambia "Dear, ungeisoma hiyo meseji pengine alietuma ana imejensi"
mkeo anasema hakuna wakumtumia imejensi yeyote, watu wasumbufu sana " Tena kama sio Mwajuma huyu atakua Nuru, maana hao ndio wanapenda sana kuchati, mi wananikera sana", mke anakwambia.
Mkeo anachukua simu yake na kuisoma meseji, ukimwangalia usoni kama anakasirika, lakini pia kama anataka kuachia tabasamu,
Mara anachanganya vidole kuandika meseji nyingine. Wewe unajua anajibu iliyoingia. Ile anaweka simu mezani tu anashika kichwa na kusema;
"Mama weee."
Kabla hujamuuliza nini kimempata, simu yako inaingia meseji, unaishika kuifungua unaona jina la mkeo, maana umemsevu 'MY WIFE.'
MY WIFE:"Tutachati baadae mpenzi wangu, niko na hili kubwa jinga. Lakini elewa nakupenda sana mwaaaaaa."
Je, kama wewe ungechukua uamuzi gani???...
Mazungumzo yenu hapo ni ya amani na vicheko kwa sana. Mara mgongeshane mikono, mara mpigane mabusu ya uhakika.
Wateja wengine wanawaangalia huku wakisema"Wale lazima watakuwa mahawara tu, mke na mume huwa hawana kawaida yakucheka na kupigana mabusu mbele ya watu"
Wewe unawasikia na unamwambia mkeo awasikilize kisha mnacheka sana maana kwenu kuoneshana upendo hadharani ni jambo la kawaida.
Mara inaingia meseji kwenye simu ya mkeo, lakini yeye badala ya kuisoma anaendelea kupiga domo na wewe, mwisho unamwambia "Dear, ungeisoma hiyo meseji pengine alietuma ana imejensi"
mkeo anasema hakuna wakumtumia imejensi yeyote, watu wasumbufu sana " Tena kama sio Mwajuma huyu atakua Nuru, maana hao ndio wanapenda sana kuchati, mi wananikera sana", mke anakwambia.
Mkeo anachukua simu yake na kuisoma meseji, ukimwangalia usoni kama anakasirika, lakini pia kama anataka kuachia tabasamu,
Mara anachanganya vidole kuandika meseji nyingine. Wewe unajua anajibu iliyoingia. Ile anaweka simu mezani tu anashika kichwa na kusema;
"Mama weee."
Kabla hujamuuliza nini kimempata, simu yako inaingia meseji, unaishika kuifungua unaona jina la mkeo, maana umemsevu 'MY WIFE.'
MY WIFE:"Tutachati baadae mpenzi wangu, niko na hili kubwa jinga. Lakini elewa nakupenda sana mwaaaaaa."
Je, kama wewe ungechukua uamuzi gani???...