Katibu mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo-CHADEMA Dr Wilbroad Slaa amesema chama chake kimeamua kupanga mikakati madhubuti ya kujiimarisha ndani ya chama.
Kiongozi huyo mashuhuri nchini aliyasema hayo alipokuwa akifungua mkutano wa baraza la Ushauri Mkoa wa Kagera lililofanyika Karagwe na kuhudhuriwa na viongozi wa majimbo yote ya mkoa wa Kagera.
Dr Slaa alisema moja ya mikakati ya chama chake ni kuajiri Makatibu wa Chama kote nchini.Pia Kiongozi huyo makini nchini alisema mikakati mingine ni kugawa Pikipiki kila Kata kwa ajili ya shughuli za chama na pia kujenga ofisi za kudumu kote nchini na zenye hadhi.
Kiongozi huyo anayetenda kwa mujibu wa maneno yake amewahakikishia viongozi hao wa chama kwamba atahakikisha mambo yote hayo yatasimamiwa kwa ukamilifu.
Source: Tanzania Daima
Kiongozi huyo mashuhuri nchini aliyasema hayo alipokuwa akifungua mkutano wa baraza la Ushauri Mkoa wa Kagera lililofanyika Karagwe na kuhudhuriwa na viongozi wa majimbo yote ya mkoa wa Kagera.
Dr Slaa alisema moja ya mikakati ya chama chake ni kuajiri Makatibu wa Chama kote nchini.Pia Kiongozi huyo makini nchini alisema mikakati mingine ni kugawa Pikipiki kila Kata kwa ajili ya shughuli za chama na pia kujenga ofisi za kudumu kote nchini na zenye hadhi.
Kiongozi huyo anayetenda kwa mujibu wa maneno yake amewahakikishia viongozi hao wa chama kwamba atahakikisha mambo yote hayo yatasimamiwa kwa ukamilifu.
Source: Tanzania Daima