TUT (TVT&RTD) kuonyesha mahojiano ya JK 00.01hrs EAT

Halisi

JF-Expert Member
Jan 16, 2007
2,802
613
Jamani TUT (TVT&RTD) leo usiku (kesho!!) wamesema wataonyesha mahojiano kati ya JK na waandishi jana IKULU, lakini naona kama wanaikebehi IKULU kwa kuwa wameambia wasitoe hadi tarehe 21 Desemba siku ya Ijumaa yaani siku ya kuadhimisha miaka miwili ya utawala wa JK.. Sasa kwani kama ni hivyo miaka miwili ilianza saa sita usiku? au ndio kama "Fataki" la mwaka mpya? Hii ya kusema watu wasubiri hadi siku hiyo wakati mahojiano yalifanyika jana, haina maana kabisa kwa Watanzania. Na nadhani wangefanya mfululizo kuanzia jana, leo na kesho kila TV/radio/gazeti likawa linatangaza ama kuandika litakavyo, ingekua na impact zaidi, lakini hili la kuzuia ni kali zaidi.
 
Jamani TUT (TVT&RTD) leo usiku (kesho!!) wamesema wataonyesha mahojiano kati ya JK na waandishi jana IKULU, lakini naona kama wanaikebehi IKULU kwa kuwa wameambia wasitoe hadi tarehe 21 Desemba siku ya Ijumaa yaani siku ya kuadhimisha miaka miwili ya utawala wa JK.. Sasa kwani kama ni hivyo miaka miwili ilianza saa sita usiku? au ndio kama "Fataki" la mwaka mpya? Hii ya kusema watu wasubiri hadi siku hiyo wakati mahojiano yalifanyika jana, haina maana kabisa kwa Watanzania. Na nadhani wangefanya mfululizo kuanzia jana, leo na kesho kila TV/radio/gazeti likawa linatangaza ama kuandika litakavyo, ingekua na impact zaidi, lakini hili la kuzuia ni kali zaidi.

Siku 100 Za Kikwete zilitangazwa kwa nderemo na vifijo na wiki moja kabla tayari mapambio yaliashaanza. Mwaka mmoja wa Kikwete nao kadhalika, huku kila wizara ikijivunia mafanikio. Na mjadala ulianza wiki ziadi ya moja. Ni wazi mafanikio yalikuwa ni ya kawaida sana tofauti ya matarajio waliyoahidi kwa wananchi. Miaka miwili ya JK, imefika kimya kimya. Kwa maoni yangu, si wakosoaji ama wapongezaji- wote tumeshindwa kutimiza wajibu vya kutosha kuichambua kwa kina hii miaka na kutoa mchango wa mapendekezo ya mwelekeo. Lakini hatujachelewa, wapo walioanza kidogo kuanzia wiki iliyopita; wengi watasema leo. Na najua baada ya hapo mjadala utafuata. Leo, saa 3 unusu kama ratiba itakwenda kama ilivyopangwa yatarushwa mahojiano ya TVT This Week in perspective kati yangu, Tendwa, Mpenda na Mwamunyage kuhusu Kura za Maoni za REDET- yatakuwa katika Lugha ya Kiingereza. Katika mahojiano hayo(kama yatakuwa hayajahaririwa) nimemsihi Rais avunje Baraza la Mawaziri(kama sehemu ya kuamsha ari, nguvu na kasi mpya kuelekea mwaka wa tatu wa uongozi wake). Lakini naona ujumbe wangu wangu umechelewa kufika, tayari Rais wetu ameweka msimamo.


JJ
 
yatarushwa mahojiano ya TVT This Week in perspective kati yangu, Tendwa, Mpenda na Mwamunyage kuhusu Kura za Maoni za REDET- yatakuwa katika Lugha ya Kiingereza.

JJ

...acheni kuchekesha nyie,nchi ya watu milioni 40 huku 99.999..% wanaongea kiswahili tuu,sijui mnataka kumfkia nani na nina uhakika hata sisi tukiyaona hatutaelewa maana najua ni shitty English with crappy accent...how convenient!
 
...acheni kuchekesha nyie,nchi ya watu milioni 40 huku 99.999..% wanaongea kiswahili tuu,sijui mnataka kumfkia nani na nina uhakika hata sisi tukiyaona hatutaelewa maana najua ni shitty English with crappy accent...how convenient!

Koba:

Nakubaliana nawe kabisa. Lakini kama jina lenyewe la kipindi kilivyo ni kipindi cha kiingereza. Nadhani ni moja ya vipindi vichache vya TVT vya ndani vinavyoendeshwa kwa lugha hiyo. Labda ni kipindi maalum chenye kulenga hadhira yenye kuzungumza lugha hiyo ama watanzania wenye kufahamu kizungu. Ningefurahi zaidi kama ningealikwa katika kipindi cha "TUAMBIE".

Lakini natumai wapo watakao elewa hicho kingereza mbovu mbovu na ujumbe utafika kwao. PK!

JJ
 
hapo mkuu i was trying to deliver the message in a funny way at your expense,glad you didnt take it personally...happy holiday from US!
 
hapo mkuu i was trying to deliver the message in a funny way at your expense,glad you didnt take it personally...happy holiday from US!

Usijali, wala sikuchulia binafsi. Ndio maana nimekwambia Pasua Kicheko(PK).

Eid Mubarak, Merry X-Mas and Happy New Year.

JJ
 
Koba, ujumbe wako naona una dalili za chuki kuliko hoja. Are sure we are 99.99% kiswahili literacy ? What do you mean by "shitty English" ? Does a Nigerian, Chinese, Russian, Arabs speaks better English the British themselves ?

Jenga hoja achana na chuki.

Hicho kipindi hakikuanza leo, kipo kila week, na kinatumia English, why "crappy anccent" now ? Is it because JJ is from Chadema ?
 
Koba, ujumbe wako naona una dalili za chuki kuliko hoja. Are sure we are 99.99% kiswahili literacy ? What do you mean by "shitty English" ? Does a Nigerian, Chinese, Russian, Arabs speaks better English the British themselves ?

Jenga hoja achana na chuki.

Hicho kipindi hakikuanza leo, kipo kila week, na kinatumia English, why "crappy anccent" now ? Is it because JJ is from Chadema ?


Jafar

Nilichokubaliana na Koba sio maneno na takwimu zake, ni dhana ya alichokisema kwamba kwanini katika taifa ambalo watu wengi wanazungumza kiswahili tuendeshe kipindi kwa kiingereza? Nadhani ufafanuzi wangu ulisaidia kumwelewesha. Hilo la maneno na takwimu alizotumia linahitaji mjadala. Endelea.

Ila nimtetee tu- katika ujumbe wake hakunilenga mimi kama mimi(kwa kuwa naamini hajawahi kunisikia nikizungumza kiingereza, na ni vyema akanisikiliza usiku wa leo- sijui kama Jump TV wanaweza kuwa na link!); yeye alizungumza kiujumla nami nikamjibu kiujumla tu- kwa maana ya wazungumzaji wote.

There was nothing personal!

BTW: Natamani lafudhi ya kisukuma ingekuwa imeniingia mpaka kwenye kiswahili na kiingereza changu. Ingekuwa rahisi sana kuonyesha msisitizo. Sisi wasukuma huongea kwa mkazo na uzito(MZAHA)



JJ
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom