Muke Ya Muzungu
JF-Expert Member
- Jun 17, 2009
- 3,444
- 264
Ndugu zangu watanzania, kama mnavyofahamu, NEC ilipoona mwelekeo wa matokeo ya Urais, mara moja walibadilisha kibao na kuanza kutangaza wenyewe toka makao makuu na siyo jimboni tena. Hii inamaanisha yakwamba wanalo lao jambo
Sisi wapiga kura tena walipa kodi kwa miaka zaidi ya 40 sauti zetu zimekuwa hazina maana, na hata kodi zetu kutumiwa vibaya na wakina Kikwete na familia zao. Kura zetu haziwezi kuchezewa tena. Kura lazima zitangazwe kwenye kila jimbo au kituo cha kupigia kura na hata NEC wakiyatangaza, yawe ni yale yale vinginevyo hatutavumilia na tutasusia hadi uchaguzi mwingine wa Rais ufanyike
Tumechoka kuburuzwa na kundi la kikwete, tumechoka naye na uvumilivu wetu umefika mwisho. Tupo tayari kujitoa mhanga ili watoto wetu wawe na maisha ya baadae. Waniue lakini msimamo wangu hautabadilika. Shida niliyonayo, ni heri nife kuliko kuona uhuru wangu na haki yangu ya msingi inachezewa na wakina Ridhiwani wakiendesha magari ya kifahari
Sisi wapiga kura tena walipa kodi kwa miaka zaidi ya 40 sauti zetu zimekuwa hazina maana, na hata kodi zetu kutumiwa vibaya na wakina Kikwete na familia zao. Kura zetu haziwezi kuchezewa tena. Kura lazima zitangazwe kwenye kila jimbo au kituo cha kupigia kura na hata NEC wakiyatangaza, yawe ni yale yale vinginevyo hatutavumilia na tutasusia hadi uchaguzi mwingine wa Rais ufanyike
Tumechoka kuburuzwa na kundi la kikwete, tumechoka naye na uvumilivu wetu umefika mwisho. Tupo tayari kujitoa mhanga ili watoto wetu wawe na maisha ya baadae. Waniue lakini msimamo wangu hautabadilika. Shida niliyonayo, ni heri nife kuliko kuona uhuru wangu na haki yangu ya msingi inachezewa na wakina Ridhiwani wakiendesha magari ya kifahari