Elections 2010 Tususie Matokeo Ya Uchaguzi

Muke Ya Muzungu

JF-Expert Member
Jun 17, 2009
3,444
264
Ndugu zangu watanzania, kama mnavyofahamu, NEC ilipoona mwelekeo wa matokeo ya Urais, mara moja walibadilisha kibao na kuanza kutangaza wenyewe toka makao makuu na siyo jimboni tena. Hii inamaanisha yakwamba wanalo lao jambo

Sisi wapiga kura tena walipa kodi kwa miaka zaidi ya 40 sauti zetu zimekuwa hazina maana, na hata kodi zetu kutumiwa vibaya na wakina Kikwete na familia zao. Kura zetu haziwezi kuchezewa tena. Kura lazima zitangazwe kwenye kila jimbo au kituo cha kupigia kura na hata NEC wakiyatangaza, yawe ni yale yale vinginevyo hatutavumilia na tutasusia hadi uchaguzi mwingine wa Rais ufanyike

Tumechoka kuburuzwa na kundi la kikwete, tumechoka naye na uvumilivu wetu umefika mwisho. Tupo tayari kujitoa mhanga ili watoto wetu wawe na maisha ya baadae. Waniue lakini msimamo wangu hautabadilika. Shida niliyonayo, ni heri nife kuliko kuona uhuru wangu na haki yangu ya msingi inachezewa na wakina Ridhiwani wakiendesha magari ya kifahari
 
Shida yako ni Demokrasia au kuona Ridhwani akipanda dala dala. Kwa hali ilivyo popote ambapo matokeo yatatangazwa JK ataibuka kidedea. Mpaka sasa maximum number of seats kwenda Chadema ni 20. Wabunge wa upinzani hawatazidi 35 kwenye bunge lenye wabunge over 250. So where is your hope?
 
Shida yako ni Demokrasia au kuona Ridhwani akipanda dala dala. Kwa hali ilivyo popote ambapo matokeo yatatangazwa JK ataibuka kidedea. Mpaka sasa maximum number of seats kwenda Chadema ni 20. Wabunge wa upinzani hawatazidi 35 kwenye bunge lenye wabunge over 250. So where is your hope?

Endelea kuota
 
Wee the Good

Unasemaje 35, wakati CUF peke yao wanao 22?

Kama 5 wa CHADEMA walifanya vizuri, 35 je?
 
Mimi nilikwisha sema si tu kwa ajili ya kutotoa matokeo ya tume lakini hata la kuzuia wapiga kura vituoni kwa ubabaishaji!!!!!!!!
 
Ndugu zangu watanzania, kama mnavyofahamu, NEC ilipoona mwelekeo wa matokeo ya Urais, mara moja walibadilisha kibao na kuanza kutangaza wenyewe toka makao makuu na siyo jimboni tena. Hii inamaanisha yakwamba wanalo lao jambo

Sisi wapiga kura tena walipa kodi kwa miaka zaidi ya 40 sauti zetu zimekuwa hazina maana, na hata kodi zetu kutumiwa vibaya na wakina Kikwete na familia zao. Kura zetu haziwezi kuchezewa tena. Kura lazima zitangazwe kwenye kila jimbo au kituo cha kupigia kura na hata NEC wakiyatangaza, yawe ni yale yale vinginevyo hatutavumilia na tutasusia hadi uchaguzi mwingine wa Rais ufanyike

Tumechoka kuburuzwa na kundi la kikwete, tumechoka naye na uvumilivu wetu umefika mwisho. Tupo tayari kujitoa mhanga ili watoto wetu wawe na maisha ya baadae. Waniue lakini msimamo wangu hautabadilika. Shida niliyonayo, ni heri nife kuliko kuona uhuru wangu na haki yangu ya msingi inachezewa na wakina Ridhiwani wakiendesha magari ya kifahari

sawa kabisa.Mpaka sasa sijaiona mantiki ya kupoteza fedha nyingi kwenye uchaguzi ikiwa maamuzi ya wananchi hayaheshimiwi.Hivi kwani wao ni nani hata watuburuze kiasi hiki?kwa nini watanzania tunakosa ujasiri wa kupambana na hawa mafirauni?Watz wenzangu,muda wa kuwaachia watuburuze umekwisha sasa,tuondoe woga tupambane nao,SHIME WATz tupiganie haki yetu!
 
MGsalon nakubaliana nawewe 101%. Ushindi wetu hautaletwa na mafisadi bali sisi wenyewe kwa kujitoa muhanga. Twende mbele na kudai haki yetu. Tusikubali kuibiwa kura kirahisi
 
Shida yako ni Demokrasia au kuona Ridhwani akipanda dala dala. Kwa hali ilivyo popote ambapo matokeo yatatangazwa JK ataibuka kidedea. Mpaka sasa maximum number of seats kwenda Chadema ni 20. Wabunge wa upinzani hawatazidi 35 kwenye bunge lenye wabunge over 250. So where is your hope?[/QUOTE

Hadi sasa
1-CHADEMA-20
2-NCCR MAGEUZI 3
CUF-23 na bado wataongezeka ukichangnya na viti maalum bunge lijalo litawaka moto
 
Shida yako ni Demokrasia au kuona Ridhwani akipanda dala dala. Kwa hali ilivyo popote ambapo matokeo yatatangazwa JK ataibuka kidedea. Mpaka sasa maximum number of seats kwenda Chadema ni 20. Wabunge wa upinzani hawatazidi 35 kwenye bunge lenye wabunge over 250. So where is your hope?

WRONG BROTHER!! what about the 18 CUF seats in Zanzibar and already TLP and NCCR-MAGEUZI each has one seat? It's coming to 40 and we count on some more!!!!!

Mind you, if the 5 MPs from CHADEMA caused that much HAVOC in the parliament, what about 50 more? SASA BUNGE LITANYOKA!!!!
 
Tumechoka kuburuzwa na kundi la kikwete, tumechoka naye na uvumilivu wetu umefika mwisho. Tupo tayari kujitoa mhanga ili watoto wetu wawe na maisha ya baadae. Waniue lakini msimamo wangu hautabadilika. Shida niliyonayo, ni heri nife kuliko kuona uhuru wangu na haki yangu ya msingi inachezewa na wakina Ridhiwani wakiendesha magari ya kifahari

Tatizo hapa ni utekelezaji wake.......

Jk na CCM yake wakishakutangazwa wao wanaendelea na kuchapa kazi kama waonavyo yafaa...........sasa utasusa vipi?
Labda uende mahakamani kupinga matokeo vinginevyo ni kujipanga upya kudai demokrasia tu................
 
Back
Top Bottom