Vato
JF-Expert Member
- Feb 15, 2009
- 249
- 139
Watanzania tunapenda sana kulalamika na kulaani bila kuchukua hatua.Hatuna courage na audacity ya kwenda step moja mbele na ku act badala ya kulalamika tu miaka nenda miaka nenda rudi. Ukimya na Uoga wetu huu ndio sababu kubwa zinazoifanya serikali ya CCM inakiburi, ina jeuri na dharau kwetu..ni ukosefu wetu wa uthubutu wa kuihoji na kuikaripia serikali ndio maana tuliambiwa mtakula hata nyasi ikibidi, lakini ndege ya rais itanunuliwa, ndio maana tuliambiwa pigeni hata mbizi mwende kigamboni kama ongezeko la nauli ya kivuko mnaona ni kubwa...viongozi wanatoa wapi huu ujasiri wa kutukashifu kama asante ya sisi kuwapa ridhaa ya kutuongoza???!!! ni kwasababu tunaogopa, hata nmaandamano yakiitishwa hatuendi, utamkuta mtu mzima kabisa anasema "nani anataka kupigwa mabomu ya machozi", anaogopa ku risk maisha yake ili atetee maslahi mapana ya kizazi hiki na zaidi kizazi kijacho.
Jana serikali kwa makusudi kabisa imewasilisha bungeni bajeti ambayo itamzidishia maskini ugumu wa maisha mara dufu...gawio la fedha kwenye sekta inayoajiri zaidi ya asilimia 50 ya watanzania wote, Kilimo, limepungua kwa kiasi kikubwa. Serikali badala ya kubuni vyanzo vipya vya mapato kila mwaka inapandisha kodi katika bidhaa na huduma zile zile, kila mwaka wa fedha utasikia sigara, bia, soda, vinywaji vikali bei juu, kila mwaka lazima bidhaa hizi zichajiwe kodi...na mwaka huu na vocha nazo zinapigwa kodi kwanzia Jully...tunaelekea wapi sasa?? makato yote haya ya kodi mwisho wa siku yanageuka kuwa mzigo mzito mabegani mwa watanzania maskini..ndio maana yake!!! kwanini serikali haibuni vyanzo vipya endelevu vya mapato???? kama hakuna wataalamu wanaoweza kufanya hiyo kazi si wawaajiri washauri elekezi/ consultants kutoka kwenye makampuni ya kimataifa ya ushauri wa mambo ya uchumi na fedha wawasaidie kubuni vyanzo vipya vya mapato??? hapa Tanzania kodi nyingi wanalipa Maskini na Middle class, makampuni makubwa kwenye sekta kama madini na huduma/ tertiary sector, na matajiri wanalipa kodi kidogo mno serikalini!!!! they do not pay their fair share of tax to tax authorities. Hivi katika kudhihirisha kuwa tumechoshwa na hii serikali mbovu isiyotujali watu wake kwanini tusisusie huu mchakato wa Sensa kama walivyofanya ndugu zetu waislamu kupitia BAKWATA??? tuususie huu mchakato wa sensa kuishinikiza serikali isikilize vilio vyetu tunavyovitoa kupitia NGOs na vyama vya siasa kama CHADEMA nk..kwanzia kwenye ile sheria ya marekebisho ya katiba, huduma mbovu za kijamii hasa afya na elimu, ufisadi uliokithiri serikalini, kupanda kwa gharama za umeme, nk..tususie huu mchakato kama taifa kila mmoja kwa wakati wake...tutumie mitandao ya kijamii kuhamasishana kuususia huu mchakato...ni wajibu wetu kama kizazi kuitaka serikali iwajibike, kuitaka serikali ifanye mabaddiliko ya kiutendaji ili iweze kuwatumikia wananchi vizuri, huu wajibu tusipoutekeleza leo vizazi vijavyo vitatudharau...alisema Frantz Fanon kuwa, EACH GENERATION MUST OUT OF RELATIVE OBSCURITY DISCOVER ITS MISSION, FULLFILL IT OR BETRAY IT..kinachotokea hapa Tanzania ni kwamba tupo katika juhudi za makusudi kabisa za kujitahidid kama taifa kutokutekeleza wajibu wetu wa kufanya mabadiliko, wajibu wa kuiwajibisha serikali ingawa hali halisi inatupa sababu ya kufanya hivyo...
Jana serikali kwa makusudi kabisa imewasilisha bungeni bajeti ambayo itamzidishia maskini ugumu wa maisha mara dufu...gawio la fedha kwenye sekta inayoajiri zaidi ya asilimia 50 ya watanzania wote, Kilimo, limepungua kwa kiasi kikubwa. Serikali badala ya kubuni vyanzo vipya vya mapato kila mwaka inapandisha kodi katika bidhaa na huduma zile zile, kila mwaka wa fedha utasikia sigara, bia, soda, vinywaji vikali bei juu, kila mwaka lazima bidhaa hizi zichajiwe kodi...na mwaka huu na vocha nazo zinapigwa kodi kwanzia Jully...tunaelekea wapi sasa?? makato yote haya ya kodi mwisho wa siku yanageuka kuwa mzigo mzito mabegani mwa watanzania maskini..ndio maana yake!!! kwanini serikali haibuni vyanzo vipya endelevu vya mapato???? kama hakuna wataalamu wanaoweza kufanya hiyo kazi si wawaajiri washauri elekezi/ consultants kutoka kwenye makampuni ya kimataifa ya ushauri wa mambo ya uchumi na fedha wawasaidie kubuni vyanzo vipya vya mapato??? hapa Tanzania kodi nyingi wanalipa Maskini na Middle class, makampuni makubwa kwenye sekta kama madini na huduma/ tertiary sector, na matajiri wanalipa kodi kidogo mno serikalini!!!! they do not pay their fair share of tax to tax authorities. Hivi katika kudhihirisha kuwa tumechoshwa na hii serikali mbovu isiyotujali watu wake kwanini tusisusie huu mchakato wa Sensa kama walivyofanya ndugu zetu waislamu kupitia BAKWATA??? tuususie huu mchakato wa sensa kuishinikiza serikali isikilize vilio vyetu tunavyovitoa kupitia NGOs na vyama vya siasa kama CHADEMA nk..kwanzia kwenye ile sheria ya marekebisho ya katiba, huduma mbovu za kijamii hasa afya na elimu, ufisadi uliokithiri serikalini, kupanda kwa gharama za umeme, nk..tususie huu mchakato kama taifa kila mmoja kwa wakati wake...tutumie mitandao ya kijamii kuhamasishana kuususia huu mchakato...ni wajibu wetu kama kizazi kuitaka serikali iwajibike, kuitaka serikali ifanye mabaddiliko ya kiutendaji ili iweze kuwatumikia wananchi vizuri, huu wajibu tusipoutekeleza leo vizazi vijavyo vitatudharau...alisema Frantz Fanon kuwa, EACH GENERATION MUST OUT OF RELATIVE OBSCURITY DISCOVER ITS MISSION, FULLFILL IT OR BETRAY IT..kinachotokea hapa Tanzania ni kwamba tupo katika juhudi za makusudi kabisa za kujitahidid kama taifa kutokutekeleza wajibu wetu wa kufanya mabadiliko, wajibu wa kuiwajibisha serikali ingawa hali halisi inatupa sababu ya kufanya hivyo...