Tusiwajadili Watu Binafsi, Tujadili Hoja na Madai ya Msingi kwa Taifa

Gwappo Mwakatobe

JF-Expert Member
Nov 22, 2019
1,494
1,874
Kwanza, katiba ya nchi inatoa haki na uhuru wa kutoa maoni yoyote kwa jambo au mtu yeyote ilimradi yasivunje sheria zilizopo. Polepole, Bulembo, Nape, nk.; wote wana haki hiyo.

Pili, si jambo la ajabu na wala si geni kwa wana CCM kutofautiana na kulumbana. CCM ni taasisi kubwa yenye watu wengi ambao si rahisi wote wawe na mtazamo na msimamo mmoja. Wanapishana makanisani na misikitini kwa watu wenye Imani moja, na pengine Bwana mmoja na Ubatizo mmoja, sembuse wanasiasa kwenye vyama vyao?!

Tatu, tusiache kujadili hoja muhimu za kubadili na/au kuboresha mifumo yetu yenye maslahi mapana kwa taifa, kama vile madai ya katiba mpya na maudhui yake, na kuanza kuwajadili watu binafsi kama akina Polepole. Tunapotea na kupoteza muda!
 
Nchi yetu inahitaji reforms nyingi ikiwemo kwenye Sheria za nchi(katiba), Vyama vya siasa, Government machinery (mf tiss,) etc. Lakini muhimu zaidi before that ni mageuzi juu ya Civilization ya watu wetu, Hii ndio Underlying Basis ya kwanza kwa taifa ku'make Progress. Si rahisi hata kidogo kufanikisha hayo
 
Kwanza, katiba ya nchi inatoa haki na uhuru wa kutoa maoni yoyote kwa jambo au mtu yeyote ilimradi yasivunje sheria zilizopo. Polepole, Bulembo, Nape, nk.; wote wana haki hiyo.

Pili, si jambo la ajabu na wala si geni kwa wana CCM kutofautiana na kulumbana. CCM ni taasisi kubwa yenye watu wengi ambao si rahisi wote wawe na mtazamo na msimamo mmoja. Wanapishana makanisani na misikitini kwa watu wenye Imani moja, na pengine Bwana mmoja na Ubatizo mmoja, sembuse wanasiasa kwenye vyama vyao?!

Tatu, tusiache kujadili hoja muhimu za kubadili na/au kuboresha mifumo yetu yenye maslahi mapana kwa taifa, kama vile madai ya katiba mpya na maudhui yake, na kuanza kuwajadili watu binafsi kama akina Polepole. Tunapotea na kupoteza muda!
Ila pia muda wakuwanyoosha wale wanaopondisha au waliopindisha maslahi mapana ya taifa tuwe na muda huo pia Kwani ujumbe kama huo unaleta hamasa kwa maeneo mengine muhimu kama katiba mpya ambayo ita yarekebisha yanayopindishwa na walionanafasi ya kufanya hivyo Kwa maslahi Yao na yawachache.
 
Nchi yetu inahitaji reforms nyingi ikiwemo kwenye Sheria za nchi(katiba), Vyama vya siasa, Government machinery (mf tiss,) etc. Lakini muhimu zaidi before that ni mageuzi juu ya Civilization ya watu wetu, Hii ndio Underlying Basis ya kwanza kwa taifa ku'make Progress. Si rahisi hata kidogo kufanikisha hayo
Naam!
 
Nchi yetu inahitaji reforms nyingi ikiwemo kwenye Sheria za nchi(katiba), Vyama vya siasa, Government machinery (mf tiss,) etc. Lakini muhimu zaidi before that ni mageuzi juu ya Civilization ya watu wetu, Hii ndio Underlying Basis ya kwanza kwa taifa ku'make Progress. Si rahisi hata kidogo kufanikisha hayo
Kwa Mtanzania kwenye hapo civilization tumelemaa kabisa, miongoni mwa mengine, tabia ya uvivu, ukosefu wa uaminifu, kutopenda fuata taratibu, uzembe, rushwa,wizi kwa walioaminiwa na kupewa mafasi kuwahudumia watanzania, Kila baya kumkosa mbongo hajapata TU nafasi mpe nafasi utaijua tabia yake
 
Kwa Mtanzania kwenye hapo civilization tumelemaa kabisa, miongoni mwa mengine, tabia ya uvivu, ukosefu wa uaminifu, kutopenda fuata taratibu, uzembe, rushwa,wizi kwa walioaminiwa na kupewa mafasi kuwahudumia watanzania, Kila baya kumkosa mbongo hajapata TU nafasi mpe nafasi utaijua tabia yake
Umenena ya uhakika. Tunajiroga wenyewe na kwahiyo lazima tuanze kujiganga wenyewe, mmoja mmoja, kidogo kidogo, mpaka tubadilike kifikra na kimtazamo.
 
Back
Top Bottom