Tusisherehekee Uhuru kwa kurusha tu ndege za kivita na kuvunja matofali

Keynez

JF-Expert Member
Feb 12, 2007
2,397
3,884
Wakuu, nawasalimu kwa jina la Bwana wa Majeshi.

Wote tunajua jinsi uhuru wa Tanganyika ulivyopatikana. Kwa kifupi ulipatikana kwa njia za majadiliano na diplomasia.

Ningependa sana kuona kila tunapokaa kusherehekea uhuru wetu, tukumbushane jinsi gani majadiliano, ustaarabu na diplomasia inavyoweza kuwa chachu ya kuimarisha uhuru wetu na kutuletea maendeleo.

Kuna kirusi kimeingia katika fikra za uongozi nchi hii zinazofanya viongozi wawe watawala. Wananchi hawasikilizwi tena wanataka nini, amri zimetawala na maamuzi ya hovyo yanafanyika na hakuna kuwajibishana.

Kutishana kumezidi sana nchi hii. Hakuna kati yetu mwenye milki ya nchi hii, haijalishi tofauti zetu za kisiasa, kiimani, kikabila wala kipato.

Turudi kwenye kusikilizana na tutoke kwenye kuumizana. Hapo ndiyo uhuru wa nchi hii utakuwa na maana kwa kila mmoja wetu.
 
Pia watuoneshe hatua tulizopiga kimaendeleo, elimu, afya, kilimo n.k tangu tupate uhuru.

Je, tunasonga mbele au tunarudi nyuma? Kama tunasonga mbele-spidi inatosha au ingezwe na kwa namna gani.

Kama hatujapiga hatua, nani wa kuwajibishwa?
 
Wakuu, nawasalimu kwa jina la Bwana wa Majeshi.

Wote tunajua jinsi uhuru wa Tanganyika ulivyopatikana. Kwa kifupi ulipatikana kwa njia za majadiliano na diplomasia.

Ningependa sana kuona kila tunapokaa kusherehekea uhuru wetu, tukumbushane jinsi gani majadiliano, ustaarabu na diplomasia inavyoweza kuwa chachu ya kuimarisha uhuru wetu na kutuletea maendeleo.

Kuna kirusi kimeingia katika fikra za uongozi nchi hii zinazofanya viongozi wawe watawala. Wananchi hawasikilizwi tena wanataka nini, amri zimetawala na maamuzi ya hovyo yanafanyika na hakuna kuwajibishana.

Kutishana kumezidi sana nchi hii. Hakuna kati yetu mwenye milki ya nchi hii, haijalishi tofauti zetu za kisiasa, kiimani, kikabila wala kipato.

Turudi kwenye kusikilizana na tutoke kwenye kuumizana. Hapo ndiyo uhuru wa nchi hii utakuwa na maana kwa kila mmoja wetu.
Utawala ni mbovu haswa tena haswa ni aibu tupu
 
Pia watuoneshe hatua tulizopiga kimaendeleo, elimu, afya, kilimo n.k tangu tupate uhuru.

Je, tunasonga mbele au tunarudi nyuma? Kama tunasonga mbele-spidi inatosha au ingezwe na kwa namna gani.

Kama hatujapiga hatua, nani wa kuwajibishwa?
Tatizo tuna viongozi walioingia madarakani bila kuchaguliwa na wananchi, awamu ya tano na ya sita ni serikali haramu
 
Wakuu, nawasalimu kwa jina la Bwana wa Majeshi.

Wote tunajua jinsi uhuru wa Tanganyika ulivyopatikana. Kwa kifupi ulipatikana kwa njia za majadiliano na diplomasia.

Ningependa sana kuona kila tunapokaa kusherehekea uhuru wetu, tukumbushane jinsi gani majadiliano, ustaarabu na diplomasia inavyoweza kuwa chachu ya kuimarisha uhuru wetu na kutuletea maendeleo.

Kuna kirusi kimeingia katika fikra za uongozi nchi hii zinazofanya viongozi wawe watawala. Wananchi hawasikilizwi tena wanataka nini, amri zimetawala na maamuzi ya hovyo yanafanyika na hakuna kuwajibishana.

Kutishana kumezidi sana nchi hii. Hakuna kati yetu mwenye milki ya nchi hii, haijalishi tofauti zetu za kisiasa, kiimani, kikabila wala kipato.

Turudi kwenye kusikilizana na tutoke kwenye kuumizana. Hapo ndiyo uhuru wa nchi hii utakuwa na maana kwa kila mmoja wetu.
Hakuna cha kusherehekea hapa. Ni masikitiko tu. Kama katika sherehe hizo wataeleza mazuri vs mabaya mizani upande wa mabaya itashinda kwa mara 1000.
 
Wakuu, nawasalimu kwa jina la Bwana wa Majeshi.

Wote tunajua jinsi uhuru wa Tanganyika ulivyopatikana. Kwa kifupi ulipatikana kwa njia za majadiliano na diplomasia.

Ningependa sana kuona kila tunapokaa kusherehekea uhuru wetu, tukumbushane jinsi gani majadiliano, ustaarabu na diplomasia inavyoweza kuwa chachu ya kuimarisha uhuru wetu na kutuletea maendeleo.

Kuna kirusi kimeingia katika fikra za uongozi nchi hii zinazofanya viongozi wawe watawala. Wananchi hawasikilizwi tena wanataka nini, amri zimetawala na maamuzi ya hovyo yanafanyika na hakuna kuwajibishana.

Kutishana kumezidi sana nchi hii. Hakuna kati yetu mwenye milki ya nchi hii, haijalishi tofauti zetu za kisiasa, kiimani, kikabila wala kipato.

Turudi kwenye kusikilizana na tutoke kwenye kuumizana. Hapo ndiyo uhuru wa nchi hii utakuwa na maana kwa kila mmoja wetu.
Aisee tumefanya mazoezi ya kutosha ya kuvunja vitofa hadi kwa shingo kwa hilo utatusamehe hakuna namba, na.hata kurusha majabari tiara angani tuko tayari.

Sent from my SM-G9350 using JamiiForums mobile app
 
Tusherekee na mfumo wa Makaburu kubaguana uongozi kwa vyama, kubambikiana kesi.
 
Back
Top Bottom