GENTAMYCINE
JF-Expert Member
- Jul 13, 2013
- 56,544
- 108,865
Wana Yanga SC wenzangu wala tusishangalie sana kwani kumbe tunacheza na Zesco B ( Kikosi cha Pili ) cha Zesco na cha Kushangaza bado wanatusumbua tu na haka ' Kagoli ' ketu Kamoja ka Kupewa na Mwamuzi. Wana Yanga SC Wenzangu tusikubali Kuyumbishwa na hawa Viongozi wetu kwani hawana la maana zaidi tu ya Kuwahonga Waamuzi ili Yanga SC ishinde lakini ukweli ni kwamba hatuna Timu ya Kufika mbali.
Kwa mfano Mimi sioni kwanini Yanga SC imesajili hawa Wachezaji wabaya kama akina Sibomana, Balinya, Balama, Lamine na Tshishimbi ambao ndiyo wanaongoza kwa Kucheza vibaya dhidi ya Zesco United leo. Hawa Wachezaji waondoke na kama Yanga SC tutaweza basi tuwaombe Simba SC baadhi ya Wachezaji wao ili watusaidie na tutafika mbali.
Wana Yanga SC tusiukubali huu Uongozi wa sasa kwani hauna Malengo mema na Timu yetu na nasikia wote kumbe ni Simba na mara nyingi sana huwa wanakuwa na Viongozi wa Simba SC hapa mjini. Na kama tutaendelea Kuwa nao hawa hadi January 2020 pale tutakapokuwa tunacheza na Simba SC basi natabiri tunaweza Kufungwa Goli 7 au hata 9 kwani hawa Viongozi watakuwa ' Wametuuza ' kwa Simba SC ambao ndiko Wanakokushabikia tokea walipokuwa Watoto.
Msipokubaliana na Mimi mwana Yanga SC mwenzenu An Eagle basi nahama Yanga SC na naenda Simba SC kwa Hasira.
Kwa mfano Mimi sioni kwanini Yanga SC imesajili hawa Wachezaji wabaya kama akina Sibomana, Balinya, Balama, Lamine na Tshishimbi ambao ndiyo wanaongoza kwa Kucheza vibaya dhidi ya Zesco United leo. Hawa Wachezaji waondoke na kama Yanga SC tutaweza basi tuwaombe Simba SC baadhi ya Wachezaji wao ili watusaidie na tutafika mbali.
Wana Yanga SC tusiukubali huu Uongozi wa sasa kwani hauna Malengo mema na Timu yetu na nasikia wote kumbe ni Simba na mara nyingi sana huwa wanakuwa na Viongozi wa Simba SC hapa mjini. Na kama tutaendelea Kuwa nao hawa hadi January 2020 pale tutakapokuwa tunacheza na Simba SC basi natabiri tunaweza Kufungwa Goli 7 au hata 9 kwani hawa Viongozi watakuwa ' Wametuuza ' kwa Simba SC ambao ndiko Wanakokushabikia tokea walipokuwa Watoto.
Msipokubaliana na Mimi mwana Yanga SC mwenzenu An Eagle basi nahama Yanga SC na naenda Simba SC kwa Hasira.