Tusishangae ya Jeetu Patel, wajinga ndio waliwao

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,790
288,006
Tusishangae ya Jeetu Patel, wajinga ndio waliwao

Johnson Mbwambo Januari 23, 2008
Raia Mwema

MWAKA 1995 mgombea urais wa chama cha NCCR-Mageuzi, Augustine Mrema alianzisha mjadala mkubwa alipotamka, kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni, kwamba haoni sababu kwa nini Wahindi wagombee nafasi za uongozi katika Tanzania.

Katika mkutano huo uliofanyika kwenye viwanja vya Jangwani, mjini Dar es Salaam, Mrema aliwataka Wahindi “wakagombee uongozi kwao India.”

Kama alivyoshambuliwa Christopher Mtikila kwa kuwaita Wahindi Magabacholi, Mrema naye alishambuliwa kila kona na wafuasi wa CCM kwa kauli yake hiyo dhidi ya Wahindi; huku akiitwa mbaguzi mkubwa wa rangi na mtu asiyefaa kuwa Rais.

Lakini walikuwepo pia maelfu ya vijana kote nchini ambao waliwaunga mkono Mrema na Mtikila kwa misimamo yao hiyo dhidi ya Wahindi. Kwa hakika, walichokifanya Mrema na Mtikila ilikuwa ni kuamsha tu hisia za muda mrefu zilizokuwa zimelala miongoni mwa Watanzania, hususan vijana, dhidi ya Wahindi.

Vijana hao ni wale wanaoamini kwamba sio tu kuwa Wahindi wamejitenga na kujibagua kwa miaka yote tangu walipoletwa hapa Afrika Mashariki kujenga reli, lakini pia baadhi yao wamethibitisha jinsi wasivyokuwa waaminifu kwa nchi hii kwa mambo wanayoyafanya.

Achilia mbali kwamba wengi wao wameendelea kuwa na uraia wa nchi mbili, baadhi wamejitokeza kuwa wahujumu wakubwa wa uchumi; huku wakiwavuta kama sumaku watawala wetu wenye tamaa ya kuishi maisha ya ubilionea na kuwashawishi kushirikiana nao katika vitendo vya ufisadi vya kuwaibia wanyonge wa nchi hii pesa zao.

Ni kweli kwamba katika dunia ya sasa huwezi kuwa na mtazamo mkali (wa kibaguzi) dhidi ya Wahindi, Waarabu, au hata Wazungu, ukafika mbali kisiasa; na hivyo Mrema na Mtikila nao hawakufika mbali kisiasa.

Lakini swali la kujiuliza ni hili: Je, hisia zile za vijana dhidi ya Wahindi, zilizoamshwa na kina Mtikila na Mrema katika miaka ile ya tisini, zimekufa moja kwa moja au zimelala tu zikisubiri mtu mwingine wa kuziamsha, au kitu kingine cha kuziamsha?

Majuzi nilikuwa katika baa moja maarufu hapa Jijini Dar es Salaam ambako niliweza kusikiliza mjadala mkali wa kikundi kidogo cha wanywaji kuhusu kashfa ya ufisadi ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Ingawa wafanyabiashara wanaotuhumiwa na ufisadi huo ni wengi, ilikuwa ni dhahiri katika mjadala wa kikundi kile kuwa hasira zao zilielekezwa zaidi kwa mmojawao ambaye ni Mhindi – Jayantkumar Chandubhai Patel, maarufu kwa jina la Jeetu Patel na mwingine ambaye sina hakika kama ni Mhindi au burushi.

Nilijiuliza kwa nini hasira za kikundi kile zisielekezwe kwa Daudi Ballali ambaye ndiye aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu wakati pesa hizo zikichotwa? Kwa nini hasira zisielekezwe kwa watuhumiwa wengine wasio Wahindi, au hata kwa Daniel Yona na Basil Mramba, waliokuwa Mawaziri wa Fedha au Benjamin Mkapa aliyekuwa Rais wakati mapesa hayo yakichotwa Benki Kuu? Kwa nini hasira zielekezwe kwa Jeetu Patel tu na wengine wasio wazawa?

Lakini ni kweli kwamba Jeetu Patel peke yake anamiliki kampuni nane kati ya 13 zilizotajwa katika taarifa ya Ernest & Young kuwa zililipwa Sh. bilioni 90.3 za akaunti ya EPA ya Benki Kuu kwa kutumia nyaraka batili na zilizoghushiwa.

Ni kweli vilevile kwamba unapozungumzia rushwa kubwa kubwa au ujambazi wa kiuchumi hapa Afrika Mashariki, majina yanayojitokeza ni ya Wahindi. Ukifikiria majina kama Chavda, Akasha, Pattni, Sailesh Vithlani au Tanil Somaiya, utaelewa ninachokizungumzia kuhusu baadhi ya Wahindi tulionao Afrika Mashariki.

Na jambo la kusikitisha zaidi ni kwamba wote hao wana uraia wa nchi mbili au nne hivi. Mbali ya uraia wa Tanzania unakuta pia kuwa ni raia wa Uingereza, India, Canada, Marekani au Australia. Ukimuuliza kati ya nchi zote hizo ambazo yeye ni raia, mapenzi yake ya dhati yako kwa nchi gani, hatakujibu.

Kwa hiyo, naielewa hasira ya kikundi kile cha wanywaji dhidi ya kina Jeetu Patel. Wenzetu hawa Wahindi (ingawa wapo wengine waaminifu na wazalendo kweli kweli) wamekuwa wanaishi Tanzania kama sehemu ya kuchuma tu mali na mahali pa kuishi pa muda tu wakati wanajiandaa kwenda mahali pa kudumu pawe Uingereza, Canada au Marekani.

Hata baadhi ya wale ambao kwa vipindi tofauti wamejiita “Watanzania” au “makada wa CCM” na hata kuvishwa majoho ya ukamanda wa vijana wa chama hicho, baadaye walibadilika na kuondoka nchini baada ya kuwa wameona wamenufaika vya kutosha kwa kuupata utajiri hapa nyumbani, mara nyingi kwa njia zisizo halali. Wako wapi, hivi sasa, kwa mfano, kina Chavda na kina Gulamani?

Kwa ufupi, mienendo yao wenyewe (Wahindi) ndiyo inayofanya hisia zile zilizoamshwa na kina Mtikila na kina Mrema, miaka ile ya tisini, zisife kabisa miongoni mwa Watanzania wazawa, hususan vijana. Kwa hakika, baadhi ya Wahindi wamefikia hata hatua ya kuingiza ubaguzi wa rangi katika ajira.

Hebu soma tangazo hili lililotoka, wiki iliyopita, kwenye ukurasa wa kwanza wa gazeti la Majira (toleo la Januari 18, 2008):

“Urgently Required: Sales person male/female for a pharmacy at Shoppers Plaza. Should be: Form 1V/V educated. Fluent in English. Tanzanian of Asian Origin. Please contact 0754-673586.”
Kwa tangazo hilo, mzawa hawezi kupata ajira hiyo hata kama ana sifa zote, kwa sababu anayetakiwa ni Tanzanian of Asian Origin; yaani Mhindi!

Binafsi, naamini kwamba wakati mwingine ni Wahindi wenyewe wanaojiponza. Laiti wangebadilika na kuifanya Tanzania ni nchi yao kweli kweli, na kuacha kuwahujumu wanyonge wa nchi hii, nina hakika fikra hizo zingekufa kabisa na kuzikwa, lakini kama nilivyoshuhudia katika gumzo lile la wanywaji kwenye baa, bado hazijafa kabisa!

Na wala sisemi jibu lipo katika kuwafukuza. Ukiachilia mbali ukweli kwamba kufanya hivyo ni kukiuka haki za binadamu, lakini Wahindi pia ni nguvu kuu ya uchumi hapa nchini; achilia mbali kwamba wanaajiri ndugu zetu wengi tu kuanzia majumbani mwao, madukani mwao, maofisini mwao na viwandani mwao.

Kwa mtazamo wangu, jibu lipo sehemu mbili. Kwanza, jibu lipo kwa Wahindi wenyewe. Ni lazima wenyewe, kama jumuiya, wabadilike kama kweli wanataka hisia hizo za baadhi ya Watanzania dhidi yao zife na kuzikwa.

Ni mabadiliko gani ninayoyazungumzia? Yapo mengi, lakini kubwa ni kufanya juhudi za kweli ku-integrate na Waafrika (wazawa). Ku-integrate kuna maana pana, lakini hebu chukulia mfano mmoja tu wa ndoa. Haiwezekani kwamba hawa jamaa wamekaa nchini mwetu miaka yote hiyo, na bado tusione idadi ya kutosha ya Wahindi waliooa/kuolewa na Waafrika au Waafrika waliooa/kuolewa na Wahindi.

Ni rahisi hapa nchini kuona machotara wa Kiarabu na Kiafrika (nina maana ya Watanzania weusi) au wa Kizungu na Kiafrika kuliko kuona machotara wa Kihindi na Kiafrika au hata wa Kihindi na Kizungu au Kihindi na Kiarabu.

Kuna imani kwamba binti wa Kihindi au kijana wa kiume wa Kihindi, akizaa mtoto na moja ya makundi hayo niliyoyataja, hutengwa na jamii. Waliopata kuiangalia filamu ya Mississippi Masala (Denzel Washington) wanalielewa hili vizuri.

Kwa hiyo, Wahindi lazima wajisaidie kwanza wao wenyewe kumaliza hisia hizo za chuki dhidi yao ambazo baadhi ya Watanzania wanazo. Na moja ya njia za kujisaidia ni kuanza ku-integrate na Watanzania weusi katika nyanja zote. Mpaka sasa integration tunayoiona ipo kidogo katika siasa na katika michezo, na hiyo, ukichunguza, ni kwa manufaa binafsi ya hao wachache waliojitosa humo.

Sambamba na hilo, Wahindi ambao ni raia wema na wanaoipenda nchi hii kwa dhati (wapo wengi wa kutosha), lazima nao wachukue hatua za makusudi kabisa za kuwasema wenzao wanaohujumu uchumi wa nchi hii masikini ili waache kuwaibia wanyonge pesa zao.

Maana, ni kweli wanatuibia. Pesa zinazoaminika kuibwa na kampuni za Jeetu Patel na zile za skandali ya Chavda na ya ununuzi wa rada inayomhusisha Sailesh Vithlan, tunaambiwa, zinatosha kujenga zaidi ya shule 1000, na bado walalahoi nchini wanachangishwa na Serikali kwa nguvu pesa za kujenga sekondari!

Hivyo, Wahindi ambao ni raia wema wanaweza kutumia jamatini zao na misikiti yao au jumuiya zao nyingine kuwaweka kiti moto kina Jeetu Patel na kina Chavda na kuwaambia kwamba wanachokifanya si kitu chema mbele ya Mungu, na kwamba kinawafanya wao (Wahindi) wachukiwe na wazawa. Hili, naamini linawezekana na likifanyika litapunguza kuibuka kwa wingi nchini kwa kina Jeetu Patel, Chavda, Sailesh na kina Pattni.

Lakini jibu la pili ambalo ndilo la msingi, ni kwa sisi wazawa (Watanzania weusi) kutokubali kuwapa uongozi wazawa wenzetu wenye tamaa ya kupindukia ya kuwa mabilionea. Hawa, huwa rahisi kugeuzwa wajinga na kina Jeetu Patel. Viongozi wetu wakishageuzwa wajinga na kina Jeetu Patel na kina Chavda, basi, sisi sote katika ujumla wetu, tunakuwa wajinga wa wenzetu hao!

Nasema hivyo, kwa sababu Jeetu Patel asingeweza kufanikisha kuunda kampuni sita kwa nyaraka za kugushi, moja baada ya nyingine, na kila moja kujichotea mapesa hayo BoT, bila kushirikisha viongozi na watawala wetu (ambao wote ni wazawa) wenye uchu mkubwa wa kuwa mabilionea.

Alichotumia Jeetu Patel, Chavda, Sailesh na wengine kadhaa, ni udhaifu wetu sisi Watanzania kuchagua viongozi na watawala wasiojali miiko ya uongozi, viongozi ambao lengo lao kubwa kuingia madarakani si kutumikia wananchi na kuwapunguzia umasikini, bali ni kuusaka utajiri kwa udi na uvumba. Hao ndiyo wanaotufanya Watanzania wote tuonekane ni wajinga tu mbele ya kina Chavda.

Hao ndiyo wanaowakubali na kuwaamini kina Chavda na maburushi wengine kuwa ni “wafadhili wa Chama” huku ufadhili wenyewe ukitokana na pesa walizotuibia. Mtu anakuibia kijanja mapesa yote hayo katika benki ya umma, na kisha kesho akijenga kisima kwa ajili ya kijiji fulani, au shule ya sekondari au akitoa pesa kidogo kusaidia Chama, tunachekelea kwa furaha huku tukimwita “mfadhili mkubwa wa Chama” na mzalendo wa kweli!

Anayekuibia kwa kutumia mkono wa kulia na kukurejeshea kidogo alichokuibia kwa kutumia mkono wa kushoto; huku akijitia ni mfadhili, utamwitaje “mzalendo wa kweli”? Huyu mahali pake ni jela!

Hivi sasa naambiwa kwamba, kama ilivyokuwa kwa Chavda, Sailesh na Gulamani, Jeetu Patel naye hayupo nchini katika kipindi hiki ambacho kashfa ya ufisadi ya BoT inachunguzwa ili wahusika wakamatwe.

Popote pale walipo huko nje, nina hakika kina Jeetu Patel, kina Chavda na kina Sailesh, watakuwa wakicheka njia nzima wakati wakienda benki (Swiss Bank?) kuchukua mapesa waliyochota kwetu, mapesa ya Watanzania masikini.

John Nolan, yule mwekezaji wa Ireland aliyataka kuighilibu Serikali ya Mkapa imruhusu kufungua mashamba ya prawns ambayo yangeiharibu kabisa Delta ya Rufiji, alipata kusema kwamba; Tanzania ndiyo nchi pekee duniani ambayo Mzungu, Mhindi au Burushi anaweza kuingia akiwa na dola tano tu mfukoni na kuondoka miaka mitano baadaye akiwa milionea! Kweli wajinga ndiyo waliwao!

Email: mbwambojohnson@yahoo.com
 
Tusishangae ya Jeetu Patel, wajinga ndio waliwao

Johnson Mbwambo Januari 23, 2008
Raia Mwema

MWAKA 1995 mgombea urais wa chama cha NCCR-Mageuzi, Augustine Mrema alianzisha mjadala mkubwa alipotamka, kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni, kwamba haoni sababu kwa nini Wahindi wagombee nafasi za uongozi katika Tanzania.

Katika mkutano huo uliofanyika kwenye viwanja vya Jangwani, mjini Dar es Salaam, Mrema aliwataka Wahindi “wakagombee uongozi kwao India.”

Kama alivyoshambuliwa Christopher Mtikila kwa kuwaita Wahindi Magabacholi, Mrema naye alishambuliwa kila kona na wafuasi wa CCM kwa kauli yake hiyo dhidi ya Wahindi; huku akiitwa mbaguzi mkubwa wa rangi na mtu asiyefaa kuwa Rais.

Lakini walikuwepo pia maelfu ya vijana kote nchini ambao waliwaunga mkono Mrema na Mtikila kwa misimamo yao hiyo dhidi ya Wahindi. Kwa hakika, walichokifanya Mrema na Mtikila ilikuwa ni kuamsha tu hisia za muda mrefu zilizokuwa zimelala miongoni mwa Watanzania, hususan vijana, dhidi ya Wahindi.

Vijana hao ni wale wanaoamini kwamba sio tu kuwa Wahindi wamejitenga na kujibagua kwa miaka yote tangu walipoletwa hapa Afrika Mashariki kujenga reli, lakini pia baadhi yao wamethibitisha jinsi wasivyokuwa waaminifu kwa nchi hii kwa mambo wanayoyafanya.

Achilia mbali kwamba wengi wao wameendelea kuwa na uraia wa nchi mbili, baadhi wamejitokeza kuwa wahujumu wakubwa wa uchumi; huku wakiwavuta kama sumaku watawala wetu wenye tamaa ya kuishi maisha ya ubilionea na kuwashawishi kushirikiana nao katika vitendo vya ufisadi vya kuwaibia wanyonge wa nchi hii pesa zao.

Ni kweli kwamba katika dunia ya sasa huwezi kuwa na mtazamo mkali (wa kibaguzi) dhidi ya Wahindi, Waarabu, au hata Wazungu, ukafika mbali kisiasa; na hivyo Mrema na Mtikila nao hawakufika mbali kisiasa.

Lakini swali la kujiuliza ni hili: Je, hisia zile za vijana dhidi ya Wahindi, zilizoamshwa na kina Mtikila na Mrema katika miaka ile ya tisini, zimekufa moja kwa moja au zimelala tu zikisubiri mtu mwingine wa kuziamsha, au kitu kingine cha kuziamsha?

Majuzi nilikuwa katika baa moja maarufu hapa Jijini Dar es Salaam ambako niliweza kusikiliza mjadala mkali wa kikundi kidogo cha wanywaji kuhusu kashfa ya ufisadi ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Ingawa wafanyabiashara wanaotuhumiwa na ufisadi huo ni wengi, ilikuwa ni dhahiri katika mjadala wa kikundi kile kuwa hasira zao zilielekezwa zaidi kwa mmojawao ambaye ni Mhindi – Jayantkumar Chandubhai Patel, maarufu kwa jina la Jeetu Patel na mwingine ambaye sina hakika kama ni Mhindi au burushi.

Nilijiuliza kwa nini hasira za kikundi kile zisielekezwe kwa Daudi Ballali ambaye ndiye aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu wakati pesa hizo zikichotwa? Kwa nini hasira zisielekezwe kwa watuhumiwa wengine wasio Wahindi, au hata kwa Daniel Yona na Basil Mramba, waliokuwa Mawaziri wa Fedha au Benjamin Mkapa aliyekuwa Rais wakati mapesa hayo yakichotwa Benki Kuu? Kwa nini hasira zielekezwe kwa Jeetu Patel tu na wengine wasio wazawa?

Lakini ni kweli kwamba Jeetu Patel peke yake anamiliki kampuni nane kati ya 13 zilizotajwa katika taarifa ya Ernest & Young kuwa zililipwa Sh. bilioni 90.3 za akaunti ya EPA ya Benki Kuu kwa kutumia nyaraka batili na zilizoghushiwa.

Ni kweli vilevile kwamba unapozungumzia rushwa kubwa kubwa au ujambazi wa kiuchumi hapa Afrika Mashariki, majina yanayojitokeza ni ya Wahindi. Ukifikiria majina kama Chavda, Akasha, Pattni, Sailesh Vithlani au Tanil Somaiya, utaelewa ninachokizungumzia kuhusu baadhi ya Wahindi tulionao Afrika Mashariki.

Na jambo la kusikitisha zaidi ni kwamba wote hao wana uraia wa nchi mbili au nne hivi. Mbali ya uraia wa Tanzania unakuta pia kuwa ni raia wa Uingereza, India, Canada, Marekani au Australia. Ukimuuliza kati ya nchi zote hizo ambazo yeye ni raia, mapenzi yake ya dhati yako kwa nchi gani, hatakujibu.

Kwa hiyo, naielewa hasira ya kikundi kile cha wanywaji dhidi ya kina Jeetu Patel. Wenzetu hawa Wahindi (ingawa wapo wengine waaminifu na wazalendo kweli kweli) wamekuwa wanaishi Tanzania kama sehemu ya kuchuma tu mali na mahali pa kuishi pa muda tu wakati wanajiandaa kwenda mahali pa kudumu pawe Uingereza, Canada au Marekani.

Hata baadhi ya wale ambao kwa vipindi tofauti wamejiita “Watanzania” au “makada wa CCM” na hata kuvishwa majoho ya ukamanda wa vijana wa chama hicho, baadaye walibadilika na kuondoka nchini baada ya kuwa wameona wamenufaika vya kutosha kwa kuupata utajiri hapa nyumbani, mara nyingi kwa njia zisizo halali. Wako wapi, hivi sasa, kwa mfano, kina Chavda na kina Gulamani?

Kwa ufupi, mienendo yao wenyewe (Wahindi) ndiyo inayofanya hisia zile zilizoamshwa na kina Mtikila na kina Mrema, miaka ile ya tisini, zisife kabisa miongoni mwa Watanzania wazawa, hususan vijana. Kwa hakika, baadhi ya Wahindi wamefikia hata hatua ya kuingiza ubaguzi wa rangi katika ajira.

Hebu soma tangazo hili lililotoka, wiki iliyopita, kwenye ukurasa wa kwanza wa gazeti la Majira (toleo la Januari 18, 2008):

“Urgently Required: Sales person male/female for a pharmacy at Shoppers Plaza. Should be: Form 1V/V educated. Fluent in English. Tanzanian of Asian Origin. Please contact 0754-673586.”
Kwa tangazo hilo, mzawa hawezi kupata ajira hiyo hata kama ana sifa zote, kwa sababu anayetakiwa ni Tanzanian of Asian Origin; yaani Mhindi!

Binafsi, naamini kwamba wakati mwingine ni Wahindi wenyewe wanaojiponza. Laiti wangebadilika na kuifanya Tanzania ni nchi yao kweli kweli, na kuacha kuwahujumu wanyonge wa nchi hii, nina hakika fikra hizo zingekufa kabisa na kuzikwa, lakini kama nilivyoshuhudia katika gumzo lile la wanywaji kwenye baa, bado hazijafa kabisa!

Na wala sisemi jibu lipo katika kuwafukuza. Ukiachilia mbali ukweli kwamba kufanya hivyo ni kukiuka haki za binadamu, lakini Wahindi pia ni nguvu kuu ya uchumi hapa nchini; achilia mbali kwamba wanaajiri ndugu zetu wengi tu kuanzia majumbani mwao, madukani mwao, maofisini mwao na viwandani mwao.

Kwa mtazamo wangu, jibu lipo sehemu mbili. Kwanza, jibu lipo kwa Wahindi wenyewe. Ni lazima wenyewe, kama jumuiya, wabadilike kama kweli wanataka hisia hizo za baadhi ya Watanzania dhidi yao zife na kuzikwa.

Ni mabadiliko gani ninayoyazungumzia? Yapo mengi, lakini kubwa ni kufanya juhudi za kweli ku-integrate na Waafrika (wazawa). Ku-integrate kuna maana pana, lakini hebu chukulia mfano mmoja tu wa ndoa. Haiwezekani kwamba hawa jamaa wamekaa nchini mwetu miaka yote hiyo, na bado tusione idadi ya kutosha ya Wahindi waliooa/kuolewa na Waafrika au Waafrika waliooa/kuolewa na Wahindi.

Ni rahisi hapa nchini kuona machotara wa Kiarabu na Kiafrika (nina maana ya Watanzania weusi) au wa Kizungu na Kiafrika kuliko kuona machotara wa Kihindi na Kiafrika au hata wa Kihindi na Kizungu au Kihindi na Kiarabu.

Kuna imani kwamba binti wa Kihindi au kijana wa kiume wa Kihindi, akizaa mtoto na moja ya makundi hayo niliyoyataja, hutengwa na jamii. Waliopata kuiangalia filamu ya Mississippi Masala (Denzel Washington) wanalielewa hili vizuri.

Kwa hiyo, Wahindi lazima wajisaidie kwanza wao wenyewe kumaliza hisia hizo za chuki dhidi yao ambazo baadhi ya Watanzania wanazo. Na moja ya njia za kujisaidia ni kuanza ku-integrate na Watanzania weusi katika nyanja zote. Mpaka sasa integration tunayoiona ipo kidogo katika siasa na katika michezo, na hiyo, ukichunguza, ni kwa manufaa binafsi ya hao wachache waliojitosa humo.

Sambamba na hilo, Wahindi ambao ni raia wema na wanaoipenda nchi hii kwa dhati (wapo wengi wa kutosha), lazima nao wachukue hatua za makusudi kabisa za kuwasema wenzao wanaohujumu uchumi wa nchi hii masikini ili waache kuwaibia wanyonge pesa zao.

Maana, ni kweli wanatuibia. Pesa zinazoaminika kuibwa na kampuni za Jeetu Patel na zile za skandali ya Chavda na ya ununuzi wa rada inayomhusisha Sailesh Vithlan, tunaambiwa, zinatosha kujenga zaidi ya shule 1000, na bado walalahoi nchini wanachangishwa na Serikali kwa nguvu pesa za kujenga sekondari!

Hivyo, Wahindi ambao ni raia wema wanaweza kutumia jamatini zao na misikiti yao au jumuiya zao nyingine kuwaweka kiti moto kina Jeetu Patel na kina Chavda na kuwaambia kwamba wanachokifanya si kitu chema mbele ya Mungu, na kwamba kinawafanya wao (Wahindi) wachukiwe na wazawa. Hili, naamini linawezekana na likifanyika litapunguza kuibuka kwa wingi nchini kwa kina Jeetu Patel, Chavda, Sailesh na kina Pattni.

Lakini jibu la pili ambalo ndilo la msingi, ni kwa sisi wazawa (Watanzania weusi) kutokubali kuwapa uongozi wazawa wenzetu wenye tamaa ya kupindukia ya kuwa mabilionea. Hawa, huwa rahisi kugeuzwa wajinga na kina Jeetu Patel. Viongozi wetu wakishageuzwa wajinga na kina Jeetu Patel na kina Chavda, basi, sisi sote katika ujumla wetu, tunakuwa wajinga wa wenzetu hao!

Nasema hivyo, kwa sababu Jeetu Patel asingeweza kufanikisha kuunda kampuni sita kwa nyaraka za kugushi, moja baada ya nyingine, na kila moja kujichotea mapesa hayo BoT, bila kushirikisha viongozi na watawala wetu (ambao wote ni wazawa) wenye uchu mkubwa wa kuwa mabilionea.

Alichotumia Jeetu Patel, Chavda, Sailesh na wengine kadhaa, ni udhaifu wetu sisi Watanzania kuchagua viongozi na watawala wasiojali miiko ya uongozi, viongozi ambao lengo lao kubwa kuingia madarakani si kutumikia wananchi na kuwapunguzia umasikini, bali ni kuusaka utajiri kwa udi na uvumba. Hao ndiyo wanaotufanya Watanzania wote tuonekane ni wajinga tu mbele ya kina Chavda.

Hao ndiyo wanaowakubali na kuwaamini kina Chavda na maburushi wengine kuwa ni “wafadhili wa Chama” huku ufadhili wenyewe ukitokana na pesa walizotuibia. Mtu anakuibia kijanja mapesa yote hayo katika benki ya umma, na kisha kesho akijenga kisima kwa ajili ya kijiji fulani, au shule ya sekondari au akitoa pesa kidogo kusaidia Chama, tunachekelea kwa furaha huku tukimwita “mfadhili mkubwa wa Chama” na mzalendo wa kweli!

Anayekuibia kwa kutumia mkono wa kulia na kukurejeshea kidogo alichokuibia kwa kutumia mkono wa kushoto; huku akijitia ni mfadhili, utamwitaje “mzalendo wa kweli”? Huyu mahali pake ni jela!

Hivi sasa naambiwa kwamba, kama ilivyokuwa kwa Chavda, Sailesh na Gulamani, Jeetu Patel naye hayupo nchini katika kipindi hiki ambacho kashfa ya ufisadi ya BoT inachunguzwa ili wahusika wakamatwe.

Popote pale walipo huko nje, nina hakika kina Jeetu Patel, kina Chavda na kina Sailesh, watakuwa wakicheka njia nzima wakati wakienda benki (Swiss Bank?) kuchukua mapesa waliyochota kwetu, mapesa ya Watanzania masikini.

John Nolan, yule mwekezaji wa Ireland aliyataka kuighilibu Serikali ya Mkapa imruhusu kufungua mashamba ya prawns ambayo yangeiharibu kabisa Delta ya Rufiji, alipata kusema kwamba; Tanzania ndiyo nchi pekee duniani ambayo Mzungu, Mhindi au Burushi anaweza kuingia akiwa na dola tano tu mfukoni na kuondoka miaka mitano baadaye akiwa milionea! Kweli wajinga ndiyo waliwao!

Email: mbwambojohnson@yahoo.com

Kweli kabisa yaliyosemwa hapa ila kizazi kipya kinachokuja Tanzania kimejiandaa kubadili haya yote. Kinachowekwa pamoja sasa hivi ni the best way to do it. Kuna wakati ikifikia kuwa serikali imeshindwa kufanya chochote kulinda maslahi ya taifa collectively, inabidi hiyo jamii iamke na kulazimisha mabadiliko kwa manufaa ya waliopo na wajao.

Countdown imeanza sasa!
 
..kwa kweli sijamaliza hata kuisoma na nimeacha makusudi maana naona kinachoendelea humo ni ubaguzi tuu juu ya wahindi na ukweli wanaotuibia mabilioni sio wahindi tuu ni hao hao weusi wenzetu,sasa why single out wahindi peke yao au rangi ya mtu kwenye huu ufisadi,too shallow kwa article kama hii kwenye gazeti linaloheshimika na ni kujenga chuki dhidi ya watu fulani kwenye jamii,huu ni upuuzi na Tanzania ni bora kuliko mawazo kama haya na wala hatuhitaji kujua rangi ya mtu kwenye vita dhidi ya ufisadi na jambo forums mjue humu ndani kuna wahindi pia ambao ni watanzania kama sisi
 
Koba, naweza kusema kuwa naelewa your reluctance to discuss something from the perspective of race. Lakini pia ni muhimu kujadili kwa wazi kabisa hisia za watanzania kwani tupende tusipende mtazamo unaozungumziwa katika article hii ni kweli. Naweza kufafananisha ishu hii na ile ya Miss Tanzania. Unapokuwa minority if the majority perceives that disproportionately more of the minority group are dishonest basi mnakuwa-labelled wote. Na ndiyo ni muhimu ku-improve your image. Where are the hard working Indians? Those who speak Kiswahili and live in Kriakoo. They are not n the public eye. Akina Jithu patel na wengine live a flashy life na akina RA na Dewji run for public office huko wakilipa rushwa njenje. It creates a bad taste in the mouth.
 
Another article on Jitu Fisadi Patel and there is no one to touch him! I guess he is no longer in the country, but no one will be able to admit that.

Latest revelations in wake of EPA scandal: Jeetu Patel also played key role in DCP scam

-1994 Bunge probe fingered him alongside V.G Chavda
Augustine Mrema: �They were fraudulently paid over 661bn/-�


THISDAY REPORTER
Dar es Salaam

DAR ES SALAAM business tycoon Jeetu Patel, a key suspect in the 133bn/- external payment arrears scandal at the Bank of Tanzania, was also involved in another embezzlement involving billions of shillings from the central bank in the 1990s, THISDAY can reveal today.

Records show that the businessman, whose full name is Jayantkumar Chandubhai Patel, was identified in a 1994 parliamentary committee investigation as one of the key architects of the infamous Debt Conversion Programme (DCP) funds misuse scam, which was quite similar to the present-day EPA scandal.

The parliamentary committee led by the then Rorya member of parliament, Ayombe Ayila, discovered in its investigation that Jeetu Patel was again a leading beneficiary of irregular payments made by BoT in the name of DCP.

The illegal payments were traced to several companies understood to be owned by Patel, including Azania Agricultural Enterprises, Liberty Leather Shoe Limited, and Azania Eximco, all of which fall under the AIMS group of companies.

Fresh investigations by THISDAY have established that the parliamentary probe committee questioned Jeetu Patel on September 9, 1994, as part of its investigation of the DCP scandal.

The committee was primarily investigating the involvement of another businessman, Vidyadhar Girdharlal (V.G) Chavda, in the same scam, and in the course of this stumbled upon the fraudulent payments also made to Jeetu Patel.

It was discovered that Jeetu Patel and V.G Chavda were both inextricably linked to the scam as leading beneficiaries.

''Jeetu Patel conspired in the preparation of forged documents purporting to show that he received 82,295,000/- from V.G Chavda for consultancy fees, stationeries, printing and equipment. A report from the office of the Director of Criminal Investigation (DCI) revealed that such payments were false,'' asserted part of the Bunge probe committee's final report.

The report quoted the then minister for home affairs, Augustine Mrema, as saying that both Jeetu Patel and V.G Chavda were fraudulently paid out of the DCP funds a total of 661,274,660/-, without practically producing any goods or services.

In its recommendations, the committee advised that a formal government investigation be launched on Jeetu Patel and the whole DCP programme.

The committee also recommended that V.G Chavda should be declared a prohibited immigrant (PI) and formally charged with embezzlement of funds from the Bank of Tanzania.

Although Chavda was indeed kicked out of the country in 1996, he returned a few years later, and is understood to be still living in Dar es Salaam while efforts by the Attorney General's Chambers to enforce the PI notice and a High Court ruling against his continued stay in the country have failed so far.

Like Chavda, Jeetu Patel has never been charged with any criminal offence in relation to the DCP scandal. On the contrary, it now appears that he later went on to be paid more billions of shillings by the same BoT via the EPA account - using forged documents yet again.

Investigations by THISDAY have already established that Jeetu Patel is the owner of eight out of 13 companies listed as beneficiaries of over 90bn/- fraudulently paid from the EPA account during 2005/06 alone.

The eight companies so linked to Patel are Navycut Tobacco (T) Limited, Ndovu Soaps Limited, Bina Resorts Limited, Bencon International Limited, Maltan Mining Company Limited, Bora Hotels & Apartments Limited, Venus Hotels Limited, and B.V. Holdings Limited.

The remaining five companies on the same EPA account fraud list are Kagoda Agriculture Limited, VB & Associates Company Limited, Changanyikeni Residential Complex Ltd, Money Planners & Consultants, and Njake Hotel & Tours Limited.


 
Koba, naweza kusema kuwa naelewa your reluctance to discuss something from the perspective of race. Lakini pia ni muhimu kujadili kwa wazi kabisa hisia za watanzania kwani tupende tusipende mtazamo unaozungumziwa katika article hii ni kweli. Naweza kufafananisha ishu hii na ile ya Miss Tanzania. Unapokuwa minority if the majority perceives that disproportionately more of the minority group are dishonest basi mnakuwa-labelled wote. Na ndiyo ni muhimu ku-improve your image. Where are the hard working Indians? Those who speak Kiswahili and live in Kriakoo. They are not n the public eye. Akina Jithu patel na wengine live a flashy life na akina RA na Dewji run for public office huko wakilipa rushwa njenje. It creates a bad taste in the mouth.

Kama wahindi wanatuibia mabilioni kwa nini tuogope kusema kwamba wahindi wanatuibia kwa kushirikiana na viongozi mafisadi!? :confused:

Watanzania woga wetu umezidi wakati mwingine na unaiangamiza nchi! Hakuna ubaya wowote na wala si ubaguzi wa rangi kusema kwamba wahindi nao ni mafisadi wakubwa nchini mwetu...:(

Thanks Susuviri!
 
Tusishangae ya Jeetu Patel, wajinga ndio waliwao

Johnson Mbwambo Januari 23, 2008
Raia Mwema

MWAKA 1995 mgombea urais wa chama cha NCCR-Mageuzi, Augustine Mrema alianzisha mjadala mkubwa alipotamka, kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni, kwamba haoni sababu kwa nini Wahindi wagombee nafasi za uongozi katika Tanzania.

Katika mkutano huo uliofanyika kwenye viwanja vya Jangwani, mjini Dar es Salaam, Mrema aliwataka Wahindi “wakagombee uongozi kwao India.”

Kama alivyoshambuliwa Christopher Mtikila kwa kuwaita Wahindi Magabacholi, Mrema naye alishambuliwa kila kona na wafuasi wa CCM kwa kauli yake hiyo dhidi ya Wahindi; huku akiitwa mbaguzi mkubwa wa rangi na mtu asiyefaa kuwa Rais.

Lakini walikuwepo pia maelfu ya vijana kote nchini ambao waliwaunga mkono Mrema na Mtikila kwa misimamo yao hiyo dhidi ya Wahindi. Kwa hakika, walichokifanya Mrema na Mtikila ilikuwa ni kuamsha tu hisia za muda mrefu zilizokuwa zimelala miongoni mwa Watanzania, hususan vijana, dhidi ya Wahindi.

Vijana hao ni wale wanaoamini kwamba sio tu kuwa Wahindi wamejitenga na kujibagua kwa miaka yote tangu walipoletwa hapa Afrika Mashariki kujenga reli, lakini pia baadhi yao wamethibitisha jinsi wasivyokuwa waaminifu kwa nchi hii kwa mambo wanayoyafanya.

Achilia mbali kwamba wengi wao wameendelea kuwa na uraia wa nchi mbili, baadhi wamejitokeza kuwa wahujumu wakubwa wa uchumi; huku wakiwavuta kama sumaku watawala wetu wenye tamaa ya kuishi maisha ya ubilionea na kuwashawishi kushirikiana nao katika vitendo vya ufisadi vya kuwaibia wanyonge wa nchi hii pesa zao.

Ni kweli kwamba katika dunia ya sasa huwezi kuwa na mtazamo mkali (wa kibaguzi) dhidi ya Wahindi, Waarabu, au hata Wazungu, ukafika mbali kisiasa; na hivyo Mrema na Mtikila nao hawakufika mbali kisiasa.

Lakini swali la kujiuliza ni hili: Je, hisia zile za vijana dhidi ya Wahindi, zilizoamshwa na kina Mtikila na Mrema katika miaka ile ya tisini, zimekufa moja kwa moja au zimelala tu zikisubiri mtu mwingine wa kuziamsha, au kitu kingine cha kuziamsha?

Majuzi nilikuwa katika baa moja maarufu hapa Jijini Dar es Salaam ambako niliweza kusikiliza mjadala mkali wa kikundi kidogo cha wanywaji kuhusu kashfa ya ufisadi ya Benki Kuu ya Tanzania (BoT).

Ingawa wafanyabiashara wanaotuhumiwa na ufisadi huo ni wengi, ilikuwa ni dhahiri katika mjadala wa kikundi kile kuwa hasira zao zilielekezwa zaidi kwa mmojawao ambaye ni Mhindi – Jayantkumar Chandubhai Patel, maarufu kwa jina la Jeetu Patel na mwingine ambaye sina hakika kama ni Mhindi au burushi.

Nilijiuliza kwa nini hasira za kikundi kile zisielekezwe kwa Daudi Ballali ambaye ndiye aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu wakati pesa hizo zikichotwa? Kwa nini hasira zisielekezwe kwa watuhumiwa wengine wasio Wahindi, au hata kwa Daniel Yona na Basil Mramba, waliokuwa Mawaziri wa Fedha au Benjamin Mkapa aliyekuwa Rais wakati mapesa hayo yakichotwa Benki Kuu? Kwa nini hasira zielekezwe kwa Jeetu Patel tu na wengine wasio wazawa?

Lakini ni kweli kwamba Jeetu Patel peke yake anamiliki kampuni nane kati ya 13 zilizotajwa katika taarifa ya Ernest & Young kuwa zililipwa Sh. bilioni 90.3 za akaunti ya EPA ya Benki Kuu kwa kutumia nyaraka batili na zilizoghushiwa.

Ni kweli vilevile kwamba unapozungumzia rushwa kubwa kubwa au ujambazi wa kiuchumi hapa Afrika Mashariki, majina yanayojitokeza ni ya Wahindi. Ukifikiria majina kama Chavda, Akasha, Pattni, Sailesh Vithlani au Tanil Somaiya, utaelewa ninachokizungumzia kuhusu baadhi ya Wahindi tulionao Afrika Mashariki.

Na jambo la kusikitisha zaidi ni kwamba wote hao wana uraia wa nchi mbili au nne hivi. Mbali ya uraia wa Tanzania unakuta pia kuwa ni raia wa Uingereza, India, Canada, Marekani au Australia. Ukimuuliza kati ya nchi zote hizo ambazo yeye ni raia, mapenzi yake ya dhati yako kwa nchi gani, hatakujibu.

Kwa hiyo, naielewa hasira ya kikundi kile cha wanywaji dhidi ya kina Jeetu Patel. Wenzetu hawa Wahindi (ingawa wapo wengine waaminifu na wazalendo kweli kweli) wamekuwa wanaishi Tanzania kama sehemu ya kuchuma tu mali na mahali pa kuishi pa muda tu wakati wanajiandaa kwenda mahali pa kudumu pawe Uingereza, Canada au Marekani.

Hata baadhi ya wale ambao kwa vipindi tofauti wamejiita “Watanzania” au “makada wa CCM” na hata kuvishwa majoho ya ukamanda wa vijana wa chama hicho, baadaye walibadilika na kuondoka nchini baada ya kuwa wameona wamenufaika vya kutosha kwa kuupata utajiri hapa nyumbani, mara nyingi kwa njia zisizo halali. Wako wapi, hivi sasa, kwa mfano, kina Chavda na kina Gulamani?

Kwa ufupi, mienendo yao wenyewe (Wahindi) ndiyo inayofanya hisia zile zilizoamshwa na kina Mtikila na kina Mrema, miaka ile ya tisini, zisife kabisa miongoni mwa Watanzania wazawa, hususan vijana. Kwa hakika, baadhi ya Wahindi wamefikia hata hatua ya kuingiza ubaguzi wa rangi katika ajira.

Hebu soma tangazo hili lililotoka, wiki iliyopita, kwenye ukurasa wa kwanza wa gazeti la Majira (toleo la Januari 18, 2008):

“Urgently Required: Sales person male/female for a pharmacy at Shoppers Plaza. Should be: Form 1V/V educated. Fluent in English. Tanzanian of Asian Origin. Please contact 0754-673586.”
Kwa tangazo hilo, mzawa hawezi kupata ajira hiyo hata kama ana sifa zote, kwa sababu anayetakiwa ni Tanzanian of Asian Origin; yaani Mhindi!

Binafsi, naamini kwamba wakati mwingine ni Wahindi wenyewe wanaojiponza. Laiti wangebadilika na kuifanya Tanzania ni nchi yao kweli kweli, na kuacha kuwahujumu wanyonge wa nchi hii, nina hakika fikra hizo zingekufa kabisa na kuzikwa, lakini kama nilivyoshuhudia katika gumzo lile la wanywaji kwenye baa, bado hazijafa kabisa!

Na wala sisemi jibu lipo katika kuwafukuza. Ukiachilia mbali ukweli kwamba kufanya hivyo ni kukiuka haki za binadamu, lakini Wahindi pia ni nguvu kuu ya uchumi hapa nchini; achilia mbali kwamba wanaajiri ndugu zetu wengi tu kuanzia majumbani mwao, madukani mwao, maofisini mwao na viwandani mwao.

Kwa mtazamo wangu, jibu lipo sehemu mbili. Kwanza, jibu lipo kwa Wahindi wenyewe. Ni lazima wenyewe, kama jumuiya, wabadilike kama kweli wanataka hisia hizo za baadhi ya Watanzania dhidi yao zife na kuzikwa.

Ni mabadiliko gani ninayoyazungumzia? Yapo mengi, lakini kubwa ni kufanya juhudi za kweli ku-integrate na Waafrika (wazawa). Ku-integrate kuna maana pana, lakini hebu chukulia mfano mmoja tu wa ndoa. Haiwezekani kwamba hawa jamaa wamekaa nchini mwetu miaka yote hiyo, na bado tusione idadi ya kutosha ya Wahindi waliooa/kuolewa na Waafrika au Waafrika waliooa/kuolewa na Wahindi.

Ni rahisi hapa nchini kuona machotara wa Kiarabu na Kiafrika (nina maana ya Watanzania weusi) au wa Kizungu na Kiafrika kuliko kuona machotara wa Kihindi na Kiafrika au hata wa Kihindi na Kizungu au Kihindi na Kiarabu.

Kuna imani kwamba binti wa Kihindi au kijana wa kiume wa Kihindi, akizaa mtoto na moja ya makundi hayo niliyoyataja, hutengwa na jamii. Waliopata kuiangalia filamu ya Mississippi Masala (Denzel Washington) wanalielewa hili vizuri.

Kwa hiyo, Wahindi lazima wajisaidie kwanza wao wenyewe kumaliza hisia hizo za chuki dhidi yao ambazo baadhi ya Watanzania wanazo. Na moja ya njia za kujisaidia ni kuanza ku-integrate na Watanzania weusi katika nyanja zote. Mpaka sasa integration tunayoiona ipo kidogo katika siasa na katika michezo, na hiyo, ukichunguza, ni kwa manufaa binafsi ya hao wachache waliojitosa humo.

Sambamba na hilo, Wahindi ambao ni raia wema na wanaoipenda nchi hii kwa dhati (wapo wengi wa kutosha), lazima nao wachukue hatua za makusudi kabisa za kuwasema wenzao wanaohujumu uchumi wa nchi hii masikini ili waache kuwaibia wanyonge pesa zao.

Maana, ni kweli wanatuibia. Pesa zinazoaminika kuibwa na kampuni za Jeetu Patel na zile za skandali ya Chavda na ya ununuzi wa rada inayomhusisha Sailesh Vithlan, tunaambiwa, zinatosha kujenga zaidi ya shule 1000, na bado walalahoi nchini wanachangishwa na Serikali kwa nguvu pesa za kujenga sekondari!

Hivyo, Wahindi ambao ni raia wema wanaweza kutumia jamatini zao na misikiti yao au jumuiya zao nyingine kuwaweka kiti moto kina Jeetu Patel na kina Chavda na kuwaambia kwamba wanachokifanya si kitu chema mbele ya Mungu, na kwamba kinawafanya wao (Wahindi) wachukiwe na wazawa. Hili, naamini linawezekana na likifanyika litapunguza kuibuka kwa wingi nchini kwa kina Jeetu Patel, Chavda, Sailesh na kina Pattni.

Lakini jibu la pili ambalo ndilo la msingi, ni kwa sisi wazawa (Watanzania weusi) kutokubali kuwapa uongozi wazawa wenzetu wenye tamaa ya kupindukia ya kuwa mabilionea. Hawa, huwa rahisi kugeuzwa wajinga na kina Jeetu Patel. Viongozi wetu wakishageuzwa wajinga na kina Jeetu Patel na kina Chavda, basi, sisi sote katika ujumla wetu, tunakuwa wajinga wa wenzetu hao!

Nasema hivyo, kwa sababu Jeetu Patel asingeweza kufanikisha kuunda kampuni sita kwa nyaraka za kugushi, moja baada ya nyingine, na kila moja kujichotea mapesa hayo BoT, bila kushirikisha viongozi na watawala wetu (ambao wote ni wazawa) wenye uchu mkubwa wa kuwa mabilionea.

Alichotumia Jeetu Patel, Chavda, Sailesh na wengine kadhaa, ni udhaifu wetu sisi Watanzania kuchagua viongozi na watawala wasiojali miiko ya uongozi, viongozi ambao lengo lao kubwa kuingia madarakani si kutumikia wananchi na kuwapunguzia umasikini, bali ni kuusaka utajiri kwa udi na uvumba. Hao ndiyo wanaotufanya Watanzania wote tuonekane ni wajinga tu mbele ya kina Chavda.

Hao ndiyo wanaowakubali na kuwaamini kina Chavda na maburushi wengine kuwa ni “wafadhili wa Chama” huku ufadhili wenyewe ukitokana na pesa walizotuibia. Mtu anakuibia kijanja mapesa yote hayo katika benki ya umma, na kisha kesho akijenga kisima kwa ajili ya kijiji fulani, au shule ya sekondari au akitoa pesa kidogo kusaidia Chama, tunachekelea kwa furaha huku tukimwita “mfadhili mkubwa wa Chama” na mzalendo wa kweli!

Anayekuibia kwa kutumia mkono wa kulia na kukurejeshea kidogo alichokuibia kwa kutumia mkono wa kushoto; huku akijitia ni mfadhili, utamwitaje “mzalendo wa kweli”? Huyu mahali pake ni jela!

Hivi sasa naambiwa kwamba, kama ilivyokuwa kwa Chavda, Sailesh na Gulamani, Jeetu Patel naye hayupo nchini katika kipindi hiki ambacho kashfa ya ufisadi ya BoT inachunguzwa ili wahusika wakamatwe.

Popote pale walipo huko nje, nina hakika kina Jeetu Patel, kina Chavda na kina Sailesh, watakuwa wakicheka njia nzima wakati wakienda benki (Swiss Bank?) kuchukua mapesa waliyochota kwetu, mapesa ya Watanzania masikini.

John Nolan, yule mwekezaji wa Ireland aliyataka kuighilibu Serikali ya Mkapa imruhusu kufungua mashamba ya prawns ambayo yangeiharibu kabisa Delta ya Rufiji, alipata kusema kwamba; Tanzania ndiyo nchi pekee duniani ambayo Mzungu, Mhindi au Burushi anaweza kuingia akiwa na dola tano tu mfukoni na kuondoka miaka mitano baadaye akiwa milionea! Kweli wajinga ndiyo waliwao!

Email: mbwambojohnson@yahoo.com

Tunalo tatizo kubwa watanzania, tatizo hilo ni viongozi ambao ni wachoyo,waroho ndo maana wanawekwa mifukoni na wahindi kirahisi.
Pia hata sisi wenyewe tunachangia maana kama kiongozi hakuingia madarakani kwa kuiba kula basi tumempigia kura,hivyo basi tunahongwa pilau na kanga vitu vya muda mfupi kwa gharama ya miaka mitano.Sasa basi tuamke tuache kupiga kura za usanii madhala yake tunayaona.
Wasomi vamieni vijijini mkauelimishe umma faida ya kuchagua viongozi bora
maana tunawajua tunaishi nao,tusisubili kuletewa tukiletewa tukatae kwa kauli moja hiyo ndo njia pekee ya kujikwamua .
 
At first nilidhani umeandika mwenye kumbe umechukua nzima nzima kutoka kwenye gazeti?........sasa kwa nini huku-summerize?.....maana wengine ni wavivu sana kusoma the whole article huwa inaumiza macho na especially ukizingatia ume bald alafu na maandishi ya blue......macho yetu wengine ni mabovu tayari...


ok now what is your point again with jeetu Patel?...
 
Fundi Mchundo na Game Theory watakuja sasa hivi waseme NYIE WABAGUZI.

Mie nimeshakubali kuitwa hivyo. Nikija pata nafasi, Wahindi watanyea Debe kwa sana.

Ikibidi kutafuta MAFIA kuwatafuta popote pale duniani ili waje Walipie maovu yao basi ntafanya hivyo. Nafikiri Russia wale Ma-Ex KGB ni bei poa kabisa. Ukraine nako wapo tu. Siku itafika tutabanana nao. M

Msiogope KUTISHWA na maneno ya Wahindi na Genge lao humu ndani. Aisifiaye Mvua imemnyeshea. Sisi mdundo mmoja. Wahindi wakae na kuheshimu nchi yetu na watakaojifanya MUCH NOW, siku moja watalia.

Siku ya kufa nyani IMEKARIBIA.
 
Hakuna ishu ya wahindi kuwaibia waafrika hapa. Ni wajanja wanaokula na wajinga wanaoliwa. Thats it.

Kuna wajanja wakiafrika, wakizungu, wakihindi, wakiarabu, wakiburushi, wakichina na wote wanakula.

Kuna wajinga wakiafrika, wakizungu, wakihindi, wakiarabu, wakiburushi, wakichina na wote wanaliwa.

Ishu hapa ni wajinga kukaa chonjo wasiliwe na wajanja. Ujinga wako usikufanya ukawabagua watu wengine ukidhani wanakuibia. Unaibiwa na wajanja. Period.
 
What if Mengi had declared that all the fisadis were from races X,Y,Z...would articles have been equally written?
 
What if Mengi had declared that all the fisadis were from races X,Y,Z...would articles have been equally written?

This is it. Its the fisadi papa's who played the race card to try and hoodwink Tanzanians, not Mengi.
 
What if Mengi had declared that all the fisadis were from races X,Y,Z...would articles have been equally written?
If Mengi happened to be in India(Indian of Tanzania origin), it would be written, condemned, jailed and his citizenship questioned and deported to unknown!!
 
Back
Top Bottom