fimboyaasali
JF-Expert Member
- Jan 14, 2011
- 8,382
- 7,909
All the best kwakeAkiwa Katibu Bashiru ndo alikuwa mtu pekee ndani ya CCM aliesema waziwazi kuwa CCM haitakubali Kumuongezea mda Rais Magufuli...
Hata kama aliposema alikuwa hana nguvu ya kuzuia...iwapo maamuzi yangejitokeza..
Mradi yupo kwenye rekodi na aliongea waziwazi kuwa ..anataka Rais Magufuli amalize mda wake ..aje mwingine kama ulivyo utaratibu...basi hili moja Tu linatosha kabisa kumkumbuka..
Kama habari za mabilioni zitakuja kujulikana si za kweli basi huyu Bashiru atakuwa kaonewa sana ...
Tusisahau haikuwa kazi rahisi kuwa na msimamo wako tofauti na MATAGA enzi
Za Magufuli na kuusemea waziwazi msimamo wako....lakini Bashiru kwenye hili alisimama na kuhesabiwa waziwazi..
Mimi Kwa hili moja heshima yangu kwake iliongezeka na tuhuma zingine zote nasubiri zithibitishwe ndo nimpe hukumu sahihi...