Tusirudie tena Makosa Kwenye mchakato wa Katiba Mpya

econonist

JF-Expert Member
Jul 11, 2015
15,751
21,740
Waziri wa katiba na sheria ameshatangaza rasmi kwamba mchakato wa katiba mpya utaanza mwezi wa Saba mwanzoni. Nilikuwa na ushauri kwamba makosa yaliyopelekea mchakato wa katiba mpya mwaka 2014 kukwama yasijirudie.

Nimeanisha makosa Kama yafuatayo:

1. Tume ya katiba ndio ipewe mamlaka ya kisheria ya kuandika rasimu ya katiba itakayojadiliwa na kupitishwa na Bunge la Katiba. Tusirudie kosa la kuliachia bunge la Katiba kuandika rasimu yake na kuitupa kapuni ile ya Tume ya Katiba.

2. Kabla ya kuanza mchakato wa katiba mpya, ningeshauri tuanze na kura ya maoni ili wananchi waamue ni mfumo gani wa muungano wanaoutaka. Je wanataka mfumo wa Unitary, Federal au confederation. Wananchi wengi wakikubali mfumo mmojawapo, basi rasimu ya Tume ya Katiba itengenezwe kwa kufuata muundo ulioamuriwa Kwenye kura ya maoni.

3. Rais asioneshe upande wake Kwenye rasimu ya katiba. Ili kosa alilifanya Mh Rais Mstaafu Kikwete. Aliposimama Kwenye bunge la Katiba na kuonesha kwamba yeye anataka katiba ya aina gani, hivyo kupelekea wajumbe wa chama chake kufuata maelekezo yake. Mwisho wa siku katiba mpya haikupatikana. Rais ajitenge kuwapelekesha wanachama wa chama chake wafuate maoni yake baadala yake awaachie Uhuru wa kujadili.

4. Tuangalie mahitaji ya Sasa na sio misismamo ya chama. Tunapoenda kuandika katiba mpya tushughulike zaidi ya matatizo yanayotukumba Leo na namna ya kuyaondoa na sio kuangalia vyama vinataka Nini. Ufisadi, maadili, Uhuru katika uchaguzi, mfumo wa kiuchumi, mamlaka ya bunge, haki jinai, sera ya kimataifa, vyombo vya ulinzi, Uhuru wa mahakama, mamlaka ya Rais, ajira, mfuko wa mapato ya gesi na mafuta, mikopo ya wanafunzi iwe Ruzuku sio mkopo, vyama vya siasa, Tume huru, shirika la Taifa la habari etc.

5. Spika au Mwenyekiti wa bunge la Katiba asitokane na chama Cha siasa. Ateuliwe jaji wa mahakama ya Rufaa ambaye atasimamia bila upendeleo bunge la katiba. Tukiweka watu wa vyama sampuli ya Tulia Akson tutapata bunge la hovyo na litakalo toa rasimu ya hovyo na ya kichama.

NB:Tukirudia makosa hatutapata katiba mpya kamwe, na Kama hatupo tayari kuandika katiba mpya ni Bora kuacha kuliko kufanya maigizo.
 
Rasimu ya Jaji Warioba imejaa madini tupu ya namna gani katiba ya nchi inapaswa kuwa sioni mantiki ya serikali kuunda tume nyingine ya kukusanya maoni wakati tayali maoni yapo wazi ya wananchi huu utakuwa uwendawazimu wa akili za mwafrika kutumia pesa za umma hovyo.

Moja ya makosa ambayo hatupaswi kufanya tena ni kuruhusu kundi kubwa la watu ambalo limejaa vilaza kujadili katiba mfano ni Bunge hivi mbunge kama Msukuma atachangia nini kuhusu katiba

Hivi Kenya mchakato wa kupata katiba mpya walitumia mbinu gani ? Na yapi yalikuwa majukumu ya bunge lao?
 
 
Chaguzi za 2024/25 zifanyike chini ya katiba mpya.

Katiba hii iwe kwa mujibu wa wananchi si chama cha siasa.

Uchawa na ufia vyama iwe kigezo cha kuwachuja wajumbe.
 
Rasimu ya Jaji Warioba imejaa madini tupu ya namna gani katiba ya nchi inapaswa kuwa sioni mantiki ya serikali kuunda tume nyingine ya kukusanya maoni wakati tayali maoni yapo wazi ya wananchi huu utakuwa uwendawazimu wa akili za mwafrika kutumia pesa za umma hovyo.

Moja ya makosa ambayo hatupaswi kufanya tena ni kuruhusu kundi kubwa la watu ambalo limejaa vilaza kujadili katiba mfano ni Bunge hivi mbunge kama Msukuma atachangia nini kuhusu katiba

Hivi Kenya mchakato wa kupata katiba mpya walitumia mbinu gani ? Na yapi yalikuwa majukumu ya bunge lao?

Kweli kabisa mkuu. Turudishe rasimu ya warioba ndio ijadiliwe bungeni.
 
Chaguzi za 2024/25 zifanyike chini ya katiba mpya.

Katiba hii iwe kwa mujibu wa wananchi si chama cha siasa.

Uchawa na ufia vyama iwe kigezo cha kuwachuja wajumbe.
Kweli kabisa. Wajumbe wawe watu wenye fikra huru sio za kushikwa na chama.
 
What's is the point ya bunge la katiba 'kujadili' ikiwa hawawezi kufanya maboresho yoyote kwenye hiyo rasimu?

Hilo la muungano ndio hata msithubutu, mtakuwa wajinga wakubwa kama hamkujifunza kwenye ile rasimu iliyokwama.

Hakuna taifa la kipumbavu duniani linalo hatarisha uhai wake kwa kura za maoni! Hilo la muundo wa muungano achaneni nalo.
 
What's is the point ya bunge la katiba 'kujadili' ikiwa hawawezi kufanya maboresho yoyote kwenye hiyo rasimu?

Hilo la muungano ndio hata msithubutu, mtakuwa wajinga wakubwa kama hamkujifunza kwenye ile rasimu iliyokwama.

Hakuna taifa la kipumbavu duniani linalo hatarisha uhai wake kwa kura za maoni! Hilo la muundo wa muungano achaneni nalo.

Na muundo wa muungano usiposhughulikiwa hakuna haha ya katiba mpya turndelee na ya Sasa hivi. Kura ya maoni ilitumika kwenye kuleta serikali ya umoja wa kitaifa Zanzibar kwanini ni ngumu kuamua muungano.
 
What's is the point ya bunge la katiba 'kujadili' ikiwa hawawezi kufanya maboresho yoyote kwenye hiyo rasimu?

Hilo la muungano ndio hata msithubutu, mtakuwa wajinga wakubwa kama hamkujifunza kwenye ile rasimu iliyokwama.

Hakuna taifa la kipumbavu duniani linalo hatarisha uhai wake kwa kura za maoni! Hilo la muundo wa muungano achaneni nalo.

Kuna maboresho na kuandika upya. Bunge la Katiba liboreshe sio kuandika rasimu yao mpya.
 
Back
Top Bottom