Tusipotoshane, kulikuwa na sababu za msingi kabisa kwanini Marais waliopita hawakununua ndege kama awamu hii ya tano ilivyofanya

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Huwa nachukia sana ninaposikiliza viongozi wetu wakitumia cheap propaganda na kutamba juu ya mafanikio yao kwa kujilinganisha na viongozi waliopita. Kwa mfano, mara kadhaa nimesikia tamko kwamba awamu zilizopita hawakuweza kununua ndege kama awamu ya sasa.

Watu wanaoeneza hizi propaganda huwa hata hawashughulishi ubongo wao kwa kujiuliza kwa nini awamu zilizopita hawakununua ndege kama awamu hii ya tano. Wanasahau kuwa hali za sasa na wakati ule ni tofauti kabisa na kwamba kila raisi anakuwa na vipao mbele vyake, hivyo huwezi kufanya huo ulinganifu.

Tumchukulie Nyerere kwa mfano. Kumbuka wakati fulani, kulikuwa na wimbi la kuanzishwa vituo vya television. Nyerere alipopewa pendekezo la kuanzisha television ya taifa alikataa. Akasema, kwanza ni nani watakaokuwa na uwezo wa kununua television nchini, hawa wakulima na wafanya kazi wetu? Pili akauliza, hizo gharama za kuendesha television ya taifa, tutazimudu vipi pamoja na kuhakikisha inapatikana nchini kote ikiwa radio tu inatupa shida kuna sehemu za nchi inasikika kwa taabu? Kisha akamalizia kwa kusema kuwa na television ya taifa kwa wakati huo hakukuwa jambo la msingi la kupewa kipao mbele, lakini itafika wakati muafaka wa kuwa na television ya taifa. Zanzibar wao walisema wangeanzisha, wakidai gharama yao isingekuwa kubwa kutokana na udogo wa kisiwa.

Sasa fast forward. Katika hali yetu hii ya sasa, fikiria Mwalimu Nyerere ndiye angekuwa Rais wa Tanzania, halafu unatoa pendekezo kwamba Tanzania tununue Dreamliner, Airbus na Bombardier, kwa kuwa fedha za walipa kodi zipo za kuweza kununua ndege hizo. Kumbuka ni Nyerere yule ambae alikuwa akisema ushindani wa kibiashara na mataifa makubwa ni mgumu sana, watatumia kila mbinu kukufanya usifanikiwe na wewe kwa umasikini wako utakuwa huna la kufanya. Hata aliwahi kuuliza, hivi mnafikrir benki yetu ya Taifa NBC inaweza kwenda Uingereza na kufungua tawi pale London ikafanikiwa kirahisi tu? Lakini wao wakitaka kuja kwetu, kwanza wanakupa masharti, ivunje NBC vipande vipande kwanza ili tushindane nayo!

Ni Nyerere huyo huyo, miaka ya 1983 - 85 dhahabu ya Bulyanhulu ilipogunduliwa kwa ubia kati ya serikali na kampuni za Outo Kumpu na Kone Corp aliwakatalia kugawana faida kwa 49% Tanzania na wao 51% akawaambia Tanzania iwe na 51% na wao 49%. Walipokataa akawaambia kama hawataki waondoke, akisema iacheni hiyo dhahabu ikae huko shimoni, kwani itaoza? Akasema wazi wakati muafaka ukifika tutaichimba hiyo dhahabu, hata kama ni vizazi vyetu vijavyo. (Kwa kusikitisha baadae Mkapa alikubali 5%, wala sio ile 49% aliyokataa Nyerere ili tupewe 51%).

Sasa tumia akili zako na za kuambiwa kutambua Nyerere angekupa jibu gani; sawa tukanunue ndege, au hapana si wakati muafaka?

Kwa hiyo kabla ya kufanya hizi cheap propaganda kuwa viongozi huko nyuma hawakununua ndege kama awamu hii, tujiulize kwanza kama hao viongozi wa huko nyuma wangekuwa ndio maraisi leo hii wangenunua ndege au la, na kwa nini.
 
Kuna mamia ya mipango kaikutaRais Magufuli ikiwa imeanzishwa na Jakaya mf. ujenzi wa kuiunganisha Katavi-Tabora,Katavi-Kigoma, Katavi-Sumbawanga leo ikikamilika sifa kwa Magufuli.

Upanuzi wa uwanja wa ndege Dar, leo unauliza mimi nimenunua ndege wao walikuwa wapi? bila kuelewa kuna mamia ya miradi ilifanyika pia ambayo leo hii wewe unapata urahisi wa kufanya mradi 1 maana mingine ishafanywa
 
Watanzania hawajaenda shule. Reasoning kwao ni mtihani.

Ndio maana kila ujinga unasemwa majukwaani na watu wanajichekesha tu.

Miaka nenda rudi mnasoma vitabu kama cha Walter Rodney cha How Europe Underdeveloped Africa. Wakati waafrika wenyewe kwa wenyewe mnanyimana maendeleo.

Unanunua ndege wakati barabara zimekatika watu wamelala njiani, kuna sehemu watu hawana maji safi na salama, elimu duni, afya ndo hohehae.

Hata hao wanaotengeneza hizo ndege hawafanyi hiyo biashara moja kwa moja. Either wananunua hisa kidogo au waachia sekta binafsi ihusike na risk zote wao wanabaki kama regulators.

Usimlaumu beberu kwa ujinga wako wa kukosa maendeleo manake hata Australia, Singapore, Japan, Brazil walitawaliwa kama nyie ila wao wakawa na vipaumbele vinavyomake sense. Wakafika hapo walipo.

Wanasema afrika ni kama jungle. Mnaishi kama wanyama.
 
kuna mamia ya mipango kaikuta magu ikiwa imeanzishwa na jakaya mf. ujenzi wa kuiunganisha katavi-tabora,katavi-kgm, katavi-sumbawanga leo ikikamilika sifa kwa magu

upanuzi wa uwanja wa ndege dar, leo unauliza mimi nimenunua ndege wao walikuwa wapi? bila kuelewa kuna mamia ya miradi ilifanyika pia ambayo leo hii ww unapata urahisi wa kufanya mradi 1 maana mingine ishafanywa
Mie naweza nisiwe na tatizo sana kuhusu Tanzania kununua ndege, ikiwa tuna mikakati madhubuti ya kujiendesha kwa faida na sio tu kutafuta sifa ya kununua Dreamliner mbili. Kinachonikera na kunishangaza ni pale ambapo tunaambiwa hawa waliopita hawakuweza kununua ndege!

Hawa waliopita walikuwa na dhamira safi kiasi kwamba wasingeweza kuvumilia kununua ndege dhidi ya vipao mbele vingine. Nyerere siku zote alikuwa anajiuliza faida na hasara ya kufanya kitu fulani - na hata kama ni faida, ni faida kwa nani, majority au minority?

Huyu Nyerere ambae aliekataa watu kununua salon cars kama Benz na BMW na kuwataka wanunue pick up, leo unaweza kudiriki kusema hakununua ndege kama awamu ya tano? Huyu ambae alisema viongozi watatumia Land-Rover 109? You have to be a psychiatric case kumfikiria Nyerere hakununua ndege kwa kuwa hakuweza kama inavyofanyika sasa. For Nyerere it was always a matter of calculated choice, not just financial capability.
 
Hotuba zote Ndege,fly over ,uwanja wa ndege na vijembe hakuna mpya
Na watu wanapolinganisha uzalendo wa awamu ya tano na Nyerere wasiwe wanasahau vitu kama hiki nilichotaja hapo juu;

Ni Nyerere huyo huyo, miaka ya 1983 - 85 dhahabu ya Bulyanhulu lipogunduliwa kwa ubia kati ya serikali na kampuni za Outo Kumpu na Kone Corp aliwakatalia kugawana faida kwa 49% Tanzania na wao 51% akawaambia Tanzania iwe na 51% na wao 49%. Walipokataa akawaambia kama hawataki waondoke, akisema iacheni hiyo dhahabu ikae huko shimoni, kwani itaoza? Akasema wazi wakati muafaka ukifika tutaichimba hiyo dhahabu, hata kama ni vizazi vyetu vijavyo. (Kwa kusikitisha baadae Mkapa alikubali 5%, wala sio ile 49% aliyokataa Nyerere ili tupewe 51%).
 
Wakati huo tukinunua mindege kwa mabilioni lukuki bado vijijini watu wetu wanaishi maisha kama haya hapa chini
Hiyo ndio sababu ungempa Nyerere kwa nini inatupasa tununue ndege? Kwamba tununue ndege ili tuwaonyeshe watu hatufi kiuchumi pamoja na kuwa sisi ni mojawapo wa mataifa ambayo ni LDC (Least Developed Countries)
tapatalk_1465466123084.jpeg
 
kuna mamia ya mipango kaikuta magu ikiwa imeanzishwa na jakaya mf. ujenzi wa kuiunganisha katavi-tabora,katavi-kgm, katavi-sumbawanga leo ikikamilika sifa kwa magu

upanuzi wa uwanja wa ndege dar, leo unauliza mimi nimenunua ndege wao walikuwa wapi? bila kuelewa kuna mamia ya miradi ilifanyika pia ambayo leo hii ww unapata urahisi wa kufanya mradi 1 maana mingine ishafanywa
Lkn bado kuna watu wanashangilia mpaka wanapoteza fahamu
 
Watanzania hawajaenda shule. Reasoning kwao ni mtihani.

Ndio maana kila ujinga unasemwa majukwaani na watu wanajichekesha tu.

Miaka nenda rudi mnasoma vitabu kama cha Walter Rodney cha How Europe Underdeveloped Africa. Wakati waafrika wenyewe kwa wenyewe mnanyimana maendeleo.

Unanunua ndege wakati barabara zimekatika watu wamelala njiani, kuna sehemu watu hawana maji safi na salama, elimu duni, afya ndo hohehae.

Wanasema afrika ni kama jungle. Mnaishi kama wanyama.
Hakika hatuwezi kuepuka kudharaulika.
tapatalk_1560223696337.jpeg
FB_IMG_1493111377454.jpeg
 
Synthesizer Huwa nachukia sana ninaposikiliza viongozi wetu wakitumia cheRejea aya yako ya mwisho ungundue kuwa umechinganya katika hoja. Katija hiyo unakubali kila nyakati ina maamuzi yake na ndivyo Baba wa Taifa alishauri/kutabiri na matokeo yake ndiyo mabadiliko tunayoshahudia kwa sasa na wala siyo kubeza tawala zilizopita.
 
Synthesizer, Huwa nachukia sana ninaposikiliza viongozi wetu wakitumia Unajichanja mwenyewe unajiinika mwenyewe, hatukuwa na TV ila yeye alikuwa nazo, huyu mwingine angenunuaje ndege wakati dhahabu iliyokataliwa 45% yeye kakubali kwa5%, kunyamaza napo ni busara
 
Rejea aya yako ya mwisho ungundue kuwa umechinganya katika hoja. Katija hiyo unakubali kila nyakati ina maamuzi yake na ndivyo Baba wa Taifa alishauri/kutabiri na matokeo yake ndiyo mabadiliko tunayoshahudia kwa sasa na wala siyo kubeza tawala zilizopita.
Sijakuambia nakataa hilo. Ninachopinga ni cheap propaganda za watu wasio na busara kupigia debe ununuaji wa ndege kwa namna ya kuonyesha wao wanafanya hivyo kwa kuwa wao ni viongozi bora kuliko hao wa nyuma ambao hawakununua ndege. Soma uelewe.
 
Nyerere alinunua ndege 12 je kipindi hicho kipaumbele cha taifa ilikuwa kununua ndege?
Ndege zitanunuliwa haijalishi mnataka au hamtaki.
Hebu tuambieni ni wakati gani Nyerere alinunua ndege 12. Ni lini ATC ilikuwa na ndege 12, zaidi sana ya zile ilizorithi toka East African Airways.

Nachokumbuka ATC walikuwa na ndege 2 Boeing 737 baada ya EAA kuvunjika, pamoja na Fokker Frienship. Na moja ya Fokker waliyotumiwa ni ile Nyerere alipewa zawadi nadhani na nchi fulani siikumbuki. Hili la wakati fulani ATC kuwa na ndege 12 zilizonunuliwa na Nyerere wengine tunahitaji kukumbushwa. Hizo ndege 12 zilikuwa zikienda wapi?
 
Back
Top Bottom