Tusipotezeane muda! Ukweli ni kwamba 'Ulidanganywa' na 'Wanafiki' kuhusu Kabudi na Lukuvi, ila sasa 'Unatuzuga' na 'Kujikosha' tu Kwao

Mtu yeyote mwenye akili timamu kama hakubaliani na jambo best option ni kujiuzuru.

Hao jamaa zako ni wachumia tumbo tu, hawajiamini na wanaona hakuna maisha nje ya mfumo wa kula kodi za wananchi.
Labda ungewashauri watoroke wakimbie nchi! Hawa viongozi wa kiafrika wengi wana hila mnoo. Ukienda kinyume chao utashangaa kesho una kesi ya mwaka juzi na sheria zetu hizi! Bora wakae tu hapo anapotaka wakae basi mradi anawalipa.
 
Siku chache baada ya Rais Samia Suluhu Hassan kusema kuwa atamvuta Ikulu aliyekuwa Waziri wa Ardhi, William Lukuvi, leo Januari 13, 2022 Rais Samia amesema kiongozi huyo atakuwa akisaidiana na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa kusimamia sekta zenye migogoro baina ya viongozi.

Chanzo: Habari Leo Online

Mpaka leo naitafuta sababu ya Kutolewa kwa akina Kabudi na Lukuvi katika Nafasi zao huku Utendaji wao ukiwa ni wa Kutukuka na Uaminifu kabisa bado sijazipata.

Kama unatambua kuwa Kabudi ni 'Baba Negotiations' kutokana na Unguli wake katika Sheria hivi Akili Kubwa ilikuwa ni Kumbakisha katika Utendaji ndani ya Wizara au kumtoa na Kumuweka karibu kama Mshauri na Msoma Magazeti tu 24/7 katika 'Chambers' za Ikulu za Magogoni na Chamwino?

Ni Mtanzania Zuzu ( Hambe ) tu pekee ndiyo hatoweza kujua Kazi Kubwa na Juhudi za Kutukuka alizofanya Lukuvi katika Sekta ya Ardhi na cha Kushangaza anatolewa na Kupelekwa kuwa Mshauri tena kwa Waziri Mkuu ambaye nae pia mpaka sasa 'anakonda' na hapati Usingizi kwakuwa ameshajua hatakiwi ila basi tu hakuna namna na anavutiwa Kasi.

Akina GENTAMYCINE mara kwa mara tuwapo hapa JamiiForums tunakuambia Wasaliti wako Wakubwa ni akina nani ( hadi kukutajia Majina ) yao cha Kushangaza unawaacha, upo nao na unakimbilia Kuwaondoa Wazee wa Watu kwakuwa tu walikuwa 'Loyal' kwa Hayati uliyemrithi na Kuhisi wanaweza 'Kukuangusha' kwa Kutumika na Unaowaogopa au Kudanganywa kuhusu Wao.

Sijui ni kwanini Viongozi wengi wa Afrika mnapenda sana kutufanya na Kudhani kuwa Waafrika wote ni Wapumbavu ( Mapopoma ) wakati kumbe kuna Wananchi ( Waafrika ) wana ( tuna ) Akili na Maono kuliko mlivyo na 'Mabenzi' yenu huko Ikulu.

Kwenu Wazee wangu Kabudi na Lukuvi poleni kwa Kudharauliwa, Kusanifiwa na Kupendwa Kimachale na Kimkakati kwani hakuna namna bali ni Kumshukuru tu Mwenyezi Mungu kwa kila Jambo na Kumuachia Yeye kila Kitu kwani inajulikana kuwa Siku zote Malipo huwa ni hapa hapa duniani.

Najua utanichukia ila Mimi Nakupenda.
Acheni serikali ichape kazi. Watanzania waliosoma na wenye uwezo wa kuongoza ni wengi mno. Acheni serikali ifanye kazi.
 
Back
Top Bottom