Tusiporudisha pesa za Covid 19 za EU nini hatima yake?

Rufiji dam

JF-Expert Member
Feb 20, 2020
3,803
8,786
Sina haja ya kusema mengi, ila mada ipo hivyo. Nchi imepakwa matope sana na muda tuliopewa wa kujieleza wa masaa 48 unaenda kujikita mwisho. Je tusiporudisha hizo pesa za Corona za EU nini hatima yetu? Je ndege zetu zinaweza kukamatwa tena? Na hizi pesa uwa zinafikia wapi je ni mtoto wa dada ndio anazilinda? Na kwanini kulikuwa na usiri mkubwa katika kupewa hizi pesa?

Sent from my SM-J260F using JamiiForums mobile app
 
Pesa hairudi hiyo. Watakwambia waliitumia kwenye preparedness actions. Afterall, COVID19 ilikuwepo na data zilikuwa shared kabla mambo kubadilika.

Hawatoshindwa kujustify matumizi.
 
Vyombo vyote vya habari vinaongelea upande wa Idd Amini hivyo misaada inavyoingia zinakuwa ni Siri zao huku TBC 'CCM wakitangaza tunatumia hela za ndani kumbe wamechukua misaada ,mnakumbuka pesa za maafa ya Kagera ,zile pesa zilihongwa watu na kununuliwa wapinzani sasa leo mumechukua pesa ya mwanaume jiandaeni kugeuzwa nyuma
 
Mpaka lini tutaendelea kusumbuliwa na pesa za watu sasa, hapa ndo umuhimu wa kuwateka upinzani unakuja
 
Sina haja ya kusema mengi, ila mada ipo hivyo. Nchi imepakwa matope sana na muda tuliopewa wa kujieleza wa masaa 48 unaenda kujikita mwisho. Je tusiporudisha hizo pesa za Corona za EU nini hatima yetu? Je ndege zetu zinaweza kukamatwa tena? Na hizi pesa uwa zinafikia wapi je ni mtoto wa dada ndio anazilinda? Na kwanini kulikuwa na usiri mkubwa katika kupewa hizi pesa?

Sent from my SM-J260F using JamiiForums mobile app
Inamaana tuliweka msiba tukafunga turubai wakati hatujafiwa?
 
Back
Top Bottom