Tusipokuwa makini, kifuatacho ni kusikia ajali za Mabasi ya Mwendo kasi na Treni ya Stesheni-Pugu

Mara zote tunasubiri ajali zitokee ndo tuchukue hatua,

Nimebahatika kuyapanda mabasi ya mwendo kasi Kivukoni - Kimara,
Gerezani- kimara,

Kwanza Utaratibu ni mbovu kuliko mabasi yetu ya zamani ya foreni,

Mle watu wanakimbilia, watu wanagombana kuingia ,mpaka unajiuliza kumbe sisi mazuzu tunaacha ya 400 wanayokaa vizuri tu, unakimbilia la 650 ambalo huna hewa , wanajaza mpaka hakuna mfno,

Hapa nawahurumia watoto wadogo, mama wajawazito, wazee, walemavu na wagonjwa, hawez kupanda mwendo kasi akiwa kimara asubuhi, wala hawez panda mwendokasi akiwa gerezani kariakoo jion, ni fujo na vurugu,

Hapa ilibidi uwepo Utaratibu wa kuwa monitor abilia kwa idadi anayekuja akiwa wa Kwanza ndo apande akiwa wa kwanza,

Nimeyapanda mwezi wa Sita nikaona kumbe tulio mbali tunarushiwa picha kuonesha yalivyo kumbe huduma zao mbaya mno,
Wao wako busy kukusanya Hela,

Kwa Treni ya Stesheni mpaka pugu huko wanajaza kupita kiasi, narudia tusitake kukaa tunaomboleza

Britannica
Siku ajali ikitokea mfano ikachinja mamia ya watu ndio kila mtu utamsikia anavyokurupuka kutoka shimoni mara kamata yule, funga yule, mara utasikia marufuku kibao. Lakini saa hivi yanafanyika makosa makubwa ya kujaza abiria kwenye mabasi yale na treni hakuna anayesema. Yale mabasi ya mwendokasi ni kama kusema hayana kiwango cha abiria mapaka wajae hadi milango ishindwe kufunga ndio basi linaondoka. Tunachezea moto!
 
Mkuu tunaomba ututolee huo uchuro wako, ungekua mtabili ungetabili kabla ya hiyo ajali, mabasi ya mwendokasi bado ni usafiri salama sana kwa abilia, na hata siku ikitokea ajali itakua ni kwa sababu zingine za kibinadamu lakini sio kwa hizo sababu ulizotaja. Kwanza inaonesha wewe sio mtu wa Dar, mradi huo walijitahidi sana kuzingatia suala zima la usalama kwa sisi tuliosoma mambo ya usalama mahali pa kazi tunajua hilo.Tatizo la watanzania kila mtu atajidai anajua, mwisho mtaanza kutwambia hata kuingia chooni ni hatari.
Mungu wangu!
 
Kwahiyo unawatetea?
Sijatetea, naweka taarifa sawa. Kusema wako na mabus 300 ni kama unawapa kitu wasichokuwa nacho, wakati uhalisia usafiri ni wa shida na walitakiwa kuwa na mabus zaidi ya hayo 300 katika hali ya kawaida.


Nadhani umenielewa
 
Mkuu kumbe umeona kero ya hayo mabasi? Mimi huwa najiuliza inakuwaje mradi ambao hauna hata miaka minne unaendeshwa kwa ubora wa chini kiasi hicho? Najiuliza iwapo rais anaweka miundo mbinu zaidi kama reli, ndege, itaendeshwa kwa ufanisi kweli? Tutaweza kulipa hilo deni iwapo uendeshaji ndio huo mbovu kiasi hicho? Mradi ulianza na mabasi 600, sasa hivi hayafiki 300 barabarani huku yakiwa yanajaza abira kila safari. Nilitarajia ndani ya awamu ya rais Magufuli nione mradi kama huo ukijiendesha kwa ufanisi lakini ni kinyume chake. Sasa najiuliza haya maendeleo ya hela za mikopo tunayojigamba nayo tutaweza kulipa hizo hela kwa uendeshaji wa mashirika kwa hali hii?
Mkuu data zako zipo sahihi kweli kama yalianza na magari 600
 
Mkuu data zako zipo sahihi kweli kama yalianza na magari 600

Inawezekana haukuanza na mabasi 600 lakini hilo ndio debe tuliloaminishwa na kwamba mabasi yangeendelea kuja kufikia idadi hiyo, ukiachia kadhaa yaliyoanza mradi. Huu ni mwaka 3+ lakini hata yaliyoanza yamepungua, na sababu za kupungua ni za kiubabaishaji.

Hali hii naifananinisha ni zile mbwembwe za gas ikifika Dar itakuwa muarobaini wa nishati nchini, saa hii tunasikia imebaki mwaka na nusu tuanze kulipa mkopo, huku bomba hilo likiwa limetumika kwa 6% na tumerukia kwenye SG.
 
Huu mradi haujawahi kuwa na mabus 600 wala sahivi hayapo 300,

Mabus yalikuwa 140 mwanzoni mwa mradi, wakaongeza mengine 70 bado yapo bandarini ili kufanya yawe 210,

Tambua bado mabus yapo 140, haya ukipunguza yanayokuwa kwenye maintenance ndo utajua yanabaki mangapi yanayofanya kazi.

Kula tano kwanza ndugu kwa kuweka rekodi sawa. Hiyo idadi ya 600 ni debe walilopiga wanasiasa ili kupata kura kwani mradi huu ulikamilika karibu kabisa na uchaguzi. Walisema mradi utaanza na 300 buses kufikia 600 kadiri mradi unavyokuwa. Sikatai kwamba ulianza na 140 buses kwani huenda ndio ukweli, lakini kilichokuwa kinahubiriwa ni hadithi za idadi ya 300+ kwenda 600.

Sishangai hadithi za kuweka chumvi kwa wanasiasa wetu kwani hiyo ndio tabia yetu. Mfano tunaambiwa miradi mingi inaendeshwa kwa pesa zetu, huku nyuma ya pazia watu wanaenda kukopa ili kuuongopea umma kwamba mambo ni mazuri kupitia fedha zetu. Ndani ya hii miaka mitatu ya awamu hii deni la taifa limepanda kwa 10t+, wastani wa 3t@yr. Je unaona popote hilo likiwekwa wazi zaidi ya kuonyesha hela yetu ya makusanyo ndio inafanya haya? Mradi wa stiegler gorge ni wa 3t kwa mijubi wa serekali, na tuliambiwa fedha za mradi zipo hadi tender ikatangazwa. Je hatujaona hela zikienda kukopwa?
 
Ungefika Tokyo usingeshangaa treni ya pugu kujaa. Kule treni rush hour zinajaa balaa. Sema zina AC na mazagazaga kibao.
 
Kiongozi wa nchi kutoa salamu za rambirambi ni sifa kwake na inamuongezea kupendwa na wananchi. Sasa wasipokufa wengi atasema nini. Tuko tayari kupata sifa binafsi kwa gharama ya maisha ya watanzania. Leo asubuhi radio moja imepiga wimbo wa mwinjilisiti mmoja unaolaumu watu kujionesha kwenye misiba badala ya kusaidia wagonjwa nikakumbuka ubani wa 500 badala ya kununua kivuko kipya.
 
Huu mradi haujawahi kuwa na mabus 600 wala sahivi hayapo 300,

Mabus yalikuwa 140 mwanzoni mwa mradi, wakaongeza mengine 70 bado yapo bandarini ili kufanya yawe 210,

Tambua bado mabus yapo 140, haya ukipunguza yanayokuwa kwenye maintenance ndo utajua yanabaki mangapi yanayofanya kazi.

Toka story za yapo bandarini miezi zaidi ya 9 imepita
 
Wamedisable mabasi mengine wakamonopolize watu wanatupanga kama kuku hakuna kwa kulalamikia anyway tuishi tu no way out
kwa mtazamo wangu tatizo lilianzia hapo.kuondoa daladala nyingine hapo ndo kufeli kulipoanzia
 
Back
Top Bottom