Tusipakane mafuta kwa mgongo wa chupa, Mwl. Nyerere hakuwa mwanademokrasia!

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,171
23,975
Nimejiuliza maswali mengi baada ya kumewasikia wachangiaji karibu wote kwenye kusanyiko linaloitwa ‘’ kongamano la kumbukizi ya miaka 20 ya kifo cha mwalimu Julius Nyerere’’ wakitoa mchanganuo wa maisha ya Mwl. Nyerere kama raia wa kawaida na Kiongozi Mkuu wa Tanganyika na Tanzania.

Miaka 29 ni mingi sana tokea Mwalimu Nyerere alipoachia ngazi ya Mwenyekiti wa CCM Taifa na kuwa mwananchi wa kawaida. Hii ina maana kuwa mtu mwenye miaka 28 hapa nchini hakuwahi kuona utendaji kazi wa Mwalimu Nyerere serikalini na ndani ya CCM. hili ni kundi la vijana ambalo kwa sasa lina watoto wenye umri wa miaka 11 kisheria kwa sababu umri wa kuanza kufanya mapenzi nchini ni miaka 18.

Kama wale wachangiaji niliowaona kwenye kongamano ndio tunawategemea sana katika mawazo yao kwenye kulijenga taifa basi hili taifa litaendelea kugubikwa na unafiki mkubwa ambao ni sumu kwa maendeleo chanya.

Bila kuondoa unafiki na kuwa wakweli hatuwezi kujua madhaifu yaliyolifanya taifa hili kupiga hatua za kusua sua katika nyanja za kisiasa, kijamii na kiuchumi.

Tunajua sheria za maumbile(laws of nature)zimetupa angalizo kuwa ili kitu kiwe kamili lazima kiwe na pande mbili. Hata nguvu za kifizikia ziko za aina mbili mbili ambazo ni hasi na chanya.

Nakumbuka wakati nikisoma shule ya ‘’ngumbalu’’ tulikuwa tunafanya makongamano na midaharo ambayo lazima iwe na pande mbili zinazoitwa wanaokubaliana (The affirmative or Aff) na wasiokubaliana (the Negative or Neg).Hii yote ni kukamilisha takwa la sheria za maumbile ambayo ndani yake kuna fikra.

Kamusi ya kiswahili sanifu inasema, kongamano/mdahalo ni majadiliano yanayofanywa na pande mbili zinazokinzana kuhusu suala fulani kwa kueleza sababu na ithibati ya msimamo wao tofauti na kufikia hitimisho la pamoja.

Kile kilichoitwa ‘’kongamano la kumbukizi ya miaka 20 ya kifo cha mwalimu Julius Nyerere’’ hakikuwa na kiwango kinachokidhi kuitwa kongamano kwa sababu wachangiaji wote walikuwa wanaonyesha upande mmoja wa Mwl. Nyerere katika maisha yake.

Mimi sina tatizo na kazi zilizofanywa na Mwl. Nyerere bali tatizo langu ni kuendelea kuchora/kutendeneza picha yake kama vile Mwl. Nyerere hakuna binadamu kwa maana kuwa hakuwa na mapungufu ya kibinadamu na kiuongozi.

Nadhani wale wanataka kumjua vizuri Mwl. Nyerere hawakuweza kupata upande wake wa pili kama ulivyobainishwa katika maandiko mengi na hasa kutoka kwa Mtanzania aitwaye Ludovic S. Mwijage katika maandiko yake kwenye vitabu mbali mbali ambavyo baadhi ni;

1)Dark side of NyerereLegacy-1996.
2) Julius K. Nyerere: Servant of God or Untarnished Tyrant?-2010.

Watu kama Ludovic Mwijage walitakiwa pia watoe michango yao katika kongamano hili ili upande wa pili wa Mwl. Nyerere ueleweke na kueleweka kwa upande wa pili ungesaidia kutoa fundisho zuri kwa vizazi vijavyo.

Waandaaji wa kongamano walishindwa vipi hata kumualika James Brennan ambaye amefanya utafiti na kukusanya mawazo ya watu mbali mbali kuhusu Mwl. Nyerere na kuyaweka katika kitabu kinachoitwa , Nyerere through the Eyes of His Critics, 1953-2013

Wangeweza hata kumualika mwanaJamiiforums mwenzetu, Mzee Mohamed Said ambaye ni mwandishi na mhariri wa maandiko mengi yenye mlengo wa kushoto kuhusu Mwl. Nyerere.

Tuache kuufanya mijadala kama hii iwe niya kinafiki kisiasa kama sehemu ya kuifundisha jamii yetu bali tufanye mijadala yenye pende mbili zenye mitazamo tofauti kama sehemu ya kuchambua ''pumba na mchele'' katika kuujua ukweli kwa sababu ukweli hujenga.

Walioandaa kinachoitwa ‘’kongamano la kumbukizi ya miaka 20 ya kifo cha mwalimu Julius Nyerere’’ haikuwa ni kongamano bali ni mkusanyiko wa wapiga propaganda zenye unafiki.

Tuache unafiki, tulitendee haki taifa letu na vizazi vijavyo!
 
Unafiki ndio maana uwa namkubali Tundu Lissu uwa amngunyi maneno inapokuja kwenye kusimamia ukweli.

Tundu Lissu : Nyerere alizoea kuishi kwa uongo.

hakuna binadamu anaweza kuwa perfect 100% ilo halipo.

Nyerere ni Baba wa Taifa letu pamoja na kuwa mzalendo na mtu wa watu ila kuna vitu aliacha vikiwa vya ovyo ni swala la muungano fake na katiba ya chama kimoja kuiweka ndani ya vyama vingi.
 
Unafiki ndio maana uwa namkubali Tundu Lissu uwa amngunyi maneno inapokuja kwenye kusimamia ukweli.

Tundu Lissu : Nyerere alizoea kuishi kwa uongo.

hakuna binadamu anaweza kuwa perfect 100% ilo halipo.

Nyerere ni babu yetu pamoja na kuwa mzalendo na mtu wa watu ila kuna vitu aliacha vikiwa vya ovyo ni swala la muungano fake na katiba ya chama kimoja kuiweka ndani ya vyama vingi.
Mkuu;

Hata Lissu ni walewale, usimpe hizo sifa kwenye kusimamia ukweli. Lissu pia ni mwanasiasa mnafiki kama walivyo wanasiasa wengi hapa nchini.

Kwa ujumla huwezi kuwa mwanasiasa nchini kama wewe sio mnafiki kwa sababu siasa zetu haziruhusu wagombea binafsi.

Vyama vya siasa vyenye madiwani na wabunge vimejengwa katika misingi ya kinafiki nchini. Huu ni ukweli.
 
Back to Histoey!! Nyerere alikuwezesha Kusoma mpaka University with Government grants hakukua na Loan Board. Ulikua
Nimejiuliza maswali mengi baada ya kumewasikia wachangiaji karibu wote kwenye kusanyiko linaloitwa ‘’ kongamano la kumbukizi ya miaka 20 ya kifo cha mwalimu Julius Nyerere’’ wakitoa mchanganuo wa maisha ya Mwl. Nyerere kama raia wa kawaida na Kiongozi Mkuu wa Tanganyika na Tanzania.

Miaka 29 ni mingi sana tokea Mwalimu Nyerere alipoachia ngazi ya Mwenyekiti wa CCM Taifa na kuwa mwananchi wa kawaida. Hii ina maana kuwa mtu mwenye miaka 28 hapa nchini hakuwahi kuona utendaji kazi wa Mwalimu Nyerere serikalini na ndani ya CCM. hili ni kundi la vijana ambalo kwa sasa lina watoto wenye umri wa miaka 11 kisheria kwa sababu umri wa kuanza kufanya mapenzi nchini ni miaka 18.

Kama wale wachangiaji niliowaona kwenye kongamano ndio tunawategemea sana katika mawazo yao kwenye kulijenga taifa basi hili taifa litaendelea kugubikwa na unafiki mkubwa ambao ni sumu kwa maendeleo chanya.

Bila kuondoa unafiki na kuwa wakweli hatuwezi kujua madhaifu yaliyolifanya taifa hili kupiga hatua za kusua sua katika nyanja za kisiasa, kijamii na kiuchumi.

Tunajua sheria za maumbile(laws of nature)zimetupa angalizo kuwa ili kitu kiwe kamili lazima kiwe na pande mbili. Hata nguvu za kifizikia ziko za aina mbili mbili ambazo ni hasi na chanya.

Nakumbuka wakati nikisoma shule ya ‘’ngumbalu’’ tulikuwa tunafanya makongamano na midaharo ambayo lazima iwe na pande mbili zinazoitwa wanaokubaliana (The affirmative or Aff) na wasiokubaliana (the Negative or Neg).Hii yote ni kukamilisha takwa la sheria za maumbile ambayo ndani yake kuna fikra.

Kamusi ya kiswahili sanifu inasema, kongamano/mdahalo ni majadiliano yanayofanywa na pande mbili zinazokinzana kuhusu suala fulani kwa kueleza sababu na ithibati ya msimamo wao tofauti na kufikia hitimisho la pamoja.

Kile kilichoitwa ‘’kongamano la kumbukizi ya miaka 20 ya kifo cha mwalimu Julius Nyerere’’ hakikuwa na kiwango kinachokidhi kuitwa kongamano kwa sababu wachangiaji wote walikuwa wanaonyesha upande mmoja wa Mwl. Nyerere katika maisha yake.

Nadhani wale wanataka kumjua vizuri Mwl. Nyerere hawakuweza kupata upande wake wa pili kama ulivyobainishwa katika maandiko mengi na hasa kutoka kwa Mtanzania aitwaye Ludovic S. Mwijage katika maandiko yake kwenye vitabu mbali mbali ambavyo baadhi ni;

1)Dark side of NyerereLegacy-1996.
2) Julius K. Nyerere: Servant of God or Untarnished Tyrant?-2010.

Watu kama Ludovic Mwijage walitakiwa pia watoe michango yao katika kongamano hili ili upande wa pili wa Mwl. Nyerere ueleweke na kueleweka kwa upande wa pili ungesaidia kutoa fundisho zuri kwa vizazi vijavyo.

Waandaaji wa kongamano walishindwa vipi hata kumualika James Brennan ambaye amefanya utafiti na kukusanya mawazo ya watu mbali mbali kuhusu Mwl. Nyerere na kuyaweka katika kitabu kinachoitwa , Nyerere through the Eyes of His Critics, 1953-2013

Wangeweza hata kumuarika mwanaJamiiforums mwenzetu, Mzee Mohamed Said ambaye ni mwandishi na mhariri wa maandiko mengi yenye mlengo wa kushoto kuhusu Mwl. Nyerere.

Tuache kuufanya mijadala kama hii iwe niya kinafiki kisiasa kama sehemu ya kuifundisha jamii yetu bali tufanye mijadala yenye pende mbili zenye mitazamo tofauti kama sehemu ya kuchambua ''pumba na mchele'' katika kuujua ukweli kwa sababu ukweli hujenga.

Walioandaa kinachoitwa ‘’kongamano la kumbukizi ya miaka 20 ya kifo cha mwalimu Julius Nyerere’’ haikuwa ni kongamano bali ni mkusanyiko wa wapiga propaganda zenye unafiki.

Tuache unafiki, tulitendee haki taifa letu na vizazi vijavyo!

Back to History!! Nyerere alikuwezesha Kusoma mpaka University Bure!!! (with Government grants hakukua na Loan Board). Ulikua Unakula + kulala Bure+ pesa ya kujikimu.
Leo Unakuja Jamii forum with Protuding Eyes Kumtusi Mwalimu.
Shame on You!!
RIP J.K. Nyerere.
 

Attachments

  • images (8).jpeg
    images (8).jpeg
    5.5 KB · Views: 5
Nyerere ndiye architect wa kuharibu chaguzi za Zanzibar

Hata hivyo tunamsamehe kwa sababu ndiye muasisi wa Taifa hili jambo hilo ni kubwa mno kuliko makosa aliyotenda akiwa madarakani
Usiweke mwanvuli wa mawazo yako kwa watu wengine. Sema NAMSAMEHE na sio TUNAMSAMEHE!

Hoja yangu sio kumuhukumu Mwl. Nyerere bali kuonyesha mapungufu ambayo yapo lakini hayakusemwa kwa makusudi kwenye kongamano.
 
Tunakumbuka alivyowashughulikia watu ambao walikuwa na mawazo mbadala enzi hizo...Marehemu Balozi KasangaTumbo yaliyomkuta baada ya kutoka uingeleza na kutaka kuunda chama cha siasa anayajua huko aliko; Marehemu Katibu Mkuu wa TANU tena nasikia the most bright person ever...Mr. Oscar Kambona...huko aliko anajua yaliyomkuta baada ya kwenda tofauti ki mtazamo na Mwalimu...

Ndiyo maana tunasema historia ya Uhuru wa nchi yetu kuna pahala imechezewa..kuna mambo yamenyofolewa kwa sababu maalum wanazohua wao...

Namuheshimi sana Mwalimu lakini angetutenda haki kulivunja hili li CCM kabla hajaondoka...maana kuna kipindi lilitaka kumgeukia haya yeye..akafoka sana pale Dodoma akasema CCM si baba yangu wala mama yangu...

Sasa li CCM linatesa wenye mawazo mbadala...limeshika kila idara Bunge, Mahakama zipo mfukoni...

Kwa uhai wa Taifa huru mawazo mbadala ni muhimu sana...na ndiyo maana tunasema Taifa huru
 
Back to Histoey!! Nyerere alikuwezesha Kusoma mpaka University with Government grants hakukua na Loan Board. Ulikua

Back to History!! Nyerere alikuwezesha Kusoma mpaka University Bure!!! (with Government grants hakukua na Loan Board). Ulikua Unakula + kulala Bure+ pesa ya kujikimu.
Leo Unakuja Jamii forum with Protuding Eyes Kumtusi Mwalimu.
Shame on You!!
RIP J.K. Nyerere.
Hakuna tusi hapo bali ninaonyesha ukweli wa upande wa pili wa Mwl. Nyerere ambao ulipaswa kusemwa kwenye kongamano.

Hata Mzazi wako kama alikuchapa kwa kosa ambalo hukufanya huwezi kuacha kusema eti kwa sababu alimekulea. Kumwambia kuwa alikuchapa sio tusi bali ni ukweli ambao hata waliodhani ulifanya kosa watajua hukufanya kosa.
 
Unafiki ndio maana uwa namkubali Tundu Lissu uwa amngunyi maneno inapokuja kwenye kusimamia ukweli.

Tundu Lissu : Nyerere alizoea kuishi kwa uongo.

hakuna binadamu anaweza kuwa perfect 100% ilo halipo.

Nyerere ni babu yetu pamoja na kuwa mzalendo na mtu wa watu ila kuna vitu aliacha vikiwa vya ovyo ni swala la muungano fake na katiba ya chama kimoja kuiweka ndani ya vyama vingi.
Kweli kabisa hakuna binadamu mkamilifu.
Kuna mitazamo ya mtu hubadilishwa na uzoefu/matukio ya kimaisha.

Kuna kipindi Mwalimu alibadili mtazamo wake kuhusu demokrasia. Tazama alivyokuja kupigania mfumo wa vyama vyingi japo kulikuwa na msukumo wa mataifa ya nje. But he played his part japo kwa majuto.

Vingine ambavyo HAKUVIFANYA MWALIMU NI JUKUMU LETU KUVIPIGANIA NA KUVIFANYA.
MAKOSA ALIYOYAFANYA YAWE FUNZO KWETU
 
K
Nimejiuliza maswali mengi baada ya kumewasikia wachangiaji karibu wote kwenye kusanyiko linaloitwa ‘’ kongamano la kumbukizi ya miaka 20 ya kifo cha mwalimu Julius Nyerere’’ wakitoa mchanganuo wa maisha ya Mwl. Nyerere kama raia wa kawaida na Kiongozi Mkuu wa Tanganyika na Tanzania.

Miaka 29 ni mingi sana tokea Mwalimu Nyerere alipoachia ngazi ya Mwenyekiti wa CCM Taifa na kuwa mwananchi wa kawaida. Hii ina maana kuwa mtu mwenye miaka 28 hapa nchini hakuwahi kuona utendaji kazi wa Mwalimu Nyerere serikalini na ndani ya CCM. hili ni kundi la vijana ambalo kwa sasa lina watoto wenye umri wa miaka 11 kisheria kwa sababu umri wa kuanza kufanya mapenzi nchini ni miaka 18.

Kama wale wachangiaji niliowaona kwenye kongamano ndio tunawategemea sana katika mawazo yao kwenye kulijenga taifa basi hili taifa litaendelea kugubikwa na unafiki mkubwa ambao ni sumu kwa maendeleo chanya.

Bila kuondoa unafiki na kuwa wakweli hatuwezi kujua madhaifu yaliyolifanya taifa hili kupiga hatua za kusua sua katika nyanja za kisiasa, kijamii na kiuchumi.

Tunajua sheria za maumbile(laws of nature)zimetupa angalizo kuwa ili kitu kiwe kamili lazima kiwe na pande mbili. Hata nguvu za kifizikia ziko za aina mbili mbili ambazo ni hasi na chanya.

Nakumbuka wakati nikisoma shule ya ‘’ngumbalu’’ tulikuwa tunafanya makongamano na midaharo ambayo lazima iwe na pande mbili zinazoitwa wanaokubaliana (The affirmative or Aff) na wasiokubaliana (the Negative or Neg).Hii yote ni kukamilisha takwa la sheria za maumbile ambayo ndani yake kuna fikra.

Kamusi ya kiswahili sanifu inasema, kongamano/mdahalo ni majadiliano yanayofanywa na pande mbili zinazokinzana kuhusu suala fulani kwa kueleza sababu na ithibati ya msimamo wao tofauti na kufikia hitimisho la pamoja.

Kile kilichoitwa ‘’kongamano la kumbukizi ya miaka 20 ya kifo cha mwalimu Julius Nyerere’’ hakikuwa na kiwango kinachokidhi kuitwa kongamano kwa sababu wachangiaji wote walikuwa wanaonyesha upande mmoja wa Mwl. Nyerere katika maisha yake.

Nadhani wale wanataka kumjua vizuri Mwl. Nyerere hawakuweza kupata upande wake wa pili kama ulivyobainishwa katika maandiko mengi na hasa kutoka kwa Mtanzania aitwaye Ludovic S. Mwijage katika maandiko yake kwenye vitabu mbali mbali ambavyo baadhi ni;

1)Dark side of NyerereLegacy-1996.
2) Julius K. Nyerere: Servant of God or Untarnished Tyrant?-2010.

Watu kama Ludovic Mwijage walitakiwa pia watoe michango yao katika kongamano hili ili upande wa pili wa Mwl. Nyerere ueleweke na kueleweka kwa upande wa pili ungesaidia kutoa fundisho zuri kwa vizazi vijavyo.

Waandaaji wa kongamano walishindwa vipi hata kumualika James Brennan ambaye amefanya utafiti na kukusanya mawazo ya watu mbali mbali kuhusu Mwl. Nyerere na kuyaweka katika kitabu kinachoitwa , Nyerere through the Eyes of His Critics, 1953-2013

Wangeweza hata kumuarika mwanaJamiiforums mwenzetu, Mzee Mohamed Said ambaye ni mwandishi na mhariri wa maandiko mengi yenye mlengo wa kushoto kuhusu Mwl. Nyerere.

Tuache kuufanya mijadala kama hii iwe niya kinafiki kisiasa kama sehemu ya kuifundisha jamii yetu bali tufanye mijadala yenye pende mbili zenye mitazamo tofauti kama sehemu ya kuchambua ''pumba na mchele'' katika kuujua ukweli kwa sababu ukweli hujenga.

Walioandaa kinachoitwa ‘’kongamano la kumbukizi ya miaka 20 ya kifo cha mwalimu Julius Nyerere’’ haikuwa ni kongamano bali ni mkusanyiko wa wapiga propaganda zenye unafiki.

Tuache unafiki, tulitendee haki taifa letu na vizazi vijavyo!
Kabla ya kuhitimisha, ungetuelezea Mwl. Ambavyo hakuwa mdemokrasia kama ulivyo andika kwenye kichwa cha habari.
 
Nyerere alifanya makosa mengi na mengine aliyakiri kabla ya kifo chake. Kitu kimoja kinachofanya nisimuhukumu kwa namna yoyote ile ni kuwa "alifanya yote hayo kwa interests za nchi na si zake binafsi hivyo, alipatia na kukosea kwa kile alichoona ni bora kwa nchi yake kitu ambacho ni tofauti na waafrika wa leo, wanakosea makusudi ili wajineemeshe"
 
Nimejiuliza maswali mengi baada ya kumewasikia wachangiaji karibu wote kwenye kusanyiko linaloitwa ‘’ kongamano la kumbukizi ya miaka 20 ya kifo cha mwalimu Julius Nyerere’’ wakitoa mchanganuo wa maisha ya Mwl. Nyerere kama raia wa kawaida na Kiongozi Mkuu wa Tanganyika na Tanzania.

Miaka 29 ni mingi sana tokea Mwalimu Nyerere alipoachia ngazi ya Mwenyekiti wa CCM Taifa na kuwa mwananchi wa kawaida. Hii ina maana kuwa mtu mwenye miaka 28 hapa nchini hakuwahi kuona utendaji kazi wa Mwalimu Nyerere serikalini na ndani ya CCM. hili ni kundi la vijana ambalo kwa sasa lina watoto wenye umri wa miaka 11 kisheria kwa sababu umri wa kuanza kufanya mapenzi nchini ni miaka 18.

Kama wale wachangiaji niliowaona kwenye kongamano ndio tunawategemea sana katika mawazo yao kwenye kulijenga taifa basi hili taifa litaendelea kugubikwa na unafiki mkubwa ambao ni sumu kwa maendeleo chanya.

Bila kuondoa unafiki na kuwa wakweli hatuwezi kujua madhaifu yaliyolifanya taifa hili kupiga hatua za kusua sua katika nyanja za kisiasa, kijamii na kiuchumi.

Tunajua sheria za maumbile(laws of nature)zimetupa angalizo kuwa ili kitu kiwe kamili lazima kiwe na pande mbili. Hata nguvu za kifizikia ziko za aina mbili mbili ambazo ni hasi na chanya.

Nakumbuka wakati nikisoma shule ya ‘’ngumbalu’’ tulikuwa tunafanya makongamano na midaharo ambayo lazima iwe na pande mbili zinazoitwa wanaokubaliana (The affirmative or Aff) na wasiokubaliana (the Negative or Neg).Hii yote ni kukamilisha takwa la sheria za maumbile ambayo ndani yake kuna fikra.

Kamusi ya kiswahili sanifu inasema, kongamano/mdahalo ni majadiliano yanayofanywa na pande mbili zinazokinzana kuhusu suala fulani kwa kueleza sababu na ithibati ya msimamo wao tofauti na kufikia hitimisho la pamoja.

Kile kilichoitwa ‘’kongamano la kumbukizi ya miaka 20 ya kifo cha mwalimu Julius Nyerere’’ hakikuwa na kiwango kinachokidhi kuitwa kongamano kwa sababu wachangiaji wote walikuwa wanaonyesha upande mmoja wa Mwl. Nyerere katika maisha yake.

Nadhani wale wanataka kumjua vizuri Mwl. Nyerere hawakuweza kupata upande wake wa pili kama ulivyobainishwa katika maandiko mengi na hasa kutoka kwa Mtanzania aitwaye Ludovic S. Mwijage katika maandiko yake kwenye vitabu mbali mbali ambavyo baadhi ni;

1)Dark side of NyerereLegacy-1996.
2) Julius K. Nyerere: Servant of God or Untarnished Tyrant?-2010.

Watu kama Ludovic Mwijage walitakiwa pia watoe michango yao katika kongamano hili ili upande wa pili wa Mwl. Nyerere ueleweke na kueleweka kwa upande wa pili ungesaidia kutoa fundisho zuri kwa vizazi vijavyo.

Waandaaji wa kongamano walishindwa vipi hata kumualika James Brennan ambaye amefanya utafiti na kukusanya mawazo ya watu mbali mbali kuhusu Mwl. Nyerere na kuyaweka katika kitabu kinachoitwa , Nyerere through the Eyes of His Critics, 1953-2013

Wangeweza hata kumuarika mwanaJamiiforums mwenzetu, Mzee Mohamed Said ambaye ni mwandishi na mhariri wa maandiko mengi yenye mlengo wa kushoto kuhusu Mwl. Nyerere.

Tuache kuufanya mijadala kama hii iwe niya kinafiki kisiasa kama sehemu ya kuifundisha jamii yetu bali tufanye mijadala yenye pende mbili zenye mitazamo tofauti kama sehemu ya kuchambua ''pumba na mchele'' katika kuujua ukweli kwa sababu ukweli hujenga.

Walioandaa kinachoitwa ‘’kongamano la kumbukizi ya miaka 20 ya kifo cha mwalimu Julius Nyerere’’ haikuwa ni kongamano bali ni mkusanyiko wa wapiga propaganda zenye unafiki.

Tuache unafiki, tulitendee haki taifa letu na vizazi vijavyo!
Uzur wa mwl Nyerere unatokaña na uongozi mbovu wa waliomfuata hvyo hákuna mtu wa ķufanana naye. Jambo kubwa ambalo halina ubishi ni uadilifu wake kwenye mali za umma na uwezo mkubwa kifikra kama kiongozi. Ináwezekana wengi wetu hatujosoma maandiko yáke ukisoma utajua dhana ya visionary leader,alikua na uwezo wa kufikiri hatua mbele zaid hata alikua na mapungufu ķama binadam kuliko waliomfuata ni vituko/very selfish hakuna cha jiwe wala nn!
 
Mkuu;

Hata Lissu ni walewale, usimpe hizo sifa kwenye kusimamia ukweli. Lissu pia ni mwanasiasa mnafiki kama walivyo wanasiasa wengi hapa nchini.

Kwa ujumla huwezi kuwa mwanasiasa nchini kama wewe sio mnafiki kwa sababu siasa zetu haziruhusu wagombea binafsi.

Vyama vya siasa vyenye madiwani na wabunge vimejengwa katika misingi ya kinafiki nchini. Huu ni ukweli.

..TL amejitahidi kumjadili Mwalimu kama unavyopendekeza ktk hoja yako.

..amefafanua kwamba Mwalimu wa 1962 mpaka 1984 aliondoa vyama vingi, aliongoza bila bill of rights, aliweka watu kizuizini bila ukomo.

..lakini vilevile TL amesema anamkubali Mwalimu yule mwaka 1990 mpaka anafariki kwasababu ya mchango wake ambao uliwezesha kurejeshwa kwa mfumo wa vyama vingi nchini.

..Mjadala unaomhusu Mwalimu Nyerere mara nyingi unaharibiwa na makada wa CCM ambao wamezoeshwa utamaduni wa kuimba mapambio ya kusifia tu, na siyo kufanya uchambuzi wa kina na kisomi kuhusu mada mbalimbali.
 
Nasikia majaribio ma4 ya kumwondoa magogoni yalishafanyika japo yalifeli,enzi ya utawala wake sikuepo najiuliza km Leo hii anapendwa kila kona ya dunia enzi ya uhai ilikuwaje wakataka kumwondoa
Mkuu;
Sio majaribio manne bali majaribio zaidi ya manane!
 
Back
Top Bottom