Harakati zangu za mazoezi zilianza tangu Enzi za ujana huko chuo hadi sasa mtu mzima, Lakini hazijawahi kudumu japo kwa wiki mbili.
Nakumbuka enzi hizo; Niliwahi andaa Jogging kuanzia mliman chuo, kupitia Ubungo > Magomeni > Morocco > Mwenge
Tuliondoka vizuri tu lakini nilipofika Manzese Nilichemsha kwakweli, ikabidi Nipande zangu daladala hadi Mwenge!
Sikurudia tena kufanya kwanza nikaanza kujifariji; Sina hela ya kula vizuri mazoezi ya nini, nikaachana na mazoezi uchwara!
Nilivyomaliza chuo; Mzuka wa mazoezi ukaanza tena; nikawa siku za weekend naenda kunduchi beach, lakini napo sikudumu sana kwasababu ya visingizio vya kukosa nguo za mazoezi,
Mungu si Athumani, nikanunua raba na pensi ya michezo, nikarudi ulingoni! Kulekule Kunduchi Beach, siku za weekend, siku ya kwanza nikakaza fresh, siku ya pili pia nikakomaa, Siku ya tatu nikawaza: Ya nini kufanya mazoezi alfajili mwisho nikabwe bure? NIKAACHA!
Maisha yakaendelea miaka na miaka, nikawaza huenda mazoezi mazuri ni yale ya GYM, wacha nikajiandikishe.
Nililipia GYM mwezi mmoja, katika mahudhurio yangu pale GYM nakumbuka nilifika siku tatu tu nikaghairi; kwanza nikawaza, mazoezi gani sina hata gari aaah? ...Nikaachana na GYM
Miaka ikasonga! Niliponunua gari, nikarudi tena GYM kujiandikisha, nikahudhuria siku mbili nikaopoa mrembo mmoja; sikurudi tena mazoezini, na mazoezi nikaacha tena. Kwanza nikawaza napoteza pesa na mafuta bure.
Nikajisemea wacha nikija jenga nyumba yangu nitaweka chumba cha mazoezi.
Miaka ikasonga, nilipojenga, nikaweka chumba cha mazoezi, lakini nakumbuka nilifanya wiki moja tu, nikawaza tena labda wacha ninunue mashine kabisa za mazoezi zitanisaidia!
Mwaka jana nilifanikiwa kuzinunua lakini nimezitumia siku chache tu nikaona miyeyusho! NIKAACHA
Hadi leo chumba cha mazoezi nimekigeuza STOO!
Nadhani kabisa wengine tumeumbiwa kula nyama choma na Bia!
Mazoezi yana wenyewe! Tuwaachie mazoezi yao EBOOOH!!.
Nakumbuka enzi hizo; Niliwahi andaa Jogging kuanzia mliman chuo, kupitia Ubungo > Magomeni > Morocco > Mwenge
Tuliondoka vizuri tu lakini nilipofika Manzese Nilichemsha kwakweli, ikabidi Nipande zangu daladala hadi Mwenge!
Sikurudia tena kufanya kwanza nikaanza kujifariji; Sina hela ya kula vizuri mazoezi ya nini, nikaachana na mazoezi uchwara!
Nilivyomaliza chuo; Mzuka wa mazoezi ukaanza tena; nikawa siku za weekend naenda kunduchi beach, lakini napo sikudumu sana kwasababu ya visingizio vya kukosa nguo za mazoezi,
Mungu si Athumani, nikanunua raba na pensi ya michezo, nikarudi ulingoni! Kulekule Kunduchi Beach, siku za weekend, siku ya kwanza nikakaza fresh, siku ya pili pia nikakomaa, Siku ya tatu nikawaza: Ya nini kufanya mazoezi alfajili mwisho nikabwe bure? NIKAACHA!
Maisha yakaendelea miaka na miaka, nikawaza huenda mazoezi mazuri ni yale ya GYM, wacha nikajiandikishe.
Nililipia GYM mwezi mmoja, katika mahudhurio yangu pale GYM nakumbuka nilifika siku tatu tu nikaghairi; kwanza nikawaza, mazoezi gani sina hata gari aaah? ...Nikaachana na GYM
Miaka ikasonga! Niliponunua gari, nikarudi tena GYM kujiandikisha, nikahudhuria siku mbili nikaopoa mrembo mmoja; sikurudi tena mazoezini, na mazoezi nikaacha tena. Kwanza nikawaza napoteza pesa na mafuta bure.
Nikajisemea wacha nikija jenga nyumba yangu nitaweka chumba cha mazoezi.
Miaka ikasonga, nilipojenga, nikaweka chumba cha mazoezi, lakini nakumbuka nilifanya wiki moja tu, nikawaza tena labda wacha ninunue mashine kabisa za mazoezi zitanisaidia!
Mwaka jana nilifanikiwa kuzinunua lakini nimezitumia siku chache tu nikaona miyeyusho! NIKAACHA
Hadi leo chumba cha mazoezi nimekigeuza STOO!
Nadhani kabisa wengine tumeumbiwa kula nyama choma na Bia!
Mazoezi yana wenyewe! Tuwaachie mazoezi yao EBOOOH!!.