Tusimsakame Zitto, Maamuzi ya Waziri kuhusu TANESCO mbali ya kuwa muhimu kuna makosa ya kisheria

Ugonvi wote wa Mhando na Maswi ni nani apewe tender ya ku supply mafuta IPTL..haya mengine ni kachumbari na Mazingaombwe kama alivyosema Mwanakijiji..

Napata taabu sana kwanini Bunge limekaa kimya uvunjaji wa sheria na taratibu aliofanya Katibu Mkuu Nishati na Madini kwa kisingizio cha maslahi ya Taifa wakati kwa mtu yeyote makini unaona ni maamuzi ambayo yamegubikwa na mazingira ya rushwa.
 
Kwanini kuna sheria? Sheria ipo ili kulinda masilahi ya watu na Taifa. Iweje sasa kama hiyo sheria hailindi masilahi mapana ya jamii iendelee kuwa cover kwa wale wanaolihujumu Taifa? Ni wazi kabisa above sheria kuna kitu kinachoitwa dhamira njema (Social capital) ambayo kama sote tungekuwa nayo hizo sheria zisingetungwa maana kila kitu kingefanywa inavyotakiwa. Huwezi kusema eti polisi akikamata mhalifu wa kubambikiza huku akiwa kafuata taratibu zote na sheria zote basi anahaki ya kufanya hivyo kwakua ana dhamana ya kipolisi kufanya hayo. Ndivyo ilivyo hata katika sheria kama sheria imetumiwa kihalifu basi hiyo sheria imeshindwa kulinda haki ya jamii na hivyo kama kuna mtu ameonekana kukiuka sheria ili kuilinda hiyo haki basi huyo eti awe ndiye wa kuadhibiwa na yule aliye tumia sheria kuhujumu eti yeye aachwe; hicho ni kituko ambacho kinaweza kufanywa na jamii isiyojitambua.

Sheria ipo kulinda haki za raia na jamii nzima lakini sheria inaposhindwa kuzilinda haki hizo hiyo sheria inakosa uhalali kwa hiyo specific case na katu hili lisiwe kisingizio eti wengine watafanya hivyo hivyo wakati mwingine maana sheria haitumiwi bila context ndiyo maana kuna watafsiri wa sheria ambao hawapo kama kasuku kuhukumu bila kuangalia context na mazingira halisi ya tukio husika.

Watu katu wasihusishe mazingira ya Richmond na haya ya wakati huu kwani sote tunazo akili na ufahamu wa kutosha kujua ni uamuzi upi umelinda haki na upi unahujumu taifa pale ambapo sheria imetokea kutumiwa kufanya uhalifu badala ya kulinda maslahi. Cha msingi ni case zote kuwa tabled kwa uwazi naiweke wazi ni maslahi yapi yalikuwa yanalindwa na nani kwa faida gani then ukweli utajiweka wazi na haki itatendeka.

Ninachosisitiza ni kuwa sheria pekee hata siku mmoja haitajisimamia kulinda haki kama wanaozitumia hizo sheria hawatakuwa na high social capital na ndiyo maana si wote wanapewa dhamana ya kuongoza bali wale tu wenye maadili mema walio fanyiwa vetting na vyombo husika (Kama hili linafanyika ama la wakati huu ni discussion nyingine). Hivyo watu wasijifiche kwenye kichaka cha sheria na kanuni kutenda na kuficha maovu yao kwani sheria yaweza ama kulinda au kuhujumu maslahi mapana ya raia na jamii kama itatumiwa tofauti na malengo yaliyokusudiwa.

Mkuu chuki na hasira kwa sababu anahusika Zitto zisisababishe uandike vitu ambavyo unajua siyo sahihi lakini unatetea uwongo! Amka kijana. Udhaifu wa watawala usikupofushe kushabikia watu wasioheshimu sheria na taratibu tulizojiwekea.
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Wengi tunaweza kusoma,
lakini hatuwezi kuchambua,
na kujua maana ya kilicho,
andikwa kwa undani.

Kuna haja ya kujielimisha,
zaidi katika uwanja wa,
kuchambua hoja kwa,
kwa umakini mkubwa,
na kuuliza maswali ya,
udadisi na kutaka kujua zaidi.

wewe umeelewa nini? au ndio wale wasio elewa
 
Wabunge mnaotetea sheria ya manunuzi TANESCO, hamuoni uchungu jinsi wananchi wanavyopata shida ya umeme na uchumi kukwama? Hivi mbona hamko makini kuona mapungufu na kuyarekebisha kwenye sheria mlizoweka wenyenywe? Mnapiga dana dana tu. Mkiendekeza kuona mambo kwa mtazamo mwepesi, badala ya kutatua matatizo kiudhati, mtasababisha nchi iingie matatani kama Libya, Syria na kwingineko. Hali hii ikijitokeza hapa kwetu mnafikiri nyie na ndugu zenu mtakuwa salama? Acheni unafiki. Hongereni sana viongozi wapya wa Wizara ya Nishati na Madini bravoooooooooooo!!!!!!!!!
 
Kwa manufaa ya Taifa,
Serikali inamteka Dr Ulimboka,
kwa nia ya kumuua.
Sheria hazifuatwi,
lakini Somo linaeleweka.

Tunapiga Kelele kudai,
Utawala bora!
Tutadai utawala bora wakati,
mawazo yetu yanaunga mkono,
uvunjwaji wa sheria?

Hiki kipengele cha "Manufaa ya Umma",
kipo ndani ya katiba,
kinarudiwa tena na tena na tena,
Nia ya kipendgele " Manufaa ya Umma"
ni kuwapa mwanya viongozi,
wa serikali kupindisha sheria,
huku wakijificha nyuma ya,
Kipengele " Manufaa ya Taifa".

Mimi sijapoteza imani kwa Zitto,
Wala sioni kosa la rushwa,
Wakti huo huo,
Nina wasi wasi na hofu,
kubwa juu ya mwenendo huu,
wa kuunga mkono,
kuvunja sheria kwa kisingizio,
cha "Manufaa ya Taifa".
 
Mkuu chuki na hasira kwa sababu anahusika Zitto zisisababishe uandike vitu ambavyo unajua siyo sahihi lakini unatetea uwongo! Amka kijana. Udhaifu wa watawala usikupofushe kushabikia watu wasioheshimu sheria na taratibu tulizojiwekea.

Alaah kumbe namchukia Zitto eeh? Ngoja nirudi tena ndani ya moyo wangu kuuchunguza sawa sawa huenda kuna ukweli who knows? Kwahiyo nampenda nani Maswi ambaye hata simfahamu au Mhongo ambaye ndiyo kwanza nimemsikia wakati huu akipewa uwaziri?

Sina haja ya kuchukia nafsi ya mtu yeyote ila nina ulazima wa kumpenda kila mwanadamu mwenye sura na mfano wa Mungu huku nikiuchukia uovu kupita chuki yenyewe maana huo nakila sababu ya kuuchukia.

Nikiri tu kwamba mwanadamu hawezi kuwa na hukumu ya haki pasipokuwa na roho wa Mungu ndani yake sasa yawezekana huu uovu unaoelezwa hapa nafsi yangu ukaihukumu kimwili na macho ya rohoni yakiwa yametiwa giza hivyo ikasababisha kumuhukumu yeyote anayetetea ukweli anaoufahamu kimakosa. Kama ndivyo basi wanaohusika na Mungu pia anisamehe vinginevyo dhamira yangu inanishuhudia kabisa katibu mkuu na prof. Muhongo wote wanania ya dhati ya kuifaisafisha hiyo wizara iliyo kamatwa na tentacles za mafisadi!
 
Back
Top Bottom