Tusimnyanyapae Matonya - Kikwete naye ni Ombaomba!

hureeeeeeeeeeeeeeeeeee,kama tumeshindwa kupata namba kwenye michezo,uchumi,nk hata hizi nafasi adimu tuzikose?rais alishasema asipoenda nje mtakufa njaa,
bravo dk jakaya mrisho kikwete kwa vile sifanyi kazi serikalini na sitegemei pesa ya nchi hii masikini kwa lolote nakushauri badili katiba ugombee tena 2015 nakupa kura yangu.
 
Unaweza tumia mda mwingi sana kuwaza kuhusu tabia na uwezo wa jk katika kufikiri na kufanya maamzi.

Kwa hesabu ndogo tu...ni aibu sana kwa mtu kusimangwa wazi wazi kwamba ww ni ombaomba uliekomaa mpaka kuchefua wengine..kuna hajaipi ya kuzurura dunia nzima kuomba omba tu kila siku,wakati nchini mwako unarasilimali za mabilion ya hela! Kwa nn ujidharaulishe hivi? Hakika hii miaka kumi tuliyempatia huyu bwana tutaijuttia sana..ameharibu nchi kiasi kwamba kila mtu na lwake..migomo kila kukicha, yy hatakujali hamna..badala ya kutoa maamuzi kama kiongozi..yy anadhani, anahisi, anafikiri...tufunge na kusali sana watanzania mana haya mateso na vifo vya ndg zetu si kwa mapenzi ya Mungu, ni uzembe,ujinga wa watu tulio waamini tukawapa madaraka..na huu ukimya wetu ndo unawafanya wao kutuona sisi wajinga nakufanya watakavyo .

Inakuwaje waziri anaweka kifua chake mbele anatetea posho za wabunge walipwe laki 2 kwa siku...eti wana madeni, wanawasaidia wapiga kura wao..nani aliwaambia wakope ?.Mungu awalaani nyie..hamjui kuna watu wanakufa kwa kukosa elfu mbili ya kununua dawa ! Hamjua kuna wakina mama wanajifungua barabarani, wengine wanakufa..wengine wananpatta maradhi kutokana na kukosa huduma...raisi wa nchi anatumia mil 300 kwenda kuongea na bill gates! Watu wanashangaza sana.

Tuombe Mungu atuvushe salama.
 
hotuba au wosia aliotuachia Nyerere iliotolea leo tbc saa 2.15 usiku huu ni zungumzia taifa omba omba , sasa sijui Nyerere aliitoa lini maana huyu Vasco da Gama hakuwepo wakati wa uhai wake, lakini kaongelea suala hilo na hulka za mawaziri wa kiongozi wa Taifa omba omba, na kwa kuongezea akasema kwanza hao matajiri/donors kwa sasa wanapunguza bajeti zao za misaada.

Pili wakiwekeza ni kwamba wanawekeza mirija yao, si kwa nia ya kutusaidia sisi, bali kujisaidia wenyewe, na akamalizia kwa kusema kwamba ili tufikie malengo yetu ni kwa kutoza na kukusanya kodi na sio kuomba omba. Aliyeweza kurekodi au anayeweza kupata hiyo audio anaweza kutuwekea hapa.
 
MATONYA PIX NO 1 (1)[1].JPG


KATIBA ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaeleza wazi kuwa kila mtu ana haki ya kuishi mahali popote pale anapotaka ili mradi havunji sheria, haki ambayo ombaomba maarufu hapa nchini, mzee Anthony Matonya, pia anastahili kuwa nayo. Kwa haki hiyo hiyo, mzee Matonya aliyejijengea umaarufu mkubwa hapa nchini kwa staili yake ya kuomba, umaarufu wake ulianzia jijini Dar es Salaam na amekuwa akizunguka katika mikoa mingine ya Dodoma na Morogoro akiendelea na kazi hiyo inayomuingizia riziki kutoka kwa wasamaria wema.

Wengi wanamuona mzee huyo kama binadamu mwenye ulemavu wa macho anayeishi kwa vituko, baadhi wamtaja kuwa ni tajiri mkubwa wa mifugo na hakustahili kuomba kwa kuwa ana mali nyingi hususani katika ukoo aliotoka.

Sijui zaidi kwa undani maisha ya mzee huyo pamoja na utajiri wake wote unaoelezwa, lakini inashangaza kwa nini mzee huyo na umri wake mkubwa aamue kuomba badala ya kusimamia mifugo yake huko Dodoma.

Hicho ni kitendawili kikubwa ambacho mzee huyo mwenyewe ndiye anayeweza kukitegua na pengine anataka aingizwe kwenye kitabu cha Guiness ambacho kinaweza kumtoa Mtanzania wa kwanza aliyefanikiwa kuomba kwa muda mrefu na akiwa na umri mkubwa kuliko wote waliowahi kuomba duniani.

Simshangai mzee Matonya na siwalaumu wale wanaofuatilia maisha ya mzee huyo kwa karibu kila kukicha kwa kuwa tayari amekwisha jijengea umaarufu mkubwa wa kuomba, kazi ambayo hawezi kuiacha hadi mauti yatakapo mkuta.

Lakini kwa mfano huo wa mzee Matonya Watanzania wanapaswa kujiuliza kuwa wapo akina Matonya wangapi wanaoshindwa kuishi kwa dola moja kwa siku kutokana na kipato duni na hawawezi kuendesha maisha yao bila kuomba.

Zipo aina mbalimbali za kuomba na si tu aina hiyo ambayo mzee wetu Matonya anaitumia, wapo waombaji wakubwa waliovuka viwango hadi wakajitokeza kuwa waombaji wa mbinu za juu za ulaghai wanaoitwa ‘matapeli’.

Kama watu wanavyodai kuwa mzee huyo ana mali nyingi na mwanzo wake umetokana na fedha anazopewa kidogo kidogo na akizipeleka kwao kununulia mifugo iliyoendelea kuzaliana kazi hiyo.

Tukimsema Matonya tusisahau kuwa haitakuwa vigumu kujisema wenyewe na serikali yetu kwa kuwa wote tumekuwa omba omba na zaidi pale tunapoomba kila kitu kwa nchi wahisani ili waweze kuendesha bajeti yetu ya nchi.

Nchi wahisani sasa zinainyooshea mkono Serikali ya Tanzania kuwa licha ya kuomba na kupatiwa misaada mingi bado wahisani hao hawaridhishwi namna fedha zao zinavyotumika katika shughuli za maendeleo.

Wahisani wameshituka wameamua kupunguza misaada yao na hali inazidi kuwa ngumu upande wa serikali, ikitarajia kuwa na bajeti ya sh trilioni 11.1 kwa mwaka 2010/2011 fedha ambazo haziwezi kupatikana moja kwa moja kutoka vyanzo vya ndani.

Nchi kama Sweden inahoji namna serikali ya Tanzania inavyoendelea kuwa masikini na watu wake huku kukiwa na rasilimali za kila aina, wanashangaa huu umaskini tulionao unatoka wapi?

Ni majuzi tu, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alinukuriwa na vyombo vya habari akiushangaa umasiki wa Watanzania, kuwa nchi hii ni ya neema imejaliwa rasilimali tele, ardhi kubwa, wasomi na wataalamu wa kila aina lakini mambo hayaendi.

Waziri Mkuu Pinda anashangaa umasikini wa nchi hii na hawezi kushangaa leo kwa kuwa yupo kwenye mfumo wa serikali tangu awamu ya kwanza na ana miaka zaidi ya 35 katika utumishi wa umma hivyo anaifahamu zaidi nchi na serikali zote zilizotangulia na hii ya awamu ya nne akiwa ndiye msimamizi mkuu wa shughuli za serikali.

Umaskini wa Watanzania ndio maajabu ya leo tunayoyaona na yanayowashangaza wahisani na waziri mkuu, kuwa inatia aibu nchi inapokuwa omba omba huku ikiwa na rasilimali tele, huko nje si bure kuwa tunaitwa kina ‘Matonya’.

Kama ilivyo kwa mzee Matonya alivyojibebea umaarufu mkubwa kwa kuomba, Watanzania tutaepukaje aibu ya kuomba kila siku nje, leo hii Pinda anahoji, hivi Watanzania nani kawaroga, mbona tuna kila kitu nchi hainyanyuki ?

Tukimshangaa mzee Matonya kumbe wote tunaomba na serikali yetu inaomba, sasa katika waombaji wote hii aibu ya kuendelea kuomba, kutegemea wahisani katika bajeti yetu itakwisha lini? Tumekosa nini?

Hii aibu ya kuomba inayofanywa na mzee Matonya na aibu ya nchi yenye neema.matonya wanatofautiana ktk kiwango.jk ni matonya wa kimataifa.ndo namba one wa dunia
 
Tumeshindwa kutambua kuwa hakuna maendeleo kwa kuendelea na Wanamagamba katika uongozi wa nchi hii. Wanaopata shida kubwa ni wale ambao hata ukiwaambia lakini siku ya kura watatawaliwa na ushabiki kama wa Simba na Yanga kwenye maswali ya kitaifa.Elimu ndogo na woga ndio wachawi wetu. Viongozi wetu wamezidi kwa kupenda anasa. WaTZ wengi wanajivunia kwenda Ulaya kila siku badala ya kufanya kazi. Kupenda anasa, matumizi ya hovyo, na mengi ya namna hiyo ndiyo mchawi. Wengine hela zetu wanaweka kwenye mabenki ya Ulaya. Mungu atunusuru kama hata Pinda hayajui hayo au anadanganya. Tz fisadi anasifiwa nchi kama China fisadi ni shaba kichwani.
 
kwa tanzania kuomba misaada kwa nchi zilizoendelea si ajabu, nakuomba msaada hatujaanza na rais j.k. Tulianza toka enzi za nyerere na si tanzania peke yake ndio inaomba misaada. Hata nchi zote za africa zinaomba misaada. Kwaio hata huyo w.slaa mnayesema atakua ombaomba zaidi ya j.k, kwaio wananchi hatudanganyiki na hayo.:mad2::mad2::mad2:

kauli yako inafanana na ileee!! Siwezi kuachana nae pamoja na uchangu doa wake maana hata nitakaekuja kumuoa atakua changudoa mara mbili ya huyu. Je umejaribu kutafakari?
 
kwa nini tunasema kikwete tusiseme serikali,Kikwete haombi misaada ya kutumia yeye na nyumba yake ni misaada ya watanzania kwa maendeleo yetu,haipendezi kumdhalilisha Rais wa taifa letu bila sababu,mbona tunakosa uzalendo kwa kiasi hiki?Nakiri kuwa hali ya taifa kuwa tegemezi ni hatari kwa uhuru naustawi wake, lakini tunachokitaka ni kujitegema mabako hakutaletwa na kikwete peke yake bali Watanzania wenyewe kawa kufanya kazi kwa juhudi na kuwa na usimamizi mzuri wa raslimali za taifa,
 
Inasikitisha, lakini tatizo ni kuwa Jk akifika kuomba kura hata hao akina mama wanasahau yote hayo. Ikifika 31.10 wataoongozwa na ushabiki wa kumpigia tena kikwete, miaka mingine mitano watasubiri katika mahangaiko kama hayo.

Kwanini hizo hela zinazofujwa na Ridhiwani na Salma zisiwafae kina mama kama hao?
Hapo ni 'core' ya nchi, Dar je mikoani hali si ndiyo haitamaniki?
Precise examination, wanafikiri kwamba kusema kwa midomo na kunung'unika ati serikal hii walioichagua haiwasaidii, km wanaelewa message wanatakiwa kuongea na kura zao, kila mmoja ano uwezo waku-influence mustakabali wa taifa, kwa kura zenu, msiyasahau haya mkaya-amount to political fanatism 2015, poleni but keep in mind!
 
Hivi nchi hii imeanza kuomba zama hizi za JK au toka zamani? Hivi rasimali hizi ziepatikana siku hizi tu au toka zamani? Hivi umeskini huu umeletwa na JK au ni nani aliyetusababishia haya yote.
 
chuki chuki chuki chuki na chuki..................kikwete akienda kuomba misaada nje,anaomba kwa ajili ya watanzania wote,ukiwamo wewe na mkeo na mama yako.tusimkejeli rais wakati anawatumikia watanzania wote.
 
mchungaji unamchukia kikwete kwa sababu ya dini yake wala hakuna kingine.mungu akusamehe sana kwani hujui ulitendalo.
 
huu ni uchochezi na ni chuki ya kutosha.umechukua vitanda vya bibi zako ukaeka waya wa kutundikia nguo unaleta hapa.

Uchochezi uko wapi wewe? huoni hizo drip zimetundikwa hapo Dirishani? na hii picha haijawekwa na mchungaji Masanilo
 
Tufike mahali watanzania tukubali kuwa nchi yetu ni masikini na tunahitaji kujenga uchumi wetu kwa nguvu za pamoja. Hizi fikra tunazokuwa nazo za kuwachukia viongozi wakuu wa nchi hususani JK hazitusaidii na wala hazitatufikisha kokote zaidi ya kubaki kurumbani bila tija. Pia lazima tutambue kuwa haya tunayoyaongea ni ya kutuaibisha wote kwa ujumla wetu na si vinginevyo... Wapo watu wanazungumza kana kwamba wao si watanzania wakati wao ni kizazi cha uzao wa nchi hii kuanzia miaka mingi iliyopita.
Kati yao na pengine walio wengi ni wale waliosomeshwa na kushika nafasi katika mashirika ya umma waliyoyaangamiza lakini leo wanamlalamikia JK.

Tufike mahali tujiulize wenyewe hayo magari mnayoyaendesha na hizo shule za kifisadi mlizosoma, ni JK aliiba na kuwapa? Kwa nini hamkubali kuwa ni baba zenu hao hao waliiba na kuyamaliza mashirika ya umma miaka mingi iliyopita pengine huyu JK akiwa hajaanza hata shule ya msingi huko Msoga lakini leo zigo lote la lawama tunamtwisha yeye.

Binafsi namuona mtu yeyote aliyetayari kuidhalilisha nchi yake badala ya kuipigania kuwa ni mpumbavu na hana uzalendo kitu ambacho ni hatari kwa amani, umoja na ustawi wa taifa lolote lenye sifa kemkem kama Tanzania.
 
Hata Mbowe na Slaa ni kama Matonya tu hakuna tofauti, wameomba msaada kwa CDU-Ujerumani na Conservative-Uingereza kwa mzee Cameroon.
 
Tatizo la JK na CCM yake haijui kua safari moja tu anayosafiri ni inaweza jenga HOSPITAL/ZAHANATI na samani zake including hospital equapiments....tunahitaji TV mbadala itakayokua inafanya kazi ya kuonesha mashule na mazahanati na majengo yaliyotelekezwa na serikali...imagine mgonjwa anapolala kwenye kitanda kisichokua na GODORO au kitanda cha futi 3 kwa 6 wanalala wanawake zaidi ya mmoja ni aibu
 
JKRonaldo.jpg


Hapa alikuwa akiomba Jezi ya Madrid

Kikwete-salutes-Maximo.jpg


Hapa toka kwa Maximo kocha wa Yanga

millet-president-jakaya-kikwete.jpg


Hapa sijui........!!
 
Back
Top Bottom