Tusimnyanyapae Matonya - Kikwete naye ni Ombaomba!

Masanilo

Platinum Member
Oct 2, 2007
22,286
4,493
MATONYA PIX NO 1 (1)[1].JPG


KATIBA ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaeleza wazi kuwa kila mtu ana haki ya kuishi mahali popote pale anapotaka ili mradi havunji sheria, haki ambayo ombaomba maarufu hapa nchini, mzee Anthony Matonya, pia anastahili kuwa nayo. Kwa haki hiyo hiyo, mzee Matonya aliyejijengea umaarufu mkubwa hapa nchini kwa staili yake ya kuomba, umaarufu wake ulianzia jijini Dar es Salaam na amekuwa akizunguka katika mikoa mingine ya Dodoma na Morogoro akiendelea na kazi hiyo inayomuingizia riziki kutoka kwa wasamaria wema.

Wengi wanamuona mzee huyo kama binadamu mwenye ulemavu wa macho anayeishi kwa vituko, baadhi wamtaja kuwa ni tajiri mkubwa wa mifugo na hakustahili kuomba kwa kuwa ana mali nyingi hususani katika ukoo aliotoka.

Sijui zaidi kwa undani maisha ya mzee huyo pamoja na utajiri wake wote unaoelezwa, lakini inashangaza kwa nini mzee huyo na umri wake mkubwa aamue kuomba badala ya kusimamia mifugo yake huko Dodoma.

Hicho ni kitendawili kikubwa ambacho mzee huyo mwenyewe ndiye anayeweza kukitegua na pengine anataka aingizwe kwenye kitabu cha Guiness ambacho kinaweza kumtoa Mtanzania wa kwanza aliyefanikiwa kuomba kwa muda mrefu na akiwa na umri mkubwa kuliko wote waliowahi kuomba duniani.

Simshangai mzee Matonya na siwalaumu wale wanaofuatilia maisha ya mzee huyo kwa karibu kila kukicha kwa kuwa tayari amekwisha jijengea umaarufu mkubwa wa kuomba, kazi ambayo hawezi kuiacha hadi mauti yatakapo mkuta.

Lakini kwa mfano huo wa mzee Matonya Watanzania wanapaswa kujiuliza kuwa wapo akina Matonya wangapi wanaoshindwa kuishi kwa dola moja kwa siku kutokana na kipato duni na hawawezi kuendesha maisha yao bila kuomba.

Zipo aina mbalimbali za kuomba na si tu aina hiyo ambayo mzee wetu Matonya anaitumia, wapo waombaji wakubwa waliovuka viwango hadi wakajitokeza kuwa waombaji wa mbinu za juu za ulaghai wanaoitwa ‘matapeli'.

Kama watu wanavyodai kuwa mzee huyo ana mali nyingi na mwanzo wake umetokana na fedha anazopewa kidogo kidogo na akizipeleka kwao kununulia mifugo iliyoendelea kuzaliana kazi hiyo.

Tukimsema Matonya tusisahau kuwa haitakuwa vigumu kujisema wenyewe na serikali yetu kwa kuwa wote tumekuwa omba omba na zaidi pale tunapoomba kila kitu kwa nchi wahisani ili waweze kuendesha bajeti yetu ya nchi.

Nchi wahisani sasa zinainyooshea mkono Serikali ya Tanzania kuwa licha ya kuomba na kupatiwa misaada mingi bado wahisani hao hawaridhishwi namna fedha zao zinavyotumika katika shughuli za maendeleo.

Wahisani wameshituka wameamua kupunguza misaada yao na hali inazidi kuwa ngumu upande wa serikali, ikitarajia kuwa na bajeti ya sh trilioni 11.1 kwa mwaka 2010/2011 fedha ambazo haziwezi kupatikana moja kwa moja kutoka vyanzo vya ndani.

Nchi kama Sweden inahoji namna serikali ya Tanzania inavyoendelea kuwa masikini na watu wake huku kukiwa na rasilimali za kila aina, wanashangaa huu umaskini tulionao unatoka wapi?

Ni majuzi tu, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda alinukuriwa na vyombo vya habari akiushangaa umasiki wa Watanzania, kuwa nchi hii ni ya neema imejaliwa rasilimali tele, ardhi kubwa, wasomi na wataalamu wa kila aina lakini mambo hayaendi.

Waziri Mkuu Pinda anashangaa umasikini wa nchi hii na hawezi kushangaa leo kwa kuwa yupo kwenye mfumo wa serikali tangu awamu ya kwanza na ana miaka zaidi ya 35 katika utumishi wa umma hivyo anaifahamu zaidi nchi na serikali zote zilizotangulia na hii ya awamu ya nne akiwa ndiye msimamizi mkuu wa shughuli za serikali.

Umaskini wa Watanzania ndio maajabu ya leo tunayoyaona na yanayowashangaza wahisani na waziri mkuu, kuwa inatia aibu nchi inapokuwa omba omba huku ikiwa na rasilimali tele, huko nje si bure kuwa tunaitwa kina ‘Matonya'.

Kama ilivyo kwa mzee Matonya alivyojibebea umaarufu mkubwa kwa kuomba, Watanzania tutaepukaje aibu ya kuomba kila siku nje, leo hii Pinda anahoji, hivi Watanzania nani kawaroga, mbona tuna kila kitu nchi hainyanyuki ?

Tukimshangaa mzee Matonya kumbe wote tunaomba na serikali yetu inaomba, sasa katika waombaji wote hii aibu ya kuendelea kuomba, kutegemea wahisani katika bajeti yetu itakwisha lini? Tumekosa nini?

Hii aibu ya kuomba inayofanywa na mzee Matonya na aibu ya nchi yenye neema kuendelea kuomba itatufikisha wapi ambako wenzetu wanazidi kwenda mbele kiuchumi sisi tunategemea kuomba?

Yupi bora, Matonya au Serikali na kama adha ya kuomba inawakera wananchi wanapomuona mzee huyo akihama huku na kule kufanya shughuli hiyo ni namna gani nchi wahisani zinavyoisema vibaya Tanzania inayoshindwa kutumia vyema rasilimali zake?

Umefika wakati ambao inatisha kusikia kuwa serikali ipo tayari kukopa benki na hilo halijalishi nchi wahisani zinapopunguza misaada kwenye bajeti ya serikali ya mwaka 2010/2011 na maneno yanayotolewa na serikali huko ni kujikaza kiume.

Muda wa kuendelea kumshangaa mzee Matonya umechukua miaka mingi huku tukishuhudia raslimali za nchi kama zingetumika vizuri watu kama akina Matonya wasingekuwepo kwa wingi.

Malalamiko kutoka kwa wafanyakazi yasingekuwepo kwa kuwa kila mtu angeweza kupata kipato cha kutosha kutokana na rasilimali zetu, wakulima na wafugaji wasingeweza kuzuiwa kuuza mazao yao, sasa wanalia kila mtu anaomba.

Kama kuomba ni aibu, basi tusimsakame vibaya mzee Matonya kwa kuwa hata serikali nayo inajiendesha kwa kuomba fedha kwenye mabenki na nchi wahisani.

Ili tuweze kuondokana na aibu hii, tujibu maswali ya Waziri Mkuu Pinda, hivi ni nani kawaroga Watanzania? Tumelaaniwa na nani, nchi haiendi, rasilimali tele, tumekosa nini ?
 
Kinachoumiza zaidi, wanatumia mabilioni kwenda kuomba omba nje ya nchi, wakirudi Tanzania, wanatumia mabilioni yote hayo kuishi maisha ya anasa.

Kwa mujibu wa msemaji wa kampeni ya Kikwete - fisadi Kinana, ccm wanatumia (pesa ya wananchi kwa kupitia ruzuku toka serikalini) dola 15,000 kwa masaa matano kukodi hii ndege ya kifahari kwa ajili ya mke wa raisi Kikwete:

2241536655_540d01c2cf.jpg
 
Speechless!!! Reason being tumeshasema na kusema na kusema.

Wakati umefika, tukaiadhibu CCM 31/10/2010. Period!
 
Upungufu+wa+vitanda+vya+kulala+hospitali+ya+Mwananyamala+7+Oktoba+2008.JPG


Hawa ni kina mama wakiwa wamelazwa Hospitali ya Mwananyamala, Dar es Salaam ilipo Ikulu ya Raisi
 
Upungufu+wa+vitanda+vya+kulala+hospitali+ya+Mwananyamala+7+Oktoba+2008.JPG


Hawa ni kina mama wakiwa wamelazwa Hospitali ya Mwananyamala, Dar es Salaam ilipo Ikulu ya Raisi

Inasikitisha, lakini tatizo ni kuwa Jk akifika kuomba kura hata hao akina mama wanasahau yote hayo. Ikifika 31.10 wataoongozwa na ushabiki wa kumpigia tena kikwete, miaka mingine mitano watasubiri katika mahangaiko kama hayo.

Kwanini hizo hela zinazofujwa na Ridhiwani na Salma zisiwafae kina mama kama hao?
Hapo ni 'core' ya nchi, Dar je mikoani hali si ndiyo haitamaniki?
 
Inasikitisha sana harafu wakitoka hapo hao akina mama watachagua CCM ndo ushangae maajabu ya dunia!
 
Mchungaji masanilo,
Hawa wakina mama pamoja na kuwaonea huruma wao wanafurahia sana hali hiyo. Ebu angalia picha hii ya wakina mama waliovalia sare ya majizi. Utashangaa kwamba karibu asilimia 70 ni wakinamama. hahahahahahahahahaha

40513_438608206224_104157016224_5148923_1611098_n.jpg
 
Mchungaji masanilo,
Hawa wakina mama pamoja na kuwaonea huruma wao wanafurahia sana hali hiyo. Ebu angalia picha hii ya wakina mama waliovalia sare ya majizi. Utashangaa kwamba karibu asilimia 70 ni wakinamama. hahahahahahahahahaha

40513_438608206224_104157016224_5148923_1611098_n.jpg

Mambo bure na 2000 ama 5000 ! Nadhani kwa umakini wao wanachukua Khanga na fedha kura wanajua!
 
Kwa TANZANIA kuomba misaada kwa nchi zilizoendelea si ajabu, nakuomba msaada hatujaanza na rais J.K. Tulianza toka enzi za nyerere na si TANZANIA peke yake ndio inaomba misaada. Hata nchi zote za AFRICA zinaomba misaada. Kwaio hata huyo W.SLAA mnayesema atakua ombaomba zaidi ya J.K, kwaio wananchi hatudanganyiki na hayo.:mad2::mad2::mad2:
 
SIYO siri tena. Tanzania imetajwa kuwa nchi ya kwanza barani Afrika na ya tatu duniani kwa kupata misaada kutoka nchi wahisani, ikiwa nyuma ya nchi zilizogubikwa na vita za Iraq na Afghanistan. Shirika moja la Marekani lijulikanalo kama ‘Visual Economics', limechapisha jarida lenye takwimu za kushtusha zinazoonyesha jinsi misaada ya maendeleo inavyotolewa duniani.

Shirika hilo linaloongoza duniani kwa kufichua takwimu za siri katika masuala ya uchumi na fedha limesema, misaada ya nchi wahisani kwa Tanzania imepaa kutoka Dola za Marekani 39.19 milioni (Sh66 bilioni) mwaka 1961 hadi Dola 2.89 bilioni (Sh3 trilioni) mwaka 2009 na kuifanya nchi hiyo kuwa kinara wa nchi za Afrika zinazopokea misaada kutoka nje na pia kushika nafasi ya tatu duniani ikitanguliwa na Iraq na Afghanistan.

Takwimu hizo zimewashtusha wananchi wengi ambao wamehoji kulikoni Tanzania imepokea misaada mingi kiasi hicho tangu ipate uhuru miaka 50 iliyopita lakini imebaki kuwa moja kati ya nchi chache duniani ambazo wananchi wake bado wanaogelea katika umaskini wa kutisha, kiasi cha wengi kuishi chini ya dola moja kwa siku. Wahisani wakubwa wa mipango ya maendeleo kwa Tanzania tangu uhuru ni Sweden, Norway, Marekani, Japan, The Netherlands, Denmark, Uingereza, Umoja wa Ulaya, Benki ya Maendeleo ya Afrika, Benki ya Dunia na Shirika la Fedha Duniani (IMF).

Inaeleweka kabisa nchi za Iraq na Afghanistan zinapoorodheshwa na shirika hilo la ‘Visual Economics' kama nchi ombaomba. Hakuna asiyejua kwamba nchi hizo zimekuwa katika vita kwa muda mrefu kiasi cha uchumi wa nchi hizo kuvurugika na watu wengi kuuawa. Katika mazingira ya vita, ambapo umwagaji damu na mauaji ya kujitoa muhanga hutawala, hakuna shughuli zozote za maendeleo zinazoweza kufanyika. Mkombozi pekee wa wananchi katika nchi hizo ni misaada ya nchi wahisani.

Lakini kitendawili kikubwa ambacho kimekuwa kigumu kuteguliwa ni juu ya Tanzania kuwa kinara wa nchi ombaomba barani Afrika na kushika nafasi ya tatu duniani, nyuma ya Iraq na Afghanistan. Kinyume na nchi hizo ambazo misaada nyingi inayotolewa ni ya kijeshi, Tanzania imekuwa ikipata misaada ya maendeleo katika nyanja za elimu, miundombinu, afya, maji, ujenzi, kilimo, nishati na usafirishaji, hivyo isingekuwa maskini iwapo misaada hiyo ingetumiwa kama ilivyokusudiwa.

Tanzania, mbali na kupata uhuru wake bila kumwaga damu mwaka 1961, nchi hiyo imekuwa kisiwa cha amani na wananchi wake wameishi miaka yote kwa amani na utulivu bila vita ya wenyewe kwa wenyewe. Nchi hii inao utajiri mkubwa na imetunukiwa na mambo mengi ya ajabu. Angalia ardhi kubwa yenye rutuba na rasilimali nyingine nyingi, zikiwamo madini ya kila aina, gesi, mbuga za wanyama, mazao ya biashara, misitu, mito maziwa, fukwe za bahari na wanyama pori.

Tafsiri ya takwimu za shirika hilo la ‘Visual Economics' ni kwamba Tanzania imeshindwa kusonga mbele kimaendeleo kwa sababu ya utegemezi mkubwa wa misaada ya wahisani na matumizi mabaya ya misaada hiyo, ikiwa ni pamoja na kukosekana kwa utawala bora, kama Ripoti ya Haki za Binadamu ya mwaka 2009 ilivyobainisha na kusema asilimia 20 ya bajeti ya Serikali kila mwaka inamezwa na vitendo vya rushwa.

Kutokana na changamoto iliyotolewa na shirika hilo, jambo la kufurahisha ni kwamba wananchi sasa wamegundua Tanzania inaweza kusonga mbele kimaendeleo bila misaada ya wafadhili, kwani misaada hiyo imeshindwa kufuta umaskini tangu tupate uhuru. Siyo siri tena kuwa, rasilimali za nchi zimenufaisha kundi dogo la watawala na mawakala wao walio nchini na nje ya nchi.

‘Visual Economics' limetufumbua macho. Yatupasa tutafakari wapi tunataka kwenda kama taifa ili tujenge uchumi wa kutukwamua katika lindi la umaskini. Misaada ya wahisani haitufai, tuachane nayo sasa. Njia pekee ni kujitegemea, kwani tunazo rasilimali za kutosha. Kinachotakiwa ni utashi wa kufanya hivyo.


Tanzania ?ombaomba? wa tatu ulimwenguni!
 
JK safari haziishi anazurura safari za nje kuomba omba na bakuli. Ndio mana tumekuwa wa kwanza kwa kupokea misaada mingi.
 
Misaada inatumika kulipa wabunge posho ya shilingi 200,000/= kwa siku wakati wananchi wanazidi kuwa maskini.
 
Wadau jee ni haki kuandaa sherehe kubwa na ghali ya miaka 50 ya uhuru ilihali dunia inatambua kuwa sisi ni taifa la tatu baada ya Iraq na Afganistani (ambazo ziko vitani) kwa kutegemea misaada?

Tunazo rasilimali nyingi sana, Madini ya aina mbalimbali,ardhi safi kwa kilimo,vivutio vya utalii, maji ya kutosha kila mahali, hakuna vita vya ndani wala nje, nk nk. lakini tumeshindwa kuzitumia rasilimali hizo ipasavyo kuinua maisha ya Mtanzania kwa miaka 50 ila tumewekeza katika kumsafirisha Rais wetu dunia nzima kila siku kutembeza Bakuli ili tusife njaa. Hili kalikiri Rais mwenyewe akitetea safari zake nyingi.

Bado pamoja na umasikini huo, mafisadi hatuwawajibishi, na kila siku wabunge wetu wanataka kujiongezea posho na marupurupu kutoka katika kapu lisilo na kitu ila misaada tuu.

Sasa nauliza jee sherehe hizi sio Aibu kwa Taifa letu?
 
Back
Top Bottom