Rais Samia hivi karibuni alifanya mabadiliko kwenye safu ya mawaziri wake na katika mabadiliko hayo mengine yamelalamikiwa na mengine yamesifiwa. Katika yale ambayo inaelekea wananchi wengi hawakupendezwa nayo ni pamoja na Waziri Madelu Mwigulu Nchemba kuachwa kuendelea kuwa Waziri wa Fedha na Waziri Mchengerwa kuondolewa wizara ya Utumishi.
Ni dhahiri kuwa Rais anapofanya mabadiliko kama haya huwa anapata ushauri toka kwa wasaidizi wake na watu wengine mbali mbali. Alipotoa hotuba yake ya kwanza baada ya kuwa Rais na kumtangaza makamu wake wa Rais kuwa angekuwa Dr. Phillip Mpango alitamka wazi kuwa huyo ndio angemtegemea sana na kumkabidhi docket ya mambo ya uchumi na hasa Fedha. Ni kwa sababu hiyo basi nachelea kusema kuwa kuendelea kuwapo kama Waziri wa Fedha Madelu Mwigulu Nchemba ni shinikizo la Mpango ili hali inafahamika kuwa Mwigulu haimudu wizara hiyo!
Ikumbukwe pia kwamba kabla ya kupata wadhifa wa kuwa makamu wa Rais, Mpango ndiye aliyekuwa Waziri wa Fedha chini ya Rais Magufuli . Maamuzi yote ya Fedha pamoja na lawama zote kuhusu Fedha ambazo marehemu analundikiwa leo hii zilikuwa na mkono wa Mpango; hivyo it is not in his interest kuona kuwa hiyo nafasi ya wizara ya Fedha inashikwa na mtu ambae ataonesha ufanisi kuliko alivyokuwepo yeye kwenye nafasi hiyo!! Nina hakika kabisa bila hiyo influence ya Mpango kwa Rais , Mwigulu leo hii baada ya malalamiko ya watu wengi kwenye platforms nyingi Rais Samia angetuteulia Waziri Mwingine katika safu yake ya mawaziri ambae angelionesha weledi zaidi kuhusu mambo ya Fedha zaidi ya yeye Mpango na Mwigulu.
Kuhusu kubadishwa Mchengerwa kutoka Utumishi na Kumleta Jennister Mhagama, wananchi wengi wanaamini huyu bwana alianza vizuri kutatua matatizo ya wafanya kazi na kuendelea kwake kwa nafasi ile kungeleta tija zaidi kuliko huyo aliyeletwa badala yake. Hilo linatokana na record ya utendaji wa huyo mwanamama huko alikotoka!!
Mawazo kama haya huko nyuma ilikuwa sio rahisi kuyatoa na kusikilizwa lakini ALLAHAMDULILLAH siku hizi tuna uhuru huo wa kutoa maoni na kusikilizwa!!!
Ni dhahiri kuwa Rais anapofanya mabadiliko kama haya huwa anapata ushauri toka kwa wasaidizi wake na watu wengine mbali mbali. Alipotoa hotuba yake ya kwanza baada ya kuwa Rais na kumtangaza makamu wake wa Rais kuwa angekuwa Dr. Phillip Mpango alitamka wazi kuwa huyo ndio angemtegemea sana na kumkabidhi docket ya mambo ya uchumi na hasa Fedha. Ni kwa sababu hiyo basi nachelea kusema kuwa kuendelea kuwapo kama Waziri wa Fedha Madelu Mwigulu Nchemba ni shinikizo la Mpango ili hali inafahamika kuwa Mwigulu haimudu wizara hiyo!
Ikumbukwe pia kwamba kabla ya kupata wadhifa wa kuwa makamu wa Rais, Mpango ndiye aliyekuwa Waziri wa Fedha chini ya Rais Magufuli . Maamuzi yote ya Fedha pamoja na lawama zote kuhusu Fedha ambazo marehemu analundikiwa leo hii zilikuwa na mkono wa Mpango; hivyo it is not in his interest kuona kuwa hiyo nafasi ya wizara ya Fedha inashikwa na mtu ambae ataonesha ufanisi kuliko alivyokuwepo yeye kwenye nafasi hiyo!! Nina hakika kabisa bila hiyo influence ya Mpango kwa Rais , Mwigulu leo hii baada ya malalamiko ya watu wengi kwenye platforms nyingi Rais Samia angetuteulia Waziri Mwingine katika safu yake ya mawaziri ambae angelionesha weledi zaidi kuhusu mambo ya Fedha zaidi ya yeye Mpango na Mwigulu.
Kuhusu kubadishwa Mchengerwa kutoka Utumishi na Kumleta Jennister Mhagama, wananchi wengi wanaamini huyu bwana alianza vizuri kutatua matatizo ya wafanya kazi na kuendelea kwake kwa nafasi ile kungeleta tija zaidi kuliko huyo aliyeletwa badala yake. Hilo linatokana na record ya utendaji wa huyo mwanamama huko alikotoka!!
Mawazo kama haya huko nyuma ilikuwa sio rahisi kuyatoa na kusikilizwa lakini ALLAHAMDULILLAH siku hizi tuna uhuru huo wa kutoa maoni na kusikilizwa!!!